Shambulizi la Lissu: Wanaomdhania dereva anahusika sio wajinga, Wana hoja za msingi. Je, anahusika?

Shambulizi la Lissu: Wanaomdhania dereva anahusika sio wajinga, Wana hoja za msingi. Je, anahusika?

Pascal Mayalla hapa huwezi jibiwa swali hata moja kati ya ulilouliza, nilichokiona hapa hawa wafuasi wa hicho chama wanapingana na wanachokipigania. Sasa tuwaelewe vipi?

Si wanataka uhuru wa kujieleza na kuhoji mambo, sasa mbona wao hawatoi huo uhuru wa kuhojiwa na wao. Wakiulizwa swali defense yao ni kushutumu mtu mara kachukue buku saba Lumumba, utasikia pia unataka uupate uteuzi.
MTU ANASHINDWA KUKIFANYA HICHO ANACHOKIPIGANIA ILI AWE MFANO BORA.... SI UNAFIKI HUU.


Hayo maswali uliyouliza, wengi wamehoji yanayofanana ila wanaambulia kashfa tu.
We nawe ni una shida mahala, mpaka sasa hujaona thread zilizomjibu na kumuuliza huyu msukuma maswali ?? Mwite arudi jukwaani ajibu pia maswali yake maana yanazidi kupile up! Au kama una mapafu ,mjibie!!
 
Hili ni bandiko la maswali kwa Tundu Lissu na dereva wake, kufuatia shambulio la Lissu,
Shambulizi la Lissu, Wanaomdhania Dereva Anahusika, Sio Wajinga!, Wana Hoja za Msingi!. Jee Anahusika?.
Maswali haya ni kufuatia hoja za Lissu kwenye bandiko hili.
Mhe. Tundu Lissu,
Kwanza pole sana kwa yaliyokusibu.
Umezungumza mengi kuhusu kilichotokea mwaka mmoja uliopita, ila watu wanaohoji kuhusu dereva wako, nakuomba sana usiwaite wajinga, au wametumwa, kwa sababu mashaka yao ni very valid.

Kwa vile mashuhuda ni nyinyi wawili tuu, wewe na dereva wako, then kuna mambo tungependa kujua kutoka kwa Lissu mwemyewe na dereva wake.

Hoja kuwa tumetoka naye mbali hivyo tunaaminiana, hazina mashiko mbele ya watu na kazi zao. Lissu alipotoka na dereva wake, anaweza kujilinganisha Dr. Slaa na mlinzi wake Kagenzi walipotoka?, halafu what happened?!. Kwenye mambo ya assignment, anaweza hata akatumika mke wako aliyekuzalia wanao, sembuse itakuwa dereva tuu mliotoka nae mbali!.
Baadhi ya maswali ni haya...
  1. Baada kuona kuna gari linawafuatilia, mlichukua hatua gani?.
  2. The common sense ya kufuatiliwa inaelekeza, uki note you're followed, hatua ya kwanza ni kumpote anaye kufollow kwa makusudi, ili kwanza kujiridhisha kuwa anakufollow.
  3. Ukiisha jiridhisha you are followed, una change direction kumpoteza maboya.
  4. Ukimuona bado yupo, then kama uko fit, unamlengesha mahali kwenye kona ambapo hawezi kuchomoka, mnamalizana!.
  5. Kama hauko fit, unamlengesha kwenye safe area ,usually sehemu open kwenye makundi ya watu na kumripoti kunakohusika.
  6. Baada ya kuona mnafuatwa, kwa nini mliendelea kuelekea nyumbani?.
  7. Mlipofika mkasimama, mkawaona watu wawili wanashuka na AK 47, kitendo tuu cha kujua tuu bunduki zile ni AK 47, hii maana yake ni close proximity, kwenye shooting that close!, risasi 38!, dereva huyu amesalimikaje asipitiwe hata na moja?.
  8. Ametokaje kwenye gari na kujificha chini ya gari ya jirani bila kugundulika?!.
  9. Anafichwa nini kuhojiwa?, kuna nini kinafichwa?.
  10. Maswali yataendelea
Huko nyuma niliisha wahi kuzungumza haya kuhusu dereva wa Lissu.

Mpaka sasa the situation ya shambulio la Lissu as it is, limefanywa na watu wasiojulikana. Serikali yetu imeshindwa kuwabaini, lakini sisi watu wa media, tunaweza kusaidia kama nilivyosema hapa.
WanaJF, Je tuisaidie Serikali yetu inaposhindwa au tusubiri ishindwe, tuibeze na kuizomea kuwa haiwezi? - JamiiForums
Hitimisho.
The only defence ya Dereva wa Lissu has nothing to do na hiyo shooting, ni uzito tuu wa serikali kugoma kuita wachunguzi wa nje. Ingekuwa ni inside job ya Chadema, tungeshuhudia serikali fasta ingechunguza!.

