Serikali iache mzaha; kuruhusu watoto waliopewa mimba kurudi shule ni anguko la taifa la kesho

Serikali iache mzaha; kuruhusu watoto waliopewa mimba kurudi shule ni anguko la taifa la kesho

Elimu pasipo maadili haina maana yoyote ile ndani ya jamii.

Sheria hiyo ilipaswa izingatie mazingira ya nchi ZETU.
Huwezi leta sheria za nchi zilizoendelea kwenye nchi masikini, labda zile sheria kuu za ulimwengu.

Magufuli licha ya kuwa nilikuwa natofautiana naye kwenye masuala ya demokrasia na utawala Bora lakini katika hili nilimuunga Mkono.

Hiyo ni adhabu na haipaswi kuwa kwa mtindo WA huruma.

Kama binti au kijana anataka kusoma achague moja kusoma au Kulea.
Kuchekeana chekeana na huruma zisizo na maana yoyote hazipaswi kupewa Nafasi.

Yaani uharibu taifa kisa misaada ya muda mfupi?
Lengo la adhabu ni kuonya ama kufundisha!

Katika kutoa funzo adhabu hio lazma iwe na hali flani ya kuumiza kinamna flani yani lazma imgharimu mtu ambaye ametenda hilo kosa na kumfanya ajutie uzembe wake.

Kama tutaruhusu watoto wakike warudi shule na vijana waliowatia mimba waachiwe waendelee kupeta mtaani! Sheria ifumuliwe sio mlete upendeleo wa kishamba.
 
Elimu pasipo maadili haina maana yoyote ile ndani ya jamii.

Sheria hiyo ilipaswa izingatie mazingira ya nchi ZETU.
Huwezi leta sheria za nchi zilizoendelea kwenye nchi masikini, labda zile sheria kuu za ulimwengu.

Magufuli licha ya kuwa nilikuwa natofautiana naye kwenye masuala ya demokrasia na utawala Bora lakini katika hili nilimuunga Mkono.

Hiyo ni adhabu na haipaswi kuwa kwa mtindo WA huruma.

Kama binti au kijana anataka kusoma achague moja kusoma au Kulea.
Kuchekeana chekeana na huruma zisizo na maana yoyote hazipaswi kupewa Nafasi.

Yaani uharibu taifa kisa misaada ya muda mfupi?

Binti chini ya miaka 18 unaanzaje kumhukumu na kumuadhibu wakati tunakubaliana sio makosa yake?
 
Nimeshangaa sana unapokomalia kuwa kila anayepata mimba n mkubwa na anajielewa ungekua kwenye jamii zetu ukaona vibinti vidogo hata balehe bado vinafanya ngono bila kujua madhara yake ungekomaa na Serikali waendelee kutoa elimu ya jinsia kwanzia primary school kunusuru kizazi na sio kufukuza wenye mimba shule. Zipo cases nyingi za waliorudi shule na wakafaulu vzr zaidi tuwasaidie watt wetu


Hapa Hatuzungumzii kufaulu au kufeli, kwani Nani kasema Mwanafunzi aliyepewa mimba hawezi kufaulu??

Hapa tunazungumzia habari za kosa na adhabu yake.

Hakuna binti anaweza akawa mdogo lakini akwa mkubwa kibaolojia, binti Yeyote mwenye uwezo wa kubeba mimba ni Mkubwa kiasili. Hayo ya kusema ni mdogo ni kulingana na mtazamo au maoni ya watu lakini kiasili ni Mkubwa.

Mtoto hawezi beba mimba Mkuu. Labda useme akili ndio yakitoto,
Lakini mbona Hilo hata wenye umri mkubwa wapo wenye akili hizo za kitoto?
 
Lengo la adhabu ni kuonya ama kufundisha!

Katika kutoa funzo adhabu hio lazma iwe na hali flani ya kuumiza kinamna flani yani lazma imgharimu mtu ambaye ametenda hilo kosa na kumfanya ajutie uzembe wake.

