Shambulizi la Lissu: Wanaomdhania dereva anahusika sio wajinga, Wana hoja za msingi. Je, anahusika?

Shambulizi la Lissu: Wanaomdhania dereva anahusika sio wajinga, Wana hoja za msingi. Je, anahusika?

..unapokabiliwa na hatari unatakiwa ukimbilie eneo salama/ lenye ulinzi lililokaribu zaidi na hatari ilipokukuta.

..kwa hili tukio la dereva na TL eneo salama lililokuwa karibu nao ni nyumbani kwao ambako walikuwa wanajua siku zote kuna ulinzi.

..kilichotokea hakina tofauti na mtu aliyeshambuliwa ktk eneo la kituo cha polisi.

..dereva angeendesha gari kwenda sehemu nyingine yoyote ile, halafu wakashambuliwa, angelaumiwa kwanini hakujisalimisha nyumbani ambako palikuwa ni karibu na inaeleweka pana ulinzi 24/7.

Kwa nini walipofika mahali salama (Nyumbani) hawakutoka kwenye gari na kupiga kelele au honi mfululizo?
 
2359886_D-86Nv3WwAA3ihc-1.jpg


Huna ushahidi hapa, unazuga tu.

Mmeshindwa kufafanua kitu cha msingi mmekalia amjungu tu sasa, TL alikaa kushoto mguu uliopigwa risasi ni wa kulia na taarifa za mwanzo walisema walifika eneo la tukio na kukaa kusubiri bila kutoka nje ya gari. Je, ni wakati gani TL aliamua kulala kifudifudi? At the same time dreva akasepa bila hata scratch wala unywele wake kung'oka?
Kamuulize BASHITE
 
K
Hapana jinai inafanyika mahala popote. Ndio maana unatakiwa uwe makini sana. Kama Laurent Kabila alipigwa risasi na mlinzi wake tena ikulu.Ije hapo area D Dodoma ampabo kila mtu anaingia muda wote? Huyu dereva ni wa kulaumiwa.

..U nailed it!!

..Kabila aliuwawa na mlinzi wake.

..ili ufanye jinai ktk eneo lenye ulinzi ni lazima uwe mlinzi wa eneo hilo, au ushirikiane na walinzi.

..na TL alishambuliwa na watu wenye mahusiano na walinzi wa area D.

..dereva kama anahusika basi alishirikiana na walioondoa walinzi wa area D.
 
Maswali ya kimantiki ni hivi;

1. Ilikuwa ni kanuni hivyo ni kawaida askari
kulinda eneo ambalo Lissu alipigwa
risasi?
2. Nani walikuwa zamu siku hiyo na
kwanini hawakuwepo wakati wa tukio
3. Afisa mpanga zamu na kiongozi wa siku
hawajui waliostahili kuwa zamu siku ya
tukio?
Maswali ni mengi kuhusu walinzi wa siku hiyo. Na kama kuna vyuo vya upelelezi bila shaka wanafunzi wake wengi wangechagua nukta hiyo kuwapata wahalifu kutoka wafyatua risasi hadi mtoa maelekezo wa mwanzo!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
..wangetoka kwenye gari wangesambaratishwa vibaya kwa risasi.

..kilichomuokoa TL ni kutokutoka ndani ya gari.
Hufahamu kingetokea nini? Huo ni mtazamo wako kwa sababu unategemea kuelemea kwenye hoja yako. Huwezi kuwa 100%
 
Majungu hayo!
Novemba mwaka 2014 alipomkunja JS Warioba pale Ubungo Plaza mlikaa kimya, kwa vile nyinyi hamkuwa upande wa Katiba Mpya ya Serikali 3. Akaingia Clouds Media na mabunduki napo mka kaa kimya kwa vile nyinyi si wamiliki wa vyombo vya habari. Alipomteka BenSaa Nane na kumuua, pia mlikaa kimya kwa kuwa nyinyi siyo CHADEMA. Hatimaye akamshambulia Tundu Lissu na kumjeruhi, mka kaa kimya vile vile kwa kuwa nyinyi siyo wana harakati wa haki za madini....

