Serikali ina cheka na nyani: Wizi wa kimtandao Arusha inaelekea ni nchi nzima!

Serikali ina cheka na nyani: Wizi wa kimtandao Arusha inaelekea ni nchi nzima!

Duuh hii kuna issue kubwa serikali itapata madudu mengi kupitia investigation itakayo fanyika, na hii itafungua macho serikali kujua wezi wa kodi za serikali katika sehemu mbali mbali za nchi yetu.

Chambulo ni mfanyabiashara mzalendo sana, na huyo Mkurugenzi ni fisadi anaonekana tu, last time alikuwa na mapete makubwa mikono yote utadhania mganga wa kienyeji, mtumishi wa umma ana mapete makubwa vile vidoleni nilijua kabisa huyo sio kabisa.
Si ajabu nchi inapitia wakati mgumu sana kiuchumi.
Hongera sana Mh. Paul C. Makonda kwa angalau kuionesha "mifumo" jinsi nchi inavyopigwa.
Kwa hili kwa kweli kama Taifa, hatukudai chochote.
Mungu akubariki sana pamoja na Mr. Chambulo.
Duuh hii kuna issue kubwa serikali itapata madudu mengi kupitia investigation itakayo fanyika, na hii itafungua macho serikali kujua wezi wa kodi za serikali katika sehemu mbali mbali za nchi yetu.

Chambulo ni mfanyabiashara mzalendo sana, na huyo Mkurugenzi ni fisadi anaonekana tu, last time alikuwa na mapete makubwa mikono yote utadhania mganga wa kienyeji, mtumishi wa umma ana mapete makubwa vile vidoleni nilijua kabisa huyo sio kabisa.
 
Halafu bahati mbaya tuliyo nayo kama Taifa, ni watendaji wengi wa serikali yetu wana roho ya kisasi kama ya Mkurugenzi wa Arusha.
Wakiambiwa madudu yanayofanyika, wanakutafutia "angle" ili uingie matatani, kitu ambacho kinawaogopesha walio wengi kufichua maovu ili wasijikute matatani.
Halafu, hivi wale jamaa wa Mbeya wao suala lao liliishaje?
Kama hakuna chochote kimefanyika, basi acha tu tuendelee kupigwa
 
Noma sana yani hapo kwenye makampuni ndio watu wanapigwa!
The Tanganyika halafu una kutana na Tanganyika…ukiwa mjinga na haujali basi wewe unalipa tuu bila kujali kumbe unawapa watu hela za bure….

Sasa serikali hapa ndio inatakiwa kuwekeza kwenye kudhibiti wezi kama hawa wanaoweza kutengeneza kampuni hewa na kuipa control number….

Na watanzania tusivyo watu wakujali tunapigwa sana…yani kampuni yako inaitwa “leak” halafu wanakulete control number inayoonesha kampuni inaitwa “The leak” na sisi watanzania tusivyo watu makini na wakuhoji unatakuta mtu analipa kwenye hiyo control number ya “ The leak” kumbe ni kampuni hewa

Aiseee huu ni wizi umekithiri sana sana kwenye control number kwa watu waoga na wasio makini wanalipa tuu na unaweza kuwapigia wahusika wakakwambia hakuna shida we lipa tuu haina shida kumbe mtu amepigwa hapo…

Hii nchi ina shida sana
Ni ku-audit tax payers kila mara, na kuweka mifumo, mifumo iwe inakutana, kama jina la kampuni, mfumo wa Brela ukutane na wa Tamisemi, jina likigongana, mfumo ukatae, mifumo, mifumo, mifumo, idhibiane yenyewe kwa yenyewe, this country needs strong institution, not strong people.

Tuliwahi kuwa na Mwaibula Dar es Salaam, lakini sasa tuna mifumo,.sio Mwaibula
 
Halafu bahati mbaya tuliyo nayo kama Taifa, ni watendaji wengi wa serikali yetu wana roho ya kisasi kama ya Mkurugenzi wa Arusha.
Wakiambiwa madudu yanayofanyika, wanakutafutia "angle" ili uingie matatani, kitu ambacho kinawaogopesha walio wengi kufichua maovu ili wasijikute matatani.
Halafu, hivi wale jamaa wa Mbeya wao suala lao liliishaje?
Kama hakuna chochote kimefanyika, basi acha tu tuendelee kupigwa
Mkuu usiwe na wasi wasi juu ya mambo ya haki kisheria kama una haki zako.
Sisi tuliwahi mshitaki Mkurugenzi wa JIJI DSM, hadi aliomba poo!
 
mbona hamna cha maana hapo, what if ni typing error tu ya aliyetengeneza Control Number, kwa sababu naamin control number sio automatic kuna human intervention, wakati mwingine tunalalamika sana na kuwahisi watu wezi tu bila vivids, hata kama ni jina la kampuni hewa lkn control number imetokea kwa system ya serikali hela bado itaenda office husika,,, labda waseme kama wametengeneza mfumo wao wenye uwezo wa kutoa control number na risiti
Hueleweki,
 
mkuu unajua procedure za kutengeneza control number
All in all, Alichofanya makonda kuanzisha uchunguzi ni sahihi ama la. Kumbuka amesema wakikutwa hawana hatia watarudi kwenye nafasi zao.
 
Ebu semeni ukweli ni wapi hakuna wizi?
Kila mtanzania ni mwizi bila kujali anacheo au hapana hata huko kwenye nyumba za ibaada kuna wizi mkubwa sana.
 
Wizi umekuwa mkubwa maana no checks and balance zinazotskiwa kuwepo.
Mkurugenzi anapiga tu kiroho mbaya.
Isingekuwa huyo mfanyabiashara mzalendo kuibua, serikali imelala tu.
Huyo mfanyabiashara apewe ulinzi,kuanzia sasa hivi lazima atakua ana windwa na wasiojulikana ili awe eliminated baada ya kumwaga.mboga ya watu!!
 
Huyo mfanyabiashara apewe ulinzi,kuanzia sasa hivi lazima atakua ana windwa na wasiojulikana ili awe eliminated baada ya kumwaga.mboga ya watu!!
Ni kweli mkuu, kajitolea mhanga kuibua wizi ndani ya serikali.
Na si ajabu waliokuwawanafaidika na wizi huu, akubwa wamo!
 
Usipoteze lengo. Sijadai nataka niwe pale juu; lakini najuwa kwa tabia zako hizi yeyote akiwa hapo juu bado tabia zako zitakuwa vilevile kama zilivyo sasa.
Huwa unajidai mjanja lakini huna unalojua!
Hujawahi kuwa na a positive contribution in anything, thats how backwards you are.
 
Huwa unajidai mjanja lakini huna unalojua!
Hujawahi kuwa na a positive contribution in anything, thats how backwards you are.
Kwa sifa hiyo. Mi ni bora zaidi kuliko mtu wa aina yako anayejikomba kinafiki kwa kila kiongozi anayekuwa madarakani, hata kama kiongozi huyo ni boya kabisa.
Mie "...sijidai mjanja..." nakueleza tu ukweli ulivyo juu ya tabia zako mbovu hizi.
 
Back
Top Bottom