Shambulizi la Lissu: Wanaomdhania dereva anahusika sio wajinga, Wana hoja za msingi. Je, anahusika?

Shambulizi la Lissu: Wanaomdhania dereva anahusika sio wajinga, Wana hoja za msingi. Je, anahusika?

Hili ni bandiko la maswali kwa Tundu Lissu na dereva wake, kufuatia shambulio la Lissu,
Shambulizi la Lissu, Wanaomdhania Dereva Anahusika, Sio Wajinga!, Wana Hoja za Msingi!. Jee Anahusika?.
Maswali haya ni kufuatia hoja za Lissu kwenye bandiko hili.
Mhe. Tundu Lissu,
Kwanza pole sana kwa yaliyokusibu.
Umezungumza mengi kuhusu kilichotokea mwaka mmoja uliopita, ila watu wanaohoji kuhusu dereva wako, nakuomba sana usiwaite wajinga, au wametumwa, kwa sababu mashaka yao ni very valid.

Kwa vile mashuhuda ni nyinyi wawili tuu, wewe na dereva wako, then kuna mambo tungependa kujua kutoka kwa Lissu mwemyewe na dereva wake.

Hoja kuwa tumetoka naye mbali hivyo tunaaminiana, hazina mashiko mbele ya watu na kazi zao. Lissu alipotoka na dereva wake, anaweza kujilinganisha Dr. Slaa na mlinzi wake Kagenzi walipotoka?, halafu what happened?!. Kwenye mambo ya assignment, anaweza hata akatumika mke wako aliyekuzalia wanao, sembuse itakuwa dereva tuu mliotoka nae mbali!.
Baadhi ya maswali ni haya...
  1. Baada kuona kuna gari linawafuatilia, mlichukua hatua gani?.
  2. The common sense ya kufuatiliwa inaelekeza, uki note you're followed, hatua ya kwanza ni kumpote anaye kufollow kwa makusudi, ili kwanza kujiridhisha kuwa anakufollow.
  3. Ukiisha jiridhisha you are followed, una change direction kumpoteza maboya.
  4. Ukimuona bado yupo, then kama uko fit, unamlengesha mahali kwenye kona ambapo hawezi kuchomoka, mnamalizana!.
  5. Kama hauko fit, unamlengesha kwenye safe area ,usually sehemu open kwenye makundi ya watu na kumripoti kunakohusika.
  6. Baada ya kuona mnafuatwa, kwa nini mliendelea kuelekea nyumbani?.
  7. Mlipofika mkasimama, mkawaona watu wawili wanashuka na AK 47, kitendo tuu cha kujua tuu bunduki zile ni AK 47, hii maana yake ni close proximity, kwenye shooting that close!, risasi 38!, dereva huyu amesalimikaje asipitiwe hata na moja?.
  8. Ametokaje kwenye gari na kujificha chini ya gari ya jirani bila kugundulika?!.
  9. Anafichwa nini kuhojiwa?, kuna nini kinafichwa?.
  10. Maswali haya yameendelea kwa msaada wa mwana jf huyu

