Serikali yasitisha Ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo. Kuimarisha Bandari za Mtwara, Dar

Serikali yasitisha Ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo. Kuimarisha Bandari za Mtwara, Dar

Status
Not open for further replies.
Hoja hapa ni kwamba project kubwa kama bandari huangalii miaka 10-20 ijayo bali unaangalia over 50 years!! Ikiwa unaona Uwanja wa abiria 6M ingekuwa ni white elephant; ni nani kati yetu na Kenya anafaidika kwa kuwa ni gateway? Ule Uwanja wa Jomo Kenyatta umejengwa miaka ya 70... leo hii, Kenya wanaona Jomo Kenyatta haitoshi na wanataka kujenga terminal itakayo-accomodate 20 million passengers annually wakati kwa sasa wanapokea roughly 6 millions!!! Na bila shaka nadhani unafahamu kwamba pamoja na Mombasa kuwa ni bandari kubwa kuliko Dar lakini kv wenzetu wanaangalia 50 years to come; nao wana mega project sawa na ya Bagamoyo ambayo wanataka kujenga Lamb! Kama kumbukumbu zangu zipo sawa, nadhani ule mradi walitaka ku-team up na China lakini China wakaamu kuja Bagamoyo probably kv tayari wana another mega project Djibouti!!

Kwa staili hii Wakenya wana kila sababu ya kutuona maboya....


Kwa kuwa Kenya wanajenga Bandari kubwa Lamu haimanishi kwambo wako sawa, isitoshe sielewi mambo ya Kenya, lkn kwa hapa kwetu huu mradi wa Bandari ya B'moyo ni white elephant na haumake economic sense Serikali ya Magufuli siyo wajinga kuupiga stop na kuhamishia nguvu kule ambako tayari kumeshajengwa na kunahitaji kuboreshwa tu!

Unajua nini? Mimi angalau ningewaelewa watu mnaong'ang'ania huu mradi kama kwa mfano Bandari za Dar, Tanga, na Mtwara zote zingekuwa zinaeffieciency ya mpaka 95% hapo sasa ndiyo mngesema Bandari zetu zimezidiwa tumefanya kila kitu na sasa tunahitaji Bandari kubwa zaidi lkn siyo kweli Bandari ya Dar yenyewe siyo kwa sababu wala ni ndogo bali ni inafanya kazi below its capacity by far , mpka leo hii hata kuhakikisha tu mzigo wa mteja haubiwi na unafika salama bado hatuwezi, ni juzi hapa Rwanda wamelalamika kuibiwa makontena yao na kupata hasara na siyo Rwanda tu Kongo hata Malawi ni kwamba hawana jinsi lkn wameshachoka sasa hapo wala bado sijaongelea mambo ya effieciency ya upakuaji mizigo, uhifadhi, n.k na hiyo ni Dar ,Tanga wala sijagusia MT sasa kama hizi Bandari zilizojengwa na Wakoloni miaka 100 iliyopita tunashindwa kuzifanya ziwe na effiecincy ya angalau 85% tunataka kujenga Bandari yaDola Bilioni 10 hiyo miuijiza itatoka wapi?

Ni sawa una nyumba ya vyumba viwili unashindwa kuisafisha na kukata majani vyoo vinanuka halafu unasema unataka kujenga nyumba mpya ya vyumba 7 ili uishi vizuri na kwa usafi zaidi hakuna atakaye kuamini!
 
Mkuu unaambiwa kupanga nikuchagua Kwa mujibu wa Mkataba inasemekana baada ya ujenzi kukamilika..mchina ataHold hiyo Bandari kwa 40yrs arudishe Gharama zake...naujue ..kwa kipindi hicho hiyo bandari itachukua mizigo mingi kuliko ya DAR..MTWARA na TANGA ziko chini ya Serikali...kwahiyo unaona nivyema mchina anufaike kuliko sisi...Inasemakana itajengwa ila kwanza tuboreshe hizi tunazomiliki kwa % 100 then wachina wataruhusiwa
Swali linabaki pale pale na wanalikimbia

Hivi akina Mh Magufuli, Mbarawa, Mwakyembe na wengine hawayakuyaona haya? Je, walipaza sauti lini kupinga haya ?

Je, maamuzi ya miradi mikubwa kama huu yanaongozwa na nini? Wataalamu au wanasiasa?

Pesa zipo kufuatana na video aliyoweka JokaKuu , nini kimebailika kiutaalamu?
 
Kwa kuwa Kenya wanajenga Bandari kubwa Lamu haimanishi kwambo wako sawa, isitoshe sielewi mambo ya Kenya, lkn kwa hapa kwetu huu mradi wa Bandari ya B'moyo ni white elephant na haumake economic sense Serikali ya Magufuli siyo wajinga kuupiga stop na kuhamishia nguvu kule ambako tayari kumeshajengwa na kunahitaji kuboreshwa tu!
Lakini Magufuli alikuwemo katika baraza la mawaziri lililokubali 'white elephant'' unataka tuelewe vipi, kwamba wakati huo alikuwaje ili kulinganisha na sasa? Please tuelezeni maana CCM ni ile ile, kamati kuu ni ile ile, magogoni ni wale wale

Hapa tusikwepe , kuna uzembe ambao hatupaswi kufunika kombe.

