Serikali yatangaza tenda ya ujenzi wa mwendokasi kutoka Maktaba ya Taifa Posta- Mwenge- Ubungo-Tegeta

Hii miradi mbona kama haieleweki
Mnataka kuleta usumbufu tu

Ova
kabisa....si kila mahali kuvurugwe eti mwendo kasi. ukanda huo wa posta mwenge ungeachwa tu. wahangaike kutokea moroco....anyway ujenzi unajumuisha tenda na rushwa kubwakubwa, tusishangae siku moja kusikia ocean rod/obama road inajengwa mwendo kasi.
 
City train ndio ingekuwa suluhisho la usafiri Jijini Dar, haya mabasi hayawezi kabisa kutatua kero ya usafiri Dar..

Njia nzote hizi za mwendo kasi ingetakiwa iwe train zote, usingeona foleni au watu wamejazana katika vituo kusubiria usafiri..

Majiji yote makubwa duniani, city train ndio suluhisho la usafiri wa majiji hayo, mfano kwa Africa, Addis Ababa, Ethiopia, au Joburg, S.A, ila Ulaya nchi nzima ni train, US train ndio kila kitu na ujenzi wake usingekuwa tofauti na huu wa mwendokasi, tena kuna train za majiji zinabeba watu 2000 kwa mkupuo, yaani Tegeta asubuhi unapeleka 3 tu kwenda na kurudi, Mbagala 3 tu kwenda na kurudi, Kibaha Posta unapeleka 4 tu kwenda na kurudi foleni ya watu kwishaa kwa asubuhi, jioni zinarudia hivyo, maana train 3 kwa route moja inabeba karibia watu 6,000 zikirudi second round watu 12,000..

Yaani haya mabasi hayana msaada kulinganisha na investments inayofanywa, foleni, watu kubanana, watu kukosa usafiri, haijapungua

Train za mijini kama ile ya Mwakyembe, inabeba watu hadi 3,000 kwa mkupuo, tokea Pugu, Gongo la Mboto to Posta.. Ikirudi mara ya pili foleni ya watu imeisha, sasa je tungeweka train kama 15 hapa mjini za aina ile, wala usingeona shida za usafiri during peak hours, asubuhi au njioni
 
Hongera serikali ya Mama Samia kwa kukumbuka hiyo barabara
 
#watakula wapi?,isipovunjwa!
[Jenga,Bomoa,Jenga]
 
Hapana hii tayari wamesha andaa sehemu itakayopita mwendokasi ukipita njia hii utaona katikati kumeachwa kusubiria ujenzi huo kuanza hivyo ina maana barabara iliyokamilika haitaguswa

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
 
Mimi namsifu mama samia barabara zake za mwendokasi katikati ya barabara haziwekwi kipande cha lami,zote zinakuwa na zege tupu,sijui Kwa nini huko zamani walikuwa wanaweka lami,mfano,zote za kuelekea ferry.
 
Pale Lugalo wanajeshi wamejitahidi sana kuitunza ile garden katikati ya barabara. Nashauri zile Palm tree zisikatwe.
Umenikumbusha way back 2018 nilikanyaga hizo garden wakati navuka barabara aisee,kitambulisho ndo kilichoniokoa..
 
Phase I alikuwa ni Mjerumani huwezi linganisha kazi zao na wachina....
 
Hapo ndipo akili ya mwafrika ilipolala!! Kila siku tunakosa vipaombele.
 
Ile nafasi kubwa katikati ulifikiri ni mapambo?
We huwa wanavunja, kama ya Mbagala ikibomolewa, labda hii kama vipimo waliweka sawa hawa Makandalas. Kumbuka vivuko vya waenda kwa miguu matuta kila kituo. Lazima watazibonda hizo road za sasa
 
We huwa wanavunja, kama ya Mbagala ikibomolewa, labda hii kama vipimo waliweka sawa hawa Makandalas. Kumbuka vivuko vya waenda kwa miguu matuta kila kituo. Lazima watazibonda hizo road za sasa
Mbagala ile barabara ni ya miaka ya 90 na haikuandaliwa kwa ajili ya mwendokasi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…