  11. Bunduki iliyotumika waliiona ni AK 47 iliyokuwa na full magazine (risasi 40) ambayo ilimimina risasi zote 40 at close range. Kati ya hizo 17 zilizama kwenye miguu, mikono na kiuno cha Tundu Lissu.
  12. Risasi zilimiminwa kutoka upande wa kulia wa gari ambao ni upande wa dreva lakini dreva hakupatwa na risasi hata moja na alipata hata fursa ya kuteremka kwenye gari na kwenda ku take cover kwenye magari yaliyokuwa yamepaki eneo hilo. Assailants walikuwa upande wa kulia wa gari, hivyo risasi zilizama zaidi kwenye mguu wa kulia, paja la kulia, mkono wa kulia, kiuno upande wa kulia na kutokea tumboni na mkono wa kushoto. These are the documented medical forensic clues.
  13. Majeshi yetu hayana bunduki za AK 47, yana SMG badala yake ambayzo full magazine zake ni risasi 30. Bunduki za AK47 zinamilikiwa na majambazi yanazozipata kutoka kwa wanajeshi wa Burundi wanaokimbilia Tanzania ambao huwa wanaziuza kwa bei ya shillingi 20,000 tu!! Silaha hizi ndizo zilitikisa huko Mkuranga, Kibiti na Rufiji.
  14. Hakuna mwanajeshi ye yote (aliyepata mafunzo ya kijeshi) ambaye ampige mtu (adui) risasi 38 from an AK 47 gun at a close range halafu mtu huyo asalimike!! Never on earth. Kwanza atahitaji risasi moja tu na atafumua kichwa au moyo. Hivyo it is so obvious kwamba assailants wa Tundu Lissu walikuwa ni wahuni tu wa mitaani wasiojua kutumia bunduki. Yaani risasi 38 zote zinakosa target (kichwa au moyo) zinaishia kupiga makalio na hewa!! Hili halihitaji askari wa Scotland yard kulitambua. Swali ni nani aliwakodi hawa wahuni wasiojua shabaha? Kwa nini dreva wa Lissu akawa mkimbizi nchi za nje? Nini kakimbia? Kwani hata polisi wetu wakienda kumhoji huko kwani atasema lo lote la maana? Huko hawawezi kumu arrest. Alipaswa kuwa behind bars ili aeleze vizuri. Tundu Lissu alipaswa kujua hili. Mara nyingi kikulacho unacho nguoni mwako. Eti ninamuamini sana. Mbele ya pesa kunakuamini mtu? Yaani apewe shillingi million 500 aache kukumaliza? Yaani Tundu Lissu hajui kwamba "Money is the source of all evils in this world?"
  15. Hospitali ya serikali ya Dodoma na madaktari wa serikali wa Dodoma hospital ndiyo waliookoa maisha yake. Kama serikali ilikuwa na mpango wa kumuua, ingalishindwaje kumumalizia hapo hapo kwenye hospitali yake ya Dodoma humo humo operation theatre? It was so simple eg hiyo damu aliyopewa hangeipata au angalipewa incompatible blood ambayo ingalimumaliza hapo kwa hapo! Lazima aishukuru serikali kwa kuokoa maisha yake badala ya kuilaumu. Upinzani haupaswi kuwa wa aina hii. Tujifunze kwenye nchi zilizotutangulia.
  16. Bunduki kama AK 47 au SMG ikiunguruma si mchezo. Kwa askari yo yote trained, hata kama naye ana bunduki ya aina hiyo hiyo lakini kashutikizwa, reaction ya kwanza ni ku take cover. Atalala chini na ku craw hadi mahala salama. Hapo ndipo atatafuta kuona adui/ maadui walipo na kutafakari kama anao uwezo wa kupambana nao au kuomba reinfocement au kutokomea kabisa kwenye eneo hilo. Trained soldier hakurupuki tu kuanza kurusha risasi ovyo ovyo anapositukizwa na milio ya risasi. Hivyo kwa jinsi tukio lilivyotokea hapo usingalitarajia askari waliokuwa karibu na eneo hilo kuwa wangaliweza kuanza kujibu mapigo kwa muda huo mfupi uliotumika kabla ya majambazi hayo kutokomea kusikojulikana. Dreva wa Lissu aliyaona live na alitaja hata aina ya gari yalilotumia na plate namba zake. Polisi walikamata magari kadhaa ya aina hiyo lakini dreva huyo alikataa kwenda kuyatambua na hivyo yakabidi yaachiwe kwani hakuna shahidi aliyejitokeza. Shahidi muhimu alikuwa Nairobi akidaiwa anapata tiba ya kisaikolojia. Sasa hivi Lissu anasema dreva huyo yuko masomoni Ubeligiji. Sijui anasoma digrii gani hapo Leuven University teaching hospital anapotibiwa boss wake. Jamani aacheni kutufanya wajinga. Pascal yuko sahihi kabisa.
  17. Huko nyuma niliisha wahi kuzungumza haya kuhusu dereva wa Lissu.

Mpaka sasa the situation ya shambulio la Lissu as it is, limefanywa na watu wasiojulikana. Serikali yetu imeshindwa kuwabaini, lakini sisi watu wa media, tunaweza kusaidia kama nilivyosema hapa.
WanaJF, Je tuisaidie Serikali yetu inaposhindwa au tusubiri ishindwe, tuibeze na kuizomea kuwa haiwezi? - JamiiForums
Hitimisho.
The only defence ya Dereva wa Lissu has nothing to do na hiyo shooting, ni uzito tuu wa serikali yetu kufanya upelelezi wa tukio hili na kugoma kuita wachunguzi wa nje. Ingekuwa ni inside job ya Chadema, tungeshuhudia serikali fasta ingechunguza!.

