Serikali imeona wabunge wamepuyanga bungeni imerudi kukusanya maoni kwa wenye akili timamu

Serikali imeona wabunge wamepuyanga bungeni imerudi kukusanya maoni kwa wenye akili timamu

Hadi baada ya saa 6 ndio ninaanza kedi na matusi kama yako....asubuhi hii mkuu....I second you.....

#MamaAnaupigaMwingi[emoji120]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Unalaana si bure haiwezikani kila mtu anamashaka na huu mkataba mpaka alioungia we umebaki anaupiga mwingi mamaye watu ka nyny hatakutolewa kafara haifai
 
Sawaaa na kitambulisho cha utanganyika ndo kitumike kutoa umiliki wa ardhi,kupata kazi n.k
Tanganyika imezikwa...ni marehemu siku nyingi....imeshajiozea huko kaburini....

Ili ulewe ni mpaka utulize akili kujifunza UJAMAA WA KIAFRIKA...uuamini kupitia "MATAMBIKO ya kisiasa ya kiafrika" na "mizimu yetu ya kisiasa ya kiafrika" ndipo hapo unapopanda ngazi ya ENLIGHTMENT ya kuufia Muungano huu....

Ngazi hiyo itakufunulia elimu kuwa TANGANYIKA iko katika "Spiritual state iitwayo Occultation".....hii ni "African spiritual state" ni imani kali sana...kali sana ina nguvu kubwa iliyoje.....

Muungano utadumu milele ,amen[emoji120]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Mh.Rais SSH ana mtihani mkubwa sana.....ila atauvuka aaamin aaamin[emoji120]

Maswali fikirishi.

Hivi wazanzibari ni raia wa daraja la pili katika JMT?!!!

Mbona wanaposhika madaraka makubwa huwa wanashambuliwa sana kwa hoja kuwa UWEZO WAO WA KIUONGOZI NI MDOGO...HAWANA MAAMUZI....WANAUZA NCHI....?!!!

Watanzania wasio wabaguzi wawe makini sana na haya mambo.....

#SayNoToRacism
#SayNoToBigotry

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Wakashike madaraka kwao,kwao hawataki ushirikiano wao wanataka kwetu ,tu...!!mnataka vya watu tu..
Nyie ndo wale changu changu,chako cheti
#Kataa Muungano,Muungano ni utapeli
 
Tuliona walichofanya wabunge Dodoma; tumeona wanachofanya wanazuoni kutoka kwenye dini na fani mbalimbali nchini. Wanajadili mule mule alipopita Mzee Mbowe na Lissu, tofauti ni kwamba wanazuoni wanawapiga shule mawaziri wakati wabunge waliwapigia makofi mawaziri bila kuwapa maarifa mapya.

Hiki kinachoendelea ni fedheha kwa bunge na wabunge; kwamba pamoja na kupitisha kumbe wao siyo final bali kazi yao ilikuwa rubber stamp au kukamilisha ratiba.

Goma limekuwa gumu na endapo Mbowe na Safu yao wataingia uwanjani kwenye mikutano ya adhara kwa agenda hii upo uwezekano pakatokea mmomonyoko mkubwa na makundi kuhusu bandari.

Changamoto kubwa ya Watanzania ni wanafiki wazuri; wakiona unataka kusikia habari hoja fulani nao wanakupigia makofi ila moyoni wana ukweli na wewe ukijiongezea unagundua huna watu nyuma yako.

Magufuli alisifika ila waliokuwa wanamsifu angewaruhusi wapige kura ya siri angelalamika kaibiwa kura kwa sababu baada ya kuondoka tu watu walewale waliokuwa mgongoni mwake walijitokeza kumkataa.

Kama walimkataa hadharani akiwa ameondoka je, walimpigia kura sirini? Kwa kuwa alifahamu fika kwamba amewakosea Watanzani aidha akiwa na nia nzuri au mbaya ndipo akaona njia sahihi ni kuchafua uchaguzi.

Kwa mantiki hii, hakuna mwenye uhakika wa nani ambaye anamkubali kiongozi wa CCM sirini. Wote tumebaki kusikia uungwaji mkono wa majukwaani ila unapokuja sirini hakuna mwenye uhakika wa kutoboa. Hii inatokana na ukweli kwamba tumewaweka makovu Watanzania kwa muda mrefu kwa kuwaaminisha tunafanya uwekezaji wenye tija matokeo yake hakuna tija.

Kwa hatua za awali Mhe. Rais ameona walipokosea wasaidizi wake, amejifunza kwa ndani nini jamii inataka, amewasikia viongozi wa kijamii na imani wanasimamia nini, lakini amewasikia wale wasaidizi wake bungeni walichangia nini; obviously amebaini wanaompotosha na kumchonganisha na jamii siyo wapinzani bali wasaidizi wake.

Inatia hasira unapodhani una wataalam wazuri kisha unagundua kazi waliyofanya inapigwa vita na kila msomi; swali la kujiuliza, hao wasomi walioteuliwa kukusaidia wameelimika? Wana exposure au wapo kwa sababu wapo?

Naamini soon Mwanasheria Mkuu wa Serikali na timu yake watapisha ofisi kwa kilichotokea, vinginevyo ikibainika mkataba haukuwa shirikishi, pamoja na kiburi cha kibinadamu bora tuchelewe kufika kuliko tufike tukiwa siyo wamoja.

Padri Kutima ametueleza Somalia na Sudan, mimi nataka niongeze Loliondo na Tarime mgodini, je, tunadhani ni nia zote nzuri ni nia nzuri?
Kusema kweli mimi huwa namuombea sana Ndugu Rais SSH. Hii nchi ina aina ya binadamu wagumu mno ambao wameamua kwa makusudi kabisa kuacha kutumia akili zao na kumshauri Rais vizuri.

Mungu aendelee kumlinda na kumpa hekima ya kuiongoza hii nchi.
 
Hujawahi kuwaona wajaluo wanaojiona kama wazungu tu?!!!

Kila alipokaa mkoloni ameacha athari...wako wanaoendeleza athari hizo....usitudanganye hapa kuwa walipokaa WAARABU pekee ndiko watu wake wameathirika....

Walipokaa WARENO ?!!
Walipokaa WAFARANSA?!!
Walipokaa WAINGEREZA?!!!

Kujiona waarabu ni kuvaa mavazi ya waarabu ?!!!

Mbona Brazil wamekaa Wareno na Wahispaniola na "natives" wanaishi kwa kuvaa kama wakoloni wao...kwanini kwa wazenji na hao waarabu tu ?!!![emoji15][emoji15][emoji1787][emoji1787]

Mbona Msumbiji (mpaka wameruhusu LGBT) wanaishi na tamaduni za kireno?!! Msumbiji imeruhusu USHOGA kwa msukumo wa waarabu?!!

Au unafananisha UARABU na dini ya kiislam ?!!

Sasa uislam na uarabu wapi na wapi ?!!!

Mbona Lebanon ni waarabu na si waislam wote?!! Kwa hiyo hawana akili hao raia wake wasio waislam?!!

Mbona Misri si wote waislam(coptics) kwa hiyo wasio waislam hawana akili?!!

Morocco Algeria na kwengineko ?!!

Kwa hiyo walikotawala wazungu ndiko kuna waafrika wenye akili ?!!

Vipi Haiti ,vipi DRC ,vipi SA ?vipi Malawi ,Vipi Zambia vipi Msumbiji?[emoji1787][emoji1787]

Halafu nikujuze we sakala....hivi sisi vijana wa kiume na kike hatuishi maisha ya wazungu huku mitaani ama vyuoni....makatakei ,dada zetu kujichubua ,nywele za kubandika(za wazungu) kope ,contact lenses...wamejifunza kwa waarabu ?!! Si uzungu...je si kwenda kinyume na uafrika wetu ?!!
Baadhi ya vijana wa kiarabu nao wanaishi kizungu..hawajaiga kwa wazungu?!!

Hivi mnakwenda shuleni kusomea "kupakana mafuta na uhobobo wa kingese" nini ?!![emoji1787][emoji1787]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Hapo ndo ninnapo waona nyie wanzibar mna shida,
Mkiletewa hoja mnakimbilia kwenye dini na uarabu,sisi tuna waisilamu pia,namm tuna kaka,dada ,ndugu wakiislam pia ...
Huarabuni hamna walichotukosea ,
Hoja ni mikataba ya ulagai,inayochochewa na katiba mbovu na Muungano wa kinafki,
Hamna hoja ya dini hapa....
Mzanzibar hawezi kuwa na uchungu na Tanganyika,wala Mtanganyika hawezi kuwa na uchungu na zanzibar,
Mikataba inajieleza wazi...
Zanzibar iwe mkoa au tuvunje Muungano,
#Kataa Muungano,Muungano ni utapeli
 
Hili ndiyo suluhisho. Ingepigwa kura 'huru' ya maoni juu ya uwepo wa muungano nina hakika asilimia 95 wangeukataa muungano huu.
Muungano ni imani yetu yenye nguvu zaidi ya kitu chengine hapa ardhini(maisha ya dunia)...

Wajamaa wa kiafrika tunaamini sana katika asili ya UDONGO....udongo wa Tanganyika ukachanganywa na Zanzibar....spiritual udongo wa kila eneo iliokuwa Tanganyika umebadilika na Zanzibar hivyohivyo....kule Zanzibar udongo wao ambao toka 1964 ni mchanganyiko wa udongo wa iliokuwa Tanganyika...SASA KILA ENEO BARA NA PWANI lina UDONGO CHOTARA....hapa "mahobobo" "mandwanye" wagonjwa wa akili ,wenye matatizo ya kisaikolojia (Post-traumatic stress disorder) secondary to "CHILD ABUSE" wanaweza wasinielewe [emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Ninaelezea kuwa imani yetu ya ujamaa wa kiafrika na mizimu yake na matambiko yake ikaamuliwa Tanganyika iende katika "spiritual occultation state" na kuzaliwa CHOTARA wa kipekee kabisa....

