Serikali ikiondoa unafiki na chuki bado Kagera inaweza kuchomoza, Chalamila unatakiwa kujua haya

Serikali ikiondoa unafiki na chuki bado Kagera inaweza kuchomoza, Chalamila unatakiwa kujua haya

Tatizo lenu ni ego ! Yaani kila kitu unalaumu serikali.

Kilimanjaro imehujumiwa sana kuliko Kagera, iko mpakani kama Kagera, wana Kahawa kama Kagera tena Kagera wana Ardhi nzuri na kubwa zaidi, wasomi kama Kagera. Sasa tofauti iko wapi ? Ni utamaduni pamoja na kwamba kuna wasomi wengi Kilimanjaro wananchi wa Kilimanjaro wana wathamini zaidi wafanyabiashara kuliko wasomi. Pili Kilimanjaro kuna utamaduni wa harambee za shule, makanisa, na hata barabara za mitaani. Tatu watu wa Kilimanjaro wana wekeza nyumbani kwao na ku lobby ili wapate pesa za maendeleo. Nne Kilimanjaro wamewawezesha wanawake kwenye maendeleo kuanzia biashara hadi kilimo.

Hakuna hujuma mpaka makatibu wa CCM walitoka huko[emoji848] badala ya kulalamika jiangalieni wenyewe
Taasisi zote za kiserikali ambazo zipo mkoani Kilimanjaro zililetwa na wananchi wa mkoa wa Kilimanjaro?
 
Tatizo lenu ni ego ! Yaani kila kitu unalaumu serikali.

Kilimanjaro imehujumiwa sana kuliko Kagera, iko mpakani kama Kagera, wana Kahawa kama Kagera tena Kagera wana Ardhi nzuri na kubwa zaidi, wasomi kama Kagera. Sasa tofauti iko wapi ? Ni utamaduni pamoja na kwamba kuna wasomi wengi Kilimanjaro wananchi wa Kilimanjaro wana wathamini zaidi wafanyabiashara kuliko wasomi. Pili Kilimanjaro kuna utamaduni wa harambee za shule, makanisa, na hata barabara za mitaani. Tatu watu wa Kilimanjaro wana wekeza nyumbani kwao na ku lobby ili wapate pesa za maendeleo. Nne Kilimanjaro wamewawezesha wanawake kwenye maendeleo kuanzia biashara hadi kilimo.

Hakuna hujuma mpaka makatibu wa CCM walitoka huko🤔 badala ya kulalamika jiangalieni wenyewe
Vita ya Kagera ilitokea Kilimsnjaro?unajua ushawishi wa Hawa watu,Cleopa Msuya,Sumaye,na gavana wa kwanza wa BOT?
Unamjua Sir George Kahama,mapinduzi aliyotaka kufanya Kagera,Nyerere na ccm yake wakaogopa wakayazima kabisa!!
Umaskini wa Kagera,unaletwa na Siasa mbovu za ccm kuingilia soko na uuzaji wa zao la kahawa!
Umaskini ulioletwa Kagera,ndio aliofanya Shetani JPM kule kusini kwenye zao la korosho
 
Vita ya Kagera ilitokea Kilimsnjaro?unajua ushawishi wa Hawa watu,Cleopa Msuya,Sumaye,na gavana wa kwanza wa BOT?
Unamjua Sir George Kahama,mapinduzi aliyotaka kufanya Kagera,Nyerere na ccm yake wakaogopa wakayazima kabisa!!
Umaskini wa Kagera,unaletwa na Siasa mbovu za ccm kuingilia soko na uuzaji wa zao la kahawa!
Umaskini ulioletwa Kagera,ndio aliofanya Shetani JPM kule kusini kwenye zao la korosho

Kila siku historia lakini mnashika mkia kimaendeleo. Muache tabia ya ulalamishi na kufanya maendeleo
 
Changamoto zifuatazo, zinafanya Kagera tuwe nyuma. Tuache visingizio.

