Mzalendo Uchwara
JF-Expert Member
- Jan 26, 2020
- 4,437
- 13,836
Serikali haiwezi kupiga marufuku hawa kisha ikawaacha wale. Itabidi ipige marufuku wote, jambo ambalo ni hatari kwa usalama wa nchi.Si unaona hata maisha yao🤔, wenzako wanaishi kwa misaada toka falme za kiarabu, weweje unataka kuishi kwa misaada ipi???
Hao wanaotibu magonjwa yote kwa maombi wanatakiwa kuthibitisha hilo kwa mamlaka za afya,wakishindwa wapigwe marufukuTatizo lipo kwa wananchi wenyewe, waache wahangaike na imani zao.!
wachungaji hawana tofauti na wanasiasa so wanaendana nao ndio maana hawawezi kuwapigia kelele. utasikia tumchagie mchungaji anunue gari, au tumchangie mwanasiasa fulani anunue gari wakati huyo ana magari mengi tu na anayechanga hata moja hana. masikini atamlisha tajiri huku yeye akiendelea kufa njaaKatika haya makanisa ya kilokole unaweza ukacheka sana yale yanayoendelea haswa ifikapo Jumapili. Wale wapambe wa mchungaji wakiliona gari la bei mbaya haraka sana wanawasogeza waumini ili lipite na aliyepo ashuke na aende kukaa katika sehemu maalum.
Kwa mchungaji na wasaidizi wake kuliona gari zuri la kisasa ni ujio wa neema fulani. Bahati mbaya kwa waumini wamekuwa sawa na waliofanywa misukule, hawaelewi kwamba wametekwa akili zao.
Serikali haiumizwi na mateso wanayoyapata wananchi wanaofanyiwa vitendo hivi vya kishenzi kwa kudanganywa wakatoa hicho hicho kidogo wanachokipata kwa taabu?.
Ifike mahali tujipunguzie hii mizigo ya dhambi kwa kutumia jina la Mungu. Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Serikali haiyaoni haya madudu ya wachungaji mpaka wanafikia kujiita kiboko ya wachawi?. Ubinadamu umepotelea wapi yarabi!.
Serikali yetu haina ule uthubutu kama alioufanya Rais Paul Kagame kule Rwanda kiasi cha kufungia makanisa ya kitapeli mengi tu. Siuoni huo uthubutu ikiwa Rais SSH anamtuma mkuu wa mkoa Chalamila kwenda kuchangia masuala ya kanisa.
Wanasiasa wanatembelea ule umaarufu wa wachungaji wakisahau kuwa wanaoumia ni wananchi wa kawaida wenye kupata pesa kwa jasho jingi. Hata kuamua kumfungia huyo kiboko ya wachqwi ni maamuzi ya kinafiki tu, ya kisiasa yasiyotoka mioyoni mwao.
Serikali inafanya lolote lile ili iweze kuendelea kuwa na uhalali wa kuchaguliwa katika miaka ya uchaguzi, baada ya hapo ni mwendo wa kufungia vioo haya mateso ya hao wanaoumizwa na wachungaji matapeli wanaoibuka kama uyoga.
ikifikia Jumapili pale Kawe hapafai kwa foleni na wingi wa waumini wanaotoka kuacha pesa zinazowatajirisha hawa wachungaji. Wao wanateseka na umaskini wao na wachungaji wanaendelea kutajirika kwa ukosefu wa maarifa wa waumini.
Siuoni ujasiri wa Rais Kagame akiwa nao Rais SSH au yoyote yule wa Tanzania. Mungu tunamhitaji siku zote kwa ustawi wa Tanzania lakini tumefungulia sana mlango masuala ya dini kiasi cha matapeli kuendelea kuwaumiza waumini wanyonge waliokata tamaa za kimaisha.
Mungu Ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.
wajinga ndio waliwao kama ww hujaweza kwenda kwann wao waende kwani hawana akili..... kwahyo mnasubiri raisi aseme hataki makanisa ili mumseme na uislamu wake.... ukiacha hisia ukaangalia uhalisia utajifunza haya mambo mtu halazimishwi ni tamaa zake za mijujiza na mafanikio bila kazi acha waliwe vichwaUlisha yasikia ya "Shakahola" hapo nchi jirani ya Kenya?
