Serikali yakwama ujenzi Mji mpya wa NSSF Dege Eco Village Kigamboni, yatangaza kuuza mradi

Serikali yakwama ujenzi Mji mpya wa NSSF Dege Eco Village Kigamboni, yatangaza kuuza mradi

Hapana.jpm alitaka kuwashughulikia walioufisadi bahati mbaya akatutoka.kwa sasa mafisadi wamerudi na wanataka wajiuzie wao ili waendeleze kunufaika hao mafisadi
Acha porojo wewe...

Yaani since 2016 hadi 2020 bado tu "alitaka kuwashughulikia"?!

Btw, kama ambavyo aliwahi "kumshughulikia" mnene yupi serikalini na taasisi zake?!

Na kama alitaka kuwashughulikia kwavile aliona kuna ufisadi, ilikuaje tena DG wa NSSF akampa Ubalozi na kumpeleka Malaysia?!

Hivi mtaendelea kudanganyana hadi lini?!

Magu HAKUWA na guts za kushughulikia watu wazito... yeye aliishia ku-deal na civil servants tu tena wale ambao hawajafikia ministerial level.

Ukiondoa hao, gut yake nyingine ilikuwa kwa BAADHI tu ya Wafanyabiashara manake watu kama Rostam Azizi aliendelea kugonga nao cheers kama kawaida!!
 
Hizi pesa za wafanyakazi ni za kuchangia wajanja wachache wafanye miradi ya ujanja ujanja kama hii kwa malengo ya kujitajirisha huku wastaafu wakisota kupata mafao yao na kubanwa na kikokotoo......nchi ya kindezi sana hii.
Aliyeshiba hamjui mwenye njaa !! Tutabaki tunasema Lakini Mungu yupo !!
 
View attachment 2398070

Baada ya kusuasua kukamilika kwa mradi wa Dege Eco Village kwa thamani ya dola 653 milioni za Marekani (zaidi ya Sh1.3 trilioni), Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) lililokuwa linautekeleza limetangaza kuuza kwa mwekezaji mwingine atakeyevutiwa nao.

Ujenzi wa mradi huo wa mji mpya wa Kigamboni jijini Dar es Salaam ulioanzishwa na NSSF mwaka 2014 ulisimama tangu Januari 2016 ukidaiwa kufisidi zaidi ya Sh179 bilioni hivyo kutokamilika kwa nyumba za kifahari, hoteli, maduka makubwa, eneo la wazi la mapumziko, baa, shule, hospitali, kumbi za mikutano, nyumba za ibada na migahawa.

Taarifa iliyosainiwa na Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Masha Mshomba na kusambazwa Jumanne Oktoba 25 imetangaza kutafutwa kwa mzabuni atakayeuendeleza mradi huo.

“NSSF inakusudia kuuza mradi mzima wa Dege Eco Village, shirika halitowajibika tena baada ya mauzo haya. NSSF inakaribisha zabuni zilizofungwa kuununua mradi huu kwa viwango vya kimataifa vilivyoainishwa kwenye Kanuni za Ununuzi wa Umma zilizochapishwa kwenye gazeti la Serikali namba 446,” inasomeka sehemu ya taarifa ya NSSF.

Kwa wawekezaji watakaovutiwa kuuendeleza mradi huo uliosimama kwa miaka saba sasa, NSSF imesema wanaweza kuutembelea huko Rasi ya Dege iliyopo Kigamboni jijini hapa ili kuukagua na kujiridhisha na mandhari yake kuanzia saa 4:00 asubuhi mpaka saa 7:00 mchana wa Novemba 3.

Zabuni zote, shirika hilo limesema zinapaswa kuwasilishwa mpaka Novemba 14, saa 9:00 alasiri kabla hazijafunguliwa mbele ya waombaji wote watakaokuwa wamejitokeza kwenye ukumbi wake uliopo ghorofa ya saba katika Jengo la Benjamin William Mkapa.

View attachment 2398094

Pia, soma=> Dar: Mradi wa Dege Eco village uliotelekezwa Kigamboni
lini NSSF na mashirika mengine ya umma yakafanya biashara ndugu zangu kama si mwanya wa kufisadi michango ya wanachama wao maskini as a result.