Wakati mradi unafanyiwa mchakato umegharimu pesa nyingi sana in terms of resource, pesa ambazo zingeweza kujenga kachuo kadogo au kurepea MRI nyingi tu.

Walikuwa kimya, leo mnasema si wajinga wa kukubali white elephant! walikuwa wapi na ujanja wameupata lini

Alinda dalili za uchovu zi wazi. Tuliwambia huwezi kumvisha chui ngozi ya kondoo ukamwaita kondoo mpya!

Nyani Ngabu The Boss wameanza kuelewa
 
Last edited:
Iko siku hapa JF tutakuja zungumzia swala hili tukiwa tumechelewa huku tukichekwa kama Mazombie kila kitu kwetu ni Ushabiki usio na tija
 
Hapo wawekezaji walioingia mikataba watakula fedha ya bure kama hii habari ni ya ukweli.
Watakulaje hela wakati wao ndio walikuwa wanatoa hela? Serikali haijaweka hela zake katika mradi huo.
 
Wakati wenzetu wananunua suruali mpya sisi tunaziba viraka.Angalia kenya wanavyochakarika port ya mombasa ilikuwa bora Africa mashariki laakini sasa wanashusha modern port lamu sisi tunaenda kuziba viraka vya kurasini na maajengo mtwara.Tusipokuwa na viongozi wenye upeo na wanaoweza kujua dunia inaenda vipi tutabaki kulalamika shilingi inashuka.Magufuli usidanganywe wenzako hawakuwa wajinga kupanga mipango ya kimaendeleo kwa kwenda na wakati port ya Bagamoyo ni uamuzi sahihi wake up man
 
Swali linabaki pale pale na wanalikimbia

Hivi akina Mh Magufuli, Mbarawa, Mwakyembe na wengine hawayakuyaona haya? Je, walipaza sauti lini kupinga haya ?

Je, maamuzi ya miradi mikubwa kama huu yanaongozwa na nini? Wataalamu au wanasiasa?

Pesa zipo kufuatana na video aliyoweka JokaKuu , nini kimebailika kiutaalamu?

Mkuu wangu hii NCHI inaongozwa kwa mihemko ya MTU yyt anaeingia Ikulu haina mipango inayoeleweka.....
 
Huu ujinga unafanyika Tanzania tuu watu wanafanya maamuzi ya kukurupuka sana
 
Kama fedha ziliishapatikana kwa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo, wakisitisha ujenzi huo, fedha hizo haziwezi kuhamishwa kufanya kitu kingine chochote!. Bandari hiyo ya Bagamoyo ingekuwa ndio bandari kubwa kuliko zote kwa bahari ya Hindi upande wa Bara la Afrika.

Huu usitishaji wa mipango iliyoshapata funding hauna tija kabisa kama hiyo mipango mbadala ndio kwanza mchakato wa kuitafutia funding ndio inaanza!.

Pasco
Hayo maneno kwenye rangi nyekundu yahusika! Ukitaka mtanzania (soma mdanganyika) asihoji chochote kuhusu mradi wa kijinga na usio na manufaa mwambie huu mradi ni mkubwa kuliko yote Afrika Mashariki au Afrika au Duniaani! Umemmaliza! Ataridhika na kuzuuza roho yake. Wala hawezi kujiuliza ''hata kama ni mradi mkubwa so what! Una faida gani kwetu!'' Pasco na hawa wanasiasa uchwara wanajua zaidi ndio maana hawaishi kubwagiza na haya maneno...
 
Swali linabaki pale pale na wanalikimbia

Hivi akina Mh Magufuli, Mbarawa, Mwakyembe na wengine hawayakuyaona haya? Je, walipaza sauti lini kupinga haya ?

Je, maamuzi ya miradi mikubwa kama huu yanaongozwa na nini? Wataalamu au wanasiasa?

Pesa zipo kufuatana na video aliyoweka JokaKuu , nini kimebailika kiutaalamu?
Walikuwa kwenye baraza la mawaziri na hawakuwahi kupinga ili hata kuweka kumbukumbu. Hii nchi ni hatari sana. Kila rais anayeingia anaingia na vituko vyake. Sasa huo mkataba ukivunjwa itakuwaje?
 
Wakati wenzetu wananunua suruali mpya sisi tunaziba viraka.Angalia kenya wanavyochakarika port ya mombasa ilikuwa bora Africa mashariki laakini sasa wanashusha modern port lamu sisi tunaenda kuziba viraka vya kurasini na maajengo mtwara.Tusipokuwa na viongozi wenye upeo na wanaoweza kujua dunia inaenda vipi tutabaki kulalamika shilingi inashuka.Magufuli usidanganywe wenzako hawakuwa wajinga kupanga mipango ya kimaendeleo kwa kwenda na wakati port ya Bagamoyo ni uamuzi sahihi wake up man
Uwe uamuzi sahihi au la, alikuwemo ndani wakati maamuzi yanapitishwa

Tusimsukumie mzigo mtu mwingine, ni hawa hawa walikuwa katika harakati tena wakipiga kampeni za kutaja mradi.

