Shaka: Rais Samia ni mbobezi katika masuala ya uongozi

Shaka: Rais Samia ni mbobezi katika masuala ya uongozi

JUMA JUMA

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2013
Posts
790
Reaction score
964
SHAKA: RAIS SAMIA NI MBOBEZI KATIKA MASUALA YA UONGOZI.

Umma waelezwe kuwa Anatosha na Atatuvusha.

Viongozi wa dini waombwa kuhubiri Amani na Mshikamano.

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema tokea Uhuru kupatikana 1961 na Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar kufanyika 1964 na hatimae Chama Cha TANU na ASP kuungana na kuzaliwa CCM 1977 hakijawahi kumpa mtu nafasi ya kuliongoza Taifa au kushika nyadhifa kubwa kama Urais wa nchi kwa majaribio au kubahatisha au bila kujiridhisha juu ya uwezo wake, maarifa yake, uzoefu wake kiungozi, na uzalendo wake kwa nchi

Kimesema kwamba sio sharti la kisheria wala kikatiba linalotaka mhusika kuifahamu jiografia na historia ya Tanzania kwa vile unaweza kuijua Kagera lakini usijue jiografia ya kisiwa cha Pemba ama unaweza kuijua Mtwara lakini usijue Jiografia ya Rombo na yote ni Tanzania ila ukipewa dhamana kubwa katika Taifa utajua kila kichochoro na kinachoendela kwa vile umebeba muhimili wenye nguzo thabiti ya kulisimamisha Taifa.

Katibu wa halmashauri Kuu ya CCM Taifa Shaka Hamdu Shaka ameyasema hayo katika Ibada ya kuweka wakfu na harambee ya jengo la Utawala na shule ya Biblia katika Kanisa la Pentacostal Moto Moto lilipo Boko Kinondoni Dar Es Saalam ambapo alisema Rais Samia ameudhihirishia Umma ndani na nje kuwa anaielewa vyema nchi anayoiyongoza, lakini pia anao washauri mahiri wenye weledi katika fani mbali mbali pamoja na kuweka mbele maslahi ya Taifa.

“Niwahakikishie watanzaia kupitia mkusanyiko huu kuwa Rais Samia ni msomi mzuri katika maendeleo ya utawala na uchumi ambae ametumikia na kushika nyadhifa mbali mbali za kiserikali (Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) pamoja na mashirika ya kitaifa na kimataifa duniani, ni mtu bigwa kabisa na anatosha hivyo atatuvusha kama alivoweza kutuvusha Taifa hili lilipopitia katika maumivu na nyakati ngumu katika historia yetu lakini leo tumebaki kuwa wamoja” Alisema Shaka

Amefahamisha kuwa kadri ya anavyoendelea kuiongoza nchi Rais Samia ameendelea kuudhihirishi Ummakuwa yeye ni msomi mbobezi kwenye maendeleo ya uchumi na ndio maana hatua ya kwanza kubwa na ya kupigiwa mfano ni kuilekeza benki kuu ya Tanzania kuhakikisha masharti na riba za mikopo katika mabenki ya kibiashara hapa nchini zinapungua na kuwa rafiki kwa wakopaji na muda mfupi ujao watanzania watarajie kuona mabadiliko makubwa katika ukuaji wa uchumi nchini pamoja na kuongezeka kwa mzunguko wa fedha kupitia kipato cha mtu mmoja mmoja

“Serikali inayoongwa na Rais Samia imepata bahati (Leo) hii milango ya uchumi wa nchi imeendelea kufunguka na kuwa wazi siku hadi siku jumuiya, mashirika, taasisi na wafanyabisahara wa kubwa wa kitaifa na kimataifa wameendelea kuja Tanzania kuitikia wito wa Rais wetu kuja kuwekeza katika maeneo muhimu ambayo yatakuwa kichocheo cha ukuaji wa uchumi wetu lakini kutoa fursa za ajira kwa Vijana na Wanawake sambamaba na kurahisha upatikani wa bidhaa muhimu kwa kuzalisha malighafi kutoka ndani baada ya kutegemea toka nchi za jirani na maeneo mengine nje ya Tanzania.

“Hii ndio faida kubwa ya kuwa na Rais anaeijua nchi yake, anaejua anaowaongoza wanahitaji nini, kwa wakati upi na yeye asimame katika mrengo upi bila ya kuyumbishwa na mikingano ya ndani na nje. Rais Samia amekamilika kwa kila sifa ambayo dunia ya leo inauhitaji mkuwa wa Rais wa nchi wa aina yake, niseme tena Tanzania Mwenyezi Mungu ametubariki” Alisema Shaka

Hata hivyo Katibu hiyo wa Itikadi na Uenezi amewahikishia viongozi wa dini kuwa Serikali za CCM daima zitaendelea kuheshimu na kuthamini jitihada za waumini wa dini zote katika kusongeza Taifa kiimani na kimaendeleo hivyo viongozi wa dini wanategemewa sana katika kuendelea kuwaunganisha Watanzania.

"Taasisi za Dini mna mchango mkubwa katika kudumisha amani, kustawisha maisha ya wananchi na kupambana na umasikini. Hivyo niwasihi waumini na watanzania wote kuendelea kuheshimiana na kuvumiliana kwenye tofauti za kidini zinazojitokeza ili kuendelea kudumisha amani na utulivu hapa nchini. Pamoja na kuendelea kukumbushana kuwa Amani na utulivu ni sehemu ya kichocheo kikubwa cha maendeleo ya taifa, hivyo ni vyema viongozi wa dini kuendelea kuhubiri amani kwa waumini wenu ili iendelee kudumu” Alisema Shaka

Katika shuhuli hiyo Mhe Rasi Samia Suluhu Hassan alichangia shillingi Millioni 10 kuunga mkono jitihada za kanisa hilo ambapo jumla ya shillingi Millioni 24 zilichngawa na waumini wa kanisa hilo .
 
Unajua viongozi wetu ndo mnasababisha jambo linakuwa kubwa.
Hilii halikuwa jambo la kutuletea sisi. Kwamba kwa sababu ni mbobezi wa masuala ya uongozi basi tumwonee huruma ama?
Mh. Rais anamda wa kutosha sana 'kuwaprove wrong' wale wenye mashaka nae, vinginevyo maneno ya katibu yatasound kama exicuse kwa kile kinachoonekana kama makosa ya wazi kwa serikali hii.
 
Ndio nani Shaka?
Sasa shaka mbona unatutia shaka,huku tulipo tunaona mambo yanakwenda mrama kwa kasi ya kutisha.Siku mia za kwanza ungeweza kutushawishi pasipo shaka,ila kwa Sasa,tuondoe shaka kwa kumshauri mkuu juu ya hali halisi ya sasa,Bila kumwacha na punje ya shaka.
 
Tukubali tukatae kwa mama tumeingia cha kike.

Hii iwape somo vyama vya siasa kwamba makamu wa rais ni rais siku moja waweke watu wanaoelewa wanachokifanya.

Hii ya kuteuana tu kwa kulipa fadhila ama kwa upendeleo itatuingiza chaka siku moja ndio kama haya ya sasa.

Huyu mama she has nothing new to offer. Na sasa amekua worse kuliko hata mzee Magufuli.

Hao kina shaka wataongea tu kwani mama amewafutia kesi zao za wizi na kuwapa cheo unafikiri watasemaje?
 


Early life​

Suluhu was born on 27 January 1960 in Makunduchi, an old town on Unguja island, in the Sultanate of Zanzibar.[2]

She completed her secondary education in 1977 and began working. Subsequently, she pursued a number of short-courses on a part-time basis. In 1986, she graduated from the Institute of Development Management (present-day Mzumbe University) with an advanced diploma in public administration.[3]

Between 1992 and 1994, she attended the University of Manchester and earned a postgraduate diploma in economics.[4] In 2015, she obtained her MSc in Community Economic Development via a joint-programme between the Open University of Tanzania and the Southern New Hampshire University.[3]
NB:Watu waliosoma kwa kuungauunga nakuwa na mashaka na IQ zao kuwa ndogo..ni jitihada na kudra ndio zinawafikisha juu

 
Unajua viongozi wetu ndo mnasababisha jambo linakuwa kubwa.
Hilii halikuwa jambo la kutuletea sisi. Kwamba kwa sababu ni mbobezi wa masuala ya uongozi basi tumwonee huruma ama?
Mh. Rais anamda wa kutosha sana 'kuwaprove wrong' wale wenye mashaka nae, vinginevyo maneno ya katibu yatasound kama exicuse kwa kile kinachoonekana kama makosa ya wazi kwa serikali hii.
They do the same mistakes kama kwenye chanjo....Unaanza kuwafanya watu waanze kudadisi na ku prove what is said...Why are our people doing this?
 
Una HAKI ya Kusema ULIKUWA NA KASHFA YA RUSHWA LAKINI KAFUMBA MACHO KAKUTEUA
 


SHAKA HAMDU SHAKA: RAIS SAMIA SULUHU HASSAN NI MBOBEZI KATIKA MASUALA YA UONGOZI.

Umma waelezwe kuwa Anatosha na Atatuvusha.

Viongozi wa dini waombwa kuhubiri Amani na Mshikamano.

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema tokea Uhuru kupatikana 1961 na Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar kufanyika 1964 na hatimae Chama Cha TANU na ASP kuungana na kuzaliwa CCM 1977 hakijawahi kumpa mtu nafasi ya kuliongoza Taifa au kushika nyadhifa kubwa kama Urais wa nchi kwa majaribio au kubahatisha au bila kujiridhisha juu ya uwezo wake, maarifa yake, uzoefu wake kiungozi, na uzalendo wake kwa nchi

Kimesema kwamba sio sharti la kisheria wala kikatiba linalotaka mhusika kuifahamu jiografia na historia ya Tanzania kwa vile unaweza kuijua Kagera lakini usijue jiografia ya kisiwa cha Pemba ama unaweza kuijua Mtwara lakini usijue Jiografia ya Rombo na yote ni Tanzania ila ukipewa dhamana kubwa katika Taifa utajua kila kichochoro na kinachoendela kwa vile umebeba muhimili wenye nguzo thabiti ya kulisimamisha Taifa.

