Serikali ingilieni kati, huu mfumo wa elimu utasababisha watoto waanze kuichukia shule

Serikali ingilieni kati, huu mfumo wa elimu utasababisha watoto waanze kuichukia shule

Nimerudi nyumbani kutoka mahali ninapofanyia shughuli zangu, nimekutana na kitu kinanipa mawazo sana.

Mwanangu wa kwanza (4yrs old) alikuwa anapenda shule sana, mwaka jana alikuwa anasoma shule si mbali sana na


Wewe ni mzungu au muafrika??
 
Mkuu upo sahihi.

Waalimu watussidie hapa. Hii kumkaririsha mtoto mpaka namba 1,000 shule ya awali inakuwaje kwani?
Lea mwanao Hadi miaka 5 , miaka 6 ndio aanze kwenda Shule ya msingi

Kabla ya hapo fanya homeschooling mwenyewe,
 
Nawaona saa 12 wanaenda shule kwa mguu, najiuliza ,saa hii wanaenda kufanya nini
Ni kutesa watoto..
Nishaona mtu kwenye daladala Yuko na kabinti kake kamesinzia na kanaonekana darasa la kwanza...na ni Saa kumi na moja alfajiri ...sijawahi kuelewa
 
Yaani hizi shule zina ujinga mwingi. Mwanangu darasa la kwanza wanatoka saa 11, anafika home saa 12, kachoka hawezi lolote, kapungua balaa. Namhamisha shule hii term ijayo, potelea mbali. Mimi nimesoma kayumba na sikuteseka hivyo na shule.
Yaani nimetoka kuwaamshia hapa, wanajifanya wanasusa eti uamuzi ni wako, nafanya utaratibu wa usafiri Kila saa 8 awe anatoka shule arudi nyumbani,muda mwingine wazazi tufanye màamuzi kwa maslahi mapana ya vizazi vyetu
 
Nimerudi nyumbani kutoka mahali ninapofanyia shughuli zangu, nimekutana na kitu kinanipa mawazo sana.

Mwanangu wa kwanza (4yrs old) alikuwa anapenda shule sana, mwaka jana alikuwa anasoma shule si mbali sana na

Elimu yenyewe hii ya kuja kukutana na mishahara ya laki 4 ukitoka chuo, upuuzi tu!
Kosa ni lako mzazi mtoto wa miaka minne unampeleka shule ya mbali.

Hapo anakuwa wa kwanza kuchukuliwa na wa mwisho kurudishwa. Unaweza kukuta anawahi kutoka ila anazunguka mji mzima kurudisha wenzake.

Mtoto mdogo unampeleka daycare za jirani za kutembea tu dada anampeleka saa saba au nane anaenda kumchukua.

Unapochagua shule ya kumpeleka mtoto unaangalia factor nyingi sana moja wapo ni umbali
 
Shule ya karibu na nyumbani wanachapa sana wanafunzi, mtoto akipata chini ya 80 atakula fimbo za maana. Siku moja nilipita nikasikia watoto wanalia balaa, kuuliza naambiwa wanakula mboko sana
Unamkimbiza asichapwe ?
 
Wazazi wa siku hizi sijui mna nini!?
Yaani mko selfish kupitilizaaaa. Unamuamsha mtoto wa miaka 4 saa11 alfajiri ili akakuletee nini huko shuleni!?
Unampeleka mtoto arasa la kwanza akiwa na miaka5 ili iweje?
Mbona mnawaonea hawa watoto!??? Yaani Mungu anakupa pesa, pesa inakupeleka kuwa mtumwa wa kuitumia bila kufikiri!?

Kama unampenda mwanao miaka minne kushuka chini unatakiwa uamue kwenda kuishi jirani na shule unayompeleka ili hata akiamka saa moja aende; au mpe homeschooling, tumia hiyo pesa kuajiri walimu watakaomfuata nyumbani

Mimi kanuni yangu ya malezi siwezi ishi umbali wa zaidi ya km 5 kwenda shuleni kwa mtoto wa primary
Hili nimeliona, nimeenda kuongea nae wananisusia eti utajua mwenyewe, nafanya utaratibu wa usafiri awe anaenda saa 2 saa 8 anatoka

Wengine tunatafuta kipato mbali kidogo na familia zetu hivyo tukipata hata muda wa kupumzika wiki 2 ndo mambo kama haya tunayaona
 
Nimerudi nyumbani kutoka mahali ninapofanyia shughuli zangu, nimekutana na kitu kinanipa mawazo sana.

