DOKEZO Serikali tusaidieni wananchi, magari yanayouzwa kwenye yard za Wapakistan mitaa ya Morocco na Victoria ni mabovu sana

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Wewe ni sehemu ya tatizo.

Hizo picha ulitakiwa kwenda nazo moja kwa moja polisi na TAKUKURU kuzipeleka kama vielelezo.

Badala yake umechukua milioni moja ya rushwa, kisha unaitaka serikali ichukue hatua.

Serikali inatakiwa kuanza kuchukua hatua kwako wewe kwa kula rushwa iliyoharibu ushahidi.
 
Ukienda kwenye yard kununa gari wewe nenda na fundi wako unayemuamini aangalie engine, gear box na body kama vipo vizuri . Ukienda na fundi janja janja mpenda pesa atakuchomesha atachukua pesa kwako na kwa hao wauza magari kwani kuna ishara atapewa arudi baadae kuja kuchukua mzigo wake. Hiyo habari ya km achana nayo kabisa utapotea. Unakuta gari ya mwaka 1995 imeletwa hapa kwetu 2022 halafu eti imetembea km 10,000 si maajabu hayo.
 
TBS wapo busy kukimbizana na akina mama walala hoi pale Kasumulu border, wanaohangaika na vibiscuits!,hii nchi ni shida kila kona!,pls my IGP chukua hawa police wako peleka Botswana,even for a 14days waone wenzao wanavyofanya kazi ,Tanzania bila RUSHWA INAWEZEKANA, why Gaborone wamefanikiwa kwa hili?,Zambia wanasogea nao kuwa wasafi sisi tumekwama wapi
 
Whistle blower nimesha fanya kazi yangu na wao serikali wafanye kazi yao
 
Mchawi wetu utawala wa CCM. CCM ina urafiki mkubwa sana na rushwa
 
Whistle blower nimesha fanya kazi yangu na wao serikali wafanye kazi yao
Wewe si whistle blower, wewe ni selfish and greedy Tanzanian.

Whistle blower angepeleka ushahidi polisi na TAKUKURU.

Wewe ni mmoja ya walioshiriki kuwawezesha hao watu kufanya biashara yao chafu.

Tena sasa hivi watafanya kwa umakini zaidi, kwa sababu umeshawastua. Umefanya iwe vigumu zaidi kuwakamata.

Umewauza wenzako kwa vipande vya fedha.

Wewe ni mla rushwa na msaliti.
 
Kwani yale maduka yamefunguliwa jana? Si yapo miaka nenda rudi? Mbona hawajawahi kamatwa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…