Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 28,722
- 20,610
Ndugu zangu Watanzania,
Kuna hatari ninayoiona ikija kupitia chama cha wanasheria Wa Tanganyika yaani TLS.Naona ni kama kinataka kutolewa kutoka kuwa chama cha kitaaluma na kujigeuza kuwa chama cha siasa kali na kinachoweza kuivuruga serikali na hata kuleta Masuala yatakayochochea vurugu,chuki,uhasama na ubaguzi miongoni Mwetu kwa kupandikiza maneno ya uongo na uzushi.
Naona chama hiki kikigeuzwa kuwa pango la wanaharakati wenye nia ovu na kuvuruga amani ya Nchi yetu. naona kuna hatari chama hiki kikaanza kuwa uchochoro wa kupitishia maburungutu ya pesa chafu kwa ajili ya kufadhili na kuwafadhili watu ambao watatumika kuvurugu amani na utulivu wa Taifa Letu. Naona chama hiki kinataka kutumika kama kichaka cha kutolea matamko ya hovyo kwa mwamvuli wa TLS.
Ni Muhimu serikali ianze kutupia jicho lake la kijasusi na kiupelelezi kuangalia muenendo mzima wa shuguli za chama hiki ,kama zinafuata taratibu au ni mtu tu au kikundi cha watu na wafadhili wao nyuma ya pazia wanataka kukitumia chama hiki kwa maslahi yao binafsi kuvuruga amani ya Taifa letu
Nasema haya kwasababu nimeona chama hiki kinakoelekea siyo kuzuri kwa mstakabali mzima wa Aman na usalama wa Taifa letu. naona ni kama kinataka kitumiwe na wanaharakati uchwara na wenye ajenda ovu kwa kutumiwa na watu wenye mapesa yao kusukuma au kupenyeza ajenda zao kwa lengo ya kuivuruga serikali yetu na kuihamisha kiajenda pamoja na kuhatarisha usalama wa Taifa letu.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Kuna hatari ninayoiona ikija kupitia chama cha wanasheria Wa Tanganyika yaani TLS.Naona ni kama kinataka kutolewa kutoka kuwa chama cha kitaaluma na kujigeuza kuwa chama cha siasa kali na kinachoweza kuivuruga serikali na hata kuleta Masuala yatakayochochea vurugu,chuki,uhasama na ubaguzi miongoni Mwetu kwa kupandikiza maneno ya uongo na uzushi.
Naona chama hiki kikigeuzwa kuwa pango la wanaharakati wenye nia ovu na kuvuruga amani ya Nchi yetu. naona kuna hatari chama hiki kikaanza kuwa uchochoro wa kupitishia maburungutu ya pesa chafu kwa ajili ya kufadhili na kuwafadhili watu ambao watatumika kuvurugu amani na utulivu wa Taifa Letu. Naona chama hiki kinataka kutumika kama kichaka cha kutolea matamko ya hovyo kwa mwamvuli wa TLS.
Ni Muhimu serikali ianze kutupia jicho lake la kijasusi na kiupelelezi kuangalia muenendo mzima wa shuguli za chama hiki ,kama zinafuata taratibu au ni mtu tu au kikundi cha watu na wafadhili wao nyuma ya pazia wanataka kukitumia chama hiki kwa maslahi yao binafsi kuvuruga amani ya Taifa letu
Nasema haya kwasababu nimeona chama hiki kinakoelekea siyo kuzuri kwa mstakabali mzima wa Aman na usalama wa Taifa letu. naona ni kama kinataka kitumiwe na wanaharakati uchwara na wenye ajenda ovu kwa kutumiwa na watu wenye mapesa yao kusukuma au kupenyeza ajenda zao kwa lengo ya kuivuruga serikali yetu na kuihamisha kiajenda pamoja na kuhatarisha usalama wa Taifa letu.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.