Serikali kuondoa udhibiti wa sukari kutoka nje kisheria. Bashe adai anaenda kuwatikisa 'Big Boys'

Serikali kuondoa udhibiti wa sukari kutoka nje kisheria. Bashe adai anaenda kuwatikisa 'Big Boys'

Asitafutwe mchawi, ni sera mbovu za serikali ya CCM katika masuala ya kiuchumi na kibiashara. Asitishie kivuli cha ruhani asiyekuwepo ambaye amebatizwa jina la kiruhani Big Boys, CCM itazidi kuaibika
Kunaweza kuwa na ka ukweli hapa, kwamba Big Boys asiyekuwepo anatwishwa gunia la misumari kumbe mchawi dola, hakuna dolare za kuagiza sukari nje!
 
Anasema anapeleka muswada bungeni kuruhusu sukari ya nje kwenye soko.

Sasa, wewe huna haki ya kumtuhumu hilo unalomtuhumu mpaka akishindwa kupeleka huo muswada bungeni.

Mfanyie haki ya kumpa muda kwanza akosee, ashindwe anachosema atafanya, akikosea, akishindwa, hapo utakuwa na haki ya kumsakama na kusema alitaka kidau kipande tu.

Ukimsakama kabla hajapeleka muswada bungeni, utakuwa unafanya tabia zenu za kulalamika kishamba tu kwa conspiracy theories bila ushahidi wala mantiki.

Wewe una tatizo la bei ya sukari. Waziri kakwambia anatatua hilo tatizo kwa kuruhusu sukari kutoka nje. Kakupa na muda maalum wa kutatua hilo tatizo, kwamba atapeleka muswada wa kubadili sheria kwenye bunge la bajeti.

Kwa nini hungojei hilo bunge la bajeti uone kitakachotokea?

Kwa nini unapenda kulalamika kwa conspiracy theories wakati jibu la uhakika utalipata kwenye bunge la bajeti?

Magafuli anaingi madarakani situation kama hii ilitokea, hatua aliyochukua ni pamoja na msako kwa wanaoficha sukari. Yeye anashindwa nn kuchukua hio hatua wakt akisubir hilo la bunge
 
Magafuli anaingi madarakani situation kama hii ilitokea, hatua aliyochukua ni pamoja na msako kwa wanaoficha sukari. Yeye anashindwa nn kuchukua hio hatua wakt akisubir hilo la bunge
Magufuli alikuwa mshamba asiyeelewa uchumi na hiyo solution yake ilikuwa ya kishamba. Huyu ndiye aliyeingusha biashara ya korosho akaiharibu, alitaka wanajeshi wabangue korosho hata kwa meno. Ujinga mtupu.

Magufuli alikuwa kama mtu mwenye nyundo ambaye tatizo lolote anaona kulitatua ni kulipiga nyundo.

Nakwambia hivi, serikali haiwezi kutatua suala la bei kwa kutumia nguvu, serikali inatakiwa kutumia akili zaidi ya nguvu.

Magufuli alikuwa anatumia nguvu zaidi ya akili.

Kutumia nguvu zaidi ya akili ndiyo hizo habari za msako wa walanguzi. Hizo habari tumezifanya tangu enzi za Sokoine na hazijawahi kufanikiwa. Ni maigizo ya kuchota akili watu wajinga wasioelewa uchumi tu.

Kutumia akili zaidi ya nguvu ni kuziachia nguvu za supply and demand zipange bei zenyewe, kwa fair competition.

Hiki ndicho Bashe anasema anaenda kufanya.
 
Wakafie mbele huko. Kama ni syndicate ya kututesa wananchi kwa kulangua sukari acha ife tu. Tunduma sukari ni 2500/- lakini ukifika Mbeya mjini ni 4800. Kwa nini watu wateseke? Wafungue mipaka sukari ya Zambia na Malawi ije kwa wingi bei zishuke.
Kabisa kama taifa limeshindwa kufanya biashara fulani waachie wengine wafanye kwa manufaa ya wananchi. Wao wanachojua ni kuvizia tu pale festoni na TRA wao na kukamata watu na bidhaa za nchi jirani hawajiulizi ni kwa nini wananchi wananunua hizo bidhaa ilihali na sisi tunazo.
 
Kwahiyo anasema hadharani hayo ili kuwatisha wenye viwanda ili wamwone au waongeze dau, kwa maana ya kwann asichukue hatua at first place ili wakilalamika yy ndiyo aje na haya majibu?
Na kwa kuwa ameshasema hadharani ni lazima aliyoyasema yaonekane yametendeka !
Short of that watu hawataacha speculations za kwamba money speaks every language !!
🙏🙏
 
Blah blah za Bashe hizo. Mnatengeneza tatizo ili mpate pa kupigia kwa kuanzisha kiwanda na shamba la Miwa kule Kilolo Iringa. Mlifanya hivyo kwenye mbolea mkaanzisha ITRACOM na Bi. Tozo sasa mnapambama ili muanzishe mashamba na kiwanda chenu cha sukari.