Kama tutaruhusu watoto wakike warudi shule na vijana waliowatia mimba waachiwe waendelee kupeta mtaani! Sheria ifumuliwe sio mlete upendeleo wa kishamba.


Ndio hapo sasa.

Hawawezi onea Vijana wakiume Kwa visingizio visivyo na maana.

Hata Vijana wakiambiwa wajieleze hawatakosa chakusema.

Ni mwanaume gani asiyejua kimbembe cha hamu ikipanda mwilini?

Kama ni adhabu watoe Kwa wote.
Wakishindwa wafute Kwa wote
 
Mkeo amevamiwa na majambazi nyumbani wakambaka na kumpa maambukizi, basi na wewe ni sawa kuja kumpa talaka kwa uzembe wake....


Ndio maana nimeandika kuna Exceptional chini Kabisa na nimeshasema kuwa Bahati nzuri no kuwa wanaopitia hayo ni wachache.

Kitoto unakikanya kila siku kinang'ang'ania maghetto ya wanaume alafu useme kimebakwa. Embu tuweni Sirius bhana.
 
Binti chini ya miaka 18 unaanzaje kumhukumu na kumuadhibu wakati tunakubaliana sio makosa yake?


Kuanzia miaka 15 mbona mtu anajitambua kabisa.

Labda wenye matatizo ya Akili ambao ni exceptional.

Wewe ulivyokuwa na miaka 15 ulikuwa haujitambui?

Anyway kujitambua kunatokana na mazingira mtu amekulia.

Kuna wengine mpaka miaka 30 hawajitambui kutokana na kutofunzwa vyema tangu wakiwa watoto.

Waulize waalimu wao ndio wanajua mtoto wa miaka 15 anafaa kuhukumiwa au laa.
 
Chief, ukumbuke huyu binti bila shaka atakuwa na umri chini ya miaka 18...
Sheria na wote tunaamini binti au kijana chini ya 18yrs wanakuwa hawana akili timamu kimaamuzi ndio maana tunasema chini ya 18yrs atakuwa amebakwa..

sasa kama wote tunakubaliana binti chini ya miaka 18 kisheria kufanya mapenzi ni makosa na anakuwa amebakwa tunaanzaje kumhukumu huyu binti na kumnyima haki yake?...
Naomba kufahamu kiongozi! Kijana miaka 16 na Binti miaka 16 akapata mimba wote wakiwa shule. Kijana huwa anchukuliwa hatua gani?
 
Ndio maana nimeandika kuna Exceptional chini Kabisa na nimeshasema kuwa Bahati nzuri no kuwa wanaopitia hayo ni wachache.

Kitoto unakikanya kila siku kinang'ang'ania maghetto ya wanaume alafu useme kimebakwa. Embu tuweni Sirius bhana.

Katika hali hiyo sasa, tunapaswa kukukamata wewe mzazi na kukufunga maana umeshindwa kumlea mwanao kiasi cha kukushinda akiwa chini ya 18yrs....

akisha kuwa chini ya 18yrs tafsiri ya kisheria ni mtoto ambaye anahitaji uangalizi na ulinzi wa jamii...
 
SERIKALI IACHE MZAHA; KURUHUSU WATOTO WALIOPEWA MIMBA KURUDI SHULENI KUSOMA NI ANGUKO LA TAIFA LA KESHO.

Anaandika Robert Heriel.

Naiomba serikali, viongozi wakubwa msikie Jambo hili, tena msifanye mzaha. Huruma huruma za ajabu ajabu katika baadhi ya ishu ni hatari Kwa ustawi wa taifa.
Nafahamu wapo watu wenye roho laini, wenye huruma, lakini siku zote huruma ikizidi huleta Matatizo.