Kwa mfano Daraja la Kigamboni wanashindwa nini kumtafuta mzabuni aendeshe pale wao wakusanye pesa, rather than wao wenyewe ku-run... wana ujuzi gani wa kukusanya mapato hawa NSSF ? walisomea wapi ?
 
Acha porojo wewe...

Yaani since 2016 hadi 2020 bado tu "alitaka kuwashughulikia"?!

Btw, kama ambavyo aliwahi "kumshughulikia" mnene yupi serikalini na taasisi zake?!

Na kama alitaka kuwashughulikia kwavile aliona kuna ufisadi, ilikuaje tena DG wa NSSF akampa Ubalozi na kumpeleka Malaysia?!

Hivi mtaendelea kudanganyana hadi lini?!

Magu HAKUWA na guts za kushughulikia watu wazito... yeye aliishia ku-deal na civil servants tu tena wale ambao hawajafikia ministerial level.

Ukiondoa hao, gut yake nyingine ilikuwa kwa BAADHI tu ya Wafanyabiashara manake watu kama Rostam Azizi aliendelea kugonga nao cheers kama kawaida!!
Nadhani alitaka kwanza kupata uhakika wa kuwepo madarakani kwa muda mrefu zaidi ndipo angekuwa na uhakika wa kuwashughulikia hao magwiji aliokuwa anazijua habari zao !! Nadhania tu. !!!
 
View attachment 2398070

Baada ya kusuasua kukamilika kwa mradi wa Dege Eco Village kwa thamani ya dola 653 milioni za Marekani (zaidi ya Sh1.3 trilioni), Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) lililokuwa linautekeleza limetangaza kuuza kwa mwekezaji mwingine atakeyevutiwa nao.

Ujenzi wa mradi huo wa mji mpya wa Kigamboni jijini Dar es Salaam ulioanzishwa na NSSF mwaka 2014 ulisimama tangu Januari 2016 ukidaiwa kufisidi zaidi ya Sh179 bilioni hivyo kutokamilika kwa nyumba za kifahari, hoteli, maduka makubwa, eneo la wazi la mapumziko, baa, shule, hospitali, kumbi za mikutano, nyumba za ibada na migahawa.

Taarifa iliyosainiwa na Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Masha Mshomba na kusambazwa Jumanne Oktoba 25 imetangaza kutafutwa kwa mzabuni atakayeuendeleza mradi huo.

“NSSF inakusudia kuuza mradi mzima wa Dege Eco Village, shirika halitowajibika tena baada ya mauzo haya. NSSF inakaribisha zabuni zilizofungwa kuununua mradi huu kwa viwango vya kimataifa vilivyoainishwa kwenye Kanuni za Ununuzi wa Umma zilizochapishwa kwenye gazeti la Serikali namba 446,” inasomeka sehemu ya taarifa ya NSSF.

Kwa wawekezaji watakaovutiwa kuuendeleza mradi huo uliosimama kwa miaka saba sasa, NSSF imesema wanaweza kuutembelea huko Rasi ya Dege iliyopo Kigamboni jijini hapa ili kuukagua na kujiridhisha na mandhari yake kuanzia saa 4:00 asubuhi mpaka saa 7:00 mchana wa Novemba 3.

Zabuni zote, shirika hilo limesema zinapaswa kuwasilishwa mpaka Novemba 14, saa 9:00 alasiri kabla hazijafunguliwa mbele ya waombaji wote watakaokuwa wamejitokeza kwenye ukumbi wake uliopo ghorofa ya saba katika Jengo la Benjamin William Mkapa.

