Shaka: Wanaotaka Urais 2025 wasahau, ni Rais Samia bara ni Rais Mwinyi visiwani mpaka 2030

2025 fomu ya Uchaguzi iprintiwe moja tu, Kila Rais wa CCM alihudumu miaka 10, tunataka amani na utulivu kwenye Taifa,
Urais ni uwezo na Si Zawadi mtu azawadiwe!!!

Kwamba wakiruhusiwa wengine kuchukua fomu watavuruga amani kivp?

What if mgombea wa CCM akionekana hatoshi dhidi ya upinzani?

Nisikuchoshe maana 2025 hapatakuwa na uchaguzi pia mwaka huo ni mbali Sana Bado.
 
Sasa Wewe Mambo makubwa anayoyafanya Rais Samia huyaoni?

Acheni wivu furahieni mafanikio ya nchi yenu,
 
Hapo kwa Ile style yetu ya bao la mkono itabidi itumike.
BAO la mkono ni Hadi mkono uwepo na ujue kufanya KAZI ya mguu Kwa kificho.

Mjadala huu utakuwa mkubwa sana 2024, Kuna Wana CCM wanaraise hoja kuwa kwake huyu ni Awamu ya pili maana anamalizia KAZI aliyoanza na Magu,

Hivyo kama anautaka, Wanachama waruhusiwe kuchukua fomu, Ili atakayekubalika apitishwe.

Pia swali ni je!!! Nani aliyekuwa nyuma ya gazeti la uhuru kumsemea kuwa HATOGOMBEA?

Hoja hizo zijibiwe vizuri.
 
Kwanza hadi saizi sijamsikia mwanaccm yeyete kutaka Urais..

Pili sidhani kama Wana hiyo sababu maana Kwa jinsia mama anaupiga mwingi hawana Sababu Wala hoja ya kwa nini asigombee tena na wao ni mashahidi wa anachofanya Rais Samia.
 
Sasa Wewe Mambo makubwa anayoyafanya Rais Samia huyaoni?

Acheni wivu furahieni mafanikio ya nchi yenu,
Unafanya utafiti kuhusu kukubalika kwake Kwa wananchi?

Mnataka Nchi iende UPINZANI?
 
Kwanza hadi saizi sijamsikia mwanaccm yeyete kutaka Urais..

Pili sidhani kama Wana hiyo sababu maana Kwa jinsia mama anaupiga mwingi hawana Sababu Wala hoja ya kwa nini asigombee tena na wao ni mashahidi wa anachofanya Rais Samia.
Subiri ifike 2024 kuanzia July joto lipande vzr.

Kuna tofauti kubwa kati ya kuona MBALI na kuona MBELE.

Tusubiri.
 
Ngumu kwako, watz wote tunalamba asali we itakuwa ni mkenya
Kwakuwa maamuzi ni ya mkutano mkuu kumpitisha mgombea, basi kiongozi shaka asubili muda na wakati utakapotimia na afahamu hakuna mkutano mkuu uliowahi kumpitisha Rais Samia kugombea nafasi hiyo bali ameupata kwa kudra za Mungu kama alivyowahi kunena mwenyewe.

Binafsi naona kuna haja ya nafasi hiyo ya urais, chama kuruhusu wanachama wake kugombea kama ilivyokuwa kwa marais waliopita na wala hakujawahi kuwa na utamaduni, mila, desturi, taratibu, kanuni, sheria au katiba yenyewe ndani ya CCM inayoeleza juu ya taratibu za kugombea nafasi hiyo nyeti ndani ya nchi endapo tu Rais aliyeko madarakani atarithi nafasi hiyo kutoka nafasi aliyepo tofauti na hivyo Shaka aeleze ni wapi pameandikwa utaratibu huo alioutaja.

Naamini muda ukiwadia,wapo wanachama watajitokeza kumpokea Rais Samia kijiti vinginevyo itolewe fomu moja kama ilivyowahi kutokea nyakati za nyuma jambo ambalo si demokrasia wala afya kwa chama.
 
Binafsi sina shida ata akikaa miaka 100 ila kila rais anasifiwa amefanya makubwa sasa mbona nchi inasogea mwendo wa tractor? Mbona nchi zenye improvements inayoonekana hawapendi kusifusifu namna hii?

Rais Samia akitaka kuacha legacy nzuri sio kusikiliza hao praise team nahisi atuachie katiba ngumu zaidi ya ile rasimu ya Warioba ili atakaetumia public fund vibaya tuu kitanzi tuu hadharani au kifungo cha maisha maana hamna iliyoendelea kilelema hapa duniani
 
Haijaandikwa popote, Kwa Katiba ya CCM Wala ya nchi.

Kamati kuu iliweka ustaarabu na desturi hiyo Kwa mgombea urais aliyepitishwa na chama term ya kwanza.

Huyu hajawahi pitishwa na kamati kama mgombea urais Bali kama Makamo.

Hivyo watu waruhusiwe kuchukua fomu, apitaye na apite.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…