Kuruhusu watoto wakike waliopata mimba kuendelea na shule kimantiki ni Kuruhusu watoto wakike wapewe MIMBA. Yaani mi Kuruhusu mimba mashuleni Kwa lugha ya kawaida.

Nyakati za Magufuli, moja ya mambo niliungana naye ni pamoja na hili. Hatuwezi kuwa wapole na wenye huruma katika masuala haya ya Msingi.

Nani asiyejua nchi yetu ni masikini, Nani asiyejua familia zetu nyingi ni familia zilizozidiwa na ufukara. Kuzaa kunahitaji maandalizi, kuzaa kunahitaji mipango, kunahitaji wazazi wawili wenye akili iliyokomaa. Kuruhusu watoto waliopewa ujauzito waendelee na shule ni kuongeza matatizo ya kimaadili na kiuchumi.

Niliwahi kuandika kuwa serikali Kwa sehemu kubwa inachangia kumomonyoko Kwa maadili ya jamii.

Unamsomesha aliyepata mimba shuleni na wakati huo huo unamfunga miaka 30 aliyembebesha mimba huyo binti, hiyo ni Akili kweli, embu tutafakari. Kama tumeamua kuwapa watu adhabu acheni wapewe adhabu.

Huyu apoteze haki ya kusoma Kwa kukubali kudanganywa akapewa mimba, huyu mwingine afungwe Kwa kushindwa kujizuia hisia zake na kumpa mimba mtoto wa kike.

Mtoto yeyote aliyebalehe mwenye uwezo wa kubeba mimba ni Mkubwa, na anavigezo vyote vya kuitwa mama ndio maana akabeba mimba.

Kuhusu suala la akili ni ishu nyingine kabisa Kwa maana wapo watu wazima kiumri lakini hawana akili za kikubwa, na wapo watu wenye umri Kati ya 15-18 ambao wanaakili za kikubwa. Hivyo logically hatuwezi kusema Umri ni Akili au akili ni Umri ikiwa wapo wenye umri mkubwa wanazidiwa akili na wenye umri mdogo.

Kuruhusu wanafunzi waliopewa mimba wasome ni kuidhinisha zinaa ndani ya nchi. Ni kuitangazia dunia kuwa nchi yetu inaruhusu zinaa. Hapatakuwa na hofu yoyote Kwa mabinti kushiriki tendo la ndoa.

Serikali na watu wote tutambue kuwa moja ya mambo yanayowatisha mabinti wa kike wasifanye zinaa ni Kama ifuatavyo;

1. Kasumba ya kuumia wakati WA kutolewa Bikra.( Hii ni Kwa ambao hawajawahi kufanya kabisa).

2. Aibu ya maumbile. Wasichana kuogopa kuonekana nyuchi na maungo Yao ya Siri kwani wanahofia Kuambiwa wanamaumbile mabaya.

3. Kupata MIMBA.
Mabinti wengi huogopa zaidi mimba kuliko magonjwa ya zinaa.

4. Kupata magonjwa ya zinaa Kama UKIMWI.
Japo hii sio Sana lakini ni moja ya sababu kuu nne zinazowafanya mabinti waogope kuingia kwenye tendo la ndoa.

5. Maadili ya Dini na wazazi.
Wapo watoto waliolelewa wakaleleka. Hawa huogopa kujiingiza kwenye tendo la ndoa mapema Kwa sababu ya Mafunzo waliyopewa. Hawa ni wachache.

Sababu namba tatu ambayo ni kupata mimba ni sababu nyeti mno ambayo mabinti huogopa kufanya ngono hovyo hovyo. Hii ni kutokana na kuwa mimba huwafanya wafukuzwe shule, lakini la pili mimba ni aibu kwao wenyewe na wazazi wao. Mimba huwaumbua kwa Yale waliyofanyia gizani sasa hutokea hadharani Kwa tumbo kuvimba.

Kuruhusu mimba shuleni ni Kuruhusu watoto wasio na Baba.