CHOTARA anaishi...ndio hii Tanzania....sisi sote tuliozaliwa 1964 kuja juu tumekula virutubisho vipya kutoka ardhi hiyo chotara...miili yetu imejaa MINERAL SALTS "CHOTARA" ,VITAMINS "CHOTARA" PROTEINS"CHOTARA"...ukitaka utumalize tusiwepo na "tuhiliki sote" hebu jaribu kuurudisha UDONGO wa mama Tanganyika halafu uone tutakavyokuwa wanyafuzi ,tukakaukiana ,tukapata "mineral deficiencies ,protein deficiencies ,avitaminosis" kifupi mdororo wa Kinga zetu za mwili (U.KI.MWI)....

Mwenye kuutaka kuuvunja muungano avunjike yeye kiuno.,aaamen aamen aaamen [emoji120]

#SiempreJMT[emoji120]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Ni imani inayohitaji "African spiritualism and awakening" kuamini MIZIMU YETU YA AFRIKA NA MATAMBIKO YETU <img src="//emoji.tapatalk-cdn.com/emoji1787.png" /><img src="//emoji.tapatalk-cdn.com/emoji1787.png" /><img src="//emoji.tapatalk-cdn.com/emoji1787.png" />

Usiwe mjinga fazili...

Acha kutanguliza HISIA zaidi ya UHALISIA uliopo
Dah! Eti muungano ni imani?! Tena African spiritism?! Ndio maana watakuambia suala la kubinafsisha bandari ya Dar ni imani na kweli nimeona wabunge wetu hawana hoja za kimantiki bali wana amini tu DP World watafanya muujiza pale bandarini.
 
Hapo ndo ninnapo waona nyie wanzibar mna shida,
Mkiletewa hoja mnakimbilia kwenye dini na uarabu,sisi tuna waisilamu pia,namm tuna kaka,dada ,ndugu wakiislam pia ...
Huarabuni hamna walichotukosea ,
Hoja ni mikataba ya ulagai,inayochochewa na katiba mbovu na Muungano wa kinafki,
Hamna hoja ya dini hapa....
Mzanzibar hawezi kuwa na uchungu na Tanganyika,wala Mtanganyika hawezi kuwa na uchungu na zanzibar,
Mikataba inajieleza wazi...
Zanzibar iwe mkoa au tuvunje Muungano,
#Kataa Muungano,Muungano ni utapeli
Acha "argumentum ad hominem" katika hoja.....

Mimi si mzanzibari .....thibitisha uzanzibari wangu....nasubiri UTHIBITISHO kabla sijaendelea zaidi.....

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Dah! Eti muungano ni imani?! Tena African spiritism?! Ndio maana watakuambia suala la kubinafsisha bandari ya Dar ni imani na kweli nimeona wabunge wetu hawana hoja za kimantiki bali wana amini tu DP World watafanya muujiza pale bandarini.
Imani ni lazima kufanya miujiza ?!!!

Kwanini Muungano wetu usiwe imani ilihali ulichanganywa mchanga wa pande mbili?!!!

Unadhani mchanganyiko ule ulikuwa ni mbwembwe tu za sherehe ?!!!

Najua unajua nguvu ya mchanga/udongo kwa maisha yetu wanadamu....

Muungano ni IMANI YENYE NGUVU SANA...MNOO...MNOO...

Narudia kusema kuwa si imani ya KIDINI...

Ila wana imani ya DINI za kikristo na kiislamu wanafanyia ibada zao na kuendelea kuamini dini zao juu ya HUU MCHANGA WA ARDHI(CHOTARA) ulio na "African spirituality & Enlightment and consciousness" ukisukumwa na IMANI kali sana ya UJAMAA WETU WA KIPEKEE WA KIAFRIKA....

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Mh.Rais SSH ana mtihani mkubwa sana.....ila atauvuka aaamin aaamin[emoji120]

Maswali fikirishi.

Hivi wazanzibari ni raia wa daraja la pili katika JMT?!!!

Mbona wanaposhika madaraka makubwa huwa wanashambuliwa sana kwa hoja kuwa UWEZO WAO WA KIUONGOZI NI MDOGO...HAWANA MAAMUZI....WANAUZA NCHI....?!!!

Watanzania wasio wabaguzi wawe makini sana na haya mambo.....

#SayNoToRacism
#SayNoToBigotry

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Kwani ni uongo? Kwani Loliondo haijauzwa? Mwinyi anaonewa kwa hilo?
 
