Serikali yatoa Tsh. Bilioni 66 Kurekebisha Miundombinu iliyoharibiwa na mvua

Serikali yatoa Tsh. Bilioni 66 Kurekebisha Miundombinu iliyoharibiwa na mvua

Ahsante kwa taarifa na inapendeza sana...


Cc: mahondaw
 
Rais wa JMT Dr Samia ametoa Jumla ya shilling billion 66 Ili kurekebisha Miundombinu iliyoharibiwa na mvua

Fedha hizo zimegawanywa Kwenye mikoa Yote iliyoathirika

---
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan ametoa Bilioni 66 kwa ajili ya kuanza urejeshaji wa miundombinu ya barabara zilizoharibika nchini.

Fedha hizo tayari zimegawanywa kwa mameneja wa TANROADS mikoa yote iliyoathirika kwa ajili ya kufanya kazi kwa haraka usiku na mchana ili kurekebisha kadhia zilizozikumbumba barabara kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha nchini.

Akizungumza Jijini Arusha mara baada ya kukagua Barabara ya Afrika Mashariki (Arusha bypass) iliyoharibiwa na mvua hizo, Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) Mha. Mohamed Besta amesema kuwa kutokana na udharula huo tayari Rais Samia ametoa fedha za matengenezo ya miundiombinu hiyo ambazo zimeshapelekwa katika Mikoa yote Nchini.

Mhandisi Besta amesema kuwa tayari kazi inaendelea katika maeneo yote nchini na fedha hizo zinaratibiwa na vitengo maalumu vya dharula vilivyopo TANROADS pamoja na ofisi za mikoa.

Ameongeza kuwa kutokana na tathimini iliyofanyika mpaka sasa zaidi ya Shilingi Bilioni 250 zinahitajika kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya Barabara kuu za Mikoa yote Nchini ambazo zimeharibika vibaya kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha sehemu mbalimbali nchini.

Amesema kuwa kuna baadhi ya maeneo kama Kanda ya Ziwa na Nyanda za juu kusini mwa Nchi mvua zimeendelea kunyesha tangu mwezi Oktoba mwaka jana, na sasa unaelekea mwezi wa saba na mvua bado zinaendelea kunyesha.

“Tunamshukuru Mhe Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwani ametupatia shilingi bilioni 66 ambazo tumezisambaza katika Mikoa yote ambapo mameneja wote wa Mikoa wamepewa kutokana na hali ya dharura ya Mkoa husika’’ ameeleza.

Chanzo: Clouds
Ametoa pesa toka mfukoni mwake? Basi jambo zuri kama kajitolea. Lakini kama kaidhinisha fedha za walipakodi zikarabati miundombinu hiyo ni habari nyingine na hajatoa yeye.
 
Ametoa kwenye account yake anayoingiziwa Mshahara?
Mkuu Mjomba Magu alikuwa anasema katoa.........,mko kimya,leo Mama yetu anatoa kamili plus mnakasirika?Acha unafiki.Mlikuwa mnasifu hata nonsense issues kama Madagascar drug pammoja na kuitwa profesa aliehitimu Germany. Tanzania ni wanafiki.
Mama Piga kazi tupo nawewe.
 
Sasa ni wakati wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na yenywe kutoa pesa maana ni Raisi tu ndo anatoa pesa zake....serikali kimya
 
Rais wa JMT Dr Samia ametoa Jumla ya shilling billion 66 Ili kurekebisha Miundombinu iliyoharibiwa na mvua

Fedha hizo zimegawanywa Kwenye mikoa Yote iliyoathirika

---
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan ametoa Bilioni 66 kwa ajili ya kuanza urejeshaji wa miundombinu ya barabara zilizoharibika nchini.

Fedha hizo tayari zimegawanywa kwa mameneja wa TANROADS mikoa yote iliyoathirika kwa ajili ya kufanya kazi kwa haraka usiku na mchana ili kurekebisha kadhia zilizozikumbumba barabara kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha nchini.

Akizungumza Jijini Arusha mara baada ya kukagua Barabara ya Afrika Mashariki (Arusha bypass) iliyoharibiwa na mvua hizo, Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) Mha. Mohamed Besta amesema kuwa kutokana na udharula huo tayari Rais Samia ametoa fedha za matengenezo ya miundiombinu hiyo ambazo zimeshapelekwa katika Mikoa yote Nchini.

Mhandisi Besta amesema kuwa tayari kazi inaendelea katika maeneo yote nchini na fedha hizo zinaratibiwa na vitengo maalumu vya dharula vilivyopo TANROADS pamoja na ofisi za mikoa.

Ameongeza kuwa kutokana na tathimini iliyofanyika mpaka sasa zaidi ya Shilingi Bilioni 250 zinahitajika kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya Barabara kuu za Mikoa yote Nchini ambazo zimeharibika vibaya kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha sehemu mbalimbali nchini.

Amesema kuwa kuna baadhi ya maeneo kama Kanda ya Ziwa na Nyanda za juu kusini mwa Nchi mvua zimeendelea kunyesha tangu mwezi Oktoba mwaka jana, na sasa unaelekea mwezi wa saba na mvua bado zinaendelea kunyesha.