Kuruhusu Mimba shuleni ni Kuruhusu watoto wa mitaani kwani familia nyingi za kibongo ni Masikini.

Kuruhusu Mimba shuleni ni Kuruhusu ongezeko la single Mama hapo Baadaye ambalo kimsingi linaathari hata hivi sasa.

Kuruhusu Mimba shuleni ni Kuruhusu taifa kuelemewa na Kundi tegemezi ambalo halilisaidii TAIFA.

Kuruhusu Mimba shuleni kutaathiri maadili ya watoto kwenye malezi kwani wamama wazazi watakuwa shuleni wakisoma wakati Mtoto akiachwa Kwa mfanyakazi wa ndani, sasa jiulize ni familia ngapi zinauwezo WA kuajiri mfanyakazi wa ndani.

Kuruhusu Mimba shuleni ni kuhujumu nguvu kazi ya nchi; kwani Mwanaume atafungwa, mama atarudi shule, Bibi naye Kwa vile bado ni kijana afanyaye kazi labda ni kilimo au ujasiriamali au kazi za ualimu, uhasibu n.k watabidi waache kazi zao wadili na mtoto au waajirifanyakazi WA ndani ili wamlipe Mshahara Mdogo usiozidi 50,000 ambao pia ni uhujumu uchumi.

Serikali iache zile sheria za shule Kama zilivyo.
Atakayempa mimba mwanafunzi apate miaka yake 30 jela, na mwanafunzi afukuzwe shule. Kumbuka nimesema hakuna mtoto anayebeba Mimba.
Mtu au kiumbe chochote chenye uwezo wa kubeba mimba ujue kimekomaa, imefikisha umri wa kuitwa Mkubwa.
Kwenye nature au asili, kubeba mimba au kutungisha mimba ni moja ya ishara ya ukubwa.

Serikali na wazazi tusiendekeze mambo haya. Nafahamu Sisi sote tuwazazi, wanaopata mimba ni binti zetu, dada zetu, watoto wetu n.k lakini lazima tuwe wakali katika hili.

Mtoto aambiwe angali mdogo, ukipata mimba shule unafukuzwa, nyumbani unafukuzwa, yaani mtoto akijua Jambo hilo hawezi pata mimba ninauhakika. Hofu ndiyo ilifanya kizazi kilichopita kubaki na maadili.

Familia zinazoendekeza watoto ndizo hupata madhara ya watoto kupatwa na mimba wakiwa shuleni, kuwa mashoga, kuvuta bango na kutumia madawa ya kulevya.

Nafahamu kuna Exceptional katika mambo mengi, hivyo hata katika Jambo hili wapo wanaopatwa na madhara Kwa bahati mbaya tuu Kama kubakwa Kwa lazima, kulazimishwa kunywa madawa ya kulevya, kulawitiwa n.k. lakini kundi hili wapo wachache mno,
Wengi Hufanya Kwa hiyari Yao wenyewe.

Serikali nafahamu inaweza ikawa inahitaji pesa Fulani kutoka nchi za nje, ikiwa ni hivyo nasi itumie Siasa katika Jambo hili. Kwenye media iwe mataifa wanajua kuwa tunaruhusu wanafunzi waliopewa mimba kuendelea kusoma lakini kiuhalisia hakuna kitu Kama hicho.


Kalagabaho!

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa OSTERBAY, DAR ES SALAAM
Taifa ililishaanguka kabla ya kufika kesho. Ngoja watoto wakimbizane na hatima ya maisha yao.
Wazazi wanapaswa kuwalea watoto katika maadili mema, wanapaswa kujua madhara ya kupata mimba na sio kuwahukumu kwa kuwakosesha fursa ya kuendelea na masomo.
 
