Serikali kukutana na Mabalozi wa nchi 9 kujadili malalamiko ya Wawekezaji kuhusu masuala ya Kodi

Serikali kukutana na Mabalozi wa nchi 9 kujadili malalamiko ya Wawekezaji kuhusu masuala ya Kodi

Gemini AI

Member
Joined
May 8, 2024
Posts
91
Reaction score
265
Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, imekubali ombi la Mabalozi wa nchi mbalimbali walioomba kikao cha kujadili masuala ya kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kwa lengo la kujadili malalamiko yalitolewa na baadhi ya wawekezaji kutoka nje.

Mabalozi waliowasilisha maombi ya kikao na serikali ya Tanzania ni pamoja na wanaotoka Marekani, Uingereza, Uholanzi, Ufaransa, Ubelgiji, Canada, Korea, Sweden, na Ujerumani.

Miongoni mwa malalamiko hayo ni pamoja na makadirio ya kodi yanayozidi uhalisia hali inayosababisha baadhi ya wawekezi kupata changamoto katika uendeshaji wa biashara zao

Akijibu ombi hilo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba, alisema serikali ipo tayari kujadiliana na mabalozi hao kama walivyoomba, wakiamini kikao hicho kitakuwa na tija na kushughulikia changamoto zilizojitokeza.

“Nimekubali maombi yenu ya kikao kujadili changamoto mlizoziorodhesha na nitaandaa uwepo wa maafisa wa serikali kutoka taasisi husika kama mlivyoomba. Ili kikao kiwe na tija tunaomba wawekezaji mnaowazungumzia waje na vielelezo vya kina vya changamoto zinazowakabili”, Alisema Waziri Makamba.

Aidha, Waziri Makamba amewahakikishia Mabalozi dhamira na nia dhabiti ya Serikali ya Awamu ya Sita kuendelea kuboresha mazingira ya kibiashara nchini, ili kuvutia uwekezaji kutoka nje (FDI) kama ambavyo imefanikiwa kufanya ndani ya muda mfupi kutoka uwekezaji wa Dola za Kimarekani Bilioni 3 mwaka 2022 mpaka Bilioni 5.5 mwaka 2023.
1719595647742.png

1719595664815.png
 
Waziri wa mambo ya nje mh January Makamba amesema Serikali itakutana na Mabalozi Kujadili Changamoto za Uwekezaji

Ni mabalozi Kutoka Marekani, Uingereza, Ufaransa, Ireland, Denmark, Korea, Uholanzi, Canada, Sweden na Ujerumani

Source Mwananchi

Mlale Unono 😂😂😂
 
Wakati mwingine wa kuteketeza pesa kwa upuuzi.

Weka mazingira Bora ya uwekezaji,na wawekezaji watakuja wenyewe, Mabalozi hawana mchango wowote kwa wawekezaji, kwa sababu investor anaangalia mazingira na wala sio usharui kutoka kwa Balozi.
😂😂😂

Acha hizo 🐼
 
Waziri wa mambo ya nje mh January Makamba amesema Serikali itakutana na Mabalozi Kujadili Changamoto za Uwekezaji

Ni mabalozi Kutoka Marekani, Uingereza, Ufaransa, Ireland, Denmark, Korea, Uholanzi, Canada, Sweden na Ujerumani

Source Mwananchi

Mlale Unono 😂😂😂
Nchi imekufa hii ,alisema mbunge wa ccm mkanchuria poa
 
Wale wa kkoo na maeneo mengine mbona hamueapi response ya upesi kama hivi?
Uko sahihi

Tatizo dharau wanadharau wazawa haya waende kuongea na hao wa nje sababu wazawa wanawaona wajinga

Chalamila mkuu wa mkoa wa Dar twende kazi ulisema Tanzania inapeleka majeshi Kongo itashindwa kupeleka wanajeshi kariakoo?

Haya Sasa kahutubie mabalozi mjinga wewe kuwa kama tunapeleka majeshi Kongo tutashindwa kupeleka Kwa wawekezaji au mabalozi?

Peleka Sasa majeshi huko Kwa mabalozi na wawekezaji mjinga wewe
 
Safi Sana ndugu J. Makamba

Safi sana? Utakuwa hujielewi wewe.
Yaani watengeneze wenyewe tatizo halafu wapongezwe wanapohangaika kulitatua? Seriusly kabisa unapongeza.
Ilishadokezwa kwamba wawekezaji nao wanataka kugoma kama walivyogoma wafanyabiashara kutokana na kusumbuliwa na TRA.
Tatizo Nchi inakopa sana inaangaika kutafuta fedha wakati nyingi wanazifisadi na kuzitumia kununulia magari ya anasa

 
Mm naona tatizo sio mama tatizo ni hizi kenge alizo ziamini zinamsifia huku zinakula kama mchwa.
 
Tatizo la kodi luluki limekuwa ni janga kubwa la kudumaza uchumi.

Serekali ilitakiwa kuangalia namna ya kupunguza matumizi yake ya anasa.

Matumizi ya magari ya anasa kupita kiasi.Siku hizi kila idara au taasisi za serekali wananunua magari ya bei kubwa na hata gharama za kuyatunza ni kubwa mno.
Mfano majuzi nilikuwa Ngorongoro nilishangaa kukuta Land cruiser V8 zaidi ya 10 nikabaki kushangaa na kusikitika.
Ukitembelea taasisi zote za serekali TANROAD,TARURA,TANAPA,TAWIRI,Muhimbili,IAA,AUWSA,MURUWASA,.........utakunana na V8 za kutosha.

Wakurugenzi wa Halmashauri,Wakuu wa Wilaya,Wakuu wa Mikoa wanatumia V8.Ukienda katika mawizara yetu kuanzia Waziri,Naibu Waziri,Katibu Mkuu,Wakurugenzi,Makamishna na wakuu wa idara V8 !.

Hii ni sekta moja tu bado sijagusa seminar,Warsha,mikutano......

Watanzania tutalipa kodi mpaka damu zitukauke kwasababu ya kugharamia mambo ya kujinga,yasiyokuwa na tija,yanayoturudisha nyuma.
 
Back
Top Bottom