“Tunamshukuru Mhe Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwani ametupatia shilingi bilioni 66 ambazo tumezisambaza katika Mikoa yote ambapo mameneja wote wa Mikoa wamepewa kutokana na hali ya dharura ya Mkoa husika’’ ameeleza.

Chanzo: Clouds
Sema watanzania kupitia kodi zao ndio wametoa hizo pesa. Na rais anawajibika kuzisimamia zikafanye kazi iliyokusudiwa.

Rais Samia hana hiyo pesa, na hata angekuwa nayo isingeweza kuitoa.
 
Hivi ni mimi au lugha imekwenda upande?! Ni Samia ametoa Jumla ya shilling billion 66 Ili kurekebisha Miundombinu iliyoharibiwa na mvua au Serikali imetoa jumla ya shilling billion 66 Ili kurekebisha Miundombinu iliyoharibiwa na mvua? Samia ametoaje bilioni 66?!
Chawa utawaweza?
 
Mkuu Mjomba Magu alikuwa anasema katoa.........,mko kimya,leo Mama yetu anatoa kamili plus mnakasirika?Acha unafiki.Mlikuwa mnasifu hata nonsense issues kama Madagascar drug pammoja na kuitwa profesa aliehitimu Germany. Tanzania ni wanafiki.
Mama Piga kazi tupo nawewe.

Mkuu nimeuliza maana mbatizaji amesema Rais samia atoa.

Wapo mbona watu wanatoa fedha zao kufanya ujenzi au ukarabati? Ndio maana nikauliza kwa Rais samia possible ametoa za kwake mfukoni.
 
Rais wa JMT Dr Samia ametoa Jumla ya shilling billion 66 Ili kurekebisha Miundombinu iliyoharibiwa na mvua

Fedha hizo zimegawanywa Kwenye mikoa Yote iliyoathirika

---
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan ametoa Bilioni 66 kwa ajili ya kuanza urejeshaji wa miundombinu ya barabara zilizoharibika nchini.

Fedha hizo tayari zimegawanywa kwa mameneja wa TANROADS mikoa yote iliyoathirika kwa ajili ya kufanya kazi kwa haraka usiku na mchana ili kurekebisha kadhia zilizozikumbumba barabara kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha nchini.

Akizungumza Jijini Arusha mara baada ya kukagua Barabara ya Afrika Mashariki (Arusha bypass) iliyoharibiwa na mvua hizo, Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) Mha. Mohamed Besta amesema kuwa kutokana na udharula huo tayari Rais Samia ametoa fedha za matengenezo ya miundiombinu hiyo ambazo zimeshapelekwa katika Mikoa yote Nchini.

Mhandisi Besta amesema kuwa tayari kazi inaendelea katika maeneo yote nchini na fedha hizo zinaratibiwa na vitengo maalumu vya dharula vilivyopo TANROADS pamoja na ofisi za mikoa.

Ameongeza kuwa kutokana na tathimini iliyofanyika mpaka sasa zaidi ya Shilingi Bilioni 250 zinahitajika kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya Barabara kuu za Mikoa yote Nchini ambazo zimeharibika vibaya kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha sehemu mbalimbali nchini.

Amesema kuwa kuna baadhi ya maeneo kama Kanda ya Ziwa na Nyanda za juu kusini mwa Nchi mvua zimeendelea kunyesha tangu mwezi Oktoba mwaka jana, na sasa unaelekea mwezi wa saba na mvua bado zinaendelea kunyesha.

“Tunamshukuru Mhe Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwani ametupatia shilingi bilioni 66 ambazo tumezisambaza katika Mikoa yote ambapo mameneja wote wa Mikoa wamepewa kutokana na hali ya dharura ya Mkoa husika’’ ameeleza.

Chanzo: Clouds
Hizo hela ni za wananchi au za rais mbona upambe umekuwa mwingi hela ni za wananchi sio za rais
 
Tz bado kiswahili kinatubabaisha, unashindwa kusema serikali imetoa???

Nadhani siyo shida ya Kiswahili, bali upungufu akili. Ukikosa akili, huwezi kujiamini, itabidi uwe chawa na kuandika hata yasiyokuwepo.

Kule Uganda, wakati wa utawala wa Kabaka, kuna machifu waliwahi kutamka kuwa hata hewa wanayoivuta waganda ni mali ya Kabaka. Angalao hao ilikuwa miaka ya 1800, lakini sisi tunao akina Mwashambwa and the like, kwenye miaka hii!!
 
Kila kona kuna kilio cha uharibifu wa miundombinu iliyosababishwa na mvua iliyonyesha kwa takriban miezi miwili sasa. Uharibifu huu haukutarajiwa na Serikali ni mambo yasiyotarajiwa. Binafsi naipa pole Serikali yetu kwa haya yaliyotokea na hayakurajiwa. Ninaishauri Serikali kuwa ione uwezekano wa kufuta baadhi ya miradi iliyotengewa fedha kwenye bajeti na fedha zitakazopatikana zielekezwe kwenye kurekebisha miundo mbinu iliyoharibika. Mfano fedha zote za REA, miradi ya maji yote haya yafutwe.
 
Back
Top Bottom