Lakini kwa vile wasiojulikana ni hawa
Shambulio la Lissu: Wajue Wasiojulikana Watakaojulikana na 'Wasiojulikana' Ambao Kamwe, Hawatajulikana!. - JamiiForums

Tusitegemee lolote jipya hapa.
Tundu Lissu, just get well soon, na sasa inakubidi uchangue kati ya kuendelea na uanaharakati na kuishi kwa mashaka, au uamue kupunguza makali na kuishi kwa amani.

Pole Sana Mhe. Tundu Lissu, Get Well Soon.
P.
Rejea
Tuacheni Ramli Chonganishi: Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!. "Karma Ndio Pekee Hutoa Hukumu ya Haki Hapa Duniani!. - JamiiForums

Handling of Serious Security Issues: Kama CHADEMA Takes Things For Granted Kwa Uzembe Hivi!, Jee Ikulu Yetu Wangeiweza?! - JamiiForums

Tundu Lissu: Polisi wa Tanzania hawana mamlaka ya kunihoji nikiwa Kenya au kwingineko nje ya mipaka ya Tanzania - JamiiForums

P.
Umenena vema,
Swala ni moja a punguza kuishi kwa hisia na kutuhu watu.Pili atambue yeye siye wa kwanza kupigwa risasi .....Kuachiliwa kwakwe kwa adui ni kwa sababu ya kujiamini zaidi kuliko kumuamini Mungu.

Kwa serikali kufanya uchunguzi ni Dereva ni mtu wa kwanza kwani kila uchunguzi una source ya kuanzia.

Mwisho aache kuwadanganya watanzania wasiojua kanuni za bunge,ni kweli hakufuata taratibu za serikali hakuzifuata,yeye siyo mtu wa pekee mpaka bunge likiuke utaratibu...amekuwa a kipiga kelele juu ya Bunge kukiuka taratibu,sasa wamemuonyesha namna gani huwa wanajitahidi na kupambana na watu wa style yake (wanaovunja taratibu) kuzisimamia.

Bado naamini hata ingekuwa Muhimbili bado angepata huduma na kulindwa...kwa kama ni ulinzi wapo madaktari na wahuguzi wengi ambayo uwenda ni wafuasi wake.Kwa maana hiyo bado nasema kimbiza kimbiza kuna jambo....polisi wasilaumiwe kwakuwa hawa kupata fursa ya kuruhusiwa kuifanya kazi yao.

Ni sisi watanzania tunaosukima vyombo vya usalama vifanye kazi kisiasa...however nawapongeza jeshi la polisi kipindi hiki hakuna wanasiasa wengi ndani yake wote wanasimamia taaluma.
Muulize Lisu kama a nafuatilia taarifa hata huko ulaya wapo viongozi wakubwa wa kisiasa waliwahi kupigwa risasi na mpaka kesho wahusika hawajakamatwa.

Ni vema sasa apunguze habari za kufikirika na kuipa nafsi yake nafasi ya kuyatambua yaliyo ya kweli.
 
Umejiona shujaa wa kuuliza maswali ya weledi? Kumbe wewe wa hovyo!
Hujiulizi
1. Kwanini sehemu yote hiyo ambayo inalindwa saa 24/7/30/365 days hapakuwa na mlinzi hata mmoja?
2. Kwanini CCTV camera zilinyofolewa mara baada ya tukio
3. Kwanini wanakataa independent investigation
4. Kwanini wasiende belgium kumhoji kama wana nia ya kweli/hawahusiki?
5. Kwanini serikali inaktaa watu kumwombea Lisu
6. kwanini serikali inaktaa watu kuvaa t shirt zenye picha na maandishi ya Lisu
7. Barabara nzima toka bungeni kuja kwa Lisu and his fellow Mps haikuwa na gari hata moja, kulikoni?

Ulitishwa Bungeni ukatishika, leo unajitokeza kutafuta uDC!
Yani kwa hoja hizi,Mayala bado yuko sahihi kabisa.Mmekazana na habari za walinzi mara CCTV nk.Kwani huyo dereva hawezi kuwa sehem ya hao waliotoa camera? Ni mambo ya ajabu lisu kupata mda wa kufanya press conference Kenya lkn akashindwa kuja kudai haki yake Tz. Anayetakiwa apiganie haki yake ni lisu na sio serikali, yani lisu ndo anapanga nini serikali ifanye ikitaka kumhoji,serious? Mara ooh polisi ya Tz haina mamlaka ya kunihoji mara wanifuate Belgium. Huyu mtu yuko serious? Wale anaodai wampe haki yake ndio haohao anakesha kuwakejeli na kuwadhihaki anafanya hivi makusudi tu
 
Ukweli wa yote, huwezi kuanza upelelezi bila shahidi/mshukiwa namba moja kuhojiwa. Yeye ndiye angetoa mwangaza upelelezi uanzie wapi, kitendo cha kumzuia shahidi ni jambo la kukwamisha upelelezi wenyewe.

Kama ni shida ni haki mnayoitafuta,kwanini shahidi namba moja azuiwe? Tukisema mlikwamisha kupatikana kwa haki tunakosea?

Tukumbuke jeshi la polisi lina taratibu zake za ufanyaji kazi pia, lilipotoka kitu kwa ajili ya ufanyaji kazi wake(kumuhoji dereva). Mlimsaidia?
Huyo ndiye aliyekuwa eneo la tukio anajua vitu vingi alivyoviona siku ile ya tukio kuliko mtu yeyote, yeye ndiye angeweza kusaidia hilo suala kiupana.

=======

Kiupande wa Lissu naye ana makosa, pamoja na kuwa mwanasheria anakiuka baadhi ya taratibu zinazofahamika. Huku akijinasibisha anafuata utawala wa sheria, napo simwelewi utawala wa sheria upi huo anaoudai?

Sote tunafahamu ukihisi hali ya hatari na namna ya kufuatiliwa. Ni Kutoa taarifa juu ya wasiwasi wa usalama wako kwa jeshi la polisi, yeye kaitisha mkutano na wanahabari ndiyo anaongea hayo na si kuripoti kwa idara husika yenye msaada kwake.
Sote tunajua Lissu ni mwanasiasa, kama ikidhaniwa ni njia yake ya kutafuta jina zaidi alilonalo. Maana kipindi kile wanasiasa wengi walitamka hayo, ila hakukuwa na chochote. Hivi kwa mantiki hii hilo suala lingepewa uzito gani kuliongea mbele ya kamera pasipo kuwapa taarifa wenye mamlaka ya kukusaidia.

Sasa kama yeye kama mwanasheria, kwanini akiuke utaratibu husika?

=========

Tukija upande wa wahalifu wale, sote hatujui ni kina nani na hatuna uhakika na tuhuma zinazotuhumiswa serikali.

Pia hatujui Tundu Antipas Lissu ana maadui wangapi, nje ya siasa, haswa kwenye taaluma yake ya sheria, kwenye biashara zake na kwingineko.

Maana hata 99% walengaji ni wahuni hawana mafunzo stahiki ya kijeshi, wamefundishiwa kichochoroni kutumia silaha. Mwenye mafunzo stahiki ya kijeshi ya utumiaji silaha, hawezi fyatua risasi kiholela namna ile.

Pia silaha iliyotumika ,(AK47 ingawa mwanzo ilisemwa ni SMG/sijui tushike lipi hapo? ) haimilikiwi na majeshi ya ndani ya nchi hii, hutumiwa kiholela na vikundi vya silaha vya nchi jirani na hivyo ndiyo huwauzia majambazi na wahuni huku.
Bado waliyofyatua risasi ni wahuni na si watu waliyofunzwa kutoka ndani ya system.

System maafisa wake wanatumia bunduki za mchina zenye kuchukua risasi 30 tu na si hiyo ya kirusi(Ak47) yenye risasi kubeba 40 .

============

Suala la kuitwa wapelelezi wa nje wasaidie upelelezi ndani ya nchi, si la kiholela kama kuita fundi bomba aje kukaza koki ya maji jikoni kwenye sink la kuoshea vyombo.

Wale wanaitwa kama kazi ya wapelelezi wa ndani ni ngumu kuwasaidia, au wanaruhusiwa kufanya kazi kama eneo husika lina kitu chenye maslahi na taifa lao.
Rejea tukio la kuungua kwa BOT, kuna wapelelezi wa nje walifika. Wale walikuja kwasababu mule kuna vitu vya taifa lao, si kuja kiholela tu.

Sasa wapelelezi wa ndani hilo suala halijawashinda, upelelezi wao walipotaka kuanzia ndiyo kumekwamishwa kisa mambo ya kisiasa.
Hawawezi kuitwa watu wa nje, kwa suala wanaloliweza watu wa ndani abadani.

