Serikali haioni huu utapeli wa wachungaji? Au wao ya kwao mazuri hivyo wananchi watajijua wenyewe?

Serikali haioni huu utapeli wa wachungaji? Au wao ya kwao mazuri hivyo wananchi watajijua wenyewe?

Si unaona hata maisha yao🤔, wenzako wanaishi kwa misaada toka falme za kiarabu, weweje unataka kuishi kwa misaada ipi???
Serikali haiwezi kupiga marufuku hawa kisha ikawaacha wale. Itabidi ipige marufuku wote, jambo ambalo ni hatari kwa usalama wa nchi.
 
Katika haya makanisa ya kilokole unaweza ukacheka sana yale yanayoendelea haswa ifikapo Jumapili. Wale wapambe wa mchungaji wakiliona gari la bei mbaya haraka sana wanawasogeza waumini ili lipite na aliyepo ashuke na aende kukaa katika sehemu maalum.

Kwa mchungaji na wasaidizi wake kuliona gari zuri la kisasa ni ujio wa neema fulani. Bahati mbaya kwa waumini wamekuwa sawa na waliofanywa misukule, hawaelewi kwamba wametekwa akili zao.

Serikali haiumizwi na mateso wanayoyapata wananchi wanaofanyiwa vitendo hivi vya kishenzi kwa kudanganywa wakatoa hicho hicho kidogo wanachokipata kwa taabu?.

Ifike mahali tujipunguzie hii mizigo ya dhambi kwa kutumia jina la Mungu. Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Serikali haiyaoni haya madudu ya wachungaji mpaka wanafikia kujiita kiboko ya wachawi?. Ubinadamu umepotelea wapi yarabi!.

Serikali yetu haina ule uthubutu kama alioufanya Rais Paul Kagame kule Rwanda kiasi cha kufungia makanisa ya kitapeli mengi tu. Siuoni huo uthubutu ikiwa Rais SSH anamtuma mkuu wa mkoa Chalamila kwenda kuchangia masuala ya kanisa.

Wanasiasa wanatembelea ule umaarufu wa wachungaji wakisahau kuwa wanaoumia ni wananchi wa kawaida wenye kupata pesa kwa jasho jingi. Hata kuamua kumfungia huyo kiboko ya wachqwi ni maamuzi ya kinafiki tu, ya kisiasa yasiyotoka mioyoni mwao.

Serikali inafanya lolote lile ili iweze kuendelea kuwa na uhalali wa kuchaguliwa katika miaka ya uchaguzi, baada ya hapo ni mwendo wa kufungia vioo haya mateso ya hao wanaoumizwa na wachungaji matapeli wanaoibuka kama uyoga.

ikifikia Jumapili pale Kawe hapafai kwa foleni na wingi wa waumini wanaotoka kuacha pesa zinazowatajirisha hawa wachungaji. Wao wanateseka na umaskini wao na wachungaji wanaendelea kutajirika kwa ukosefu wa maarifa wa waumini.

Siuoni ujasiri wa Rais Kagame akiwa nao Rais SSH au yoyote yule wa Tanzania. Mungu tunamhitaji siku zote kwa ustawi wa Tanzania lakini tumefungulia sana mlango masuala ya dini kiasi cha matapeli kuendelea kuwaumiza waumini wanyonge waliokata tamaa za kimaisha.

Mungu Ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.
wachungaji hawana tofauti na wanasiasa so wanaendana nao ndio maana hawawezi kuwapigia kelele. utasikia tumchagie mchungaji anunue gari, au tumchangie mwanasiasa fulani anunue gari wakati huyo ana magari mengi tu na anayechanga hata moja hana. masikini atamlisha tajiri huku yeye akiendelea kufa njaa
 
Ulisha yasikia ya "Shakahola" hapo nchi jirani ya Kenya?
Hata kama mtu huyo binafsi anahatarisha maisha yake na wengine? Hiyo ni serikali ya wapi hiyo?
wajinga ndio waliwao kama ww hujaweza kwenda kwann wao waende kwani hawana akili..... kwahyo mnasubiri raisi aseme hataki makanisa ili mumseme na uislamu wake.... ukiacha hisia ukaangalia uhalisia utajifunza haya mambo mtu halazimishwi ni tamaa zake za mijujiza na mafanikio bila kazi acha waliwe vichwa
 
Serikali ifanye nini kwenye Imani za watu so long as haujalazimishwa wala sio kero kwa wanaokuzunguka wenye imani tofauti?