Lakini kwa vile wasiojulikana ni hawa
Shambulio la Lissu: Wajue Wasiojulikana Watakaojulikana na 'Wasiojulikana' Ambao Kamwe, Hawatajulikana!. - JamiiForums

Tusitegemee lolote jipya hapa.
Tundu Lissu, just get well soon, na sasa inakubidi uchangue kati ya uanaharakati na kuishi.

Pole.
P.
Rejea
Tuacheni Ramli Chonganishi: Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!. "Karma Ndio Pekee Hutoa Hukumu ya Haki Hapa Duniani!. - JamiiForums

Handling of Serious Security Issues: Kama CHADEMA Takes Things For Granted Kwa Uzembe Hivi!, Jee Ikulu Yetu Wangeiweza?! - JamiiForums

Tundu Lissu: Polisi wa Tanzania hawana mamlaka ya kunihoji nikiwa Kenya au kwingineko nje ya mipaka ya Tanzania - JamiiForums

P.
Pascal

hayo maswali yote Lissu keshayajibu,

better stay quite than openly demonstrate to people kwamba now unalilia sana mkate.

Bro...this is too low to your level
 
Aisee kweli walimu wana kazi ngumu hivi na wewe ni great thinker?wewe utakuwa sijui mtu wa namna gani? Yaani dah!unasikitisha labda kama hujui ajali au hata uvamizi huwa hautokei wala hauwezi kufanikiwa 100%.katika kitu ambacho wasiojulikana ukiwapo na wewe wanashangaa basi ni kusalimika kwa watu hawa wawili.Ila ujue kuwa Mungu yupo na anatenda kazi maana alisha ahidi kutuokoa dhidi ya watesi wetu.Mungu yupo na alishajidhihirisha katika tukio hilo.Shetani Umeshindwa
Great thinker always anauwezo mkubwa wa kubadili text message to image or picture message. Sasa wewe ktk tukio hili la lisu umefeli kabisa
 
Great thinker always anauwezo mkubwa wa kubadili text message to image or picture message. Sasa wewe ktk tukio hili la lisu umefeli kabisa
Ok sawa.Tatizo nililogundua ni kuwa tupo tofauti kiitikadi na kifalsafa kwa hiyo tukiendelea kueleweshana katika hili hatutafika.Ila kaama unadhani Lissu alijishambulia,sawa.Na kama unaona mbowe ndo alomshambulia Lissu sawa.kama unaona kuna mtu nje ya taasisi zote 2 ndo amehusika,sawa.kama huoni mkono wa serikali pia kwako ni sawa ila kwangu naona serikali ikihusika 100%.
 
Kaka Pascal ata Mimi huwa nina mashaka na yule dereva.Maana ata ukimuangalia usoni anaonekana ana mengi kuhusu like tukio.
Mimi nahisi yule jamaa kama pandikizi Fulani maana Tundu Lissu aliisumbua sana serikali sakata la watu kufukiwa mgodini Bilyanhulu.
Tusubiri KARMA itaamua.
 
Bro...this is too low to your level
Unaangusha hiyo ID(2008)...Read Paskal between lines (his whole work while thinking critically)! For sure,....you will find out ...that He is putting on the table a serious allegation against the government regarding 'Lissu Saga'!! He has to come forward for this and explain in details.
 
Acheni porojo nyie,hivi unajua kuvamiwa wewe?Yani wavamizi walitoa hadi mda wa lisu kulaza kiti na dereva kushusha ndipo wakaanza kumimina risasi ovyo?Alijuaje kama wamekuja kumshambulia na sio kumteka?Hili tukio ukilijengea image unakuta unapata movie ya kibongo ambayo muuaji anaonja sumu ka imekolea.
Sasa si mkamkamate dereva ahukumiwe? mnangoja nini?
 
Hili ni bandiko la maswali kwa Tundu Lissu na dereva wake, kufuatia shambulio la Lissu,
Shambulizi la Lissu, Wanaomdhania Dereva Anahusika, Sio Wajinga!, Wana Hoja za Msingi!. Jee Anahusika?.
Maswali haya ni kufuatia hoja za Lissu kwenye bandiko hili.
Mhe. Tundu Lissu,
Kwanza pole sana kwa yaliyokusibu.
Umezungumza mengi kuhusu kilichotokea mwaka mmoja uliopita, ila watu wanaohoji kuhusu dereva wako, nakuomba sana usiwaite wajinga, au wametumwa, kwa sababu mashaka yao ni very valid.

