Shaka: Rais Samia kuwalipa waliofukuzwa kwa vyeti feki ni ishara ya huruma, upole na upendo kwa Watanzania

HAKIKA RAIS SAMIA NI " RAIS NA MAMA "
 
Yani mtu ana vyeti fake analipwa wakati kuna vijana kibao hawana kazi na wanavyeti halali, sisi watu weusi kwakweli tuna laana flani hapa duniani si bure. 60 yrs of independence bado tupo hapa na siasa uchwara.
Acha roho mbaya,
 
Nzuri hii
 
Rais binadamu,
 
Muajiri wako akikuajiri kwa kuwa ulimdanganya, haikupi haki pale anapogundua umemdanganya akuache tu kazini kwa kuwa hakugundua utapeli wako wakati anakuajiri.
Unajua kwenye hili suala kuna watu wa aina tofauti. Mfano kuna wale ambao hawakufika Form IV ila wakatafuta vyeti kuonyesha walifika kidato hicho. Hao wengi walikuwa ni wahudumu na madereva na pia police ingawa kwenye military hawakuondolewa.

Kuna wengine walisoma wenyewe lakini kwa kutumia majina au vyeti ambavyo siyo vyao hao pia waliondolewa. Mimi kwa maoni yangu mtu ambaye kasoma kwa jina la mtu mwingine kusema ni vyeti fake ni kumuonea. Hao sikuona sababu ya kumuondoa kazini.
 
Nenda kavifakiki wewe,

Mtu amekuwa mbunge, Waziri, makamu wa Rais na leo Rais,

Eti vyeti fake, You can't be stupid YEHODAYA
Usiseme hivyo. Kuna kitabu aliwahi kuandika mtu mmoja anaitwa Kainerugaba. Alitoa siri za elimu ya viongozi wengi wa Tanzania kitabu kikapigwa marufuku na yeye nadhani alihamia nchi za nje. Katika watu waliotajwa hakuna hata mmoja alishtaki.
 
Huruma isibague uhalifu. Hivi imefanyika Tathmini faida na hasara ya kutumia wafanyakazi hao huku wakiwa na vyeti fake kabla ya kufikia uamuzi huu?

Nadhani Kuna haja ya baadhi ya watu waelezwe kuacha kutumia nia njema na huruma ya Mama vibaya
Kuna baadhi ya kada wala hakukuwa na ulazima wa kuwaondoa kazini. Mfano madereva na wahudumu.
 
Kweli huyu alikua mtoto mdogo akina lisu walipiga kelele zotezile hakusikia ....Leo anazungumzia matapishi ya ccm
 
Hili halina ubishi ila malipo yao wapewe,
Kwani walikua hawalipwi mshara Kwa Kazi walizokuwa wanazifanya kitapeli.

Ni sawa na Mtu anayemuuzia mtu mche wa sababu badala ya simu hasa enzi za simu za vitochi.
Akikamatwa hawezi kudai ooh basi nlipe Hela ya Kipande changu Cha Sabuni. [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Huyu kaka yuko smart enough
 
Kazi iendelee
 

Shaka ni Katibu mwenezi wa hovyo kuwahi kutokea tangu CCM ilipozaliwa mwaka 1977​

 
Naona wazee wa kuchapicha vyeti feki wanatabasamu, nahitaji Cheti cha pharmacy diploma, kiwe na ufaulu mzuri, sh ngapi?
 
Kumbe kugushi vyeti ni Hali sio kosa,kumbe walikosea kuwafukuza,muwalipe na fidia Kwa mda waliokaa bila kazi ndo tutajua mnaupendo na huruma
 
Yani mtu ana vyeti fake analipwa wakati kuna vijana kibao hawana kazi na wanavyeti halali, sisi watu weusi kwakweli tuna laana flani hapa duniani si bure. 60 yrs of independence bado tupo hapa na siasa uchwara.
Miaka 60 unaona miiiingi, kuna nchi zina miaka 200 ya uhuru usijilinganishe nazo
 
Hata ivyo vyeti vingi vilivyokutwa ni feki si vile vya ujuzi, bali vya elimu ya secondary f4 na f6.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…