Hata kama mtu huyo binafsi anahatarisha maisha yake na wengine? Hiyo ni serikali ya wapi hiyo?
Wajinga ndiyo mtajiDuh!
Kwa kweli leo nimecheka, tena sana! Na hapa kwenye hayo maneno niliyo nyanyua ndipo mbavu zilikaribia kuvunjika kabisa!
Kinacho changia nicheke hivi, ni kukusoma wewe kwenye mada kama hii uliyo ileta leo hapa; tofauti, tena mbali kabisa na zile tulizo zoea kukutana.
Niwe mkweli wa nafsi yangu, ninakubaliana kabisa na maudhui ya mada yako hapa. Lakini, kama ujuavyo, na katika mwelekeo ule ule unao elezwa na mistari niliyo nukuu hapo juu; makanisa haya ni biashara, tena biashara zakulaza akili za watu, na hasa waliochanganyikiwa na hali ngumu za maisha. Husemwa, "Wajinga ndio waliwao",...; na kama ujuavyo kwenye nchi yetu hii, muumini mkubwa wa "ujinga" wa waTanzania ni CCM na serikali yake, ambayo kwa bahati nzuri au mbaya umeikutanisha na washirika wenzake katika kuwalaza akili waTanzania.
Sikuendelea kusoma hayo mengine huko chini, lakini nahisi mwelekeo wake ni huo huo nilio upata tokea huko juu hadi hapo nilipo ishia na kunukuu hayo maneno uliyo andika wewe.
Sijui hili taifa tutaishia wapi, iwapo kila mwenye nafasi anatafuta ku'take advantage' ya hawa maskini; siyo kwa mali tu, bali hadi kwenye fikra!
😂😂😂😂Hao wanaotibu magonjwa yote kwa maombi wanatakiwa kuthibitisha hilo kwa mamlaka za afya,wakishindwa wapigwe marufuku
Dini zikizidi ni umaskini mtupu unaosambazwa kwa kasi. Umaskini wetu wa vichwani unaendelea kusambaza umaskini mbaya zaidi kila kona ya TZ.Nani anakupa haki ya kuamua makanisa gani ya kweli na yapi ya uongo? Hilo dhehebu lako una uhakika gani ni la kweli?
Kama serikali ikitaka kufungia makanisa ya uongo litabaki kanisa Katoliki pekee. Je uko tayari kuuishi ukweli huo?
Nchi hii katiba imetoa uhuru wa kuabudu sio kazi ya serikali kuwaamulia watu wapi waabudu.
Watu kuibiwa kanisani kwa kudanganywa ni sawa na watu kutumia vipato vyao vyote kwa uasherati na ulevi, kila mmoja ana uhuru wa kutumia pesa yake jinsi anavyopenda.
Hao wahuni wa makanisa ya kiroho lao moja na wahuni wa huko serikalini.RC Chalamila anaenda kumpa saport yule jamaa kujaza nyomi inaelekea CCM inafarijika kuona jamii iliyowapa umasikini inamlilia Mungu kupitia wahuni wa makanisa ya kiroho badala ije iwalaumu wao.
Stupidity of africansKuna muumini mmoja wa Mwamposa alitoa ushuhuda eti baada ya kubandika picha ya Mwamposa kwenye mtungi wa ges hadi leo miezi 6 imepita gesi haijaisha, na watu wakapiga makofi niliwaonea huruma sana.
Uwepo wa Mungu haukwepeki lakini uvivu wetu hauwezi kuhalalishwa kwa kumtumia Mungu.Kwa hiyo unataka ushauri nini watu warudishwe Roma kwa viboko? Au unataka serikali ifute makanisa zibaki bar
Mtoa mada najaribu kukuelewa ila naomba nikuulize.Katika haya makanisa ya kilokole unaweza ukacheka sana yale yanayoendelea haswa ifikapo Jumapili. Wale wapambe wa mchungaji wakiliona gari la bei mbaya haraka sana wanawasogeza waumini ili lipite na aliyepo ashuke na aende kukaa katika sehemu maalum.