WANAZUONI WATOA TAMKO JUNE 2023

KUUZA LANGO LA UCHUMI WA NCHI AU KUTAFUTA WANAHISA NI USARITI MKUBWA KATIKA KUVUNJA KATIBA YA NCHI: BANDARI NI MALI ZA WATANZANIA WOTE HATUNA WANAHISA (SHAREHOLDERS) NA HATUHITAJI WANAHISA.

WARAKA WA WAZI KWA WAHESHIMIWA WABUNGE
NAKALA KWA WAHESHIMIWA VIONGOZI WA DINI
NAKALA KWA TAASISI YA MWALIMU NYERERE CHINI YA MZEE JOSEPH BUTIKU
NAKALA KWA VIONGOZI WA CCM
NAKALA KWA WASOMI WOTE NCHINI
NAKALA KWA UMMA WA WATANZANIA
NAKALA KWA WAPENDA AMANI DUNIANI KOTE

Jumuiya ya Wanazuoni nchini ambao tumekaa pamoja kutoka vyuo vikuu mbali mbali kutimiza wajibu wetu kama katiba ya Nchi inavyotaka pamoja na ya Chama Tawala iliyorisi misingi ya TANU kwamba nitajielimisha kwa uwezo wangu wote kwa manufaa ya nchi yangu na Elimu yangu ni kwa manufaa ya Taifa. Wanazuoni tunaanza kwa kutumia busara na kujenga hoja mahususi kupinga nchi yetu kuuzwa kienyeji kwa kisingizio cha mashirikiano ya Nchi yetu na Nchi za Falme ya Kiarabu. Hoja zetu ni kama ifuatavyo;
Kwanza; Bandari zetu zote ni mali za Watanzania zinazosimamiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hatuna ubia na mtu yoyote wala Taifa lolote. Wanazuoni baada ya kusoma kwa kina kile kinachoitwa mkataba wa kubadilisha uendeshaji wa Bandari zetu na kwa jinsi tulivyofuatilia hoja mbali mbali za wanaunga mkono na wanaopinga, Wanazuoni tunapenda kutoa tafsiri sahihi ya hicho kinachoitwa mkataba kwa lugha rahisi , Wanazuoni tumetafsiri kuwa ni kitendo cha kuuza Nchi kwa bei rahisi sana na kuingiza mwanahisa mpya kwenye umiliki wa Bandari zetu ambao utakuwa umiliki wa milele au wa muda husiokuwa na kikomo maana hata waziri ameshindwa kusema huo mkataba utakwisha lini? Tafsiri yetu inatokana na jinsi hao wanaoitwa washirika wanavyogawiwa bure Bandari zetu eti kwa kigezo wanajua kuendesha Bandari. Hata kama wanaleta mtaji bado kwa kupewa mkataba tu kwao ni pesa na watapata mikopo midogo na mikubwa huko Duniani kwa kutumia Bandari zetu. Kwa kuwa Waheshimiwa Wabunge wameamua kulisariti Taifa na kupitisha ridhio la makubaliano hayo wajue kuwa mkataba huo utalindwa na sheria za Kimataifa huwezi kuuvunja na ukifanya hivyo Nchi itaingia kwenye Vita maana kila upande wa umiliki wa Bandari utatumia jeshi kulinda haki zake za kiuchumi (economic interests). Hoja yetu ya msingi hapa kuwa tutapoteza umiliki ambao tulipewa na Mungu “Sovereign ownership of the ports”. Wanazuoni tunasikitika kwani serikali zilizotangulia zote zimewekeza sana kwenye maboresho ya Bandari zetu kwa kiwango cha juu mno kwa viwango vya Afrika. Ni ujinga (ignorance) wa kiwango cha juu sana kujilinganisha na Nchi za Falme za Kiarabu (Emirates au Dubai) ambazo zinamilikiwa na falme au koo(familia). Ni rahisi sana Mabeberu wa Kimarekani kujificha kwenye kivuli cha Falme za Kiarabu au Vivyo hivyo hata Umoja wa Ulaya ambao wanao mkataba mbovu wa EPA uliokataliwa na Afrika nao ni rahisi sana kuwa kwenye kivuli cha Falme za Kiarabu au Dubai.
Kumbuka Umoja wa Ulaya ulitumia pesa nyingi na muda wa miaka mingi kutaka moja ya masharti yao ya EPA ni kutumia Bandari zetu bila malipo yoyote as Free ports for European goods/products. Ukizingatia uchumi wa Marekani na Umoja wa Ulaya upo kwenye kipindi kigumu sana kuliko wakati wowote. Marekani na Umoja wa Ulaya wanaongezeko kubwa la umasikini, ukosefu wa Ajira na wamezidiwa na China katika uzalishaji viwandani (Manufacturing industries). Hivyo basi , sehemu pekee ya wao kupona na kushindana na China ni kupora utajiri wa Tanzania (Afrika) na kuendeleza unyonyaji ili waweze kuwatunza wazungu wenzao kwa kuwapa sera kinga (social Protection policies). Cha ajabu kubwa na ya karne Tanzania ambayo inataka kugawa Bandari zetu Bure kwa madalali wa Dubai ni moja ya Nchi Duniani ambayo haina sera kinga kwa watu wake na hasa makundi maalum (Lack of National Social Protection Policy). Ina viproject kama vile TASAF nayo inategemea pesa za wafadhili na mikopo ya Benki ya Dunia.
