Serikali yasitisha Ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo. Kuimarisha Bandari za Mtwara, Dar

Serikali yasitisha Ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo. Kuimarisha Bandari za Mtwara, Dar

Status
Not open for further replies.
Mmmmhhhhh Kila zama na kitabu chake Mzee wa Lupaso aliondoka na mtwara corridor yake na sasa Mzee wa Msoga Ana ondoka na Bandari ya Bagamoyo
 
Alafu wachina ndio wangeiendesha bandaribkwa kitu kama miaka50 ivi.¡¡¡¡¡kweli kahawa zinadhohofisha uwezo wa kufikiri
 
Hii project haikuwa ya kujenga bandari tu...bali ni pamoja na kuboresha eneo la viwanda vya processing ili tuuze bidhaa nje.
Ahadi ya Magufuli ni Tanzania ya viwanda sasa kama mradi unaohusiana na viwanda unakatwa na sisi tunaanza kuchekelea eti Mkwere anakomolewa basi watanzania wana Tatizo kubwa la udumavu wa akili.

Tusijadili kwa chuki dhidi ya mkwere bali tujadili kwa utaalamu
Hamna lolote ndugu yangu. Hiyo bandari ni white elephant na ingetugharimu sana. Haina kipaumbele chochote ukilinganisha na kuboresha bandari ya dar, tanga na mtwara. Ingepaisha deni la taifa mpaka tuchanganyikiwe. Kama ni viwanda bado vinaweza kujengwa huko bagamoyo.
 
bandar ya dar iko hovyoo,..local sana,,.wanaangaika na bandar mpya,...jk hovyoooooooo sana,.....ashitakiwee kwa matumiz mabaya
Kuna kinga ya rais kutoshtakiwa, bila hivyo Kwa hali jinsi ilivyokuwa wakati wa kuelekea kwenye uchaguzi Mzee wa msoga angeng'ang'ania madarakani
 
bagamoyo kina kifup toka enzi ya mjeruman alishaona ndio mana akahamishia bandari dar, cost za kuchimba chini ni kubwa sana ili kina kiwe kikubwa meli kubwa zipite pili shippers walishasema haitakua na faida yoyote maana bandari ya dar inaitaj improvement tu finally the project is dead and we can all be happy now!!!
 
Magufuli anafanya maamuzi bila kujali nani atafurahi au kununa .... Miaka kumi iliyopita ni kama system nzima ilipigwa ganzi ...
 
...hayo mapesa / watupatie nusu tu,kama kweli walikuwa na nia njema tuimarishe bandari ya dar!,tuipanue ya tanga na mtwara!
yakhee!
 
....lkn, kuna suala la uwezo wa bandari zetu kuhudumia meli kubwa,zinazobeba mpaka kontena elfu kwa mkupuo(3G&4G sea vessels), ambazo lamu port itakuwa na uwezo wa kuzihudumia...tunatazamaje hilo? Au sisi tutabaki tunapokea meli ndogo tu na kuacha biashara kubwa ya bandari, kwa wakenya, djibout, na south afrika?

weka maslahi yako pembeni, umeambiwa bandari za Dar na Mtwara zinaimarishwa.....over
 
This is beyond my comprehension yaani bandari ambayo kwa sasa inatumiwa na mataifa jirani Congo, Rwanda, Burundi na mataifa mengine ya chini mwa Tanzania iwe katikati ya jiji.

Kwa sasa tu magari inabidi ya pakie usiku ambapo ni time consuming kwa wateja wengine kulaza magari ambayo yangekuwa yanawatengezea hela, port ya Bagamoyo si ndio ideal ipo nje ya mji kidogo na eneo linaweza wekewa mazingira tu suit entry and exit ya kumudu foleni za baadae ata mji ukikuwa na tena kuna investor ambaye yuko tayari, ajira ambazo zingepatikana kwa wadau maana dar is congested surely bagamoyo ingekuwa sababu ya kulitanua jij la Dar ambalo kwa sasa lipokea malaki ya economic migrants kila mwaka.

Kuna vitu vingine maamuzi anayaelewa anaenua mwenyewe lakini sio duniani nzima hili ni moja wapo ina maana awaoni location wise tu bandari ya Dar sio sawa kwa volume inazobeba sehemu na sio sahihi kwa jiji leo.
 
Last edited:
Watu Wa Ajabu Sana Kwani Akitokea Bagamoyo Maana Yake Bagamoyo MIRADI Isifanyike????
Tuangalie Merits Sio Nani Anatoka Wapi?
Mbona Magufuli Ameanzisha Usanifu wa Daraja Kuvuka Ziwa Victoria BUSISI Akija Rais Mwingine Asitishe??
Mbona JK Alianzisha MIRADI UDOM,MALAGARASI, KIGAMBONI, KILOMBERO Mingi Tu Huko Ni Kwao.
Wanaotizama Kwa Mtazamo Huo Ni WAKABILA TU.
Fedha Hizi Ni Grant Zingejengwa Reli Na Highways Kuelekea Maziwa Makuu Bagamoyo Ni Pori Na Eneo Kubwa DAR Itakuwaje???
Mtaboresha Bandari Msongamano Wa Malori KUINGIA Na Kutoka Port.
Fanyeni Muende Leo Muone Foleni Inaanzia Uwanja wa TAIFA KUINGIA.
Kutoa Unapakia Kutoka Saa 4 Na Zaidi Bagamoyo Tulikuwa Na Option ya Kudesign Tutakavyo.
Nchi Hii Wivu, Cheap Politics Na Uswahili.
Fedha Sio Zetu Wataondoka Wapeleke Kwingine.
Kenya, Uganda Na RWANDA 4 Billion Za Standard Gauge Na 6 Billion Za LAPPSET Wanahangaika Miaka 6 Sasa Nchi 3.
Sisi Tumebahatika SIASA ZA FITNA NA UKABILA Kuliko Mantiki Tunaharibu.
Tutajuta Nipo.
Huu ni mradi mzuri kuuelezea lakini kivitendo una maswali na nadhani JPM kajiuliza hayo maswali na hakupata majibu.
Unaongelea Bagamoyo kutokuwa na foleni lakini ukumbuke pia hakuna barabara za kuiunganisha hiyo bandari hivyo itatakiwa kujengwa reli, barabara za kisasa na mioundombinu mingine.
Dar es salaam wanasema karibia 80% ya mji umejengwa bila kupimwa, kwa maana hiyo wakifanya overhaul na kurudisha master plan ya mji na kujenga 50% tu ya highways/barabara kama inavyotakiwa naamini foleni zitapungua kwa 90%. Kwa maana hiyo hizo foleni za kuanzia uwanja wa taifa unaweza ukashangaa zinapote.
Alafu kuna kitu ambacho wengi hatukisemi hapa, hiyo Bagamoyo wanasema ni 'wawekezaji' lakini kwa upande wa pili wanatukopesha hizo pesa na mikataba yake wengi mnajua ilikuwa na usiri kiasi gani! Maeneo asilia ya bandari ya Dar es Salaam yanajulikana lakini pia yamevamiwa na wnaojiita 'wawekezaji' na kujenga ICDs ambazo zinafanya kazi hizo hizo za bandari! Sasa ukipinga hasara ya mkopo wa kujenga Bagamoyo na kulinganisha na gharama za kuwafidia na kuwahamisha 'majirani' wa bandara ya Dar es Salaam kuanzia Mivinjeni mpaka Mtoni ni wazi itakuwa ni gharama kubwa lakini bado zitakuwa ni kidogo mno kulinganisha na hii mikopo tata yenye masharti ya kuuana.
 
Watanzania tuna safari ndefu sana-- siumi maneno, this's MISTAKE! Nitarudia tena na tena, hapa serikali ya Magufuri itakuwa inakosea sana! Bandari ni zaidi ya meli kufunga gati bali container terminals! Bandari zote duniani zinapimwa kwa uwezo wake wa kuhudumia makoentena. Dar es salaam hakuna eneo linaloweza kutufikisha miaka 50 ijayo! Sisi watu wa Kurasini tunaifahamu vizuri hii! Kurasini ya miaka ya 80 sio ya miaka ya 90 na Kurasini ya miaka ya 90 sio ya miaka 2000! Kurasini yote imeisha kwa ajili ya Bandari na sooner or later watahamia Mtoni manake hata Mivinjeni nayo imebaki historia!

Pamoja na Kurasini na Mivinjeni ku-RIP lakini bado bandari ya Dar es salaam haipokei mzigo mwingi wa angalau kulinganisha na Mombasa. Pamoja na Mombasa kupokea mzigo mwingi kuliko sisi lakini nao wameshaona bandari ya Mombasa haitawafikisha miaka 50 ijayo na ndo maana wanaanzisha grand project kule Lamu! Kama lengo la serikali ni kuipanua zaidi bandari ya Dar es salaam basi wafanye declaration kabisa kwamba Temeke yote iwe ni eneo la bandari ya Dar es salaam!!

Kwamba waimarishe bandari ya Mtwara hii ni mistake nyingine! Unless kama tunadanganywa kuhusu gas boom huko Lindi na Mtwara lakini kama ni kweli basi itakuwa taabu sana siku za usoni kuifanya bandari ya Mtwara kuwa multi-purpose... yaani ku-accommodate gas and petroleum shipping lines together with other cargo shipping lines. Sehemu nyingi duniani, bandari zinazo-accomodate meli za mafuta zinakuwa na separate habors coz' ile mimeli ni mikubwa mno!

At least ningewaelewa kama wangesema mradi wanauhamishia Tanga lakini Dar es salaam au Mtwara... hili ni kosa la kiufundi!
we mtu unafikiri. safi sana.
 
....lkn, kuna suala la uwezo wa bandari zetu kuhudumia meli kubwa,zinazobeba mpaka kontena elfu kwa mkupuo(3G&4G sea vessels), ambazo lamu port itakuwa na uwezo wa kuzihudumia...tunatazamaje hilo? Au sisi tutabaki tunapokea meli ndogo tu na kuacha biashara kubwa ya bandari, kwa wakenya, djibout, na south afrika?
Kuna aliyesema mtwara inafaa kwa hilo na ina kina kirefu cha maji.
 
Kama tuboresha bandari ya mtwara, vipi bandari ya dangote
 
Habar

Habari ina ukweli kabisa, soma The Citizen, huwa gazeti hili hawaongei mambo ya mitaani.
Serikali Awamu ya Nne inaelekea ilitumia vigezo visivyoeleweka vyema katika sekta nzima ya usafirishaji, hususan bandari.
Bagamoyo haina hata reli ya kuunga bandarini, jipu hilo!



Kwa sababu ni linaandikwa kwa kiingereza? The Citizen ni Mwnanchi Kampuni ile ile falsafa ile, ila kwa kuwa wameandika Kiingereza basi unaamaini lkn kama Mwananchi wangeandika usingeamini, kweli sisi Waafrika ni zaidi ya utujuavyo!
 
Bandari ya mwaa kivyake na ile kivyake.

Habari imekaaa kiudaku zaidi na siwezi kuishadidia mpaka nione tamko rasmi la serikali.

Strategically Bagamoyo Port ni better kuliko Dar.
Na tukishajenga bagamoyo bandari ya dar ipelekwe wapi?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom