DOKEZO Serikali imchunguze Mwalimu huyu wa Shule ya Mandimu (Singida), matendo yake ni tishio kwa Wanafunzi

DOKEZO Serikali imchunguze Mwalimu huyu wa Shule ya Mandimu (Singida), matendo yake ni tishio kwa Wanafunzi

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Kila siku humu tunaambiwa wanaume wa vijijini ni mashababi ukilinganisha na Dar kumbe Huwa tunalishwa matongo pori.

Baadhi ya Walimu hasa wa kiume wakiwa huko vijijini Huwa wanajiona kama watawala kwenye hilo eneo ovyo kabisa hao watu.

Niliendaga Namanyere Rukwa kumsalimia kaka yangu ambaye ni mwalimu, siku tukaamua kutembea tembea kujionea mji Kila tunakopita mwalimu anajulikana vibaya mno na wanakijiji basi tukapita mtaa mmoja tunasikia kelele watoto kama miaka 12-16 wamefungiwa ndani wanachapwa kufika tu mwalimu hata hajauliza akaomba fimbo na yeye akaingia ndani kuanzia kuwatandika wale madogo wakati zinaondoka nikamwambia sasa wewe jamaa unawachapa watoto wa watu kiasi hiko ikitokea mtu akakata moto ghafra hujui kama ni kesi ?
Kiukweli walimu wanahitaji ushauri wa kisaikolojia maana inaonekana wana shida kubwa vichwani mwao hivyo wanaamini kumalizia stress zao kwa watoto kutapunguza changamoto walizonazo.

Wapo baadhi ya walimu wanaojitambua walishaapa hawatahangaika kuchapa mtoto wa mtu maana ikitokea bahati mbaya mtoto akadhurika basi kibarua chake kinaishia hapo hapo na jela inamchungulia.

Hivi walimu hawawezi kufanya kazi yao ya ualimu ambayo jukumu la kwanza ni kufundisha wakaachana na stress za kuadhibu watoto hovyo?

Sema walimu ni sikio la kufa kila siku wanapatwa na majanga kutokana na adhabu kwa watoto lakini hawajifunzi tu.
 
HIvi karibuni katika hekaheka za kutafuta mashamba kwa ajili ya msimu ujao wa kilimo nilifika katika kijiji kimoja kinaitwa Mandimu kilichopo Kata ya Mungaa, Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida.

Baada ya kukamilisha mambo yangu nikakaa kijiweni na Vijana wa eneo hilo kujua mbili tatu za eneo hilo.
Katika storI za hapa na pale akapita kijana mmoja ambaye alionekana kumfokea mzee mmoja, nikauliza kulikoni mbona 'dogo' anakosa adabu.

Nikaambiwa bwana huyo ni Mwalimu flani (akamtaja kwa jina la kwanza - Frank) huyo bwana hachezewi hakuna anayemgusa. Ilibid nidadisi zaidi kwani ana ishu gani. Ndipo wakanipa kisanga kizima.

Soma Pia: Mwalimu huyu wa Shule ya Msingi Mungu Maji aangaliwe, ananyanyasa Wanafunzi
Wakasema tangu Mwalimu Frank afike kijijini hapo kabla ya kuwa Mwalimu Mkuu amekuwa akitandika watoto wetu kinyama sana.

Watoto wanashika nondo juu kwenye dirisha ndio wanachapwa, kutandikwa huko sio kwenye makalio tu. Fimbo zinachapwa mgongoni miguuni hadi kichwani, sio fimbo tu anatumia hadi mateke na ngumi. Vipigo hivi ni wasichana na wavulana.

Nikaelezwa kuwa Watoto wengi wameacha shule kwa kuhofia kipigo cha kinyama cha mwalimu huyo pindi wanapokosea. Baadhi ya Wazazi hawana budi kukubali watoto kubaki nyumbani kwani wanahofia pia wanaweza kuumizwa vibaya kwasababu ilishawahi kutokea mtoto mmoja ambaye angemaliza la saba mwaka huu (2024) alichapwa na Mwalimu huyo baadaye akaanza kulalamika maumivu ya tumbo na wiki moja baadaye alipoteza maisha, so haikujulikana wazi kama chanzo ni mwalimu au alikuwa na changamoto zake nyingine.

Wakazidi kunieleza kuwa kuna Wazazi wawili walikwenda kumhoji kwa nini anawatesa watoto wao nasikia yalitokea mabishano na mama huyo wakashikana na mwalimu kupigana. Mama mwingine yeye aliwashwa kibao hakuthubutu tena kuuliza chochote.

Naiomba Serikali imchukulie hatua mwalimu huyu kwani anawakatili watoto sio kwa kipigo cha kinyama bali pia kukosa haki yao.ya msingi ya kupata.elimu. Pili anawanyanyasa wanakijiji hiko yy amekuwa mungumtu.

Tanzania yetu ni nchi ya Amani mtu mmoja anawezaj3 kunyanyasa watoto na wazazi wao kwnye ardhi yao?

NAOMBA SERIKALI IMSHUGHULIKIE MTU HUYU HARAKA.
Hapo kijijini pana uongozi, mwenyekiti na mtendaji, pale shule pana mkuu wa shule.. Ulienda kuwaona Ili upate picha ya upande wa pili. Hizo ni stori za kijiweni
 
Kama unaweza kupata access ya nmaba yake ya simu nicheki PM.

Tusiwe watu wa kushughulikia maafa baada ya kutokea bali tuwe watu wa kuzuia maafa.

Huyo anaelekea kuua muda sio mrefu halafu ndiyo nchi nzima ianze kupiga kelele wakati tayari mtoto kapoteza maisha hata huyo mwalimu akinyongwa haitarudisha uhai wa mtoto asiye na hatia.
Nakubaliana nawewe no iwekwe hapa Haina haja ya pm tumshughulikie tu ataelewa
 
Nakubaliana nawewe no iwekwe hapa Haina haja ya pm tumshughulikie tu ataelewa
Sahihi kabisa. Kufikia muda huu namba haijawekwa kitu ambacho nakisubiri kwa hamu ili tuanze kuchukua hatua za awali za kukomesha tabia hii mbaya ya baadhi ya walimu wasio na maadili ya kazi yao.

Tukikaa kimya kusubiri matukio ya vifo na ulemavu kwa watoto kutokana na vipigo vya kipumbavu kutoka kwa walimu vilaz,a haitasaidia kitu.

Prevention is better than cure. Huu usemi umebeba ujumbe muhimu sana.
 
Wewe kama premacy wa wanakijiji ulipaswa kuchukua hatua ya kumuona frenk umuulize kuhusu hizo tuhuma kisha upate uhakika.
Kuja hapa jukwaani kulalamika pasipo kumuona mhusika ni uoga na uongo.
Acha frank afundishe watoto wenu.
 
Sahihi kabisa. Kufikia muda huu namba haijawekwa kitu ambacho nakisubiri kwa hamu ili tuanze kuchukua hatua za awali za kukomesha tabia hii mbaya ya baadhi ya walimu wasio na maadili ya kazi yao.

Tukikaa kimya kusubiri matukio ya vifo na ulemavu kwa watoto kutokana na vipigo vya kipumbavu kutoka kwa walimu vilaz,a haitasaidia kitu.

Prevention is better than cure. Huu usemi umebeba ujumbe muhimu sana.
Kwenye kifo mbali sana mkuu. Ile hali ya mtoto kuacha masomo kwa sababu ya kipigo hii kifo tyr
Haiwezekani watoto waache shule kwa sababu ya kilaza mmoja asijua taaluma. NO Iwekwe hapa apigiwe simu
asbh mchana usiku,usiku wa manane na alfajiri.
 
Wewe kama premacy wa wanakijiji ulipaswa kuchukua hatua ya kumuona frenk umuulize kuhusu hizo tuhuma kisha upate uhakika.
Kuja hapa jukwaani kulalamika pasipo kumuona mhusika ni uoga na uongo.
Acha frank afundishe watoto wenu.
uko sawa mkuu ila hii ..........
Acha frank afundishe watoto wenu.
haikubariki kwa namna alivyo repot kama nikweli
 
Walimu wa aina hii wana mchango mkubwa sana katika Taifa hili, wawe wengi haswa shule za vijijini.
 
