KERO Serikali imeongeza tozo LUKU kutoka Tsh 1,500 mpaka Tsh 2,000 kimya kimya

KERO Serikali imeongeza tozo LUKU kutoka Tsh 1,500 mpaka Tsh 2,000 kimya kimya

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Attachments

  • Screenshot_20240701-214931.jpg
    Screenshot_20240701-214931.jpg
    129.1 KB · Views: 4
Kwa sasa makato ya kodi unaponunua LUKU yameongezeka kutoka TZS 1,000 mpaka TZS 2,000.

Tunaomba maelezo kwanini gharama hizi zineongezeka? Kuna sababu gani ya kuendelea kufanya maisha ya watanzania kuwa magumu ili hali mabwawa ya umeme yaliyotumia matrilioni ya kodi za wananchi yameshafunguliwa?

Je, kodi wanazotozwa wananchi bado hazitoshi? Je, mmeshindwa kutumia rasilimali zilizopo nchini, kuna madini, maliasili na vivutio mbalimbali vya utalii n.k pamoja na vyanzo hivi vya mapato, serikali imeshindwa kuwa bunifu na kutegemea tozo na kuendelea kunyonya na kufanya maisha ya watanzania yazidi kuwa magumu?

Hali hii itaendelea mpaka lini?

View attachment 3030797
Mawazo ya waziri wa fedha ni finyu sana kama mtu wa diploma tuu. Ni kweli lengo ni Zuri kuongeza makusanyo ya kodi. Lakini swali langu kwanini mzigo mkubwa unabebwa na wachache??? Kama lengo ni kupata kodi kupitia hiyo ya makato ya umeme nyumba zenye umeme ni kama 1/3 ya nyumba zote Tanzania sasa kwanini asije na sera ya kila nyumba lazima iwe na umeme ila akusanye kodi kubwa?? Jamaa ana PhD ila namuona kama ana diploma tuu. Hana ubunifu
 
Hii ni dharau kubwa sana kwa wananchi mimi naipenda CCM ila kwa hili hapana.angalau wananchi tungepewa taarifa.
 
Kwa sasa makato ya kodi unaponunua LUKU yameongezeka kutoka TZS 1,000 mpaka TZS 2,000.

Tunaomba maelezo kwanini gharama hizi zineongezeka? Kuna sababu gani ya kuendelea kufanya maisha ya watanzania kuwa magumu ili hali mabwawa ya umeme yaliyotumia matrilioni ya kodi za wananchi yameshafunguliwa?

Je, kodi wanazotozwa wananchi bado hazitoshi? Je, mmeshindwa kutumia rasilimali zilizopo nchini, kuna madini, maliasili na vivutio mbalimbali vya utalii n.k pamoja na vyanzo hivi vya mapato, serikali imeshindwa kuwa bunifu na kutegemea tozo na kuendelea kunyonya na kufanya maisha ya watanzania yazidi kuwa magumu?

Hali hii itaendelea mpaka lini?

View attachment 3030797
Mama anaupiga mwingi sana
 
Hata mimi nilinua umeme wa elfu 9000 nikitegemea kupata unit 60+ sababu nipo matumizi madogo na nimetoa service charge. Cha ajabu nilipata unit 57 tena bila maelezo ya makato. Hatari sn hii.

Ila suala la ndugu yetu ni kwamba atakuwa aliingiza umeme kwenye nyumba yake na akapewa unit za kuanzia km 30. Hivyo, Hilo deni huwa wanakata hiyo elf 6 kwa kipindi cha mwaka 1. Labda akiona meseji hii atakuja kithibitisha niliyosema au atoe ufafanuzi.
Sh 9000 unapata unit 57? Ni umeme upi huo? Zanzibar au Rea?
 
Sasa Msigwa Alipofika Bei Pesa Zinatakiwa Zitoke Huko Alipwe
CCM Haina Aibu
 
Umeongea Point sana Dr.

Wanasema kwamba Tar 26 July 2023 Serikali ilipandisha kodi kutoka 1000 hadi 1500 ,kwahiyo kama walinunua umeme kati ya tar 1 hadi 25 July 2023 basi kuna deni la 500/= Tsh ,kwahiyo mwaka Mpya wa Serikali umebadilika leo tar 1 July 2024 ,kama una deni la 500 basi litajumlishwa na 1500 na kuwa 2000 kwa Mwezi huu wa July ,ila mwezi ujao ukinunua LUKU utakatwa 1500 kama kawaida ,hayo ni Maelezo ya TANESCO wenyewe baada ya kubananishwa na wadau kwanini bei imepanda.
Sasa kwa nini wasitoe taarifa kwa umma watu wakajua nini kinaendelea, hii nayo ni taharuki kwa wananchi. Watu wanaichukulia jero kimasihara sana hawa.
 
Shida ya watanzania ni moja tuh, wanaopenda kufanya maandamano hewa yaani ya mtandaoni tuh.

Twende Kwenye uharisia pesa za wa Tanzania Kwenye nyumba tu mfano tuna nymba milioni kumi zenye umeme maana yake Kwa buku tu wanakusanya bilioni kumi Kwa mwezi.

Ukija Kwenye matozo mengine ni mamia ya mabilioni Kwa mwezi.

Je kama tunakopa pesa za ndani hizi zinaenda wapi??
 
There are news circulating that the Property Tax has been increased and now Tanesco after these monthly deductions will be paying the Municipal directly?
 
Kwa sasa makato ya kodi unaponunua LUKU yameongezeka kutoka TZS 1,000 mpaka TZS 2,000.

Tunaomba maelezo kwanini gharama hizi zineongezeka? Kuna sababu gani ya kuendelea kufanya maisha ya watanzania kuwa magumu ili hali mabwawa ya umeme yaliyotumia matrilioni ya kodi za wananchi yameshafunguliwa?

Je, kodi wanazotozwa wananchi bado hazitoshi? Je, mmeshindwa kutumia rasilimali zilizopo nchini, kuna madini, maliasili na vivutio mbalimbali vya utalii n.k pamoja na vyanzo hivi vya mapato, serikali imeshindwa kuwa bunifu na kutegemea tozo na kuendelea kunyonya na kufanya maisha ya watanzania yazidi kuwa magumu?

Hali hii itaendelea mpaka lini?

View attachment 3030797
Kama hamtaingia barabarani hamna jambo litafanyika. Shauri yenu
 
Back
Top Bottom