Malawi now wanafikiria uwekezaji wa BANGE.......kila mmoja apambanie ya kwake......nashauri wapunguze ile 30yrs.....wahasiwe kabisa....then apewe mtoto amtunze
 
Katika hali hiyo sasa, tunapaswa kukukamata wewe mzazi na kukufunga maana umeshindwa kumlea mwanao kiasi cha kukushinda akiwa chini ya 18yrs....

akisha kuwa chini ya 18yrs tafsiri ya kisheria ni mtoto ambaye anahitaji uangalizi na ulinzi wa jamii...
hii pia ni njia nzuri....wazazi wawajibishe...wote wawili.......kuna adabu itajirekebisha kdg
 
Tunatumia muda mwingi kupromote na kutetea mambo ya hovyo kwenye jamii.

Yani asiyefuata maadili anaenda kuchanganywa na wanaofuata maadili baada ya miaka 10 wote unakuta wameoza.

Wamemwandaa nani wa kuacha shughuli zake alee hao watoto watakao zaliwa na kuachwa na wazazi wao? Maana baba ataenda jela miaka 30 na mama atarudi shule.

Muda si mrefu na haki ya vilainishi itaruhusiwa
We naye una mindset ya 20th century!! Kwamba eti aliyezaa hana maadili ila wasiozaa wana maadili? Kwani issue ni ngono au mimba? Kwamba wanao sex na condom hao wana maadili si ndio?

Anyway unaposema wasichanganywe, kwani watoto washule hawaishi mtaani? Hawaoni mabinti wengine wakizalia nyumbani kiasi kwamba waje kuharibiwa shuleni sio mtaani??

Ww ungeshauri wanawake wajengewe mabweni ili wawe wanasoma huko huko wanarudi likizo tu pengine ita control muingiliano na wahuni wa mtaani ila kudai kwamba kuwachanganya ndio sababu ya maadili kushuka ni mentality ya ajabu sana.
 
Ndio maana ya Adhabu,
Lengo la adhabu ni kukuonya na kumfundisha mtu.

Huyo binti na kijana kila mmoja atumikie adhabu yake ili iwe fundisho Kwa wengine.

Elimu pasipo na maadili haina maana yoyote.
Lete stats za kuonyesha hiyo adhabu imesaidia maadili kusimama
 
Hata Maghufuli hakuwazuia kupata elimu alikuwa anasema akipata mimba atolewe huko elimu akaendelee nayo kwenye kundi la wakubwa, maana elimu siyo lazima itolewe na mwalimu hata yeye anaweza akawa anawaelimisha wenzie jinsi ya kupata mtoto mwisho wa siku kila mhitimu anarudi nyumbani akiwa na ufaulu wa elimu na malezi ambayo siyo sahihi kabisa kwa jamii zetu, nami naunga la kuwakazia watambue ni kosa kuzaa ukiwa unasoma kwa kumtengenisha na aliokuwa nao.
 
Mabeberu wamesema sasa kama kweli mnaweza kujisimamia mambo yenu ya ndani ebu jaribuni na hilo tuone sasa kama huwezi kujisimamia kaaa utulie ili wakubwa waamue juu ya hatma yako
 
hili taifa lishaanguka siku nyingi mkuu
yaani tunaenda kwa matamko ya watu, akiamka anaamua tu anavyojisikia
Kwani Tz, ina kitu gani cha kipekee, kwani mbona nchi nyingine za kiafrika wameruhusu, na kielimu, kiuchumi wako juu zaidi yetu!!yaani hii nchi huwa tunajifanya kama ina upekee wa aina yake vile!??
 
SERIKALI IACHE MZAHA; KURUHUSU WATOTO WALIOPEWA MIMBA KURUDI SHULENI KUSOMA NI ANGUKO LA TAIFA LA KESHO.

Anaandika Robert Heriel.

Naiomba serikali, viongozi wakubwa msikie Jambo hili, tena msifanye mzaha. Huruma huruma za ajabu ajabu katika baadhi ya ishu ni hatari Kwa ustawi wa taifa.
Nafahamu wapo watu wenye roho laini, wenye huruma, lakini siku zote huruma ikizidi huleta Matatizo.