Alipomteka RomaMkatoliki mka kaa kimya tena kwa vile nyie siyo wana HipHop...
Subiri zamu yenu ndiyo mtajua BASHITE ni muuaji kichaa ambaye hajali kumwaga damu ya binadamu nwingine
 
Novemba mwaka 2014 alipomkunja JS Warioba pale Ubungo Plaza mlikaa kimya, kwa vile nyinyi hamkuwa upande wa Katiba Mpya ya Serikali 3. Akaingia Clouds Media na mabunduki napo mka kaa kimya kwa vile nyinyi si wamiliki wa vyombo vya habari. Alipomteka BenSaa Nane na kumuua, pia mlikaa kimya kwa kuwa nyinyi siyo CHADEMA. Hatimaye akamshambulia Tundu Lissu na kumjeruhi, mka kaa kimya vile vile kwa kuwa nyinyi siyo wana harakati wa haki za madini....

Alipomteka RomaMkatoliki mka kaa kimya tena kwa vile nyie siyo wana HipHop...
Subiri zamu yenu ndiyo mtajua BASHITE ni muuaji kichaa ambaye hajali kumwaga damu ya binadamu nwingine

Those issues does not justify what TL or Mbowe is doing?
 
Wanabodi

Hili ni bandiko la maswali kwa Tundu Lissu na dereva wake, kufuatia shambulio la Lissu,
"Shambulizi la Lissu, wanaomdhania dereva anahusika, sio wajinga!, wana hoja za msingi!" Swali ni Jee Dereva Anahusika?.
Si maanishi kuwa dereva wa Lissu anahusika, bali mazingira ya tukio, yanahalalisha watu wenye udadisi kujiuliza maswali kihusu tukio lenyewe, hivyo kuhisi uhusika wa dereva wa Lissu, sio jambo la ajabu, tena uhusika wenyewe sio lazima uwe expressly but impliedly kwa negligence iliyopelekea Lissu kuwa reached na watu wasiojulikana na kushambuliwa, wakati alikuwa na uwezo wa kumuepusha na shambulizi hili.
Maswali haya ni kufuatia hoja za Lissu kwenye bandiko hili.
Mhe. Tundu Lissu,
Kwanza pole sana kwa yaliyokusibu.
Umezungumza mengi kuhusu kilichotokea mwaka mmoja uliopita, ila watu wanaohoji kuhusu dereva wako, nakuomba sana usiwaite wajinga, au wametumwa, kwa sababu mashaka yao ni very valid.

Kwa vile mashuhuda ni nyinyi wawili tuu, wewe na dereva wako, then kuna mambo tungependa kujua kutoka kwa Lissu mwemyewe na dereva wake.

Hoja kuwa tumetoka naye mbali hivyo tunaaminiana, hazina mashiko mbele ya watu na kazi zao. Lissu alipotoka na dereva wake, anaweza kujilinganisha Dr. Slaa na mlinzi wake Kagenzi walipotoka?, halafu what happened?!. Kwenye mambo ya assignment, anaweza hata akatumika mke wako aliyekuzalia wanao, sembuse itakuwa dereva tuu mliotoka nae mbali!.
Baadhi ya maswali ni haya...
  1. Kwa vile Lissu aliwahi kuripoti kufuatiliwa, kupitia press conference, kwa nini hakuripoti polisi?!.
  2. Baada ya Chadema kupokea taarifa ya Mnadhimu wake kufuatiliwa, walichukua hatua gani?.
  3. Baada kuona kuna gari linawafuatilia, mlichukua hatua gani?.
  4. The common sense ya kufuatiliwa inaelekeza, uki note you're followed, hatua ya kwanza ni kumpote anaye kufollow kwa makusudi, ili kwanza kujiridhisha kuwa anakufollow.
  5. Ukiisha jiridhisha you are followed, una change direction kumpoteza maboya.
  6. Ukimuona bado yupo, then kama uko fit, unamlengesha mahali kwenye kona ambapo hawezi kuchomoka, mnamalizana!.
  7. Kama hauko fit, unamlengesha kwenye safe area ,usually sehemu open kwenye makundi ya watu na kumripoti kunakohusika.
  8. Baada ya kuona mnafuatwa, kwa nini mliendelea kuelekea nyumbani?.
  9. Mlipofika mkasimama, mkawaona watu wawili wanashuka na AK 47, kitendo tuu cha kujua tuu bunduki zile ni AK 47, hii maana yake ni close proximity, kwenye shooting that close!, risasi 38!, dereva huyu amesalimikaje asipitiwe hata na moja?.
  10. (Mimi niliwahi kuwa mwanajeshi wa JWTZ hivyo kuna kitu nakijua kuhusu hizi AK47 ndani ya jeshi letu, lakini vitu vingine ni siri za usalama wa taifa letu, sina uhakika mtu asiyepitia JWTZ, ana uwezo gani kuijua AK 47!.)
  11. Ametokaje kwenye gari na kujificha chini ya gari ya jirani bila kugundulika?!.
  12. Anafichwa nini kuhojiwa?, kuna nini kinafichwa?.
  13. Maswali haya yameendelea kwa msaada wa mwana jf huyu