Kwa mchungaji na wasaidizi wake kuliona gari zuri la kisasa ni ujio wa neema fulani. Bahati mbaya kwa waumini wamekuwa sawa na waliofanywa misukule, hawaelewi kwamba wametekwa akili zao.
Serikali haiumizwi na mateso wanayoyapata wananchi wanaofanyiwa vitendo hivi vya kishenzi kwa kudanganywa wakatoa hicho hicho kidogo wanachokipata kwa taabu?.
Ifike mahali tujipunguzie hii mizigo ya dhambi kwa kutumia jina la Mungu. Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Serikali haiyaoni haya madudu ya wachungaji mpaka wanafikia kujiita kiboko ya wachawi?. Ubinadamu umepotelea wapi yarabi!.
Serikali yetu haina ule uthubutu kama alioufanya Rais Paul Kagame kule Rwanda kiasi cha kufungia makanisa ya kitapeli mengi tu. Siuoni huo uthubutu ikiwa Rais SSH anamtuma mkuu wa mkoa Chalamila kwenda kuchangia masuala ya kanisa.
Wanasiasa wanatembelea ule umaarufu wa wachungaji wakisahau kuwa wanaoumia ni wananchi wa kawaida wenye kupata pesa kwa jasho jingi. Hata kuamua kumfungia huyo kiboko ya wachqwi ni maamuzi ya kinafiki tu, ya kisiasa yasiyotoka mioyoni mwao.
Serikali inafanya lolote lile ili iweze kuendelea kuwa na uhalali wa kuchaguliwa katika miaka ya uchaguzi, baada ya hapo ni mwendo wa kufungia vioo haya mateso ya hao wanaoumizwa na wachungaji matapeli wanaoibuka kama uyoga.
ikifikia Jumapili pale Kawe hapafai kwa foleni na wingi wa waumini wanaotoka kuacha pesa zinazowatajirisha hawa wachungaji. Wao wanateseka na umaskini wao na wachungaji wanaendelea kutajirika kwa ukosefu wa maarifa wa waumini.
Siuoni ujasiri wa Rais Kagame akiwa nao Rais SSH au yoyote yule wa Tanzania. Mungu tunamhitaji siku zote kwa ustawi wa Tanzania lakini tumefungulia sana mlango masuala ya dini kiasi cha matapeli kuendelea kuwaumiza waumini wanyonge waliokata tamaa za kimaisha.
Mungu Ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.
HUYU ALIKUWA ANAPIGWA PINI KALI SANA POO YAKE ILIKUWA NI KUUNGANA NA WATESI..hujaona Raisi anatuma Wasaidizi wake kuchangia ktk Makanisa yao hao wahuni?
..Na inashangaa nini ikiwa Mch.Gwajima ni mbunge wa Ccm?
Kagame aliyafunga makanisa 400 baada ya kuwataka wanaoyaendesha kuonyesha vyeti vya theolojia. Wakijipunguza wenyewe na Rwanda ina makanisa machache yamebakia.Mtoa mada najaribu kukuelewa ila naomba nikuulize.
Makanisa ya kilokole ni yapi?
Unasema waumini wao wametekwa kiakili, una ushahidi gani kwamba wametekwa kiakili?
Je yakifanyika kama ya Rwanda una uhakika hakuna atakayetekwa kiakili?
Je unadhani katiba yetu inatoa uhuru wa kuabudu uliopitiliza?
Hao wanaoenda Kawe hawana haki ya kutoa sadaka kama sehemu ya ibada zao hata kama ni maskini ?
Nakubaliana na serikali kuyafungia makanisa yote yanaoenda kinyume na sheria na katiba zetu, mfano yule anayejiita kiboko ya wachawi naona serikali imechelewa sana kumfungia maana alikuwa analeta uchonganishi wa waziwazi.
Tuisadie serikali kubainisha ukiukwaji wa katiba/sheria zetu unaofanywa na makanisa, kuilaumu kwa ujumla tu utakuwa unaionea.