Serikali kutodhibiti idadi ya wageni wanaoingia nchini kwa kisingizio cha Utalii, inahatarisha Usalama wa Taifa dhidi ya virusi vya Corona

Hili si jambo la dhana ni jambo la uhakika! Ndio Mana aliyekoment aliomba uthibitisho iwapo watalii ni wale wa WUHAN?



Sent using Jamii Forums mobile app
CHINA yote sio salama ndugu, maambukizi mapaya yanagunduliwa kila siku hata nje ya Wuhan, wewe unasema mpaka wawe wametokea Wuhan? Tanzania ina akili na wataalamu sana kuliko nchi nyingine zilizopiga marufuku raia wa China kuwasili nchini kwao?
 
Slay Queen ukipata tu huchukui round ni 14 days tu dalili zinaonesha,utakohoa wewe mpaka watu watakushtukia tu
Bora slay Queen nitafikisha hata siku 14, wewe Marioo siku 3 tu tushakula ubwabwa ya nne tumekusahau umekua chakula cha funza.
 
CHINA yote sio salama ndugu, maambukizi mapaya yanagunduliwa kila siku hata nje ya Wuhan, wewe unasema mpaka wawe wametokea Wuhan? Tanzania ina akili na wataalamu sana kuliko nchi nyingine zilizopiga marufuku raia wa China kuwasili nchini kwao?
Naona umemuacha mtoa koment umeamua kula sahani moko na mimi kwa vihoja vyako uchwara;

China inaongoza kwa idadi ya watu duniani ikikadiriwa kuwa na 1,409,641,539 sasa vifo ss vimefikia 2500 na maambukizi yanayokadiriwa kuwa 80,000 unadhani ni wastani wa wachina wangapi katika ratio hapo.

Media zimeamua kuzua taharuki ambayo si sahihi sana badala ya kujikita kwenye kutafuta dawa.

Akili za kuambiwa changanya na zako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haya, kwa hiyo hao waliosambaza huo ugojwa nchi nyingine walisamabazaje kama wachina walioathirika ni wachaceh kiasi hicho? Huo mji wa Wuhan upo kwenye karantini , lakini bado maambukizi yanaenea, huo ugonjwa unaeneaje? nakuuliza hivi hao majirani wa China kama vile Urusi ambao wamepiga marufuku Wachina nchini kwao hawana akili? Austaralia, New zealand, Ufilipino, Singapore etc ambao wote hawa wamepiga marufuku raia wa China, hawa hawana akili? manawazidi kwa teknolojia na wataalamu dhidi ya huu ugonjwa? unajua athari tu ya mtu mmoja mwenye maambukizi kutua Tanzania?

Unafahamu nguvu ya kuenea kwa huu ugonjwa ama unauikia tu juu kwa juu?
 
Watalii wapi hao,wamejaa kariakoo huko wengine ni machinga na wanavitambulisho vya Magu kabisa,ni wawekezaji wetu a.k.a Machinga.

Soon Corona itatua bongo maana Nigeria tayari na sisi hatuna tahadhari yoyote
 
Ngozi nyeusi haiwezi kufa kwa huo ugonjwa wa CORONA ukiambukizwa CORONA wee kunywa Allkasusu na nyama ya kukaanga ya nguruwe aka mdudu kinga hii

Sent from my iPhone 12 using Jamiiforums App
 
Ina uma Sana ndugu Zanguni

Imagine Mwanao yupo China amekataliwa kuja Tanzania Wakati huo huo Nchi inapokea Watalii kutoka kutoka huko huko China

Mbona Mnatufanyia hivi Serikali ya Awamu ya Tano ??

Mnataka tufe Kama kuku waliovamiwa na Mdondo ??
Angalia Kenya walivyoserious na hizi issue ila Tanzania kimya as nothing happened.
 

Attachments

  • IMG-20200228-WA0018.jpg
    60.1 KB · Views: 2
Ikiwa jambo kubwa kama kuhiji lakini saudia ikapiga marufuku watu kuingia nchini mwao ili kuudhibiti ugonjwa sisi tamaa tumeweka mbele tunakaribisha mamia ya wachina ukilipuka hapa sijui tutakimbilia wapi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu huu ugonjwa ukiripuka hapa Tz nakuhakikishia tutakufa kama kuku wenye mdondo. Kama kusambaza madawa tu ya malaria nchi nzima ni tatizo how do you think the government will be able to prevent and eradicate such a contagious and deadly CONV?
angalia video niliyoiambatanisha wenzetu wachina wanavyofight against it na bado madhala makubwa yanazidi kuwakumba. Wanatumia njia ambazo ziko very advanced in some how we can't afford them.
Nawaza na kuhuzunika mpaka kichwa kinauma.
 

Attachments

  • VID-20200227-WA0077.mp4
    10.9 MB
Tanzania ni ya waTanzania sio ya ccm wala ya viongozi, hawa tuliowapa madaraka wanapaswa kufuata matakwa yetu, kama wanataka kuwaingiza wachina basi wawarudishe wale waTanzania waliopo china kwanza.
 
Nimeangalia hii video nasikitika namna tulivyo na ujinga wa kupindukia. Dunia nzima inahaha na huu ugonjwa na wanajitahidi kuzuia wasafiri kutoka China.

Sisi kwa ujinga wetu tunajisifu kupokea wachina wengi. Let not be fooled by prosperous tourism industry citzens first.

Ugonjwa ukilipuka hapo hautachagua chama. let work together, raise voice.

Serikali kama haioni umuhimu wa maisha yetu basi tunafaa kuikumbusha kutumia akili. Yaani polepole ndo wakuja kuzungumzia masuala sensitive kama coronavirus kweli.

Halafu tunajisifu eti watalii wameongezeka. Gharama za huu ujinga zitakuwa kubwa sana tusipo zuia leo. Mark my word.

Swali ni kuwa huyu jamaa hajasikia kabisa hatari ya huu ugonjwa kweli?. Poor Africa, poor Tanzania.

Your browser is not able to display this video.
 
Reactions: PNC
kweli maviongozi yetu ni majinga sana
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukiingia Tanzania tutaanza tafutana.Mask,gloves,vifaa vingine,vipimo,vitanda,kutibu dalili.Yaani itakuwa mass extinction.
 
Ukiingia Tanzania tutaanza tafutana.Mask,gloves,vifaa vingine,vipimo,vitanda,kutibu dalili.Yaani itakuwa mass extinction.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…