  14. Bunduki iliyotumika waliiona ni AK 47 iliyokuwa na full magazine (risasi 40) ambayo ilimimina risasi zote 40 at close range. Kati ya hizo 17 zilizama kwenye miguu, mikono na kiuno cha Tundu Lissu.
  15. Risasi zilimiminwa kutoka upande wa kulia wa gari ambao ni upande wa dreva lakini dreva hakupatwa na risasi hata moja na alipata hata fursa ya kuteremka kwenye gari na kwenda ku take cover kwenye magari yaliyokuwa yamepaki eneo hilo. Assailants walikuwa upande wa kulia wa gari, hivyo risasi zilizama zaidi kwenye mguu wa kulia, paja la kulia, mkono wa kulia, kiuno upande wa kulia na kutokea tumboni na mkono wa kushoto. These are the documented medical forensic clues.
  16. Majeshi yetu hayana bunduki za AK 47, yana SMG badala yake ambayzo full magazine zake ni risasi 30. Bunduki za AK47 zinamilikiwa na majambazi yanazozipata kutoka kwa wanajeshi wa Burundi wanaokimbilia Tanzania ambao huwa wanaziuza kwa bei ya shillingi 20,000 tu!! Silaha hizi ndizo zilitikisa huko Mkuranga, Kibiti na Rufiji.
  17. Hakuna mwanajeshi ye yote (aliyepata mafunzo ya kijeshi) ambaye ampige mtu (adui) risasi 38 from an AK 47 gun at a close range halafu mtu huyo asalimike!! Never on earth. Kwanza atahitaji risasi moja tu na atafumua kichwa au moyo. Hivyo it is so obvious kwamba assailants wa Tundu Lissu walikuwa ni wahuni tu wa mitaani wasiojua kutumia bunduki. Yaani risasi 38 zote zinakosa target (kichwa au moyo) zinaishia kupiga makalio na hewa!! Hili halihitaji askari wa Scotland yard kulitambua. Swali ni nani aliwakodi hawa wahuni wasiojua shabaha? Kwa nini dreva wa Lissu akawa mkimbizi nchi za nje? Nini kakimbia? Kwani hata polisi wetu wakienda kumhoji huko kwani atasema lo lote la maana? Huko hawawezi kumu arrest. Alipaswa kuwa behind bars ili aeleze vizuri. Tundu Lissu alipaswa kujua hili. Mara nyingi kikulacho unacho nguoni mwako. Eti ninamuamini sana. Mbele ya pesa kunakuamini mtu? Yaani apewe shillingi million 500 aache kukumaliza? Yaani Tundu Lissu hajui kwamba "Money is the source of all evils in this world?"
  18. Hospitali ya serikali ya Dodoma na madaktari wa serikali wa Dodoma hospital ndiyo waliookoa maisha yake. Kama serikali ilikuwa na mpango wa kumuua, ingalishindwaje kumumalizia hapo hapo kwenye hospitali yake ya Dodoma humo humo operation theatre? It was so simple eg hiyo damu aliyopewa hangeipata au angalipewa incompatible blood ambayo ingalimumaliza hapo kwa hapo! Lazima aishukuru serikali kwa kuokoa maisha yake badala ya kuilaumu. Upinzani haupaswi kuwa wa aina hii. Tujifunze kwenye nchi zilizotutangulia.
  19. Bunduki kama AK 47 au SMG ikiunguruma si mchezo. Kwa askari yo yote trained, hata kama naye ana bunduki ya aina hiyo hiyo lakini kashutikizwa, reaction ya kwanza ni ku take cover. Atalala chini na ku craw hadi mahala salama. Hapo ndipo atatafuta kuona adui/ maadui walipo na kutafakari kama anao uwezo wa kupambana nao au kuomba reinfocement au kutokomea kabisa kwenye eneo hilo. Trained soldier hakurupuki tu kuanza kurusha risasi ovyo ovyo anapositukizwa na milio ya risasi. Hivyo kwa jinsi tukio lilivyotokea hapo usingalitarajia askari waliokuwa karibu na eneo hilo kuwa wangaliweza kuanza kujibu mapigo kwa muda huo mfupi uliotumika kabla ya majambazi hayo kutokomea kusikojulikana. Dreva wa Lissu aliyaona live na alitaja hata aina ya gari yalilotumia na plate namba zake. Polisi walikamata magari kadhaa ya aina hiyo lakini dreva huyo alikataa kwenda kuyatambua na hivyo yakabidi yaachiwe kwani hakuna shahidi aliyejitokeza. Shahidi muhimu alikuwa Nairobi akidaiwa anapata tiba ya kisaikolojia. Sasa hivi Lissu anasema dreva huyo yuko masomoni Ubeligiji. Sijui anasoma digrii gani hapo Leuven University teaching hospital anapotibiwa boss wake. Jamani aacheni kutufanya wajinga. Pascal yuko sahihi kabisa.
  20. Huko nyuma niliisha wahi kuzungumza haya kuhusu dereva wa Lissu.