Hakuna cha uchunguzi huru wala uchunguzi utumwa, hilo jambo kisheria halipaswi kushirikishwa majasusi wa nje ilihali wa ndani wanaliweza. Hebu tusitie siasa kwenye kazi za watu
 
Aliyesema kuwa askari hawakuwepo ni nani na alikuwa wapi akiangalia kuwa askari hawapo?


Kwa mada hii tunaomba ukae utulie tu maana uwezo wako tunaufahamu tuachie tuongee na kina paskali mayalla, gentamycine, misuli nk, hawa wanauwezo wa kuongea jambo likaeleweka. Ww nenda kaandae tu lile jedwali la viwanda mia moja kila mkoa. Mwaka unaenda ukingoni huu.
 
Muuaji huyu alikua anajifunza kuua kwa kutumia mwili wa lisu hahahahah risasi 38.Yani hata ktk movie sijawahi ona wingi wa risasi ka huu.Hili tukio liingizwe Guinness World Records.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
Ajabu la dunia, au ni mtoto anayecheza kibunduki kashika akijua ni ya gololi


Halafu Maafisa wa system risasi zao full magazine ni risasi 30 tu na hawatumii AK47
 
Paskali, wewe mbona hukuwakwepa na kuwapoteza? Walichokufanya ni wewe na wao mnaojuana. You fit to be potential "usiyejulikana". Poor you.
HUYO ACHANA NAE...NI MMOJA KWENYE KIKOSI CHA WASIOIJULIKANA...NA AKIENDELA NA YEYE ATAOKOTWA COCO BEACH.
 
Kwa mada hii tunaomba ukae utulie tu maana uwezo wako tunaufahamu tuachie tuongee na kina paskali mayalla, gentamycine, misuli nk, hawa wanauwezo wa kuongea jambo likaeleweka. Ww nenda kaandae tu lile jedwali la viwanda mia moja kila mkoa. Mwaka unaenda ukingoni huu.
mkuu nimecheka sana..KULA LIKE KAMA CHAI IVI...YAANI CHAI 3 ASUBUHI!!!!
 
Risasi 38 jembe bado lipo hai linarudi tena na moto ule ule, mjipange upya ss sijui mtatumia nyuklia???!
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
Ajabu la dunia, au ni mtoto anayecheza kibunduki kashika akijua ni ya gololi


Halafu Maafisa wa system risasi zao full magazine ni risasi 30 tu na hawatumii AK47
HAWATUMOO AK7 COZ IMEPITWA NA WAKATI...KUNA GOOGLE GLASS....DO YOU KNOW IT?
 
Hivi unajua unachokisema?
NDIYO NAJUA. KWANINI HIYO PRODUCT ILIPIGWA VITA? NI KWASABABU ILIKUWA INFUNUA MBINU/BIDS/KAMPUNI ZA SIRI AMBAZO WATEJA WAKE NI SERIKALI TU...HIVYO HATA TEKNOLOJIA PUBLIC ITASUBIRI SANA...

na mimi nikuulize:
UNANIJUA?
2. UNAIJUA INTERPOL?
 
Hata kama wangemuhoji huko Nairobi au Ubeligiji angesema hayo hayo ambayo amekuwa akiyasema kwenye social media na vyombo vingine vya habari kila mara ambayo hayana msaada wo wote wa kuwanasa hao assailant wake.

Kwa dalili zo zote dreva wake ni suspect number one.
1. Bunduki iliyotumika waliiona ni AK 47 iliyokuwa na full magazine (risasi 40) ambayo ilimimina risasi zote 40 at close range. Kati ya hizo 17 zilizama kwenye miguu, mikono na kiuno cha Tundu Lissu.

2. Risasi zilimiminwa kutoka upande wa kulia wa gari ambao ni upande wa dreva lakini dreva hakupatwa na risasi hata moja na alipata hata fursa ya kuteremka kwenye gari na kwenda ku take cover kwenye magari yaliyokuwa yamepaki eneo hilo. Assailants walikuwa upande wa kulia wa gari, hivyo risasi zilizama zaidi kwenye mguu wa kulia, paja la kulia, mkono wa kulia, kiuno upande wa kulia na kutokea tumboni na mkono wa kushoto. These are the documented medical forensic clues.

3. Majeshi yetu hayana bunduki za AK 47, yana SMG badala yake ambayzo full magazine zake ni risasi 30. Bunduki za AK47 zinamilikiwa na majambazi yanazozipata kutoka kwa wanajeshi wa Burundi wanaokimbilia Tanzania ambao huwa wanaziuza kwa bei ya shillingi 20,000 tu!! Silaha hizi ndizo zilitikisa huko Mkuranga, Kibiti na Rufiji.

4. Hakuna mwanajeshi ye yote (aliyepata mafunzo ya kijeshi) ambaye ampige mtu (adui) risasi 38 from an AK 47 gun at a close range halafu mtu huyo asalimike!! Never on earth. Kwanza atahitaji risasi moja tu na atafumua kichwa au moyo. Hivyo it is so obvious kwamba assailants wa Tundu Lissu walikuwa ni wahuni tu wa mitaani wasiojua kutumia bunduki. Yaani risasi 38 zote zinakosa target (kichwa au moyo) zinaishia kupiga makalio na hewa!! Hili halihitaji askari wa Scotland yard kulitambua. Swali ni nani aliwakodi hawa wahuni wasiojua shabaha? Kwa nini dreva wa Lissu akawa mkimbizi nchi za nje? Nini kakimbia? Kwani hata polisi wetu wakienda kumhoji huko kwani atasema lo lote la maana? Huko hawawezi kumu arrest. Alipaswa kuwa behind bars ili aeleze vizuri. Tundu Lissu alipaswa kujua hili. Mara nyingi kikulacho unacho nguoni mwako. Eti ninamuamini sana. Mbele ya pesa kunakuamini mtu? Yaani apewe shillingi million 500 aache kukumaliza? Yaani Tundu Lissu hajui kwamba "Money is the source of all evils in this world?"

5. Hospitali ya serikali ya Dodoma na madaktari wa serikali wa Dodoma hospital ndiyo waliookoa maisha yake. Kama serikali ilikuwa na mpango wa kumuua, ingalishindwaje kumumalizia hapo hapo kwenye hospitali yake ya Dodoma humo humo operation theatre? It was so simple eg hiyo damu aliyopewa hangeipata au angalipewa incompatible blood ambayo ingalimumaliza hapo kwa hapo! Lazima aishukuru serikali kwa kuokoa maisha yake badala ya kuilaumu. Upinzani haupaswi kuwa wa aina hii. Tujifunze kwenye nchi zilizotutangulia.

6: Bunduki kama AK 47 au SMG ikiunguruma si mchezo. Kwa askari yo yote trained, hata kama naye ana bunduki ya aina hiyo hiyo lakini kashutikizwa, reaction ya kwanza ni ku take cover. Atalala chini na ku craw hadi mahala salama. Hapo ndipo atatafuta kuona adui/ maadui walipo na kutafakari kama anao uwezo wa kupambana nao au kuomba reinfocement au kutokomea kabisa kwenye eneo hilo. Trained soldier hakurupuki tu kuanza kurusha risasi ovyo ovyo anapositukizwa na milio ya risasi. Hivyo kwa jinsi tukio lilivyotokea hapo usingalitarajia askari waliokuwa karibu na eneo hilo kuwa wangaliweza kuanza kujibu mapigo kwa muda huo mfupi uliotumika kabla ya majambazi hayo kutokomea kusikojulikana. Dreva wa Lissu aliyaona live na alitaja hata aina ya gari yalilotumia na plate namba zake. Polisi walikamata magari kadhaa ya aina hiyo lakini dreva huyo alikataa kwenda kuyatambua na hivyo yakabidi yaachiwe kwani hakuna shahidi aliyejitokeza. Shahidi muhimu alikuwa Nairobi akidaiwa anapata tiba ya kisaikolojia. Sasa hivi Lissu anasema dreva huyo yuko masomoni Ubeligiji. Sijui anasoma digrii gani hapo Leuven University teaching hospital anapotibiwa boss wake. Jamani aacheni kutufanya wajinga. Pascal yuko sahihi kabisa.