Katibu wa halmashauri Kuu ya CCM Taifa Shaka Hamdu Shaka ameyasema hayo katika Ibada ya kuweka wakfu na harambee ya jengo la Utawala na shule ya Biblia katika Kanisa la Pentacostal Moto Moto lilipo Boko Kinondoni Dar Es Saalam ambapo alisema Rais Samia ameudhihirishia Umma ndani na nje kuwa anaielewa vyema nchi anayoiyongoza, lakini pia anao washauri mahiri wenye weledi katika fani mbali mbali pamoja na kuweka mbele maslahi ya Taifa.

“Niwahakikishie watanzaia kupitia mkusanyiko huu kuwa Rais Samia ni msomi mzuri katika maendeleo ya utawala na uchumi ambae ametumikia na kushika nyadhifa mbali mbali za kiserikali (Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) pamoja na mashirika ya kitaifa na kimataifa duniani, ni mtu bigwa kabisa na anatosha hivyo atatuvusha kama alivoweza kutuvusha Taifa hili lilipopitia katika maumivu na nyakati ngumu katika historia yetu lakini leo tumebaki kuwa wamoja” Alisema Shaka

Amefahamisha kuwa kadri ya anavyoendelea kuiongoza nchi Rais Samia ameendelea kuudhihirishi Ummakuwa yeye ni msomi mbobezi kwenye maendeleo ya uchumi na ndio maana hatua ya kwanza kubwa na ya kupigiwa mfano ni kuilekeza benki kuu ya Tanzania kuhakikisha masharti na riba za mikopo katika mabenki ya kibiashara hapa nchini zinapungua na kuwa rafiki kwa wakopaji na muda mfupi ujao watanzania watarajie kuona mabadiliko makubwa katika ukuaji wa uchumi nchini pamoja na kuongezeka kwa mzunguko wa fedha kupitia kipato cha mtu mmoja mmoja

“Serikali inayoongwa na Rais Samia imepata bahati (Leo) hii milango ya uchumi wa nchi imeendelea kufunguka na kuwa wazi siku hadi siku jumuiya, mashirika, taasisi na wafanyabisahara wa kubwa wa kitaifa na kimataifa wameendelea kuja Tanzania kuitikia wito wa Rais wetu kuja kuwekeza katika maeneo muhimu ambayo yatakuwa kichocheo cha ukuaji wa uchumi wetu lakini kutoa fursa za ajira kwa Vijana na Wanawake sambamaba na kurahisha upatikani wa bidhaa muhimu kwa kuzalisha malighafi kutoka ndani baada ya kutegemea toka nchi za jirani na maeneo mengine nje ya Tanzania.

“Hii ndio faida kubwa ya kuwa na Rais anaeijua nchi yake, anaejua anaowaongoza wanahitaji nini, kwa wakati upi na yeye asimame katika mrengo upi bila ya kuyumbishwa na mikingano ya ndani na nje. Rais Samia amekamilika kwa kila sifa ambayo dunia ya leo inauhitaji mkuwa wa Rais wa nchi wa aina yake, niseme tena Tanzania Mwenyezi Mungu ametubariki” Alisema Shaka

Hata hivyo Katibu hiyo wa Itikadi na Uenezi amewahikishia viongozi wa dini kuwa Serikali za CCM daima zitaendelea kuheshimu na kuthamini jitihada za waumini wa dini zote katika kusongeza Taifa kiimani na kimaendeleo hivyo viongozi wa dini wanategemewa sana katika kuendelea kuwaunganisha Watanzania.

"Taasisi za Dini mna mchango mkubwa katika kudumisha amani, kustawisha maisha ya wananchi na kupambana na umasikini. Hivyo niwasihi waumini na watanzania wote kuendelea kuheshimiana na kuvumiliana kwenye tofauti za kidini zinazojitokeza ili kuendelea kudumisha amani na utulivu hapa nchini. Pamoja na kuendelea kukumbushana kuwa Amani na utulivu ni sehemu ya kichocheo kikubwa cha maendeleo ya taifa, hivyo ni vyema viongozi wa dini kuendelea kuhubiri amani kwa waumini wenu ili iendelee kudumu” Alisema Shaka

Katika shuhuli hiyo Mhe Rasi Samia Suluhu Hassan alichangia shillingi Millioni 10 kuunga mkono jitihada za kanisa hilo ambapo jumla ya shillingi Millioni 24 zilichngawa na waumini wa kanisa hilo .

IMG-20210815-WA0049.jpg


IMG-20210815-WA0051.jpg


IMG-20210815-WA0050.jpg


IMG-20210815-WA0042.jpg


IMG-20210815-WA0045.jpg
 
Back
Top Bottom