Mpaka sasa the situation ya shambulio la Lissu as it is, limefanywa na watu wasiojulikana. Serikali yetu imeshindwa kuwabaini, lakini sisi watu wa media, tunaweza kusaidia kama nilivyosema hapa.
WanaJF, Je tuisaidie Serikali yetu inaposhindwa au tusubiri ishindwe, tuibeze na kuizomea kuwa haiwezi? - JamiiForums
Hitimisho.
The only defence ya Dereva wa Lissu has nothing to do na hiyo shooting, ni uzito tuu wa serikali yetu kufanya upelelezi wa tukio hili na kugoma kuita wachunguzi wa nje. Ingekuwa ni inside job ya Chadema, tungeshuhudia serikali fasta ingechunguza!.

Lakini kwa vile wasiojulikana ni hawa
Shambulio la Lissu: Wajue Wasiojulikana Watakaojulikana na 'Wasiojulikana' Ambao Kamwe, Hawatajulikana!. - JamiiForums

Tusitegemee lolote jipya hapa.
Tundu Lissu, just get well soon, na sasa inakubidi uchangue kati ya kuendelea na uanaharakati na kuishi kwa mashaka, au uamue kupunguza makali na kuishi kwa amani.

Pole Sana Mhe. Tundu Lissu, Get Well Soon.
P.
Rejea

  1. Tuacheni Ramli Chonganishi: Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!. "Karma Ndio Pekee Hutoa Hukumu ya Haki Hapa Duniani!. - JamiiForums
  2. Handling of Serious Security Issues: Kama CHADEMA Takes Things For Granted Kwa Uzembe Hivi!, Jee Ikulu Yetu Wangeiweza?! - JamiiForums
  3. Tundu Lissu: Polisi wa Tanzania hawana mamlaka ya kunihoji nikiwa Kenya au kwingineko nje ya mipaka ya Tanzania - JamiiForums
  4. Tundu Lissu ndiye asimame na Magufuli 2020? Ameonyesha Uwezo Zaidi ya Magufuli! - JamiiForums
    TISS Ikanushe tuhuma za uvamizi, utekaji, utesaji na mauaji!. Wasijadiliwe na Bunge kwa uwazi bali wachunguzwe, wakithibitika wafumuliwe! - JamiiForums
  5. Bandiko la 5 Handling of Serious Security Issues: Kama CHADEMA Takes Things For Granted Kwa Uzembe Hivi!, Jee Ikulu Yetu Wangeiweza?! - JamiiForums
  6. Bandiko la 6 Shambulio la Lissu: Wajue Wasiojulikana Watakaojulikana na 'Wasiojulikana' Ambao Kamwe, Hawatajulikana!. - JamiiForums
  7. Bandiko la 7 https://www.jamiiforums.com/threads...je-tukahukumiwa-karma-ndio-pekee-hutoa-hukumu
  8. Bandiko la 8 Tuacheni Ramli Chonganishi: Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!. "Karma Ndio Pekee Hutoa Hukumu ya Haki Hapa Duniani!. - JamiiForums