Mwanangu wa kwanza (4yrs old) alikuwa anapenda shule sana, mwaka jana alikuwa anasoma shule si mbali sana na hapa, walikuwa wanatoka saa 6 mchana, sasa mwaka huu nikaona nimtafutie nursery bora angalau hata mwakani aanze
Unasema kweli kabisa. Ila mimi naona hili ni suala la wazazi wenyewe na uongozi wa shule na siyo serikali. Mimi nikiona mushkeli kidogo tu kwenye shule huwa nawasiliana na uongozi na wakileta ujuaji namhamisha kwenda shule nyingine. Japokuwa shule za Tanzania ni kama wanaigana namna ya kuendesha shule (miundo na uendeshaji umejaa makosa mengi) lakini bado kuna chache wanazingatia taratibu nzuri.

Kuna shule moja nilimhamisha kwa sababu ya kuchapa. Ilikuwa gari la shule likifika mtoto anaanza kuangua kilio, wakati alikuwa anapenda sana shule, kuuliza anasema wanachapwa. Nikaenda shuleni mwalimu mkuu anasema hii shule inapendwa na wazazi kwa sababu ya kuchapa watoto ili waelewe vizuri na wawe na adabu. Ujinga ulioje!
 
Kosa ni lako mzazi mtoto wa miaka minne unampeleka shule ya mbali.
Hapo anakuwa wa kwanza kuchukuliwa na wa mwisho kurudishwa. Unaweza kukuta anawahi kutoka ila anazunguka mji mzima kurudisha wenzake.
Mtoto mdogo unampeleka daycare za jirani za kutembea tu dada anampeleka saa saba au nane anaenda kumchukua.
Unapochagua shule ya kumpeleka mtoto unaangalia factor nyingi sana moja wapo ni umbali
Hizi daycare kasoma mwaka Jana ilikua hapa tu, mwaka huu nikapewa recommendation na mtu Kuna nursery nzuri ndo nikawa nimempeleka huko, ila nimegundua nilifanya Kosa kubwa sana

Leo nimeenda shuleni nimewaambia mwanangu ataripoti saa 2 saa 8 anatoka usafiri ntamtafutia mwenyewe au nimtoe hapa, wamekubal kishingo upande
 
Changamoto hapo Mtoto wako anaweza akawa anakaa mbali na Shule kwahiyo anakuwa wa kwanza kuchukuliwa halafu wa mwisho kurudishwa na gari la shule.!

Na kule shule unakuta ratiba ya masomo inaisha saa nane au tisa mda uliobaki unapotelea njiani.!
Kama mzazi angalia shule iliyopo karibu na Mtoto wako kuepusha vitu kama hivi kwa mtoto wako.!
 
Labda wanaamini wazazi wengi muda wa saa 7 wanakuwa wako kazini kwahiyo wanawachelewesha ili wakutane jioni.
Hiyo ni kwa sababu wapo wazazi huwapeleka watoto nursery kama kumtunza tu(huku alison's) wakati yeye akiwa kazini.
Ni kosa kuamini bila kushirikisha wazazi.
 
Unamkimbiza asichapwe ?
Kuna kuchapwa lakini sio viboko vilivyopitiliza. Sisi tulichapwa lakini sio kwa ajili ya kupata chini sijui ya 80, tulichapwa kwa makosa yakueleweka. Utampchapaje mtoto kapata chini ya 80, huu ni ukatili kwa watoto.
 
