Serikali kutoa ruzuku ya bilioni 100 kunusuru bei ya mafuta. Yaomba mkopo IMF na Benki ya Dunia

Kufikia hiyo June mosi tayari bei ya mafuta itakuwa kwenye 3800/l.

Wakisema waondoe kodi&tozo pekee ambayo ni kama 800/l tutakuwa tunanunua kwa 3000/l.

Hii 3000/l nayo haimalizi hata wiki ipande.

Sioni umuhimu wa vyama vya siasa kugawiana ruzuku kila mwezi na hiyo misamaha ya kodi kwa taasis za dini ifutwe.

Serikali ifute kodi yote kwenye mafuta na itie 1000/l ili tuyapate kwa 2000/l mikoa na 1700/l Kwa DSM.😁.
 
"Katika mazungumzo yake kwenye kikao chetu usiku, Rais Samia alionesha kusononeshwa na kusikitishwa kwake na hata kama bei za soko la dunia ziko juu, lakini tutangulize utu na huruma na kuwajali wananchi" - January Makamba,
 
Mkuu, Mwezi ujao inawezekana bei ikapanda zaidi.

Solutions ilikuwa ni kuondoa hizo tozo za ajabu, mwisho wa siku wanasema tozo zinaenda kwenye kujenga BARABARA alafu barabara zenyewe kwa sasaivi hatuzioni wakijenga

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Tatizo wanasiasa ni wanafiki sana. Mama mwenyewe kasema mafuta yatapanda bei. Kila kitu kitapanda Bei. Na yeye ndo aliondoa hiyo 100. Na huyu huyu hangaya kasema mafuta USA yako juu kuliko Tanzania. Leo anasikitika na kusononeka.

Yaan wanaccm wanatuona wananchi wote ni mazuzu. Hawa jamaa ni wanafik sana aisee

Sent from my TECNO KG6 using JamiiForums mobile app
 
"Bei kubwa ya mafuta tuliyoishuhudia nchini sasa inatokana na bei kubwa ya mafuta duniani kuanzia mnamo mwezi Machi mwaka huu, ni bei ambayo haikuwahi kufikiwa katika kipindi cha miaka 14 sasa"
 
Utu kutoka kwa nani? MSD wamepiga ela nyingi za UVICO yaani mamilioni ya pesa bila hata huruma!

kwa nini MSD wasionyeshe utu kwa watu maskini?

Tuanzie hapo!
 
[emoji3][emoji3][emoji3] wamenishangaza sana kukopa Ili kuleta unafuu wa mafuta.
.
Siyo Wana cut expenditure na wanaendelea na expenditure zile zile ila wanaenda kukopa

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
1.* IMETOA RUZUKU YA SHILINGI BILIONI 100, ILI KUTOA AHUENI YA BEI YA MAFUTA KWA WANANCHI KUANZIA 1, JUNE 2022.

2. KURUHUSU WATU WA KUINGIZA MAFUTA KWA BEI NAFUU KUANZA MAFUTA NA GHARAMA ITAPUNGUA TENA AGOSTI 2022

3. KUANZISHWA KWA MFUKO WA KUKABILIANA NA MFUMUKO WA BEI YA MAFUTA (FUEL PRICES STABILIZATION FUND)

4. KUANZISHA UTARATIBU WA KUHIFADHI MAFUTA YA KIMKAKATI.

5. KUJENGA MAGHALA MAKUBWA YA KUHIFADHI MAFUTA KWA AJILI YA KUUZA NDANI NA NJE YA NCHI.

6. KUANZA UPOKEAJI WA MAFUTA KATIKA GHALA MOJA (SINGE RECEIVING TERMINAL), ILI KUPUNGUZA MUDA WA MELI KUSUBIRI PINDI INAPOLETA MAFUTA AMBAPO NAYO ILIKUA SABABU YA KUPANDA KWA GHARAMA ZA BEI YA MAFUTA.

7. KUONGEZEWA UWEZO WA TAASISI YA TPDC ILI KUFANYA BIASHARA YA MAFUTA.

8. KUBORESHA UTENDAJI KAZI WA TAASISI ZINAZOJIHUSISHA NA MASUALA YA MAFUTA IKIWEMO EWURA.

#KaziIendelee
#TanzaniaSalamaNaSamia
#SisiTumekubali
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…