  9. Bandiko la 9 Serious Media inaweza kuwabaini "wasiojulikana" Deo Masakilija - JamiiForums
  10. Bandiko la 10 WanaJF, Je tuisaidie Serikali yetu inaposhindwa au tusubiri ishindwe, tuibeze na kuizomea kuwa haiwezi? - JamiiForums
  11. Bandiko la 11 Siku ya Sheria: No mention of Tundu Lissu!, Je ni amesahaulika tu kutajwa, amepuuzwa au ameepukwa?!. - JamiiForums
  12. Bandiko la 12 Shambulizi la Lissu: Wanaomdhania dereva anahusika sio wajinga, Wana hoja za msingi! Je, anahusika? - JamiiForums
  13. Bandiko la 13 Kwa mliomsikia Tundu Lissu kwenye Hard Talk, unadhani atarejea nchini? Mimi sina hakika na akirejea, atakuwa ni shujaa kuliko hata Nelson Mandela! - JamiiForums
  14. Bandiko la 14 Je, Tundu Lissu anaichafua nchi yetu au anasema ukweli wa kilichomtokea? Je, Serikali yetu iwe Proactive kusema ukweli au Reactive kumjibu? - JamiiForums
Mayalla pole na hongera sana, umewezaje kuwa reqular contributor hapa Jamii Forum kwa kiwango hichi katika jumuia ambayo au hawana ufahamu wa kuchangia au maadili ya kuchangia yako chini sana au ufahamu wa somo na tukio uko chini mnoo.
Pamoja na hayo kuna kiwango kikubwa sana cha watu wanao jilazimisha kuonekana wajinga. Au tuseme ushabiki uliopindukia na hauwezi kupiwa kwa instrument yeyote.
Nimepita jeshini kwa mwaka mmoja, kuna suala la matumizi ya bunduki umeliibua la aina ya AK 47 katika kushambulia. This is very partinent questions you raised. Japo lazima uwe na kaba kwa kuelezea masuala ya majeshi kwa aifa lako, lakini nawaambia wanaousoma huu uzi kuwa na wanajeshi au waliopita jeshini watathibitisha Taifa la tanzania lina walenga shabaha majeshini ambao ukimpa risasi 100 kati ya risasi 95 mpaka 100 zina piga target. Kama ni pua pua tuu risasi zitarudia mara 95 mpaka 100. na tukio hilo linatokea ukiwa mita 50 mpaka100. Wapo wengi mno wakuujaza uwanja wa taifa muda wowote utakapo waita wapo.

Maswali ya aina ya bunduki na ushambuliaji uluofanywa unatoa lead ya kutosha sana what the investigators must focus on. Siwezi kuchangia zaidi lakini naamini kutakuwa na majibu. Pole sana, unabishana na wengi wasio jua na wenye kujua wanakalia ushabiki ambao unadhalilisha Jamii Forum,Hasa kwa wenye kujua Machine guns zinafanyaje kazi kuna ulazima na sio kubeza Dreva wa Lisu kusaidia upelelezi. Mayalla una ngozi ngumu , Asante.
 