Hizi daycare kasoma mwaka Jana ilikua hapa tu, mwaka huu nikapewa recommendation na mtu Kuna nursery nzuri ndo nikawa nimempeleka huko, ila nimegundua nilifanya Kosa kubwa sana

Leo nimeenda shuleni nimewaambia mwanangu ataripoti saa 2 saa 8 anatoka usafiri ntamtafutia mwenyewe au nimtoe hapa, wamekubal kishingo upande
Wazazi huwa tunaangalia shule inayofanya vuzuri bila kuangalia vitu vinginr. Kuna rafiki yangu nilimshauri amwamishe mtoto shule ya karibu aachane na huo ujinga. Ndani ya miezi miwili mtoto alinenepa. Tunawapa watoto mateso sana
 
Nimerudi nyumbani kutoka mahali ninapofanyia shughuli zangu, nimekutana na kitu kinanipa mawazo sana.

Mwanangu wa kwanza (4yrs old) alikuwa anapenda shule sana, mwaka jana alikuwa anasoma shule si mbali sana na hapa, walikuwa wanatoka saa 6 mchana, sasa mwaka huu nikaona nimtafutie nursery bora angalau hata mwakani aanze la kwanza.

Aisee sasa hivi ndio nimekaa nyumbani, yapata muda kidogo wife alinambia siku hizi dogo hapendi shule, nikamwambia labda hajapata marafiki hiyo shule mpya!

Sasa hawa watoto wa nursery wanaamka saa 11:30 saa 12 gari lipo getini, kutoka shule saa 12, homework kibao, mtoto muda wote namuona kachoka.

Leo kaamshwa kwenda shule mtoto analia tu, yaani hawa watoto wana ratiba ngumu kuliko hata watumishi, hivi kweli nursery mkiwaachia saa 7 kuna tatizo gani? Wanacheza na kurelax saa ngapi hawa watoto?

Leo naenda kukiwasha shuleni, mwanangu mwisho saa 8 atakua anakuja kuchukuliwa anapelekwa nyumbani, kama hawataki poa tu nitatafuta shule nyingine, uzuri private zipo kama utitiri.

Serikali wekeni miongozo ya elimu, hwa watoto wana ratiba ngumu hata physiological sidhani kama wanafurahia shule kama miaka yetu ile.

Elimu yenyewe hii ya kuja kukutana na mishahara ya laki 4 ukitoka chuo, upuuzi tu!
Heri uvuje damu wakati wa mazoezi ili uje kutoka jasho kidogo wakati wa vita. .....ukipenda iwe kama uanvyotaka wewe au ukimuonea huruma chalii wako kuna uwezekano mkubwa wa kuja kujuta baadae
 
Siku moja nawahi usafiri nimeamka zangu saa kumi natoka nje nakutana na mwanafunzi na begi lake anaenda shule ,nilishangaa sana

Hizi elimu za sasa ni utumwa kabisa
 
Mfumo wa Elimu au ni utaratibu wa genge la watu flani wenye kupambania maslahi yao binafsi? Mimi nina jirani yangu watoto wake wanatoka nyumbani saa kumi na mbili kasoro wakiwa na mabegi makubwa mno kama kilo 15 hivi za vitabu na madaftari kila mmoja na wanarudi saa 12++ jioni kila siku mpaka jumapili! Wanasoma shule ya serikali kabisa ya msingi ya kingleza inayopatikana iringa mjini!

Elimu hasa hii ya shule ya msingi imekuwa changamoto mno yaani huko mashuleni hakuna ratiba na mwalimu yoyote anaweza kuingia muda wowote kufundisha somo lolote hii inasababisha wanafunzi kubeba madaftari yote kabisa kitu ambacho hata sisi tuliosoma zama za mawe tulikuwa tunafuata ratiba!

Tunao walimu wakuu waliochoka kufikiria wanatumia mabavu kuliko akili na kama mjuavyo walimu walivyo waoga hakuna anayeweza kukemea hili hata kama na wao linawabana kufanya mambo yao
 
Heri uvuje damu wakati wa mazoezi ili uje kutoka jasho kidogo wakati wa vita. .....ukipenda iwe kama uanvyotaka wewe au ukimuonea huruma chalii wako kuna uwezekano mkubwa wa kuja kujuta baadae
Wewe unaona Sawa?
 
Back
Top Bottom