View attachment 2398094

Pia, soma=> Dar: Mradi wa Dege Eco village uliotelekezwa Kigamboni
Kama wanauza kiwepo kiwango cha chini kitakachohakikisha fedha ya umma ie nssf inarudi. Vinginevyo tutaona wizi wa mali ya umma kwa mradi kuuziwa mhuni au wahuni fulani kwa bei ya kutupa. Serikali isiachie bodi ya nssf maana ufisadi ndio unatawala shirika hilo.
Hebu tujiulize ni nani aliingia mradi huu na ilikua kwa faida ya nani?
Magufuli alipoamua nyumba za mradi huo ziwe hosteli za vyuo vikuu, je sio ndio ulikua uamuzi bora kuliko risk ya kuporwa mradi na fisadi kwa kujidai wanauza au kununua mradi?
Je si bora nyumba hizo kuuziwa wananchi kwa bei nafuu maana ujenzi wake umejaa gharama za upigaji wa wakurugenzi na management ya nssf?
 
Kila alipojitahidi kuwakamata mnadai hawapendi matajiri anakinyongo nao,akina Manji wote walifirisi NSSF kwa kukopa, lakini Magufuli alivyoanza kumshugulikia makelele kibao,akina Lugemalira wa IPTL walipigiwa kelele na akina Lissu bungeni, lakini Magufuli alivyoanza kuwashugulikia mkaanza kusema wanaonewa, Watanganyika kwa unafiki hawajambo.
Kwani hizo kelele lini zilimzuia kuwakamata? Na kwanini hakuwashughulikia akina dau basi kama ni kweli maana akina manj kama waliiba nssf basi walishirikiana na bodi ya nssf.
 
🤣🤣🤣kaka Pascal PPR itaweza hiyo ligi kweli?hapo tayari wakubwa washapangana,DG anakamilisha tu maandalizi ya mchezo.PPR jikite kwenye low cost housing,maeneo ya Kibaha,Kimara Bonyokwa,Kirungure,Mkuranga,Vianzi.nk.
Kutakatisha!!
 
Mpaka wakasema wanaboresha kikokotoo kumbe pesa hamna zimeishia kwenye magofu
 
Kama wanauza kiwepo kiwango cha chini kitakachohakikisha fedha ya umma ie nssf inarudi. Vinginevyo tutaona wizi wa mali ya umma kwa mradi kuuziwa mhuni au wahuni fulani kwa bei ya kutupa. Serikali isiachie bodi ya nssf maana ufisadi ndio unatawala shirika hilo.
Hebu tujiulize ni nani aliingia mradi huu na ilikua kwa faida ya nani?
Magufuli alipoamua nyumba za mradi huo ziwe hosteli za vyuo vikuu, je sio ndio ulikua uamuzi bora kuliko risk ya kuporwa mradi na fisadi kwa kujidai wanauza au kununua mradi?
Je si bora nyumba hizo kuuziwa wananchi kwa bei nafuu maana ujenzi wake umejaa gharama za upigaji wa wakurugenzi na management ya nssf?
Unawaza ki masikini sana
Jifunze kuwaza kibiashara
 
🤣🤣🤣kaka Pascal PPR itaweza hiyo ligi kweli?hapo tayari wakubwa washapangana,DG anakamilisha tu maandalizi ya mchezo.PPR jikite kwenye low cost housing,maeneo ya Kibaha,Kimara Bonyokwa,Kirungure,Mkuranga,Vianzi.nk.
PPR kama PPR haiwezi, bali una download tender documemts na ku parter na wanene, wao ndio watafanya kila kitu, wewe unakuwa local partner.
P
 
Purchasing power ya Wa Tanzania ni ndogo sn especially kwenye really Estate kupata muwekezaji DEGE ni ndoto ya asubuhi wewe Tazama tu palm village wanavyo hangaika kuuza apartments zao ndio utajua soko lipoje Tz mifano ipo mingi tizama yale majengo ya PSPF asilimia kubwa yapo wazi Tena City center huko ni Mji kama umekufa kabisa.
 
View attachment 2398070

Baada ya kusuasua kukamilika kwa mradi wa Dege Eco Village kwa thamani ya dola 653 milioni za Marekani (zaidi ya Sh1.3 trilioni), Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) lililokuwa linautekeleza limetangaza kuuza kwa mwekezaji mwingine atakeyevutiwa nao.

