Wakuu nchi haina dini hii, mimi mitihani yangu mingi sana nimefanya jumapili na wala sikulalamika kwakua nililijua hiloSidhani kama ni fahari kutamba kuwaumiza watu wa Imani nyingine kwa sababu tu wamesimamia misingi ya Imani yao,, na umewataja kabisa waliohusika kuwasitishia masomo. Huyo Padri alipata faida gani. Serikali inatakiwa kulizingatia hili.
Ingekuwa secular state ingepanga Jumapili pia. Lakini kama Jumapili shughuli za kiserilali zinasimama unasemaje ni secular state ?Kwani kuna sehemu serikali imekukataza kuabudu siku yako ya sala?
Serikali imeweka siku ya usaili ni jumamosi, Kama mtu ataona ibada ni muhimu kuliko usaili. Aende ibadani.
Serikali haiwezi kuacha kufanya mambo yake kwa kigezo cha dini za watu.
Tanzania ni secular state.
Nakwambia hivi 👇Kama ungekuwa unatumia Logical ya kawaida ungeelewa kuwa kuweka Siku ya usaili katika siku ya ibada ungeona ni kumkataza mtu indirectly asiende kuabudu. Ni vile hujataka kuifikirisha akili yako.
Kama kanisa ni muhimu kwako nenda kanisani.Au mtu anaweza kujigawa mara mbili. Wakati huohuo awe Kanisani na wakati huohuo kwenye Usaili?
Serikali imepanga siku ya usaili kuwa jumamosi.Bado unasema serikali haijazuia mtu kuabudu? Unatumia akili yako sawasawa
Ambacho huelewi ni kipi hapo?Unajua maana ya Secular State?
Mtoto wa Shule ninayejua mambo makubwa kukuzidi wewe mkubwa. Mimi ni genius!
Waislamu usiwaingize humu. Jiteteeni peke yenu. Waislamu Ijumaa wanaingia kazini kama kawaida. Saa sita na nusu wanaenda Masjid. Ukiwaambia baada ya Swala warudi kazini, hawana noma wala nini. Wanarudi na wanachapa kazi kama kawaida! Ninyi Wasabato ni kimeo!!!Lakini huo ni udini
Waislam nao vivyohivyo watasema hayo.
Walokole nao vivyohivyo!
Unajua matokeo yake?
Na ndicho anachosema Heriel. Kumbe kwa kuwashughulikia hao Wasabato kimkakati na kuwatesa kimasomo wakapanda vyeo.Father Dk. Kitima sasa hivi Katibu wa TEC (sijui unaijua?)? Na Dk. Mfumbusa sasa hivi ni Askofu wa Jimbo la Kondoa. Wamepata zaidi ya kile walichokuwa nacho kipindi wanawashughulikia hao Wasabato.
Hawa wasabato ni kakundi kadogo sana ka watu wasiojielewa. Yesu alishaweka sabato mpya wao wapowapo tu kufata uongo wa Hellen G White.Serikali kuweka siku ya jumamosi kuwa siku ya Usaili ni kuwakosea HAKI Wahitimu waumini wa kisabato.
Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli
Sabato Njema. (itikia Njema Sana).
Wahitimu wa kisabato wanasikitika baada ya baadhi Yao kukosa kwenda kwenye Usaili kutokana na siku iliyowekwa kwaajili ya Usaili ni siku ya ibada. Sikukuu ya Mungu wao wanaomuamini.
Ikumbukwe kuwa Sabato kwa waumini wa kisabato ni Moja ya amri kubwa na kuu wanaamini wameagizwa kuifuata na Mungu wao wakirejelea Torati ya Musa katika Biblia, katika Kutoka 20:8-11
Tunafahamu kuwa serikali huenda ilifanya kwa bahati mbaya kwa kusahaukundi hili la Wasabato. Na hatutaki kuamini kuwa imefanywa makusudi bila kujali au kwa kudharau Wasabato kwa Sababu zozote zile.
Wasabato sio Watu wakujihusisha na mambo ya siasa na kiserikali na hii huenda ni Moja ya sababu ya wao kusahaulika hata kwa mambo muhimu kama ya Ajira.
Mimi Kama Taikon Master, ambaye ni Msabato. Baada ya kupewa taarifa hiyo kwa kweli nilisikitika Sana. Nikaona kuinyamazia inaweza kujirudia na kuwafanya Wananchi wa Kitanzania, wanaoabudu katika dhehebu la Wasabato wanaweza kukosa Haki Yao kwa wakati Mwingine.
Serikali kupitia Wizara husika, ifuatilie Jambo hilo na kulifanyia marekebisho.
Taikon Acha nipumzike sasa.
Kesho tukutane, KANISA LA MWENGE SDA, DAR ES SALAAM.
SABATO NJEMA
Serikali ndio yenye maamuzi. Kulingana na ratiba zake.Ingekuwa secular state ingepanga Jumapili pia. Lakini kama Jumapili shughuli za kiserilali zinasimama unasemaje ni secular state ?
🙋♂️✍️🎯👍🤝🙏💐🎁Serikali kuweka siku ya jumamosi kuwa siku ya Usaili ni kuwakosea HAKI Wahitimu waumini wa kisabato.
Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli
Sabato Njema. (itikia Njema Sana).
Wahitimu wa kisabato wanasikitika baada ya baadhi Yao kukosa kwenda kwenye Usaili kutokana na siku iliyowekwa kwaajili ya Usaili ni siku ya ibada. Sikukuu ya Mungu wao wanaomuamini.