Lakini kwa Wazungu wa Ulaya na Wamarekani wanazo sera kinga ambazo zinalipiwa na pesa za Serikali za Walipa kodi wao na nyingine wanapora nje ya Nchi kama vile Ufaransa inavyopora west Afrika. . Na hii inawezekana tu kwa kuendelea kupora rasimali za Afrika na kupora uchumi wa Nchi zetu. Wanajua wakichukua Bandari zote za Tanzania watakuwa wanamiliki uchumi wa Nchi Karibia kumi zinazotegemea Bandari zetu kwa sababu Nchi yetu ipo kijiographia eneo la kimkakati sana na ndiyo moyo wa Nchi zote zinazotuzunguka. Ukiharibu uchumi wa Tanzania na Amani ya Tanzania umeharibu uchumi wa majirani zetu, Rejea Wosia wa Baba Taifa Mwalimu Nyerere kwenye hotuba aliyotoa SADC mwaka 1984 ikiwa sehemu ya kuaga kama Mkuu wa Nchi. Hivyo Wanazuoni tunawaomba Waheshimiwa Wabunge wetu wakatae kabisa siyo tu kubadili vipengele vya mkataba waachane kabisa kucheza na Taifa letu maana historia itawahukumu vibaya sana. Wajifunze Libya jinsi Mabeberu walivyowatumia wanasiasa na kuharibu Taifa lile. Ukiingiza Mabeberu wa kimarekani na Ulaya kwenye umiliki wa Nchi kama wanahisa wa Bandari zetu kwa mgongo wa Madalali wa Vinchi vya Falme za Kiarabu vinavyomilikiwa na kuendeshwa na familia za Kifalme ujue umeuza Nchi kabisa na Rushwa waliokupa utajuta maana watakutupa mbali na kutafuta serikali ya kulinda masilahi yao ya kiuchumi. Na hiki ndicho kitakuwa kifo cha chama Cha Mapinduzi na laana ya Waasisi na Watangulizi itatutafuna na kuwatafuna wabunge wote pamoja na spika wao. Mungu tuepushe laana hii. Ndiyo maana tunawaomba wazee wa Taifa hili kupitia Mwalimu Nyerere Foundation wajaribu kumshauri Mh. Rais aweze kupata Neema ya kuona hatari tunayoiona.Wazee mkikaa kimya Taifa letu likauzwa basi mjue nanyi historia haiwezi kuwaacha salama nyinyi na vizazi vyenu.
Hoja ya pili ya Wanazuoni ni kwamba Uchumi wa Tanzania tangia awamu zilizopita na kuchagizwa na awamu ya Tano imeweka Miundo Mbinu mikubwa sana ya Matrilioni ya Shilingi. Tumejenga reli ya Kisasa na tunamiliki wenyewe hatuna ubia, tumejenga vyanzo vya umeme ili kuweza kuendesha Treini za umeme. Tumewekeza sana kuboresha Bandari zetu kwa uwekezaji wa matrilioni ya shilingi na hatuna ubia. Tunahitaji kuendesha wenyewe Bandari na kutumia treini ya umeme kufikisha mizigo ndani ya masaa 20 kwenye Nchi zinazotuzunguka na tutaweza kupata pesa nyingi za kulipa madeni ya miundo mbinu. Ukiweka mbia yaani shareholder kwenye Bandari zetu hutaweza kucontrol mapato na matumizi ili uweze kulipa deni.
Hawa Madalali wa mabeberu wa Vinchi vya Falme za Kiarabu watapewa mgao wao yaani dividends na Tanzania itapewa dividends na tutakuwa wajinga kusaini mikataba kama iliyosainiwa na Kar Peter karne za 14 na Chifu Mangungo wa Msovero. Mikataba siyo tu ya kitapeli bali ni ya kinyonyaji maana thamani ya Bandari ni kubwa mno ni Sovereign wealth na hawa madalali wa Mabeberu watatumia bandari zetu kukopa Duniani hawaji na chochote bali pesa za kuwahonga viongozi wetu pamoja na kuwapa ahadi hewa za umiliki sehemu ya shares. Watawatupa nje kama Mobutu wa Congo zamani Zaire. Imperialists have permanent interests not permanent friends. Baada ya miaka ishirini Nchi itakuwa imeuzwa kabisa kwa Mabeberu ambao watajitanua sana na tutajiingiza kwenye mgongoro wa kiuchumi wa Kimtaifa (Geo political conflicts among imperialists powers). Tujifunze kwa Ufaransa na Nchi walizozitawala wanaendelea kuzinyonya kiuchumi. Hivyo basi tunawaomba Waheshimiwa Wabunge tusikubali kupuuza ushauri huu wa wasomi na kukubali mawazo ya kijinga ya wanaojiita darasa la saba ambao hawana uelewa wa uchumi wa Dunia na vita ya kiuchumi Duniani.

