CM 1774858
JF-Expert Member
- May 29, 2021
- 5,621
- 5,029
MABILIONI YA RAIS SAMIA YAMPA IMANI SHAKA KUWAKOMBOA VIJANA KATIKA KILIMO
KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka amesema dhamira ya dhati ya Rais Samia Suluhu Hassan, kuitazama kwa karibu sekta ya kilimo, ikiwemo kuongeza bajeti ya Wizara Kilimo, kutoka sh. Bilioni 254 mwaka wa fedha 2021/2022 hadi sh bilioni 954 kwa 2022/2023, italeta mabadiliko makubwa katika uchumi.
Miongoni mwa mabadiliko hayo ni pamoja na kutengeneza fursa nyingi za ajira, hatua ambayo imemfanya Shaka atoe muelekeo wa kutatua changamoto ya ajira kwa vijana hususan wasomi wa vyuo vikuu ambao ametaka watambuliwe na kuwezeshwa kupitia kilimo.
Shaka amesema hayo leo Agosti 7, 2022 alipotembelea Maonesho ya Kilimo (Nanenane) Kanda ya Mashariki yanayofanyika mkoani Morogoro ambapo amesema kupitia maonesho hayo lipo jambo la faraja ambalo ameliona.
Ameeleza kuwa, hata baada ya uhuru wa nchi haijapata kutokea kama bajeti ya mwaka 2022/2023 ambapo Rais Samia ametenga Sh. bilioni 954 ukingalisha na bajeti ya mwaka 2021/2022 ya Sh.bilioni 254 karibia asilimia 224 ya ongezeko hilo la bajeti.
“Lengo kuonesha mkazo zaidi katika Serikali hii ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imewekeza nguvu huko na dhamira kubwa ikiwa kuwakomboa vijana pamoja na wanawake.
“Katika hilo Ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi imeahidi katika kipindi cha miaka mitano tutazalisha ajira milioni nane kwa Watanzania, sasa kwenye kutafsiri maelekezo ya Ilani Serikali ya Rais Samia imeshajiwekea mwelekeo ama imeshajiwekea matatarajio yake katika ajira hizo,”alisema Shaka.
Alifafanua kuwa Serikali inatarajia hadi kufikia 2025 karibia ajira milioni tatu zitakuwa zimezalishwa kupitia sekta hii ya kilimo huku akiongeza kwamba hayo ni mageuzi makubwa na huo ni ukombozi kwa vijana na wanawake.
=== ===