Ulichoandika hapa ni kuonyesha kwamba una uwezo wa kufikiri na hata ukipewa kazi ya kutetea watuhumiwa wa kumshambulia Lissu unaweza kutetea kwa kiwango fulani kimantiki. Hii ni haki yako kutumia akili yako kwa jambo lolote ambalo una maslahi nalo ama kwa kuwiwa kufanya hivyo. Lakini napenda nikuambie kwamba utetezi wako huu ungeweza kufanya kazi sehemu ambayo kuna watu wenye upeo finyu. Kama askari waliokuwepo eneo hilo walitishika na mlio wa hiyo AK47, je CCTV Camera nazo zilitishwa na nini? Pole ndugu, hata kama una maelezo yenye mantiki lakini kumbuka huwezi kuficha ukweli kwa maelezo mazuri. Hapa ulichoandika ni sawa na kuanika nguo kavu.
 
NDIYO NAJUA. KWANINI HIYO PRODUCT ILIPIGWA VITA? NI KWASABABU ILIKUWA INFUNUA MBINU/BIDS/KAMPUNI ZA SIRI AMBAZO WATEJA WAKE NI SERIKALI TU...HIVYO HATA TEKNOLOJIA PUBLIC ITASUBIRI SANA...

na mimi nikuulize:
UNANIJUA?
2. UNAIJUA INTERPOL?
Jamaa kabla ya kujibu maswali yako hayo, hiyo mbinu unayotaka kuitumia nikwambie ni ya kizamani sana. Hao Interpol nawajua vilivyo ni international police.

Hilo la kukujua wewe sina haja nalo
 
Hahahahah nyinyi watu mnafurahisha sana,So Lisu na huyo dereva hawatarudi Tz?Huo usalama wa kuhojiwa ni upi?Yani hawatak kuhojiwa Tz kisa Usalama?So serikali iwafuate huko?Sijawahi ona muathirika wa janga flani anaweka mashariti tena ya kipuuzi jinsi gani asaidiwe.Huwa nashangaa sana nkimsikia lisu et ka serikali ka inataka kunihoji kwanini isije kunihoji au kutafuta njia za kumhoji.Hivi nani anayetakiwa aangaike kuhakikisha haki inapatikana kati ya lisu na serikali? Hivi kuna kitu inapoteza kwa kutomhoji lisu?Ni maajabu lisu kupata mda wa kufanya press conference Kenya lkn sio mda wa kupigania haki yake Tz.Hizi ni siasa uchwara
Lissu ameshasema atarudi. Na ndiye aliyepigwa risasi hivyo yeye tusimuongelee sana. kama ni lazima ahojiwe nchini na si kwingine atahojiwa atakaporudi. Na asiporudi yeye ndiye atakayepoteza haki lakini ataendelea na maisha. Mm siangalii haki wala siasa. Nimeangalia uwezekano wa dereva kuongeza dakika za kuishi duniani esp kama si muhusika. Kama anaona uwepo wake hapa utapunguza dakika zake za kuishi ni sawa akibaki huko alipo mpaka itakapolazimika yeye kuwepo. Jiulize tu mtu akifanya uhalifu akakimbilia nje ya nchi, hakuna utaratibu wa kumpata pale vyombo vya usalama vitakapotoa ushahidi? Kama ni dereva kafanya uhalifu serikali itaweza tu kupata ushahidi na atarudishwa kwa ushirikiano wa nchi zote mbili. Kwa sasa ngoja aishi.
 
Ulichoandika hapa ni kuonyesha kwamba una uwezo wa kufikiri na hata ukipewa kazi ya kutetea watuhumiwa wa kumshambulia Lissu unaweza kutetea kwa kiwango fulani kimantiki. Hii ni haki yako kutumia akili yako kwa jambo lolote ambalo una maslahi nalo ama kwa kuwiwa kufanya hivyo. Lakini napenda nikuambie kwamba utetezi wako huu ungeweza kufanya kazi sehemu ambayo kuna watu wenye upeo finyu. Kama askari waliokuwepo eneo hilo walitishika na mlio wa hiyo AK47, je CCTV Camera nazo zilitishwa na nini? Pole ndugu, hata kama una maelezo yenye mantiki lakini kumbuka huwezi kuficha ukweli kwa maelezo mazuri. Hapa ulichoandika ni sawa na kuanika nguo kavu.
HUYU NAE TUTAMLA RISASA...anaingila maslahi, achana nae.
 
Jamaa kabla ya kujibu maswali yako hayo, hiyo mbinu unayotaka kuitumia nikwambie ni ya kizamani sana. Hao Interpol nawajua vilivyo ni international police.

Hilo la kukujua wewe sina haja nalo
MAANA YAKE WEWE NAE NI KICHAA...KAMA RAIS WAKO.
 
Back
Top Bottom