Ukishaanza kuingia kwenye mambo ya mtu anavyoamini (ukizingatia zote ni Imani sio Facts) na kuna mambo ya perception na subjective-ness Amini nakwambia hakuna Imani hata moja itakayobaki.... Tuendelee na Msimamo wetu Serikali haina Dini ila fanya Imani yako kwa faida yako na bila Kero kwa wengine labda cha kusanya sababu hizi taasisi zimekuwa za kibiashara na kama hazitoi direct physically aids kwa watu basi zianze kulipa Kodi....
 
Hii serikali Wacha iendelee kukaa kimya na kufumbia macho matapeli haya mpaka yatokee ya Kibwetere na msitu shakhahoa ndio waamke.
Yule aliyejiita "Kiboko ya Wachawi" anatamka waziwazi redioni kuwa anamuua mtu kisa eti ni mchawi na anafufua maiti na serikali ipo pono tuu
 
Duh!
Kwa kweli leo nimecheka, tena sana! Na hapa kwenye hayo maneno niliyo nyanyua ndipo mbavu zilikaribia kuvunjika kabisa!

Kinacho changia nicheke hivi, ni kukusoma wewe kwenye mada kama hii uliyo ileta leo hapa; tofauti, tena mbali kabisa na zile tulizo zoea kukutana.

Niwe mkweli wa nafsi yangu, ninakubaliana kabisa na maudhui ya mada yako hapa. Lakini, kama ujuavyo, na katika mwelekeo ule ule unao elezwa na mistari niliyo nukuu hapo juu; makanisa haya ni biashara, tena biashara zakulaza akili za watu, na hasa waliochanganyikiwa na hali ngumu za maisha. Husemwa, "Wajinga ndio waliwao",...; na kama ujuavyo kwenye nchi yetu hii, muumini mkubwa wa "ujinga" wa waTanzania ni CCM na serikali yake, ambayo kwa bahati nzuri au mbaya umeikutanisha na washirika wenzake katika kuwalaza akili waTanzania.

Sikuendelea kusoma hayo mengine huko chini, lakini nahisi mwelekeo wake ni huo huo nilio upata tokea huko juu hadi hapo nilipo ishia na kunukuu hayo maneno uliyo andika wewe.

Sijui hili taifa tutaishia wapi, iwapo kila mwenye nafasi anatafuta ku'take advantage' ya hawa maskini; siyo kwa mali tu, bali hadi kwenye fikra!
Wajinga ndiyo mtaji
Na kuna watu huko serikalini
Wameingizwa kwenye hayo makanisa....ni kama wanawalinda
We si unaona hao mitume manabii wanakaribishwa mpaka mjengoni
Kikubwa za kuambiwa changanya
Na zako

Ova
 
Watajijua wenyewe wajinga ndio waliwao tukiwambia waje kwenye dini haki wanakaa wakidanganyana kule ati magaidi na wanafuga majini
 
Kwa Kuhani Musa
Sadaka za
Partnership
Ujenzi wa vyoo
Ujenzi wa ghorofa tatu
Asali ya mwambani toka Israel
Maji ya mifuniko rangi mbalimbali
Chumvi
Udongo
Meza ya bwana
Damu ya Yesu
Ununuzi wa vyombo
... .... itaendelea
 
Nani anakupa haki ya kuamua makanisa gani ya kweli na yapi ya uongo? Hilo dhehebu lako una uhakika gani ni la kweli?

Kama serikali ikitaka kufungia makanisa ya uongo litabaki kanisa Katoliki pekee. Je uko tayari kuuishi ukweli huo?

Nchi hii katiba imetoa uhuru wa kuabudu sio kazi ya serikali kuwaamulia watu wapi waabudu.

Watu kuibiwa kanisani kwa kudanganywa ni sawa na watu kutumia vipato vyao vyote kwa uasherati na ulevi, kila mmoja ana uhuru wa kutumia pesa yake jinsi anavyopenda.
Dini zikizidi ni umaskini mtupu unaosambazwa kwa kasi. Umaskini wetu wa vichwani unaendelea kusambaza umaskini mbaya zaidi kila kona ya TZ.

