#COVID19 Serikali inatudanganya kuhusu Corona au ni siasa za kuomba hela IMF na Europian Union?

The Saver

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2014
Posts
202
Reaction score
651
Jana ilikuwa final za Euro 2020, 95%ya mashabiki wameingia uwanjani bila barakoa, chini za wenzetu wanaona haya mambo ya barakoa ni UPUUZI, England imetanganza from 19th July hamna haja ya Barakoa





Sasa serikali ya Mama Samia kila siku mabarakoa na kuwatia watu hofu


Nawashukuru watanzania wengi wamepuuzia kuvaa haya mabarakoa

Sasa nashangaa mkuu wa mkoa dodoma kulazimisha watu kuvaa haya mabarakao
 
Korona ipo, na watu wanapata maambukizi wengine hawaugui, wengine wanaugua na wengine wanakufa kabisa kama ilivyo kwa magonjwa mengine

Kikubwa ni kuchukua tahadhari na kumwona Daktari mapema mara tuu unaposihisi haupo sawa
 
Kwani huku mnalazimishwa au mnashauriwa; pia kumbuka huko chanjo wamechanja watu wao majority..., anyway maisha ni yako wewe ndio unajua jinsi ya kujikinga; ila wizara ya Afya ni jukumu lao kutoa ushauri kama wanavyoona inafaa....
 
Uingereza asilimia ya waliopata chanjo ni ngapi, Tanzania ni ngapi?
 
Subiri ipite na dingi ako ndiyo utajua kama ni uongo ama kweli, tuache utani watu wamelazwa kibao sasahivi
Mkuu samahani, MaCCM hayatapeleka hiyo pesa ikasadie watu, sasa maanake nini , acha tu tukose wote. Sisi wanyonge kufa na wao kosa pesa.
”sisi kosa na wao kosa” ubaya ubaya tu.!
 
Mkuu samahani, MaCCM hayatapeleka hiyo pesa ikasadie watu, sasa maanake nini , acha tu tukose wote. Sisi wanyonge kufa na wao kosa pesa.
”sisi kosa na wao kosa” ubaya ubaya tu.!
Hawawezi kukosa pesa ipo wanaipiga vizuri sn, kodi si tunalipa?
 
Kwani walichokifanya Uingereza ni sawa na tulichokifanya mpaka tujilinganishe nao ? Ni kama umelala mwaka mzima halafu jirani yako alikuwa analima halafu ukifika msimu wa mavuno unataka mvune sawa. Utavuna ulichokipanda !
 
Uingereza asilimia ya waliopata chanjo ni ngapi, Tanzania ni ngapi?
34M vaccinated and 36M not vaccinated


Kuwa vaccinated sio kigezo, mbona wameambiwa wote hukuna mambo ya barakoa

Mambo ya barakoa ya kipuuzi tu
 
Ukifuatilia vizuri, UK walishamaliza kuvaccinate wananchi wake sisi huku tunaendelea kusema hakuna ugonjwa na mpaka leo watu hawaamini kuna ugonjwa.

Wenzetu wameshaomdoka kwenye hiyo level, sasa wanaosubiri tuanze kufa na amini nakuambia wao wakimaliza nchi zao tutakoma.

Tuendelee kubisha tu, wanapiga vaccination hawaangalii nyuma. Asiyetaka wanamuacha Ila ndio events kama hizo hairuhusiwi kuingia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…