1. Ardhi ni ndogo
Kupata mkulima mwenye acre 2 au zaidi ni shida. Maeneo mengi yaliyotumika na jamii kwa kuchungia, kulima nafaka kama karanga n.k. yalichukuliwa na watu wachache wakapanda miti ya mbao, na kuacha watu wengi wakabaki wanahangaika.

2. Utamaduni wa kilimo cha migomba.
Migomba ni utamaduni wa Mhaya. Migomba hii haizalishi tena kwa wingi. Mashamba mengi ni yamechoja. Siyo rahisi kuwashauri watu kung'oa na kupanda mazao yenye tija. Hii ni crop rotation ambayo ingesaidia kurudisha rutuba na kutokomeza mnyauko.

3. Matumizi ya mbolea
Watu wengi wanaamini kwamba, mbolea inaharibu ardhi. Kwa hiyo, mapinduzi ya kilimo kwa kutumia ardhi iliyochoka ni ngumu.

4. Kaitu kaila
Acceptance ya aina mpya ya mazao ni ngumu. Tukubaliane, Mhaya anapenda sana migomba.

Pia, Takwimu zinaonyesha Kagera unaoongoza uzalishaji wa maharage kitaifa. Tatizo kubwa ni kwamba hawalengi soko. Maharage yanalimwa kwa wingi, lakini ni local na mchanganyiko. Yaani kila variety kidogo kidogo kiasi kwamba ukiyachambua na kukusanya, kiasi kinachopatikana hakikidhi soko individually.

5. Vijana na akina baba kutoshiriki kilimo
Mathalani, vijana wengi wilaya ya Missenyi hasa Kiziba na Kibumbilo, wamejikita sana kwenye kunywa karadarugo ambayo ni starehe ya vijana wengi. Hii inua nguvukazi.

Fursa za masoko

Masoko siyo shida. Kuna kipindi nimeshuhudia mihogo inatoka Lindi na Kigoma kupita Mutukula kwenda South Sudan. Vivyo hivyo, maharage na mahindi kutoka Rukwa na Mbeya. Halafu, wakati wa vita ya Rwanda, Kulikuwa na soko kubwa la WFP. Waliofaidi ni watu wa mbali.

Kuna mashule ya bweni pamoja na majeshini. Maharage yanayotumika huko ni ROZIKOKO. Soko siyo shida.

Kwa hiyo, swala la Stendi au Soko Kuu, havitaongeza chochote kwenye mfuko wa mwananchi. Vitabadili mandhari tu na kuongeza mapato ya serikali. Ni sawa na kuvaa suti huku una njaa.

Ili kubadili wananchi, inatakiwa nguvu kiasi, hasa ya kisiasa. RC ameanza vizuri japo tunataka zaidi action.

Nashauri kampeni kubwa iwe ni kubadili mindset za watu. Mfano, badala ya radio nyingi(Kasibante, Fadeco n.k) kushinda wanajadili mpira na miiziki, wajikite kutoa elimu ya kilimo na uchumi muda mwingi.

Ianzishwe TV station ya Kagera. Hii itakuwa na muda mwingi wa kutoa elimu kwa vitendo. Mpaka sasa kuna watu hawajui hata namna ya kupanda mahindi na maharage kitaalamu!. Watu hawajui kama kuna aina mpya za migomba na kahawa inayogawiwa bure.

Nashauri vikundi vya kilimo, vilivyo na uwezo wa kuunganisha wakulima pamoja, kama kule Kenyana Kilimilile, vipewe elimu na misaada ili kuleta chachu kwa wakulima wengine.

Nashauri pia, Maafisa ugani wapewe mafunzo ambayo ni 'tailor made' kwa ajili ya kupeleka elimu sahihi kwa wakulima.

Inawezekana. Hapo chini ni shamba la maharage katika kijiji cha Kenyana, 2021View attachment 2345873
Umejadili uhalisia kwa utaalamu kabisa. Hawa wengine wanarukaruka.
 
Back
Top Bottom