Ikumbukwe kuwa Sabato kwa waumini wa kisabato ni Moja ya amri kubwa na kuu wanaamini wameagizwa kuifuata na Mungu wao wakirejelea Torati ya Musa katika Biblia, katika Kutoka 20:8-11
Tunafahamu kuwa serikali huenda ilifanya kwa bahati mbaya kwa kusahaukundi hili la Wasabato. Na hatutaki kuamini kuwa imefanywa makusudi bila kujali au kwa kudharau Wasabato kwa Sababu zozote zile.
Wasabato sio Watu wakujihusisha na mambo ya siasa na kiserikali na hii huenda ni Moja ya sababu ya wao kusahaulika hata kwa mambo muhimu kama ya Ajira.
Mimi Kama Taikon Master, ambaye ni Msabato. Baada ya kupewa taarifa hiyo kwa kweli nilisikitika Sana. Nikaona kuinyamazia inaweza kujirudia na kuwafanya Wananchi wa Kitanzania, wanaoabudu katika dhehebu la Wasabato wanaweza kukosa Haki Yao kwa wakati Mwingine.
Serikali kupitia Wizara husika, ifuatilie Jambo hilo na kulifanyia marekebisho.
Taikon Acha nipumzike sasa.
Kesho tukutane, KANISA LA MWENGE SDA, DAR ES SALAAM.
SABATO NJEMA
Nakubaliana na wewe serikali ina maamuzi ,, Ipange hiyo Jumapili basi hata kwa bahati mbaya tuone. Kama sivyo inakuwa ni mkakati na makusudi.Serikali ndio yenye maamuzi. Kulingana na ratiba zake.
Hata ikiamua kupanga jumapili, Ijumaa au jumamosi ni sawa.
Wewe raia ndio utaamua kipi kina umuhimu kwako, ibada au kazi.
Kipindi hicho nikisoma hapo kina "Mzee" mmoja Msabato akivaa mashati meupe pee na tai. Very smart. Yeye baada ya kuona hapo SAUT mambo ya Kisabato yamekuwa magumu, aliomba kuhamia Chuo Kikuu cha Wasabato kile Cha Arusha.Na ndicho anachosema Heriel. Kumbe kwa kuwashughulikia hao Wasabato kimkakati na kuwatesa kimasomo wakapanda vyeo.
Ibada sio tuu muhimu kwa mtu binafsi Bali hata kwa Serikali yako hiyo ambayo wewe unasema ni Secular lakini hujui maana hata ya hiyo istihali.Nakwambia hivi 👇
Serikali haiwezi kuacha kufanya kazi zake kwa kigezo cha dini za watu.
Kama ibada ni muhimu kwako nenda ibadani.
Kama usaili ni muhimu kwako nenda kwenye usaili.
Yani wewe huna tofauti na muislamu aje kulalamika hapa usaili kuwekwa Ijumaa.
Sasa kila mtu akitaka serikali ifanye vitu kwa kuangalia imani yake, shughuli zitaenda kweli?
Si kila mtu atataka upendeleo kwenye imani yake.
Wewe ndio hutumii logical ya kawaida.
Kama kanisa ni muhimu kwako nenda kanisani.
Kama usaili ni muhimu kwako nenda kwenye usaili.
Serikali haiwezi kuvuruga ratiba yake kwa kigezo cha dini au imani yako.
Serikali imepanga siku ya usaili kuwa jumamosi.
Halafu wewe unaleta imani zako kwenye mambo ya kiserikali.
Una utimamu kweli wewe?
Au unafikiri serikali ni kanisa au msikiti?
Ambacho huelewi ni kipi hapo?
Kwamba Hujawahi kusikia neno secular state.
Au unataka ufafanuzi gani zaidi?
Hawa wasabato ni kakundi kadogo sana ka watu wasiojielewa. Yesu alishaweka sabato mpya wao wapowapo tu kufata uongo wa Hellen G White.
🤔 🤔 🤔Hawa wasabato ni kakundi kadogo sana ka watu wasiojielewa. Yesu alishaweka sabato mpya wao wapowapo tu kufata uongo wa Hellen G White.
Kwani serikali yenyewe si inatambua siku za kazi kuwa ni Jumatatu hadi Ijumaa?Na waislam wakisema ijumaa iwe mapumziko hii nchi itaendelea? Punguzeni upuuzi
Unaijua katiba ya nchi? Unajua kama katiba inatambua na kuheshimu dini za raia wa Tz?Samahani,naomba ushahidi kuwa Jumamosi ni siku ya saba na ni siku ya sabato.Jibu ukitumia 'common sense' plus fikra tunduizi.Zingatia neno Jumamosi
Vipi wale wanaobadu Ijumaa, Jumapili,Jumatatu n.k?? Punguza ubinafsi na kujiona ninyi ni so special!
Kama wewe ni Mkristo na unasoma Biblia utazikuta hizo sheria kwenye biblia. Hazikuanzishwa na Ellen.Mwongozo wao unawataka wakaswali mida wa swala lakini wengine wanakua kwenye majukumu wanashindwa. Wasabato punguzeni kujidekeza utadhani mbingu mmeandikiwa nyie tu kumbe hellen na kikundi chake ndo watunga sheria zote hizo
Dr. Ulisubyisa Mpoki, Chief Executive Officer of the Muhimbili Orthopaedic and Neurosurgery Institute (MOI), aligoma kufanya mitihani siku ya sabato wakati anasoma chuo miaka hiyo. Igeni mfano wake.
Kwani mkuu wewe siku zako unazitofautishaje? Au zote ni Jumatatu? Na ni mfumo gani umeamua kufuata?Hujatumia common sense, kama ungetumia hizo siku plus kalenda ni utashi wa watu na siyo Mungu.Onyesha sehemu yoyote Mungu anataja majina ya siku.