Wahindi wametapakaa dunia nzima wakiwa ni wataalam wa IT na masuala yote yenye kuhitaji shule kubwa, lakini wanaabudu Ng'ombe yaani ile mboga unayokula nyumbani wewe na familia yako ndio mungu wao.

Wachina hawamuabudu Mungu wetu wao pia wana miungu yao ya kila aina, lakini maarifa yao yanawapa uwezo wa kuuza bidhaa za kila aina dunia nzima.

Ubunifu tumepewa na Mungu tuutumie kwa ajili ya vizazi vyetu, tunashindwa kwenye mifumo ya elimu na ubunifu wetu unakuwa ni zero halafu tunategemea maji ya Mwaposya na mafuta ya mchungaji mwingine viwe ni vitu vya kutuokoa, hakuna kitu kama hicho.
 
RC Chalamila anaenda kumpa saport yule jamaa kujaza nyomi inaelekea CCM inafarijika kuona jamii iliyowapa umasikini inamlilia Mungu kupitia wahuni wa makanisa ya kiroho badala ije iwalaumu wao.
Hao wahuni wa makanisa ya kiroho lao moja na wahuni wa huko serikalini.

Ni ubinafsi kwa kwenda mbele. CCM wanaangalia kura na hao wachungaji wanajali pesa anayeumia ni huyo muumini anayeshinda juani kutwa nzima.
 
Kuna muumini mmoja wa Mwamposa alitoa ushuhuda eti baada ya kubandika picha ya Mwamposa kwenye mtungi wa ges hadi leo miezi 6 imepita gesi haijaisha, na watu wakapiga makofi niliwaonea huruma sana.
Stupidity of africans
 
Serikali hasa ile ya JPM (RIP), iliwapigania sana wanyonge ila haya makanisa wanawaona wanyonge kama "malofa fulani". Hawapeleki fungu lililoshiba kanisani. Naomba serikali iwakalie kooni, TRA wawe mlangoni na kapu lao, jamaa wanachuma sana tena kilaiiiiiiiiiiini!
 
Kwa hiyo unataka ushauri nini watu warudishwe Roma kwa viboko? Au unataka serikali ifute makanisa zibaki bar
Uwepo wa Mungu haukwepeki lakini uvivu wetu hauwezi kuhalalishwa kwa kumtumia Mungu.

Katupa akili vichwani mwetu, katupa nguvu za miili yetu. Ni wajibu wetu kuchangamsha vichwa vyetu kufanya kazi na kuwa wabunifu.

Kuna watu hawamuamini huyu Mungu tunayemuamini sisi lakini kila kukicha maisha yao yamejaa baraka tele.

Ambani bilionea wa India anaabudu ng'ombe yeye na familia yake.
 
Katika haya makanisa ya kilokole unaweza ukacheka sana yale yanayoendelea haswa ifikapo Jumapili. Wale wapambe wa mchungaji wakiliona gari la bei mbaya haraka sana wanawasogeza waumini ili lipite na aliyepo ashuke na aende kukaa katika sehemu maalum.

Kwa mchungaji na wasaidizi wake kuliona gari zuri la kisasa ni ujio wa neema fulani. Bahati mbaya kwa waumini wamekuwa sawa na waliofanywa misukule, hawaelewi kwamba wametekwa akili zao.

Serikali haiumizwi na mateso wanayoyapata wananchi wanaofanyiwa vitendo hivi vya kishenzi kwa kudanganywa wakatoa hicho hicho kidogo wanachokipata kwa taabu?.

Ifike mahali tujipunguzie hii mizigo ya dhambi kwa kutumia jina la Mungu. Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Serikali haiyaoni haya madudu ya wachungaji mpaka wanafikia kujiita kiboko ya wachawi?. Ubinadamu umepotelea wapi yarabi!.

Serikali yetu haina ule uthubutu kama alioufanya Rais Paul Kagame kule Rwanda kiasi cha kufungia makanisa ya kitapeli mengi tu. Siuoni huo uthubutu ikiwa Rais SSH anamtuma mkuu wa mkoa Chalamila kwenda kuchangia masuala ya kanisa.

Wanasiasa wanatembelea ule umaarufu wa wachungaji wakisahau kuwa wanaoumia ni wananchi wa kawaida wenye kupata pesa kwa jasho jingi. Hata kuamua kumfungia huyo kiboko ya wachqwi ni maamuzi ya kinafiki tu, ya kisiasa yasiyotoka mioyoni mwao.