Ujenzi wa mradi huo wa mji mpya wa Kigamboni jijini Dar es Salaam ulioanzishwa na NSSF mwaka 2014 ulisimama tangu Januari 2016 ukidaiwa kufisidi zaidi ya Sh179 bilioni hivyo kutokamilika kwa nyumba za kifahari, hoteli, maduka makubwa, eneo la wazi la mapumziko, baa, shule, hospitali, kumbi za mikutano, nyumba za ibada na migahawa.

Taarifa iliyosainiwa na Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Masha Mshomba na kusambazwa Jumanne Oktoba 25 imetangaza kutafutwa kwa mzabuni atakayeuendeleza mradi huo.

“NSSF inakusudia kuuza mradi mzima wa Dege Eco Village, shirika halitowajibika tena baada ya mauzo haya. NSSF inakaribisha zabuni zilizofungwa kuununua mradi huu kwa viwango vya kimataifa vilivyoainishwa kwenye Kanuni za Ununuzi wa Umma zilizochapishwa kwenye gazeti la Serikali namba 446,” inasomeka sehemu ya taarifa ya NSSF.

Kwa wawekezaji watakaovutiwa kuuendeleza mradi huo uliosimama kwa miaka saba sasa, NSSF imesema wanaweza kuutembelea huko Rasi ya Dege iliyopo Kigamboni jijini hapa ili kuukagua na kujiridhisha na mandhari yake kuanzia saa 4:00 asubuhi mpaka saa 7:00 mchana wa Novemba 3.

Zabuni zote, shirika hilo limesema zinapaswa kuwasilishwa mpaka Novemba 14, saa 9:00 alasiri kabla hazijafunguliwa mbele ya waombaji wote watakaokuwa wamejitokeza kwenye ukumbi wake uliopo ghorofa ya saba katika Jengo la Benjamin William Mkapa.

View attachment 2398094

Pia, soma=> Dar: Mradi wa Dege Eco village uliotelekezwa Kigamboni

FOR SALE DEGE ECO VILLAGE, RESIDENTIAL PROPERTIES IN KIGAMBONI TANZANIA



Before abandoned Dege Eco village was designed to be a satellite township of Dar es salaam, being built on an area covering 300 acres at Kigamboni. A mixed use residential project addressing all segments of society, from high end to medium, as well as those who need affordable housing.
Source : Uniq Traveller
 
Toka maktaba:
Mnada ulitangazwa toka mwezi September 2017 leo October 2022 unatangazwa tena baada ya miaka mitano kupita.

Nini kimefeli ? Hatuna kampuni za udalali zenye ubavu na ujuzi wa kuchukua tenda hii hapa Tanzania kutokana na upungufu wa uwezo wa kufanya biashara ya shilingi trilioni 1 na zaidi za kiTanzania.

Je serikali na NSSF hawajaona upungufu huu hivyo kushirikisha wadau wa kimataifa wenye uwezo wa kifedha na ujuzi kutangaza mnada huu kimataifa

20 September 2017
BREAKING: Nyumba za NSSF Kigamboni zapigwa mnada

Mradi mkubwa wa ujenzi wa mji mpya wa Kigamboni Dar es Salaam uitwao Dege Eco Village ulioanzishwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya jamii 'NSSF' na kusimama ujenzi wake mwaka 2016 unapigwa mnada. Kuliripotiwa kuwepo kwa ufisadi wa zaidi ya TSH bilioni 179 katika mradi huo na sasa anatafutwa Mwekezaji atakaeuchukua.
Source : millard ayo
 
Duh...!. Bonge la fursa hili!.
Hapa Mchechu hawezi kuacha hii opportunity!.
Hapa matajiri watauwana!.
Huu ni wakati sasa wa PPR kuachana na media business na kuingia kwenye real estate na property!.
P
Pascal....acha kuota. Hapo anachukua Mwarabu mmoja kwa ulaini. Watu washakula vyao. Ikibuma hii, pale patakuwa magofu ya ukumbusho tu kwa vizazi vijavyo
 
SEMDOI REAL ESTATE madalali wa kiTanzania wajitupa ktk deal hili lakini mradi huu ni mkubwa umewazidi kimo

SITE VISITS AT DEGE - KIGAMBONI

 
Back
Top Bottom