Hoja ya tatu ya Wanazuoni kwa Waheshimiwa Wabunge ni kuomba kabisa kukataa kabisa kutumika kuuza Nchi. Tunapinga hoja ya kusema kuwa wenzetu wana mitaji na technolojia hivyo tutaboresha uendeshaji siyo kweli. Hatuwezi kujilinganisha na Vinchi vinavyomilikiwa na familia za Kifalme ambavyo ni madalali wa mabeberu. Tutaboresha kwa viwango vyetu na tunaweza kuajili mtu yoyote kutoka dunia kuboresha uendeshaji. Tunaweza kuajili Mzungu, au Mhindi, au Mwarabu au Mkorea au MwaAfrika yoyote na tunaweza kununua technolojia popote duniani na kuweka mifumo ya Komputer ili kuondoa kero na Rushwa Bandarini. Mkataba wa TICS wa zamani husitumike kama kigezo siyo kweli, hata TICS hatutaki iwepo kabisa tunatakiwa kuimarisha mamlaka ya Bandari Nchni. Ni Ujinga wa kiwango cha Uprofesa au PhD kwa kudhani kuuza Nchi kwa kumpa mtu ubia ili aweze kuendesha Bandari zetu kwa niaba ni jambo zuri. Tutakuwa tumewasaliti watanzania. Waheshimiwa wabunge mkataba huo hata ukimpa GSM au mfanyabiashara mmarufu Mzee Bharesa au Jumuiya ya Wafanya biashara Nchini watafanya maboresho na utajiri utabaki hapa hapa na usalama wa Taifa utabaki pale pale. Huhitaji kuwa Profesa wa Uchumi kuona kuwa mkataba tajwa ni utapeli wa kimataifa na kuuza Nchi kienyeji ni mtu mjinga pekee anayeweza kukubali bila kupovushwa na Rushwa kubwa (grand corruption).

Hoja ya Nne kutoka kwa Wanazuoni, tunakataa Madalali wa Kiarabu wanaotumiwa na Mabeberu na wanaomiliki Vinchi vyao kupitia familia za kifalme zenye idadi ya watu ndogo na wote wananufaika na utajiri wa Nchi zao, mfano Dubai watu milioni mbili tu na wote wanatunzwa na serikali ya kifalme. Hivyo Social anthropology ya WaAfrika na WaTanzania ni tofauti na hao WaArabu kabisa kwa idadi ya watu na mambo mengine mengi ya kijamii, kisiasa, kiuchumi , kiutamaduni na kihistoria. Kugawa Bandari zetu ni sawa na kuuza Nchin yetu, hivyo tusitafute short cut. Lazima tupambane na Rushwa na tuongeze ufanisi katika Bandari zetu ambazo ni nguzo ya Uchumi wa Taifa letu.

Bunge lenye maprofesa wengi wazuri wakiwepo Prof. Kabudi, Prof. Kitila , Prof. Mkenda, Prof. Ndalichako na wengine. Halafu Bunge lenye Madaktari wa kusomea (PhD) nao ni wengi pia. Wapo Madaktari wa Binadamu (MD) nao wengi. Wapo wasomi wa aina mbali mbali wakiwemo wachumi . Hivyo sisi Wanazuoni tunaomba mkataba wa kukodisha Bandari husipitishwe kwani ni kuuza Nchi. Hawa wasomi wakikaa kimya historia itawaukumu huko mbele ya safari.

MAPENDEKEZO
Wanazuoni tunatoa mapendekezo yafuatayo kwa Waheshimiwa Wabunge pamoja na viongozi wote ambao wamepewa nakala ya wakara huu kutoka kwa wasomi wa Taifa. Tunawaomba wazee kama vile Mzee Butiku, Mzee Msekwa , Wastaafu wa vyombo vya ulinzi na Usalama na viongozi wa Chama Tawala wasikubali huu mkataba hata kama Bunge limepitisha wakatae maana Watanzania waliowengi wanapinga kabisa Nchi yao kuuzwa kwa mgongo wa mashirikiano kati ya Nchi na Nchi.
Kwanza; tunaomba kabisa Bunge lisitishe kabisa mkataba huu siyo kuboresha bali kusitisha mara moja na ktunga sheria ya kutoweka mbia yoyote kwenye Bandari zetu zote , iwe Bagamoyo au iwe yoyote. Liwepo katazo la kibunge .
Pili, tunaomba wabunge na spika wamshauri vizuri Mh. Rais kwa upole na uzalendo wa hali ya juu. Inawezekana washauri wa uchumi wa Rais hawajaliona jambo hili kwa bahati mbaya hivyo ushauri wetu utawaamusha uzingizini.