Serikali inafanya lolote lile ili iweze kuendelea kuwa na uhalali wa kuchaguliwa katika miaka ya uchaguzi, baada ya hapo ni mwendo wa kufungia vioo haya mateso ya hao wanaoumizwa na wachungaji matapeli wanaoibuka kama uyoga.

ikifikia Jumapili pale Kawe hapafai kwa foleni na wingi wa waumini wanaotoka kuacha pesa zinazowatajirisha hawa wachungaji. Wao wanateseka na umaskini wao na wachungaji wanaendelea kutajirika kwa ukosefu wa maarifa wa waumini.

Siuoni ujasiri wa Rais Kagame akiwa nao Rais SSH au yoyote yule wa Tanzania. Mungu tunamhitaji siku zote kwa ustawi wa Tanzania lakini tumefungulia sana mlango masuala ya dini kiasi cha matapeli kuendelea kuwaumiza waumini wanyonge waliokata tamaa za kimaisha.

Mungu Ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.
Mtoa mada najaribu kukuelewa ila naomba nikuulize.

Makanisa ya kilokole ni yapi?

Unasema waumini wao wametekwa kiakili, una ushahidi gani kwamba wametekwa kiakili?

Je yakifanyika kama ya Rwanda una uhakika hakuna atakayetekwa kiakili?

Je unadhani katiba yetu inatoa uhuru wa kuabudu uliopitiliza?

Hao wanaoenda Kawe hawana haki ya kutoa sadaka kama sehemu ya ibada zao hata kama ni maskini ?

Nakubaliana na serikali kuyafungia makanisa yote yanaoenda kinyume na sheria na katiba zetu, mfano yule anayejiita kiboko ya wachawi naona serikali imechelewa sana kumfungia maana alikuwa analeta uchonganishi wa waziwazi.

Tuisadie serikali kubainisha ukiukwaji wa katiba/sheria zetu unaofanywa na makanisa, kuilaumu kwa ujumla tu utakuwa unaionea.
 
Mtoa mada najaribu kukuelewa ila naomba nikuulize.

Makanisa ya kilokole ni yapi?

Unasema waumini wao wametekwa kiakili, una ushahidi gani kwamba wametekwa kiakili?

Je yakifanyika kama ya Rwanda una uhakika hakuna atakayetekwa kiakili?

Je unadhani katiba yetu inatoa uhuru wa kuabudu uliopitiliza?

Hao wanaoenda Kawe hawana haki ya kutoa sadaka kama sehemu ya ibada zao hata kama ni maskini ?

Nakubaliana na serikali kuyafungia makanisa yote yanaoenda kinyume na sheria na katiba zetu, mfano yule anayejiita kiboko ya wachawi naona serikali imechelewa sana kumfungia maana alikuwa analeta uchonganishi wa waziwazi.

Tuisadie serikali kubainisha ukiukwaji wa katiba/sheria zetu unaofanywa na makanisa, kuilaumu kwa ujumla tu utakuwa unaionea.
Kagame aliyafunga makanisa 400 baada ya kuwataka wanaoyaendesha kuonyesha vyeti vya theolojia. Wakijipunguza wenyewe na Rwanda ina makanisa machache yamebakia.

Dini ni biashara katika hali ngumu ya kiuchumi ya kidunia ya miaka ya sasa. Wateja ni mamilioni ya watu wanaoishi kwa shida wakitafuta riziki kwa ugumu usioweza kuelezeka.

Tatizo ni maarifa, wengi wetu hatuna hayo maarifa na kibaya zaidi serikali inayoongoza inaendelea kujiweka katika hali ya kuutumia ujinga wa wengi kama mtaji wa wao kuendelea kuwepo madarakani.

Waumini wa Mwamposya kule Moshi walikanyagana wakigombea mafuta yenye upako na watu kadhaa wakafariki dunia, ulisikia kauli yoyote ya maana kutoka seriikalini?. Kwa kanisa la Mwaposya kusababisha mauaji ya raia wasio na hatia alipaswa kushtakiwa kwa Manslaughter lakini serikali ilifumbia macho kwa sababu huyu mchungaji ni sehemu ya wale wanaoiombea serikali katika vipindi mbalimbali.
 
Back
Top Bottom