DOKEZO Serikali imuangalie IGP Mstaafu Omari Mahita, anatoa silaha yake ovyo hadharani anaweza kumjeruhi mtu

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
πŸ™πŸ™πŸ™
 
Kwa nchi zetu hizi za kujuana sana.

Kufunga lock gari ya IGP mstaafu ni kujitafutia matatizo tu. Huyo mfunga lock ni mpumbavu pia.

IGP mstafu huwezi kwenda kumshitaki popote ukamshinda.
Atakuwa mpumbavu tu kama alichofanya kinakinzana na mwongozo wa kazi yake. Lakini kama alilofanya ni hitaji la Kisheria, basi anastahili pongezi. Ameiheshimu kazi yake na ameukataa unyonge.

Miaka ya nyuma, kulikuwa na utaratibu wa ulinzi shirikishi maarufu kama sungususungu mkoani Arusha.

Siku moja, wakati vijana waliohitimu mafunzo ya mgambo wakiwa kwenye doria, waliliona gari linakuja na mmoja akalisimamisha. Hilo gari halikusimama mahali lilikopaswa, lilienda kama mita hamsini mbele zaidi ndipo likasimama.

Kumbe gari lilikuwa la wanajeshi (JWTZ). Kitendo cha kufahamu kuwa wamelisimamisha gari la Jeshi, wanasungusungu wote isipokuwa mmoja walikimbia na kutokomea machakani. Mwenzao kwa ujasiri kabisa, huku akijua alichokuwa akikifanya, alilifuata hilo gari na kuwaamuru wote waliokuwemo washuke. Waliposhuka tu, aliwaamuru waanze kuruka kichura kwa kosa la kutokusimama kwenye kizuizi. Kama vile maigizo, masoja walitii walichoamriwa. Baada ya kuruka hatua chache, aliwaamuru warudi kwenye Lori lao na kisha kuondoka.

Inawezekana hao Askari walitii kwa vile walikuwa na mkubwa wao. Huyo mgambo alionesha ujasiri wa hali ya juu kwa kuwatendea wanajeshi vile walivyomfundisha alipokuwa kwenye mafunzo ya mgambo.

Kesho yake, wanajeshi wakiwa kwenye Land Rover ya Jeshi walienda eneo husika kumtafuta huyo mgambo. Wenzake waliposikia, waliamini kuwa mwenzao kayatimba, kumbe ni kinyume chake.

Alienda kupongezwa kwa ujasiri aliouonesha, Jana yake Usiku na akaishia kupewa ajira Jeshini.

Huyo aliyelifunga gari la Mahita hakukosea kama alichofanya ni matakwa ya Sheria. Aliyekosea ni Mahita. Alichofanyiwa kilikuwa ni fursa ya kuonesha hekima yake au upumbavu wake.

Nina mashaka kama alichokionesha ni hekima.
 
U
Uzushi mtupu
 
Huko ni Kuchanganyikiwa aniona hali ya mtaani pale mwanzo milango yote ilikuwa wazi anapopita kila kitu kinafunguka sasa mambo ni moto ndio maana anatoa silaha yake na bado atatoa hata rocket ranger sio poa kaka ni moto fire.
 
Hata mimi nikiwa na Bastola hawa wazee wa parking lazima nifyatue Lock zao kama sio miguu yao
 
Mzee yuko sawa kabisa kufanya hivyo na ilibidi aje amnase makofi ya kutosha [emoji16] sio kenya hapa
 
Hao watia loki na wamezidi kuvizia, angejitokeza alambwe risasi ya makalio.

Hata ukiwa huna akili ni lazima uiheshimu gari ya Mahita. Unafikiri ana maadui wangapi huyo mzee? Yupo tense kila wakati.
 
Jambazi hilo
 
Ujinga wa hawa wanao funga magari wanafunga alafu wew unarudi yeye kaenda kula sasa pengine mzee ametoka zake kununua dawa za presha huyu kijana mvaa moka hayupo kwanin chuma isitumike kwanza hana adabu unafungaje prado wew [emoji16][emoji16]
 
