Serikali fuatilieni hizi kampuni za kitapeli zinazodai zinakopesha mitandaoni, mama zetu wanalizwa vibaya sana

Serikali fuatilieni hizi kampuni za kitapeli zinazodai zinakopesha mitandaoni, mama zetu wanalizwa vibaya sana

Vigezo vya kukopa Tala Ni gani
Screenshot_20230911-101329.png

Master wa kutoa mikopo ni huyo hapo.. 👆👆
 
Wewe utakuwa ndio tala yenyewe hakuna mtu aliweka pesa akapewa mkopo wake ni matapeli huo ni uongo hakika
Hapana mimi siye, ila sikushauli uende huko mkuu..

Kama unataka mkopo watafute Hawa, ingawa wana riba kubwa sana. 👇👇👇
Screenshot_20230911-101329.png
 
Watu waache tamaa,utapeli upo mpaka kanisani na haya yote ni kutaka mafanikio ya haraka,serikali ifanyeje ikiwa watu wenyewe wana vichwa vigumu,mara pakua mkwanja,mara vuka na chako yaani ilimradi tafrani,
Eti unaweka kianzio tena 2M ndo upate mkopo serious?mnailaumu bure serikali

Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app
 
Hizi kampuni fake zinadai zimesajiliwa na serikali lakini zinafanya kazi ya utapeli, zipo nyingi, cjui tala imarisha maisha. Tulia mikopo online na zingine zinatumia majina ya Jokate Mwegelo na kuna hawa wanatumia matangazo na video za watu mashuhuri kwa kuziedit.

Watanzania wamepigika wanaamini kila kitu ni fursa jambo ambalo sio kweli. Kuna dada anaitwa Lilian jana kashawishiwa na kampuni moja jina ninalo, kwamba aweke kuanzio cha milion 2 apewe mkopo wa milioni kumi kapigwa kapoteza fahamu kwa sababu hiyo pesa na yeye alikopa sehemu. Kwanini polisi mnashindwa kupambana na wizi wa mitandaoni?

Serikali yetu inamifumo yote lakini inaacha makanjanja wanawaliza watu mitaani ,onyo na angalizo hakuna taasisi inaweza kumkopesha mtu online labda songesha ya Vodacom.
Serikali iache ku deal na Tundu Lissu huko Loliondo ikusaidie vimikopo vidogo dogo vya biashara ya vitumbua?
Hizo mirofinance inatoa mikopo midogo, mikopo ya kuzungumzia ni ile ya MABENKI kamili , tena kuanzia milioni 50 kuendelea si mikopo ya kununulia IST.
 
Kwa nini ulikopa umeshindwa kuwalipa ndio unawaita matapeli?ila riba zao ni kaushA damu na wanapiga simu hao na vitisho juu
Je, wako kisheria !!? Kwa maana wana Kibali cha BOT, Leseni ya Biashara toka BRELA, TIN number !!?? Na je Sera yao (Company's Business/Lending Policy) inawaruhusu kufanya hivyo kwa mujibu wa sheria na taratibu !!!??? Kama sivyo kuna tatizo mahali na ukitapeliwa kwa asilimia kubwa, ni jambo la kujitakia.
 
mimi naona ni ujinga wetu ndiyo kwa kiwango kikubwa unatufanya tutapeliwe.

Kabla ya kupewa mkopo hebu jaribu kuuliza kwanza, ni bora ulipe japo vishilingi vidogo ili mwanasheria aupitie na akupe fikra zaidi.

Lakini wewe ukiambiwa utapewa mkopo ulipe kwa miaka 10 unaona siyo shida matokeo yake unakuja kulalama humu ambapo hatuwezi kutoa msaada wo wote.
 
Kukopa kwa ujumla ni janga kwa kweli. Ni muhimu kuyaelewa masharti ya mikopo unapotaka kukopa. Mikopo huwa hailengi kumsaidia anayekopa, bali ni kutatua tatizo aliyonayo kwa kipindi hicho na kuongezea matatizo mengine mbele ya safari. Nidhamu ni kuchukua mkopo pale ambapo it's a matter of life and death. Na ujue kwamba utasumbuka sana kuurudisha mkopo
 
TALA TANZANIA = Nadaiwa 500000/-
Mtandao X = Nadaiwa 780000/-
😊😊😊😊😊😊
Unawezaje kukukopa hadi kufikisha kiwango hicho?
Ninavyojua wanakutegeshea ahadi za kukopa kiwango kikubwa lakini ukitaka kiwango hicho wanakupatia pesa ndogo sana!
 
Back
Top Bottom