Kwa vile mashuhuda ni nyinyi wawili tuu, wewe na dereva wako, then kuna mambo tungependa kujua kutoka kwa Lissu mwemyewe na dereva wake.

Hoja kuwa tumetoka naye mbali hivyo tunaaminiana, hazina mashiko mbele ya watu na kazi zao. Lissu alipotoka na dereva wake, anaweza kujilinganisha Dr. Slaa na mlinzi wake Kagenzi walipotoka?, halafu what happened?!. Kwenye mambo ya assignment, anaweza hata akatumika mke wako aliyekuzalia wanao, sembuse itakuwa dereva tuu mliotoka nae mbali!.
Baadhi ya maswali ni haya...
  1. Baada kuona kuna gari linawafuatilia, mlichukua hatua gani?.
  2. The common sense ya kufuatiliwa inaelekeza, uki note you're followed, hatua ya kwanza ni kumpote anaye kufollow kwa makusudi, ili kwanza kujiridhisha kuwa anakufollow.
  3. Ukiisha jiridhisha you are followed, una change direction kumpoteza maboya.
  4. Ukimuona bado yupo, then kama uko fit, unamlengesha mahali kwenye kona ambapo hawezi kuchomoka, mnamalizana!.
  5. Kama hauko fit, unamlengesha kwenye safe area ,usually sehemu open kwenye makundi ya watu na kumripoti kunakohusika.
  6. Baada ya kuona mnafuatwa, kwa nini mliendelea kuelekea nyumbani?.
  7. Mlipofika mkasimama, mkawaona watu wawili wanashuka na AK 47, kitendo tuu cha kujua tuu bunduki zile ni AK 47, hii maana yake ni close proximity, kwenye shooting that close!, risasi 38!, dereva huyu amesalimikaje asipitiwe hata na moja?.
  8. Ametokaje kwenye gari na kujificha chini ya gari ya jirani bila kugundulika?!.
  9. Anafichwa nini kuhojiwa?, kuna nini kinafichwa?.
  10. Maswali yataendelea
Huko nyuma niliisha wahi kuzungumza haya kuhusu dereva wa Lissu.

Mpaka sasa the situation ya shambulio la Lissu as it is, limefanywa na watu wasiojulikana. Serikali yetu imeshindwa kuwabaini, lakini sisi watu wa media, tunaweza kusaidia kama nilivyosema hapa.
WanaJF, Je tuisaidie Serikali yetu inaposhindwa au tusubiri ishindwe, tuibeze na kuizomea kuwa haiwezi? - JamiiForums
Hitimisho.
The only defence ya Dereva wa Lissu has nothing to do na hiyo shooting, ni uzito tuu wa serikali kugoma kuita wachunguzi wa nje. Ingekuwa ni inside job ya Chadema, tungeshuhudia serikali fasta ingechunguza!.

Lakini kwa vile wasiojulikana ni hawa
Shambulio la Lissu: Wajue Wasiojulikana Watakaojulikana na 'Wasiojulikana' Ambao Kamwe, Hawatajulikana!. - JamiiForums

Tusitegemee lolote jipya hapa.
Tundu Lissu, just get well soon, na sasa inakubidi uchangue kati ya uanaharakati na kuishi.

Pole.
P.
Rejea
Tuacheni Ramli Chonganishi: Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!. "Karma Ndio Pekee Hutoa Hukumu ya Haki Hapa Duniani!. - JamiiForums

Handling of Serious Security Issues: Kama CHADEMA Takes Things For Granted Kwa Uzembe Hivi!, Jee Ikulu Yetu Wangeiweza?! - JamiiForums

Tundu Lissu: Polisi wa Tanzania hawana mamlaka ya kunihoji nikiwa Kenya au kwingineko nje ya mipaka ya Tanzania - JamiiForums

P.
Pascal Hiyo nadharia hapo juu no. 7 wengi inatuacha na maswali mengi ya kujiuliza.Jinsi dereva alvyopona bila hata kupata mkwaruzo katikati ya mvua ya risasi.
Mkanganyiko mwingine ni pale tulipoambiwa dereva alimgeuza Lissu akalalia kiti kiasi ambacho mguu wa kulia ukaathirika zaidi, halafu ndipo dereva akateremka na kujificha.Hapa kuna wingu zito.
 
Pascal,subiri teuzi.