Tatu tunashauri Treini ya Umeme ambayo Mh. JPM aliacha imekamilika kipande cha DSM na kipande chas Dodoma ilikuwa imefikia asilimia 80%. Tunaomba mshauri Rais azindue Treini hiyo na kwenye bajeti ya mwaka huu tuwekeze kujenga reli mpaka Bandari . Tujenge Bandari kavu kubwa Dodoma kwa kutumia SUMA JKT kwa muda mfupi na gharama ndogo ili treini ianze kubeba mizigo na kuongeza ufanisi wa Bandari bila kuweka madalali wa Mabeberu wanaokuja kwa mgogo wa Vinchi vy Falme za Kiarabu wanavyomilikiwa na Familia. Tanzania ni Nchi yenye hadhi kubwa ndani ya Umoja wa Mataifa na Jumuiya ya Kimtaifa. Tanzania ni Nchi na Taifa ambalo halimilikiwi na Familia ni Nchi solid kabisa yenye kuheshimika Duniani tusipoteza mwerekeo tuungane na tujenge Nchi yetu kwa uzalendo na Umoja na tuache ubinafsi maana utaliangamiza Taifa.

Nne Wanazuoni tunashauri Waheshimiwa Wabunge wetu waweze kutafuta busara za wazee wa Taifa , Mzee Joseph Butiku , Mzee Warioba, Mzee Mangula, Wastaafu wa Jeshi , Wastaafu wa Usalama wa Taifa, Marais Wastaafu, Maprofesa Wastaafu , Wasomi wabobezi kama vile Profesa Shivji na wengine wengi. Wabunge aandaa semina huko Dodoma na Waite hawa Watanzania Wazalendo wawepe Busara zao ili mkifia maamuzi mtaweza kuliokoa Taifa.
Tano Wanazuoni tunashauri Waheshimiwa Wabunge wamuombe Mh. Rais amsimamishe kazi waziri Mbarawa kupisha uchunguzi maana wizara yake ndiyo inataka kuleta majanga ya Taifa.

Tunatanguliza Shukrani
Wenu Katika Ujenzi wa Taifa
Wanazuoni
Naunga mkono hoja,waweke na hoja ya katiba mpya,na kuukataa Muungano
Viva Ccm
 
Imani ni lazima kufanya miujiza ?!!!

Kwanini Muungano wetu usiwe imani ilihali ulichanganywa mchanga wa pande mbili?!!!

Unadhani mchanganyiko ule ulikuwa ni mbwembwe tu za sherehe ?!!!

Najua unajua nguvu ya mchanga/udongo kwa maisha yetu wanadamu....

Muungano ni IMANI YENYE NGUVU SANA...MNOO...MNOO...

Narudia kusema kuwa si imani ya KIDINI...

Ila wana imani ya DINI za kikristo na kiislamu wanafanyia ibada zao na kuendelea kuamini dini zao juu ya HUU MCHANGA WA ARDHI(CHOTARA) ulio na "African spirituality & Enlightment and consciousness" ukisukumwa na IMANI kali sana ya UJAMAA WETU WA KIPEKEE WA KIAFRIKA....

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Mkataba unanufaisha Zanzibar zaidi, ni mkataba wa kinyonyaji sana.
 
Acha "argumentum ad hominem" katika hoja.....

Mimi si mzanzibari .....thibitisha uzanzibari wangu....nasubiri UTHIBITISHO kabla sijaendelea zaidi.....

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Tafuta sehemu nilipo sema,mtoa mada ni mzanzibar,
Nimeongea lugha jumuishi "wazanzibar"
Halafu usiepuke hoja ,usilete hisia jikite kwenye hoja
 
Tuliona walichofanya wabunge Dodoma; tumeona wanachofanya wanazuoni kutoka kwenye dini na fani mbalimbali nchini. Wanajadili mule mule alipopita Mzee Mbowe na Lissu, tofauti ni kwamba wanazuoni wanawapiga shule mawaziri wakati wabunge waliwapigia makofi mawaziri bila kuwapa maarifa mapya.

Hiki kinachoendelea ni fedheha kwa bunge na wabunge; kwamba pamoja na kupitisha kumbe wao siyo final bali kazi yao ilikuwa rubber stamp au kukamilisha ratiba.