#Hapa kazi tu, hapamauza uza tu
 
Walikuwa kwenye baraza la mawaziri na hawakuwahi kupinga ili hata kuweka kumbukumbu. Hii nchi ni hatari sana. Kila rais anayeingia anaingia na vituko vyake. Sasa huo mkataba ukivunjwa itakuwaje?
Hapa tunaimba nyimbo tu wenzetu wanachanja mbuga. JK ana la kusema kuwa mradi huo ulikuwa na faida

Magufuli alikuwemo, sasa anasema hapana. Huyu ndiye wa kutueleza nini kimebadilika alichokuwa hakioni wakati huo?

Kila siku tunalishwa 'kashata' mpya, tunaimba tu hatufikirii. Hatuna maono na nchi yetu

Tusubiri tangazo siku moja, mtu ataamka asubuhi na kusema akina baba wahasiwe, population imekuwa kubwa!

Mungu pishilia mbali , twaweza fyekwa tu.
 
Kiroho saaaaaaafi na kwaaaaaaaaaaaaaaaaaatuuuuuuuuuuuuuuuuu......! Nampongeza Waziri wa Kazi, Uchukuzi na mawasiliano kwa kutumia Weledi wake katika mambo ya kitaifa kama haya.
 
The Construction of the 10 billion (about Sh22 trillion) Bagamoyo Port has been suspended, The Citizen has learnt. The government wants to focus instead, on improving the capacity, performance and efficiency of the Mtwara and Dar es Salaam ports.

The Minister for Works, Transport and Communications, Prof. Makame Mbarawa, confirmed yesterday that the construction of what would be the largest port in Africa has been suspended, not shelved to pave way for upgrading berths 13 and 14 as well as developing the Mtwara Port depending on the availability of Funds. The activities would take years to complete, the minister said because the process has to start from finding funding.


Source: THE CITIZEN
View attachment 315504
EDDO alipokuwa anapinga hilo swala wengi walimkejeli sana
 
Shikamoo yako baba maghufuli!! Kweli wewe jembe na ni mzalendo wa kweli endelea vivyo hivyo wasiopenda wale malimao
 
Ombeni kwani ni mshauri wa rais?acheni kumharibia mzee wa watu,kwanza walimtoa UN ambako huko hamna uswahili lkn akivoletwa huku ndo akakutana na habati ya mkwere ss hata ungekuwa ww ungefanyaje?
 
...mimi pia nikipendelea na nikidhani hivo, lkn usanifu ulionesha kuwa ni bagamoyo tu, ndipo pana mazingira ambayo kitaalam yanatoa fursa ya ujenzi wa bandari kubwa na ya kisasa, huku bandari zingine zote zikiwa zina mapungufu ya aina moja au ingine, ktk mazingira ya ujenzi wa bandari kubwa....
Nilisikia mkataba huu unawapa wawekezaji wa China kuendesha hiyo bandari kwa muda wa miaka 50 mpaka watakaporudisha pesa zao na hapo Tanzania ndo itapewa bandari yake.
 
It's about time!! The only port worth of spending that kind of dough is Mtwara because the benefits are known, and return to investment is quicker and realistic. Instead of developing Bagamoyo port they should have strengthened the road/rail to Bagamoyo and strengthened the Dar port. Even Tanga has better development merit than Bagamoyo! Bravo the new government.
The Construction of the 10 billion (about Sh22 trillion) Bagamoyo Port has been suspended, The Citizen has learnt. The government wants to focus instead, on improving the capacity, performance and efficiency of the Mtwara and Dar es Salaam ports.

The Minister for Works, Transport and Communications, Prof. Makame Mbarawa, confirmed yesterday that the construction of what would be the largest port in Africa has been suspended, not shelved to pave way for upgrading berths 13 and 14 as well as developing the Mtwara Port depending on the availability of Funds. The activities would take years to complete, the minister said because the process has to start from finding funding.


Source: THE CITIZEN
View attachment 315504
 
Habar

Habari ina ukweli kabisa, soma The Citizen, huwa gazeti hili hawaongei mambo ya mitaani.
Serikali Awamu ya Nne inaelekea ilitumia vigezo visivyoeleweka vyema katika sekta nzima ya usafirishaji, hususan bandari.
Bagamoyo haina hata reli ya kuunga bandarini, jipu hilo!
Yaan we acha tu.. Bila KATIBA MPYA YA WARIOBA hii nchi akija rais mwingine yatarudi hayahaya tunayoyalalamikia..
Pigania Katiba Mpya kwa maslahi mpana na ya mbele ya nchi..
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom