Uchaguzi 2020 Serikali ya Marekani yaonya "Vitisho na mabavu dhidi ya upinzani si dalili nzuri ya Uchaguzi Huru Tanzania Oktoba 2020"

Tunamulikwa kwa taa yenye mwanga mkali mno. Tulistulia kwa Makonda kufungiwa kwenda USA tukatia kejeli sasa tena tunakumbushwa.
CCM mtashinda uchaguzi huu bila shaka yoyote, ondoeni mikono yenu kwenye vyombo vya dola ili tuwasaidie kushangilia ushindi na kuwazomea walioshindwa.
 
USA linaendelea kuwa taifa kubwa na la hovyo sana dunia, kila siku kutoa matamko ya siyo kuwa na kichwa wala miguu.

Walionya na kutoa tamko la kuhusu corona kiko wapi? Watuache nani huwa anaingila mambo yao wao ya ndani? Ukitaka kujua USA wakati mwengine ni wajinga angalia aina ya rais waliye naye wakati huu.
 
Mwenye masikio na asikie!
 
Ukishakuwa muumini wa ushoga hata akili zinapukutika. USA linaendelea kuwa taifa kubwa na la hovyo sana dunia, kila siku kutoa matamko ya siyo kuwa na kichwa wala miguu...
Lazima wakuingilie sababu wao ndio wanakulisha. Kila siku mnapeleka bakuli huko halafu mnataka wawaache tu mfanye upuuzi?

Mkitaka msiingiliwe msiende kukopa wala kuomba, na madeni yote ya nyuma mlipe. Mkifanya hivyo mtakuwa free country na mtafanya mtakayo, mkiamua hata kuubeba mlima Kilimanjaro to Chato watakaa kimya
 
Amini nawaambieni TL anajua kabisa hawezi kushinda ila mabwana zake wanachotaka ni kuona vurugu za kisiasa tu Tz

sasa mpaka sasa upinzani umekandamizwa wap?

Na tuendelee na moyo huo wa kutokandamizana. Tuwakemee wale wahuni wachoma ofisi Arusha, watupa mawe Hai, na yule polisi Mbeya.

Tuwakemee wote wa aina hii washindwe na walegee.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…