"Baada kuona kuna gari linawafuatilia, mlichukua hatua gani?".
Walichukuwa tahadhali,ndiyo maana wakanusurika.

"Ukiisha jiridhisha you are followed, una change direction kumpoteza maboya"
Hiyo Dodoma ina ukubwa gani hadi ukampoteza anayekufuatilia.

"Ukimuona bado yupo, then kama uko fit, unamlengesha mahali kwenye kona ambapo hawezi kuchomoka, mnamalizana!".
Wangemalizanaje wakati Lissu ana mkoba wa files za mambo ya bunge na wasiojulikana wana SMG.Hiyo mbinu yako haiwezekani kwani kwa vyovyote vile anayekufuatilia atakuwa amejiandaa.Jambo la kustukizwa unaweze kujiandaa?.

'Kama hauko fit, unamlengesha kwenye safe area ,usually sehemu open kwenye makundi ya watu na kumripoti kunakohusika'.
Hivi kuna safe area kuzidi yale makazi ya viongozi wa serikali yenye walinzi waliyosheheni silaha za kivita na CCTV camera?.Una nini wewe Mayalla.Fikiri angeenda sehemu ya wazi,unadhani wangeacha kummininia marisasi na tukaambia majambazi walitaka kupora hela.Lissu amewazidi maafira.Wchuchumae tu,wamevuliwa nguo.

"Baada ya kuona mnafuatwa, kwa nini mliendelea kuelekea nyumbani"?.
Nyumbani kwake ndiko nyumbani kwa viongozi wa serikali.Kama nyumbani kwa viongozi wa serikali zinamininwa makuni ya risasi,sina hakika eneo gani lingine wangeshindwa kufanya hivyo.


"Mlipofika mkasimama, mkawaona watu wawili wanashuka na AK 47, kitendo tuu cha kujua tuu bunduki zile ni AK 47, hii maana yake ni close proximity, kwenye shooting that close!, risasi 38!, dereva huyu amesalimikaje asipitiwe hata na moja"?.
Wangekuwa na shida na dereva naye wangemcharaza risasi.HAWAKUWA NA HAJA NAYE.

"Ametokaje kwenye gari na kujificha chini ya gari ya jirani bila kugundulika"?!.
Narudia.Wangemhitaji wangemfuata,ndiyo maana hata baada ya tukio hawakushaghulika nae hadi pale walipoona mipango imeshindikana.

"Anafichwa nini kuhojiwa?, kuna nini kinafichwa"?.
HIZO BLA BLA TU.Alikuwepo Nairobi,na sasa Ubelgiji.Lissu katoa mwongozo.Ulikuwa ni wakati muafaka kuruhusu uchunguzi HURU ili kama hawa akina Mbowe ndiyo watekelezaji wa huu unyama WASHIKISHWE ADABU maana wanatuchafulia Taifa letu.Cha ajabu wanaogopa uchunguzi huru wa kimataifa.AJABU.

MWISHO WA UBAYA NI AIBU.
 
Pascal - kama Dereva unamtilia shaka kwanini CCTV camera zilitolewa? Na kwanini zisiachwe ili kuisaidia Polisi katika upelelezi? Mkapa hakukosea kusema waandishi Makanjanja[emoji41]
Kwanini hamtaki kuwaza kama huyo dereva alishirikiana na waliotoa camera?Kuondolewa kwa camera kunamtoa vipi dereva kuhusika na tukio?
 
Pascal Hiyo nadharia hapo juu no. 7 wengi inatuacha na maswali mengi ya kujiuliza.Jinsi dereva alvyopona bila hata kupata mkwaruzo katikati ya mvua ya risasi.
Mkanganyiko mwingine ni pale tulipoambiwa dereva alimgeuza Lissu akalalia kiti kiasi ambacho mguu wa kulia ukaathirika zaidi, halafu ndipo dereva akateremka na kujificha.Hapa kuna wingu zito.
Na wakati huo wauaji walikua bado wanasubiri akina lusu wamalize kujificha ndo waanze kumimina risasi
 
Nukuu

ni uzito tuu wa serikali kugoma kuita wachunguzi wa nje. Ingekuwa ni inside job ya Chadema, tungeshuhudia serikali fasta ingechunguza!.

Pascal Mayalla kwa kuwa na wewe ushaonja uchungu wa Serikali ya Awamu 5 kwa aina yake.

Nakuuliza swali.
Kwa nini serikali inaogopa uchunguzi huru ikiwemo kusaidiwa na wachunguzi kutoka nje ya nchi?
 
Back
Top Bottom