Mayalla pole na hongera sana, umewezaje kuwa reqular contributor hapa Jamii Forum kwa kiwango hichi katika jumuia ambayo au hawana ufahamu wa kuchangia au maadili ya kuchangia yako chini sana au ufahamu wa somo na tukio uko chini mnoo.
Pamoja na hayo kuna kiwango kikubwa sana cha watu wanao jilazimisha kuonekana wajinga. Au tuseme ushabiki uliopindukia na hauwezi kupiwa kwa instrument yeyote.
Nimepita jeshini kwa mwaka mmoja, kuna suala la matumizi ya bunduki umeliibua la aina ya AK 47 katika kushambulia. This is very partinent questions you raised. Japo lazima uwe na kaba kwa kuelezea masuala ya majeshi kwa aifa lako, lakini nawaambia wanaousoma huu uzi kuwa na wanajeshi au waliopita jeshini watathibitisha Taifa la tanzania lina walenga shabaha majeshini ambao ukimpa risasi 100 kati ya risasi 95 mpaka 100 zina piga target. Kama ni pua pua tuu risasi zitarudia mara 95 mpaka 100. na tukio hilo linatokea ukiwa mita 50 mpaka100. Wapo wengi mno wakuujaza uwanja wa taifa muda wowote utakapo waita wapo.

Maswali ya aina ya bunduki na ushambuliaji uluofanywa unatoa lead ya kutosha sana what the investigators must focus on. Siwezi kuchangia zaidi lakini naamini kutakuwa na majibu. Pole sana, unabishana na wengi wasio jua na wenye kujua wanakalia ushabiki ambao unadhalilisha Jamii Forum,Hasa kwa wenye kujua Machine guns zinafanyaje kazi kuna ulazima na sio kubeza Dreva wa Lisu kusaidia upelelezi. Mayalla una ngozi ngumu , Asante.

..hata sisi tumepita jeshini.

..kuna elements nyingi ambazo zilikuwa against walenga shabaha waliotumwa kumuua TL.

..TL alikuwa ndani ya gari / haonekani kwa macho hivyo hiyo ilikuwa challenge kubwa kwa mlenga shabaha yeyote.

..pamoja na kwamba walikuwa hawamuoni lakini waliweza kumdungua kwa risasi kadhaa na kumjeruhi mwilini kati ya magotini na tumboni.

..kitu kingine unachotakiwa kuzingatia ni kuwa tukio lile lilikuwa ni HIT & RUN.
 
Kabla ya kutoa hio dhana yako ningekuomba ujibu Masuala 3 tu:-
1. Kwa nini siku ya tukio hapakua na Mlinzi Bungeni
2. Jee kwanini Picha za Camera ulinzi hazijuilikani zilipo?
3. Kwa nini Serikali ikatae uchunguzi huru ukishirikisha vyombo vya Kimataifa?
Huyu jamaa nilikuwa namuelewa na kuzielewa.sana mada zake humu Jf lakini sasa nimemdharau sana tena sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa nini walipofika mahali salama (Nyumbani) hawakutoka kwenye gari na kupiga kelele au honi mfululizo?
Jiulize kati ya kelele na honi mfululizo na milio mfululizo ya risasi ipi ingeweza kuleta taharuki na kuhakikisha wanausalama wanafika kwenye eneo lile on time?? Ulitaka washuke wakati tayari wameshawaona watu wasiojulikana wakiwa na silaha pembezoni mwa gari lao?? Kwanini mnajitoa ufahamu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
No file halijafungwa because they survived. Sasa ndio wanasubiriwa wahojiwe uchunguzi ndipo uanze.
P
Kwa hiyo yakitokea mauaji, uchunguzi hakuna kwa sababu huyo aliyekufa ndio anajua kilichotokea? Tuseme ndio sababu hakuna kesi ya mauaji ya AKWILINA sababu hayuko hai? Naomba unifafanulie hapo maana mimi sijui sheria.

Ila natambua kwamba suala hili la kushambuliwa Tundu Lissu, lina makandokando ya kisiasa zaidi kuliko kisheria. Tundu Lissu mwenyewe ameshangazwa na kutokuwepo na uchunguzi wa tukio hilo.

Kwangu mimi ni wazi kwamba katika awamu hii, kuna maelekezo yanatolewa "toka juu" ambayo ni kinyume kabisa na sheria, kanuni na miongozo, kiasi cha kuwafedhehesha wale wanaopewa maelekezo hayo. Naamini ni katika mtizamo huo, Rais Magufuli aliwahi kutamka kwamba anatamani angekuwa IGP. Pia IGP Sirro naye alitamka kusikitishwa na suala la AKWILINA ilivyoshughulikiwa na polisi.
 
Back
Top Bottom