Kwenye kifo mbali sana mkuu. Ile hali ya mtoto kuacha masomo kwa sababu ya kipigo hii kifo tyr
Haiwezekani watoto waache shule kwa sababu ya kilaza mmoja asijua taaluma. NO Iwekwe hapa apigiwe simu
asbh mchana usiku,usiku wa manane na alfajiri.
Nafurahi kuona mwamko mzuri wa members wenzangu kuhusu haki za watoto.

Mtoto asipolindwa atafanyiwa ukatili wa kila aina na mtoto kubaki mnyonge huku akiona dunia chungu na kujiona hana mtetezi hivyo kupelekea mtoto kuwa mpweke.

Tuungane kwa pamoja kuwalinda watoto wetu dhidi ya ufedhuli wa wapumbavu wachache wasiojua maadili ya taaluma zao.

Shukrani sana mkuu kwa kuonesha uzalendo kwa watoto wetu.
 
Habari za Mwalimu Mkuu wa Mandimu Frank Boniphace Kalani zinasikitisha sana. Huyu jamaa ht ukiangalia profile fb ameweka picha ya mtoto kabebeshwa tofali inaonesha uhalisia wake. Serikali isilale...mkuu wa wilaya Ikungi, Thomas Apson na mkurugenzi Justice Kijazi tunaomba msimuache huyu mwalimu
 

Attachments

  • Screenshot_20241027_161212_Samsung Internet.jpg
    Screenshot_20241027_161212_Samsung Internet.jpg
    234.7 KB · Views: 4
Ni Stress sijui baadhi ya walimu wanayo..Kwanini umpe mtoto wa mtu mwingine kipigo kikali ??Ukiona ni mkorofi ameshindikana achana naye

Kujitafutia matatizo bure,mara umeua unajitafutia matatizo bure.
Naonewa tu kaka hakuna lenye ukweli Kuna mwalimu anapanga kunichafua tu na aliwaandaa Hawa watu wakanunulia mpaka miwa watu wale ili awahoji
Nimewaita katika kikao cha kamati ya shule wakasema wao hawakuhojiwa hivyo japo anasema alihoji vijana si ukweli aliwahoji wa mama
Kikubwa kazi naipenda siwe kurudi nyuma na siogopi uchunguzi I'm very hopeful sijafanya hivyo
 
Habari za Mwalimu Mkuu wa Mandimu Frank Boniphace Kalani zinasikitisha sana. Huyu jamaa ht ukiangalia profile fb ameweka picha ya mtoto kabebeshwa tofali inaonesha uhalisia wake. Serikali isilale...mkuu wa wilaya Ikungi, Thomas Apson na mkurugenzi Justice Kijazi tunaomba msimuache huyu mwalimu
Kaka sijafanya kitu kama hicho ni hivyo wenye nguvu wameamua kunichafua lakini naimani wananiimarisha
 
Na wewe umeamini ulichoammbiwa kwa stori za kijiweni na kutoa hitimisho mazima,
Unaweza kufuatilia hilo jambo kwa viongozi wa bodi ya shule na uongozi wa kijiji wakupe ukweli wa jambo husika au umfuate yeye mwenyewe,
Ni ajabu sana kijiji kumhofia mtu mmoja mpaka wake zao ndiyo wanafuatilia usalama wa watoto wao huku wanaume hawachukui hatua yoyote wanapiga stori za vijiweni
Afadhari ndugu yangu natuhumiwa kwa interest ya mtu mvivu kazini na ndiye alietengeneza haya
 
Mtoa mada ana aleji na walimu sijui tumemfanya nini?
Usikute ni wale form six au graduates majobless
 
Nataka kumleta mtoto wangu shule hiyo akae miezi miwili tu ili nidili na huyo ticha vizuri
 
Inawezekana mwalimu Frank anafanya yasiyofaa. Lakini pia inawezekana kuna watoto watafaidika kwa kubadilishwa tabia kutoka mbaya kuwa nzuri. Ni vizuri uchunguzi ukafanyika na ukweli ufahamike na maamuzi sahihi yafanyike. Kama anafanya yasiyofaa, achukuliwe hatua, na kama anasingiziwa na anawanyoosha wanafunzi kwenye uelekeo sahihi, apongezwe.
 
Back
Top Bottom