Wacha janja Janja, Iwezeshe kwanza TFC ili yule Mshote aache kuwadanganya wakulima.
 
Waziri Bashe akiwa Ikulu, Dar ameongelea sakata la sukari nchini.

Bashe: Wafanyabiashara wana option mbili tu, waache kuuza sukari, Serikali itatafuta option nyingine. Wenye viwanda wana option mbili, wafate utaratibu wa Serikali au waache hii kazi.

Serikali haiwezi kuruhusu, tumewaprotect vya kutosha kama nchi lakini kwa uwezo wa mwenyezi Mungu mwezi wa sita kwenye Bunge la bajeti kama waziri mwenye dhamana ninapeleka mabadiliko ya sheria kwaajili ya ku libelarize biashara ya sukari, wata- compete na competing companies kutoka nje na wenyewe watapata incentives zilizo ndani ili kuwaprotect.

Hatuwezi kuendelea na irresponsible private sector kwenye nchi kwa hali hii inayoendelea. Wakulima wa miwa wako 12,500 nchini, tutasota mwaka mmoja, mabonde yale tutayageuza ya mpunga, there is no problem.. zipo nchi ambazo zimeacha kulima sukari.

makampuni mengi nchi hii ni makanjanja, hawana hata aibu. Wanaihujumu serikali, hawabebeki. Acha soko huria ifanye kazi. Ndio maana matajiri wa nchi hii wanachukiwa sana na wananchi na walifurahia kipindi MAgu anawashughulikia. Hawana utu wala ubinadamu. Sijui ni kwa kuwa utajiri wao mwingi ni wa shirki? Wana roho mbaya kuliko shetani, ndio maana Magu aliwaambia wataishi km mashetani. Wanajilimbikizia mali ya dhuluma wakati wanaziacha hapa duniani. Washenzi kabisa, wafungiwe hizo biashara zao nao waje kuishi km mashetani
 
Si kwamba waziri anataka kuiua sekta fulani.

Waziri anawaambia watu wa kwenye hiyo sekta waache kupenda kubebwa na protectionism, ni muda kwa kushindana na bei ya sukari kutoka nje.

Waliosoma uchumi wanajua kitu kinaitwa "competitive advantage".

Anachosema Bashe ni kwamba, kama Tanzania hatuna competitive advantage katika sukari, sukari yetu ina gharama ya juu zaidi kuizalisha, tuseme labda tunazalisha kilo moja kwa shilingi 6,000, wakati wenzetu wanaweza kuzalisha kilo hiyo kwa shilingi 3,000, hapo labda inawezekana ikawa busara kuacha kuzalisha sukari, tuagize ya nje, na hiyo ardhi ya kulima sukari tulime mpunga.

Hapo hatuna "competitive advantage" katika kutengeneza sukari.

Kauli hii pia inaweza kuwa silaha ya kisiasa, kwa mfano, ikiwa waziri anajua kuwa wafanyabiashara wa sukari wanapandisha bei kwa hila, na wanaweza kabisa kupunguza bei ikawa sawa na ile ya sukari kutoka nje ya shilingi 3,000 , kwa kupunguza gharama za uzalishaji na kuondoa upandishaji bei wa kiholela wa kutafuta faida tu, kauli hii inaweza kutumika kulazimisha wadau wa sekta ya sukari kupunguza bei.

Bei ya sukari Tanzania haipo juu naturally, ipo juu artificially. Ndiyo maana sukari ya nchi jirani kama Malawi bei yake iko chini zaidi.

Serikali inafanya kitu sahihi kuruhusu sukari ya nje ije kushindana na ya ndani kwenye soko.

Hili jambo lilitakiwa kufanyika zamani sana. Naona kama wamechelewa.
Kwa umeme huu watashindana vipi bila kuwabeba labda waambiwe wafunge viwanda! Au serikali ipunguze makodi tuu!
 
Ame admit kuna 'monopoly'.

Ni hatari.

Kweli usalama wa nchi unaweza kua vibindoni mwa watu wachache. Duh
Ame admit kuna 'monopoly'.

Ni hatari.

Kweli usalama wa nchi unaweza kua vibindoni mwa watu wachache. Duh
Well iko hivi kwa muda mrefu, just tu imefumbiwa macho, ila wafanya biashara wanalifahamu hili
 
Back
Top Bottom