Goma limekuwa gumu na endapo Mbowe na Safu yao wataingia uwanjani kwenye mikutano ya adhara kwa agenda hii upo uwezekano pakatokea mmomonyoko mkubwa na makundi kuhusu bandari.

Changamoto kubwa ya Watanzania ni wanafiki wazuri; wakiona unataka kusikia habari hoja fulani nao wanakupigia makofi ila moyoni wana ukweli na wewe ukijiongezea unagundua huna watu nyuma yako.

Magufuli alisifika ila waliokuwa wanamsifu angewaruhusi wapige kura ya siri angelalamika kaibiwa kura kwa sababu baada ya kuondoka tu watu walewale waliokuwa mgongoni mwake walijitokeza kumkataa.

Kama walimkataa hadharani akiwa ameondoka je, walimpigia kura sirini? Kwa kuwa alifahamu fika kwamba amewakosea Watanzani aidha akiwa na nia nzuri au mbaya ndipo akaona njia sahihi ni kuchafua uchaguzi.

Kwa mantiki hii, hakuna mwenye uhakika wa nani ambaye anamkubali kiongozi wa CCM sirini. Wote tumebaki kusikia uungwaji mkono wa majukwaani ila unapokuja sirini hakuna mwenye uhakika wa kutoboa. Hii inatokana na ukweli kwamba tumewaweka makovu Watanzania kwa muda mrefu kwa kuwaaminisha tunafanya uwekezaji wenye tija matokeo yake hakuna tija.

Kwa hatua za awali Mhe. Rais ameona walipokosea wasaidizi wake, amejifunza kwa ndani nini jamii inataka, amewasikia viongozi wa kijamii na imani wanasimamia nini, lakini amewasikia wale wasaidizi wake bungeni walichangia nini; obviously amebaini wanaompotosha na kumchonganisha na jamii siyo wapinzani bali wasaidizi wake.

Inatia hasira unapodhani una wataalam wazuri kisha unagundua kazi waliyofanya inapigwa vita na kila msomi; swali la kujiuliza, hao wasomi walioteuliwa kukusaidia wameelimika? Wana exposure au wapo kwa sababu wapo?

Naamini soon Mwanasheria Mkuu wa Serikali na timu yake watapisha ofisi kwa kilichotokea, vinginevyo ikibainika mkataba haukuwa shirikishi, pamoja na kiburi cha kibinadamu bora tuchelewe kufika kuliko tufike tukiwa siyo wamoja.

Padri Kutima ametueleza Somalia na Sudan, mimi nataka niongeze Loliondo na Tarime mgodini, je, tunadhani ni nia zote nzuri ni nia nzuri?
Hivi Elieza Feleshi AG bado yuko ofisini anakula kodi yangu!? Ninakulaani hadi kizazi cha nne!
 
Hapo ndo ninnapo waona nyie wanzibar mna shida,
Mkiletewa hoja mnakimbilia kwenye dini na uarabu,sisi tuna waisilamu pia,namm tuna kaka,dada ,ndugu wakiislam pia ...
Huarabuni hamna walichotukosea ,
Hoja ni mikataba ya ulagai,inayochochewa na katiba mbovu na Muungano wa kinafki,
Hamna hoja ya dini hapa....
Mzanzibar hawezi kuwa na uchungu na Tanganyika,wala Mtanganyika hawezi kuwa na uchungu na zanzibar,
Mikataba inajieleza wazi...
Zanzibar iwe mkoa au tuvunje Muungano,
#Kataa Muungano,Muungano ni utapeli
Thibitisha uzanzibari wangu...

Nithibitishie hapa kuwa mimi ni mzanzibari....[emoji15][emoji15]

Mwenye kuutaka kuuvunja muungano atavunjika yeye kiuno....hakitavunjika kwa kupigwa na askari bali "mizimu yetu ya ujamaa wa kiafrika wa juu ya pande la ardhi la Tanzania utamvunjilia mbali kiuno na uti wa mgongo wake....

Hivi UAMSHO wako ?!!!

Hivi G55 wako ?!!!

Unatumikia maslahi ya wasiotakia mema Tanzania?!!![emoji15]

Nje ya MUUNGANO kuna :-

1)UGAIDI WA KIDINI (dini yoyote inaweza kutumiwa mifano iko tele duniani )

2)UGAIDI WA KIKOMUNISTI (Afrika ni eneo linalopiganiwa na mataifa makubwa kwa ajili ya raslimali )

3)UZANZIBARA NA UZANZIBARI

4)SIASA ZA KIKABILA ,KIKANDA NA KIDINI

Nje ya Muungano hiyo "Tanganyika" kamwe haitosimama kuwa moja.....

Nje ya Muungano kamwe hiyo Zanzibar haitokuwa moja.......

Hivi mnakwenda shule kusomea "kupakana ma...ta na kuwa wangse"?!!![emoji1787][emoji1787]

#SiempreJMT[emoji120]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom