Serikali haioni huu utapeli wa wachungaji? Au wao ya kwao mazuri hivyo wananchi watajijua wenyewe?

Serikali haioni huu utapeli wa wachungaji? Au wao ya kwao mazuri hivyo wananchi watajijua wenyewe?

Steven Joel Ntamusano

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2023
Posts
5,203
Reaction score
3,913
Katika haya makanisa ya kilokole unaweza ukacheka sana yale yanayoendelea haswa ifikapo Jumapili. Wale wapambe wa mchungaji wakiliona gari la bei mbaya haraka sana wanawasogeza waumini ili lipite na aliyepo ashuke na aende kukaa katika sehemu maalum.

Kwa mchungaji na wasaidizi wake kuliona gari zuri la kisasa ni ujio wa neema fulani. Bahati mbaya kwa waumini wamekuwa sawa na waliofanywa misukule, hawaelewi kwamba wametekwa akili zao.

Serikali haiumizwi na mateso wanayoyapata wananchi wanaofanyiwa vitendo hivi vya kishenzi kwa kudanganywa wakatoa hicho hicho kidogo wanachokipata kwa taabu?.

Ifike mahali tujipunguzie hii mizigo ya dhambi kwa kutumia jina la Mungu. Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Serikali haiyaoni haya madudu ya wachungaji mpaka wanafikia kujiita kiboko ya wachawi?. Ubinadamu umepotelea wapi yarabi!.

Serikali yetu haina ule uthubutu kama alioufanya Rais Paul Kagame kule Rwanda kiasi cha kufungia makanisa ya kitapeli mengi tu. Siuoni huo uthubutu ikiwa Rais SSH anamtuma mkuu wa mkoa Chalamila kwenda kuchangia masuala ya kanisa.

Wanasiasa wanatembelea ule umaarufu wa wachungaji wakisahau kuwa wanaoumia ni wananchi wa kawaida wenye kupata pesa kwa jasho jingi. Hata kuamua kumfungia huyo kiboko ya wachqwi ni maamuzi ya kinafiki tu, ya kisiasa yasiyotoka mioyoni mwao.

Serikali inafanya lolote lile ili iweze kuendelea kuwa na uhalali wa kuchaguliwa katika miaka ya uchaguzi, baada ya hapo ni mwendo wa kufungia vioo haya mateso ya hao wanaoumizwa na wachungaji matapeli wanaoibuka kama uyoga.

ikifikia Jumapili pale Kawe hapafai kwa foleni na wingi wa waumini wanaotoka kuacha pesa zinazowatajirisha hawa wachungaji. Wao wanateseka na umaskini wao na wachungaji wanaendelea kutajirika kwa ukosefu wa maarifa wa waumini.

Siuoni ujasiri wa Rais Kagame akiwa nao Rais SSH au yoyote yule wa Tanzania. Mungu tunamhitaji siku zote kwa ustawi wa Tanzania lakini tumefungulia sana mlango masuala ya dini kiasi cha matapeli kuendelea kuwaumiza waumini wanyonge waliokata tamaa za kimaisha.

Mungu Ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.
 
Imani ni zaidi ya uchawi,watu walifunga mpaka kufa ili wakamuone Yesu kwa sababu ya imani,watu waliamini watafika ulaya kuhubiri injini kwa kupanda ndege bure passport biblia kwa sababu ya imani,Kibwetere wa Uganda aliwalipua waumini wake kwa sababu ya imani na bado watu hawakomi,ukiona serekali ikiingilia imani ya mtu ujue kuwa imani hiyo imegusa maslahi ya serekali.
 
Yanayoendelea huko waachie wenyewe.

Kazi ya serikali ni kuhakikisha watu wake wanapata elimu bora. Kama pamoja na elimu zao watu hao wameamua kuendelea kwenda misikitini na makanisani basi hayo ni maamuzi yao na haki yao.

Waache na imani zao, hayakuhusu!!
 
Imani ni zaidi ya uchawi,watu walifunga mpaka kufa ili wakamuone Yesu kwa sababu ya imani,watu waliamini watafika ulaya kuhubiri injini kwa kupanda ndege bure passport biblia kwa sababu ya imani,Kibwetere wa Uganda aliwalipua waumini wake kwa sababu ya imani na bado watu hawakomi,ukiona serekali ikiingilia imani ya mtu ujue kuwa imani hiyo imegusa maslahi ya serekali.
CCM wanafaidika na huu ujinga wa halaiki alioutabiri marehemu Profesa Chachage.
 
Yanayoendelea huko waachie wenyewe.

Kazi ya serikali ni kuhakikisha watu wake wanapata elimu bora. Kama pamoja na elimu zao watu hao wameamua kuendelea kwenda misikitini na makanisani basi hayo ni maamuzi yao na haki yao.

Waache na imani zao, hayakuhusu!!
Ninayaona mahangaiko yao na wanapoishiwa pesa tunalazimika kuwasaidia kibinadamu.
 
Katika haya makanisa ya kilokole unaweza ukacheka sana yale yanayoendelea haswa ifikapo Jumapili. Wale wapambe wa mchungaji wakiliona gari la bei mbaya haraka sana wanawasogeza waumini ili lipite na aliyepo ashuke na aende kukaa katika sehemu maalum...
usiilaumu serikali wakati maamuzi ni ya mtu binafsi kujihusisha au kutojihusisha na hizo dini
 
usiilaumu serikali wakati maamuzi ni ya mtu binafsi kujihusisha au kutojihusisha na hizo dini
Serikali kutokuwa na dini sio kigezo cha raia maskini kugeuzwa mtaji wa kuwatajirisha wachungaji kwa kuleta utapeli kwenye maisha yao kwa njia ya biashara ya Mungu.

Upo mchango wa serikali. Kagame aliwafungia vioo hawa wachungaji na leo Rwanda imesimama kiuchumi.
 
Yanayoendelea huko waachie wenyewe.

Kazi ya serikali ni kuhakikisha watu wake wanapata elimu bora. Kama pamoja na elimu zao watu hao wameamua kuendelea kwenda misikitini na makanisani basi hayo ni maamuzi yao na haki yao.

Waache na imani zao, hayakuhusu!!
Hili jambo siyo la kuchukulia mzaha kama unavyofikilia, ukiwaacha taifa litageuka kuwa la ombaomba, wengi hawapati muda wa kuzalisha muda mwingi ni kwenye maombi. Jumapili asubuhi hadi jioni, Jumanne kwenye kwaya, Jumatano maombi ya pamoja, Ijumaa maombezi na uponyaji, Jumamosi maombi ya kuombea familia🤔🤔, huo muda wa kufanya kazi na kuzalisha uko wapi?? Kama siyo kuwa ombaomba ni nini?? Wanamadeni mpaka uvunguni
 
Serikali kutokuwa na dini sio kigezo cha raia maskini kugeuzwa mtaji wa kuwatajirisha wachungaji kwa kuleta utapeli kwenye maisha yao kwa njia ya biashara ya Mungu.

Upo mchango wa serikali. Kagame aliwafungia vioo hawa wachungaji na leo Rwanda imesimama kiuchumi.
kwani wamelazimishwa kwenda huko asee kama mleta mada kaona ni utapeli hao wanaokwenda wao hawana akili? ni swala la kuchagua wakiacha kwenda kwenye hayo makanisa hawatatapeliwa muda mwingine nchi yetu haiendelei si kwakua tuna viongozi hovyo tu ila hata wananchi ni maiti zilizooza
 
Imani huwezi kuicontroo kwa politics analysis,hao unaosema wanatapeliwa hawajaenda kushtaki popote ? Na hawajawahi kulalamika popote ,tatizo wewe huna hela kwa hiyo unataka kuwapangia watu matumizi ya pesa zao !? Tafuta hela kuku wewe ukisema makanisa yanatapeli watu vipi betting na slot za kichina ? Tafuta hela acha umama muraa!!
 
..hujaona Raisi anatuma Wasaidizi wake kuchangia ktk Makanisa yao hao wahuni?

..Na inashangaa nini ikiwa Mch.Gwajima ni mbunge wa Ccm?
Ubinafsi wa hali ya juu wanatumia mbinu ile ile ya miaka mingi nikune mgongo wangu niukune wa kwako.

Ubinafsi ni mbaya sana na serikali imeamua kuulea.
 
Imani huwezi kuicontroo kwa politics analysis,hao unaosema wanatapeliwa hawajaenda kushtaki popote ? Na hawajawahi kulalamika popote ,tatizo wewe huna hela kwa hiyo unataka kuwapangia watu matumizi ya pesa zao !? Tafuta hela kuku wewe ukisema makanisa yanatapeli watu vipi betting na slot za kichina ? Tafuta hela acha umama muraa!!
Waumini ni wengi huko makanisani kuliko hao jamaa wa betting. Ukosefu wa maarifa unatumiwa kama mtaji na mamlaka za kisiasa, mchezo mchafu sana.
 
Kagame kapiga marufuku makanisa 400 na Rwanda ipo kibiashara zaidi hakuna hawa wachungaji na maaskofu wenye kufanya shughuli za kishirikina.
Usije kukuta hayo makanisa yameshakimbilia Tanzania! Mungu atusaidie!

Ila kelele na vyombo vya habari vikiendelea kufichua huu utapeli Tz tutapona. Tusiache huu mzigo kwa Serikali pekeee!!!!
 
Back
Top Bottom