Namkumbuka IGP Mahita kwa jambo la heri alilonifanyia. Niliajiriwa Polisi nikiwa na Elimu ya Kidato cha Nne. Ndani ya mwaka mmoja nikajiendeleza na kufanya Mtihani wa Kidato cha Sita kama Private Candidate. Matokeo kutoka nikafaulu na nikachaguliwa kwenda kusoma Nje ya Nchi tena kwa Udhamini wa Serikali. Nikafuata taratibu zote za kuomba ruhusa Polisi,Faili langu kufika Makao Makuu Dar likakwama,wale wasaidizi wa IGP wote Makamishna wakawa hawataki kusaini tena wakawa wananipiga mikwala hatari. Nilipanda sana ngazi pale Makao Makuu kufuatilia ruhusa bila mafanikio, yaani Chuo kikawa kimeshafunguliwa na nimeshachelewa mwezi mzima na nusu sijaripoti nafuatilia ruhusa. Siku ya mwisho nikasema leo liwalo na liwe,naenda kumuona IGP moja kwa moja,nikikosa ruhusa basi na kazi yenyewe naacha naondoka kwenda Chuoni. Kufika siku hiyo nikamuona Msaidizi wake Afande Diwani Athuman(huyu baadaye alikuja kuwa Mkurugenzi Mkuu TAKUKURU na Usalama wa Taifa),kipindi hicho alikuwa na Nyota Tatu(ASP),nikamuamkia na kumueleza shida yangu na kumuonyesha Vyeti vyangu na Barua ya kuitwa masomoni. Alishangaa sana kwa nini nazungushwa kupewa ruhusa. Huyu Diwani Athuman (Mungu ambariki),alinishika mkono akanipeleka mpaka ofisini kwa IGP Mahita na kumuelezea suala langu(kumbuka mimi ni Askari mdogo Constable),nafasi ya kuingia tu ofisini kwa IGP na kumuona nilitetemeka hatari. Huyu mwamba Mahita alishika simu na kumpigia Kamishna wa Mafunzo na kumuita aje ofisini kwake na Faili langu,ndani ya dakika 3 akawa amefika ameshika Faili langu. Alichukua Kalamu akaandika kwamba nipewe ruhusa ndani ya dakika 2 na ahakikishe kesho naondoka kuwahi masomo nje ya Nchi na taarifa amletee kesho asubuhi kwamba nimeshaondoka🀣. Kwa kweli sikuamini,nilipewa ruhusa dakika hiyohiyo na siku ya pili nikaondoka kwenda masomoni. Kwa kweli huwa namkumbuka sana Mkuu Diwani Athuman pamoja na IGP Mahita kwa wema ule walionitendea
 
Kama hiyo gari haina identity ya kutambulisha gari ya former igp aliyepiga Lock hana makosa ya kumsema kwamba hana adabu isipokuwa alikuwa anatimiza majukumu aliyopewa katika kazi yake.
 
Hayo unayoyasema ni vitisho vya kizamani huu ni ulimwengu wa kidigital huwezi kujitamba kwamba wewe ni mtu hatari sana sijui nini na nini jambo la pekee ishi na watu vizuri usalama wako unategemea watu wengine ,alafu busara zikuongoze
 
Suala hapo ni tabia ya umimi na afya ya akili ndio kiini cha matendo yake kuendelea.

Kam walivyowahi kusema wahenga
"Karma is a bitch it revolves back to the actor as a reciprocate"
 
Safi sana mzee Ngunguli! Huyo kenge hajui wewe enzi hizo uliweka maisha yako rehani ili baba na mama yake wapate amani ye azaliwe?
Huyo kenge anaweza kuthubutu kutia rock dungu la cdf mstaafu ama pm mstaafu?

Kama hakufahamu basi tumsamehe ila kama lifanya kwa kusudi akifahamu fika anamfanyia hivyo VIP mstaafu hakika ni kukosa adabu. Hiyo shaba iliyotandika kufuli ilitakiwa itandike fuvu la huyo kenge wa carparking.
Watu wa carparking wana ungese sana.
Hongera mzee Ngunguli umetendea haki jina lako kwa wakati sahihi. Hakuna kukubali unyonge mbele ya wapumbavu wenye nia ya kuwadhalilisha wazee wetu viongozi wastaafu.

Hata ingekuwa mimi akaja mbuzi mmoja kuniletea ungese ningemtia adabu kwa mtindo huo huo ili akamhadithie mkewe.
 
Hawa wajinga muda mwingine wanakera sana kufunga funga magari ya watu wakitaka rushwa, ni usumbufu tu.
Hapa pia nukupa support, Kuna kizee kimoja kinatembea na Hilo la kufungia hapa DSM mtaa wa Livingston, kinaudhi sana, hakuna parking ila analazimishia wrong parking how!? Ila hizi halmashauri na mamea sijui wanasimamia kitu Gani!! Foolish
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…