Kuruhusu watoto wakike waliopata mimba kuendelea na shule kimantiki ni Kuruhusu watoto wakike wapewe MIMBA. Yaani mi Kuruhusu mimba mashuleni Kwa lugha ya kawaida.

Nyakati za Magufuli, moja ya mambo niliungana naye ni pamoja na hili. Hatuwezi kuwa wapole na wenye huruma katika masuala haya ya Msingi.

Nani asiyejua nchi yetu ni masikini, Nani asiyejua familia zetu nyingi ni familia zilizozidiwa na ufukara. Kuzaa kunahitaji maandalizi, kuzaa kunahitaji mipango, kunahitaji wazazi wawili wenye akili iliyokomaa. Kuruhusu watoto waliopewa ujauzito waendelee na shule ni kuongeza matatizo ya kimaadili na kiuchumi.

Niliwahi kuandika kuwa serikali Kwa sehemu kubwa inachangia kumomonyoko Kwa maadili ya jamii.

Unamsomesha aliyepata mimba shuleni na wakati huo huo unamfunga miaka 30 aliyembebesha mimba huyo binti, hiyo ni Akili kweli, embu tutafakari. Kama tumeamua kuwapa watu adhabu acheni wapewe adhabu.

Huyu apoteze haki ya kusoma Kwa kukubali kudanganywa akapewa mimba, huyu mwingine afungwe Kwa kushindwa kujizuia hisia zake na kumpa mimba mtoto wa kike.

Mtoto yeyote aliyebalehe mwenye uwezo wa kubeba mimba ni Mkubwa, na anavigezo vyote vya kuitwa mama ndio maana akabeba mimba.

Kuhusu suala la akili ni ishu nyingine kabisa Kwa maana wapo watu wazima kiumri lakini hawana akili za kikubwa, na wapo watu wenye umri Kati ya 15-18 ambao wanaakili za kikubwa. Hivyo logically hatuwezi kusema Umri ni Akili au akili ni Umri ikiwa wapo wenye umri mkubwa wanazidiwa akili na wenye umri mdogo.

Kuruhusu wanafunzi waliopewa mimba wasome ni kuidhinisha zinaa ndani ya nchi. Ni kuitangazia dunia kuwa nchi yetu inaruhusu zinaa. Hapatakuwa na hofu yoyote Kwa mabinti kushiriki tendo la ndoa.

Serikali na watu wote tutambue kuwa moja ya mambo yanayowatisha mabinti wa kike wasifanye zinaa ni Kama ifuatavyo;

1. Kasumba ya kuumia wakati WA kutolewa Bikra.( Hii ni Kwa ambao hawajawahi kufanya kabisa).

2. Aibu ya maumbile. Wasichana kuogopa kuonekana nyuchi na maungo Yao ya Siri kwani wanahofia Kuambiwa wanamaumbile mabaya.

3. Kupata MIMBA.
Mabinti wengi huogopa zaidi mimba kuliko magonjwa ya zinaa.

4. Kupata magonjwa ya zinaa Kama UKIMWI.
Japo hii sio Sana lakini ni moja ya sababu kuu nne zinazowafanya mabinti waogope kuingia kwenye tendo la ndoa.

5. Maadili ya Dini na wazazi.
Wapo watoto waliolelewa wakaleleka. Hawa huogopa kujiingiza kwenye tendo la ndoa mapema Kwa sababu ya Mafunzo waliyopewa. Hawa ni wachache.

Sababu namba tatu ambayo ni kupata mimba ni sababu nyeti mno ambayo mabinti huogopa kufanya ngono hovyo hovyo. Hii ni kutokana na kuwa mimba huwafanya wafukuzwe shule, lakini la pili mimba ni aibu kwao wenyewe na wazazi wao. Mimba huwaumbua kwa Yale waliyofanyia gizani sasa hutokea hadharani Kwa tumbo kuvimba.

Kuruhusu mimba shuleni ni Kuruhusu watoto wasio na Baba.

Kuruhusu Mimba shuleni ni Kuruhusu watoto wa mitaani kwani familia nyingi za kibongo ni Masikini.

Kuruhusu Mimba shuleni ni Kuruhusu ongezeko la single Mama hapo Baadaye ambalo kimsingi linaathari hata hivi sasa.

Kuruhusu Mimba shuleni ni Kuruhusu taifa kuelemewa na Kundi tegemezi ambalo halilisaidii TAIFA.

Kuruhusu Mimba shuleni kutaathiri maadili ya watoto kwenye malezi kwani wamama wazazi watakuwa shuleni wakisoma wakati Mtoto akiachwa Kwa mfanyakazi wa ndani, sasa jiulize ni familia ngapi zinauwezo WA kuajiri mfanyakazi wa ndani.

Kuruhusu Mimba shuleni ni kuhujumu nguvu kazi ya nchi; kwani Mwanaume atafungwa, mama atarudi shule, Bibi naye Kwa vile bado ni kijana afanyaye kazi labda ni kilimo au ujasiriamali au kazi za ualimu, uhasibu n.k watabidi waache kazi zao wadili na mtoto au waajirifanyakazi WA ndani ili wamlipe Mshahara Mdogo usiozidi 50,000 ambao pia ni uhujumu uchumi.

Serikali iache zile sheria za shule Kama zilivyo.
Atakayempa mimba mwanafunzi apate miaka yake 30 jela, na mwanafunzi afukuzwe shule. Kumbuka nimesema hakuna mtoto anayebeba Mimba.
Mtu au kiumbe chochote chenye uwezo wa kubeba mimba ujue kimekomaa, imefikisha umri wa kuitwa Mkubwa.
Kwenye nature au asili, kubeba mimba au kutungisha mimba ni moja ya ishara ya ukubwa.

Serikali na wazazi tusiendekeze mambo haya. Nafahamu Sisi sote tuwazazi, wanaopata mimba ni binti zetu, dada zetu, watoto wetu n.k lakini lazima tuwe wakali katika hili.

Mtoto aambiwe angali mdogo, ukipata mimba shule unafukuzwa, nyumbani unafukuzwa, yaani mtoto akijua Jambo hilo hawezi pata mimba ninauhakika. Hofu ndiyo ilifanya kizazi kilichopita kubaki na maadili.

Familia zinazoendekeza watoto ndizo hupata madhara ya watoto kupatwa na mimba wakiwa shuleni, kuwa mashoga, kuvuta bango na kutumia madawa ya kulevya.

Nafahamu kuna Exceptional katika mambo mengi, hivyo hata katika Jambo hili wapo wanaopatwa na madhara Kwa bahati mbaya tuu Kama kubakwa Kwa lazima, kulazimishwa kunywa madawa ya kulevya, kulawitiwa n.k. lakini kundi hili wapo wachache mno,
Wengi Hufanya Kwa hiyari Yao wenyewe.

Serikali nafahamu inaweza ikawa inahitaji pesa Fulani kutoka nchi za nje, ikiwa ni hivyo nasi itumie Siasa katika Jambo hili. Kwenye media iwe mataifa wanajua kuwa tunaruhusu wanafunzi waliopewa mimba kuendelea kusoma lakini kiuhalisia hakuna kitu Kama hicho.


Kalagabaho!

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa OSTERBAY, DAR ES SALAAM
Nashauri watoto wako wakipata mimba ndio wasirudi shule, ila watoto wa sisi wenzio wakipata mimba bado tunawapenda watimize ndoto zao, waendelee kuupewa nafasi nyingine ya kusoma. sioni shida yeyote mtoto aliyepata mimba kuendelea na shule, shida hiyo ipo kwenye vichwa vya watu wa aina yako.
 
Back
Top Bottom