‘Shark loans’ namna taasisi za fedha za nchi tajiri wanavyowalewesha mikopo nchi maskini na kuweka mazingira ya kufubaza uchumi

‘Shark loans’ namna taasisi za fedha za nchi tajiri wanavyowalewesha mikopo nchi maskini na kuweka mazingira ya kufubaza uchumi

Biashara ya kutoa mikopo ni biashara kama biashara nyingine. Unavyouza mikopo Zaidi ndivyo unavyopata faida Zaidi.

Kwa nchi zilizoendelea kama Marekani, mataifa ya Ulaya, Japan, na hata China, hizi ni nchi ambazo zimefanikiwa kuwa na efficiency kubwa sana kwenye mabenki, na pia benki kuu katika nchi hizo kwa ndani ya miaka 15 iliyopita, walikuwa na sera ambazo zilipelekea interest rates (au kiwango cha riba) kwenye hizo nchi, kuwa chini sana.

Matokeo yake ni kwamba, benki na wakopeshaji wengie sana wa hizi nchi tajiri, wamekuwa ni kama wana struggle kwenye kutengeneza faida, hususani kwasababu, cost of funds ni ndogo lakini pia lending costs ni ndogo, kwahiyo wamekuwa wakitengeneza ‘a very thin margin’ kwenye mikopo yao, kitu ambacho kwa investors huwa hakifurahishi.

Kwahiyo trick ikawa ni kwamba, hizi nchi tajiri ikabidi wa dizaini namna ya kuwabambika mikopo nchi maskini the likes of Zambia, Tanzania, Kenya nk. Kwasababu kama nilivosema kwenye utangulizi wangu, biashara ya mikopo, ni kama biashara nyingine, unavyouza mikopo Zaidi ndo unavyozidi kutengeneza pesa.

Na kwa kutumia taasisi zao zao kwenye assessment ya credit ratings, imejikuta kwamba kumejengek mfumo wa kuhakikisha kwamba risk profile ya mataifa mengi maskini inakuwa juu sana, ili basi hata riba ya mikopo ambayo watapewa pia itakuwa ni kubwa.

Mikopo inayofubaza uchumi – mikopo isiyoelekezwa kwenye matumizi yenye tija

Kikubwa ni kwamba, hizi taasisi za kifedha za nchi tajiri, wanataka kuhakisha kwamba, mikopo mingi ambayo nchi masikini watakopa, basi isiweze kulipika daima, ili kwamba iwe ni kama vile Ng’ombe unayemkamua maziwa kila siku.

Kwa hivo basi, nchi maskini zimekuwa zikijikuta zina finance miradi ambayo ‘payoff’ yake ni ndogo iki maanisha kwamba, mradi husika unaweza kuwa na impact ndogo kwenye uchumi kitu ambacho kitapelekea kukosekana kwa cash flow ya kulipa hiyo mikopo husika.

Lakini ni kama pia kuna agenda ambayo huwa inajificha kwenye hii mikopo ya kimataifa. Ni kwanini mikopo ambayo huwa inalenga mambo ya kipuuzi huwa inakuwa inatolewa haraka haraka sana? Na ile ambayo ina maslahi mapana nay a muda mrefu huwa inapigwa danadana?

Ukijijibu hayo maswali ni kwamba, hizi taasisi ni kwamba, huwa hazina malengo ya kuona kwamba uchumi wa hizi nchi unaboreka, ndio maana kuna mikopo serikali inapata kwa haraka haraka na ukiangalia matumizi yake unaona ni matumizi ya kipumbavu.

Zaidi Zaidi nadhani hii ni form mpya ya ukoloni mamboleo kwa kutumia taasisi za kifedha za kimataifa kuhakikisha kwamba wanawalesha na kufubaza maendeleo ya hizi nchi kupitia mikopo. Kwasababu ni mikopo isiyolipika, yenye riba kubwa, na ambayo inabeba systemic risks za kuangusha hata mfumo mzima wa uchumi wa nchi – ukiangalia kinachowakuta Ghana kwa sasahivi.

Inavoonekana ni kwamba pia Tanzania, hatuwezi kujikwepa na huu mtego, tayari tupo kwenye ile debt trap, maana kwa miaka saba iliyopita nchi imeongeza deni kwa karibu USD 12 billion (TZS 27 Trillioni) ambazo mimi binafsi ukiniuliza zilipokwenda, bado ntachelea kukupa majibu.

External debt stock as per BOT

December 2015 – USD 15,408 millions

October 2022 – USD 27,482 millions

Changes between Dec 2015 to Oct 2022 = USD 12,074 millions

Watu wengi wanasema ‘Tanzania bado haipo kwenye high risk category na deni ni stahimilivu kwa just kuangalia tu upande wa debt to GDP ratio’ lakini ukiangalia kwenye upande wa ‘cash flow’ iliyopo na projected cash flow ya hivi vilivyoombewa mikopo, huwezi kuona huo ustahimilivu ulipo.

Nawaachia swali serikali, ‘pesa unayokopa unaifanyia nini?’ hilo swali nadhani ndio tungependa kuskia bunge likijadili kabla ya serikali kwenda kukopa, vinginevyo naona hizi deal zinafanyia kimya kimya na wizara ya fedha, naona kila kukicha kwa miaka 7 iliyopita wakisaidi mikataba ya kukopeshwa mabilioni lakini hawataki kutujibu hilo swali.

Ni hayo tu.

N.Mushi
Mwaka huu unaokuja nataka kuongeza mazungumzo yanayokwenda kwa hoja za kiunazuoni na vitabu, data, research.

Hata kama ni kwa kutaja waandishi na kuweka vitabu tu watu tusome tujue zaidi.

Na pia na sisi tuandike zaidi.

Ukitaka kuanza kuyaelewa vizuri mambo haya, kama hujamsoma, mfuatilie muandishi anaitwa John Perkins.

Nikisoma vitabu vyake vinavyoelezea economic espionage katika geopolitics, halafu nikiangalia uongozi wetu na uwezo wake, naona tumepwaya sana, sana tu.

John Perkins ameandika au kuhariri vitabu hivi.

The Secret History of the American Empire: The Truth About Economic Hitmen, Jackals, and How to Change the World

A Game as Old as Empire: The Secret World of Economic Hit Men and the Web of Global Corruption

Confessions of An Economic Hitman

Hoodwinked. An Economic Hit Man Reveals Why the World Financial Markets Imploded--and What We Need to Do to Remake Them

Not One Drop: Betrayal and Courage in the Wake of the Exxon Valdez Oil Spill

The New Confessions of an Economic Hit Man


Vitabu hivi, kasoro kimoja ambacho kipo katika epub format, nimeviweka katika attachments.
 

Attachments

Economical model ya TZ ndiyo ina attract loans appetite.
 
Naantombe Mushi mbon inajulikana Tanzania iko sokoni. Mwigulu analifahamu vizuri ila kwa sababu wao watawala wanajiandalia future ya familia zao wanajua watapona. Kitakachofuata baada ya madeni ni vita ya sisi kwa sisi. Na hapo hesabu ni vizazi kazaa. Ni ajabu sana tena sana vyombo vya ulinzi na usalama kukaa tu wanaona kabisa muelekeo mbaya bila hata kuchukua hatua za kushauri. Inasikitisha. Dkt Magufuli alituaminisha nchi hii ni tajiri ila sasa hivi tunaambiwa ni maskini ya kutupwa bila mikopo mishahara hailipwi.
Na ukiona nchi inakopa kulipa mishahara ambayo ni operating expenses na sio capital expenditure... hapo ndo unajua kwamba hii ni house or cards inatengenezwa
 
Wananchi tulieni. Bado tunakopesheka [emoji706][emoji706][emoji706]


IMG-20221221-WA0012.jpg
 
Mambo magumu kama haya huwa hawataki yaongelewe utaanza onekana adui wa serikali badala ya mzalendo.

Kwao mzalendo ni kuwa Chawa na kumsifia sifia Rais Kila ndio mzalendo.

Mambo ya kijinga kabjsa.

"Tatizo hapa hatuna akili kabisa..." -Dr Godwin Mollel.
 
Mwaka huu unaokuja nataka kuongeza mazungumzo yanayokwenda kwa hoja za kiunazuoni na vitabu, data, research.

Hata kama ni kwa kutaja waandishi na kuweka vitabu tu watu tusome tujue zaidi.

Na pia na sisi tuandike zaidi.

Ukitaka kuanza kuyaelewa vizuri mambo haya, kama hujamsoma, mfuatilie muandishi anaitwa John Perkins.

Nikisoma vitabu vyake vinavyoelezea economic espionage katika geopolitics, halafu nikiangalia uongozi wetu na uwezo wake, naona tumepwaya sana, sana tu.

John Perkins ameandika au kuhariri vitabu hivi.

The Secret History of the American Empire: The Truth About Economic Hitmen, Jackals, and How to Change the World​


A Game as Old as Empire: The Secret World of Economic Hit Men and the Web of Global Corruption​


Confessions of An Economic Hitman​

Hoodwinked. An Economic Hit Man Reveals Why the World Financial Markets Imploded--and What We Need to Do to Remake Them​


Not One Drop: Betrayal and Courage in the Wake of the Exxon Valdez Oil Spill​

The New Confessions of an Economic Hit Man​

Vitabu hivi, kasoro kimoja ambacho kipo katika epub format, nimeviweka katika attachments.
Asante sana mkuu.. na mimi ni mdau mkubwa wa kufuatilia Geopolitics.. ni somo pana sana maana linaenda pia kwneye mbinu za kiuchumi ...

Sidhani kama mataifa mengi ya nchi masikini kwenye idara zao za usalama wa taifa, huwa kuna ma analyst kwenye issue nzima ya Geopolitics na economics.. maana haya ni mambo ambayo yanaweza kuweka taifa kwenye risk kubwa sana ..

Asante kwa vitabu
 
Asante sana mkuu.. na mimi ni mdau mkubwa wa kufuatilia Geopolitics.. ni somo pana sana maana linaenda pia kwneye mbinu za kiuchumi ...

Sidhani kama mataifa mengi ya nchi masikini kwenye idara zao za usalama wa taifa, huwa kuna ma analyst kwenye issue nzima ya Geopolitics na economics.. maana haya ni mambo ambayo yanaweza kuweka taifa kwenye risk kubwa sana ..

Asante kwa vitabu
Anytime.

Nakubaliana na wewe sana. Nimeanza kusoma tu "A Game As Old As Empire". Kinaanza tu na mi data ya kufa mtu kuonesha how the game is stacked against us, halafu nikiangalia tulivyokuwa addicted na mikopo, naona kabisa "this is a train wreck waiting to happen".

Ukisoma "Confessions of An Economic Hitman" unaona kabisa tunapitishwa mulemule.
 
Economical model ya TZ ndiyo ina attract loans appetite.
Wanatukopesha kwa sababu walifanya assessment zao wakaona Tanzania ni kama vile msitu wa miti mizuri ya mkaa, ambayo kwao kwasababu wao ni wachoma mkaa wanahitaji miti hiyo kuchoma mkaa.

Lakini jiulize, kuna pori la miti ya kuchoma mkaa ambalo limedumu daima?

Maana yake ukiona wanakimbilia kuikopesha Tanzania ni kwa sababu wanaona bado hii nchi haijaelemewa na madeni na kwamba zerikali yao bado inahitaji kukopa zaidi na zaidi.

Kwahiyo na wao wanafurahi kwasababu wanapata wakuwashikisha hela zao za moto.
 
Ukitaka kuanza kuyaelewa vizuri mambo haya, kama hujamsoma, mfuatilie muandishi anaitwa John Perkins.

Ameandika

The secret history of the American empire: the truth about economic hit men, jackals, and how to change the world​


A Game as Old as Empire: The Secret World of Economic Hit Men and the Web of Global Corruption​


Confessions of an economic hit man​

Hoodwinked. An Economic Hit Man Reveals Why the World Financial Markets Imploded--and What We Need to Do to Remake Them​


Not One Drop: Betrayal and Courage in the Wake of the Exxon Valdez Oil Spill​

The New Confessions of an Economic Hit Man​

Vitabu hivi vyote nimeviweka katika attachment ya zip file.

Anytime.

Nakubaliana na wewe sana. Nimeanza kusoma tu "A Game As Old As Empire". Kinaanza tu na mi data ya kufa mtu kuonesha how the game is stacked against us, halafu nikiangalia tulivyokuwa addicted na mikopo, naona kabisa "this is a train wreck waiting to happen".

Ukisoma "Confessions of An Economic Hitman" unaona kabisa tunapitishwa mulemule.
Powa powa mkuu naahidi kuvifuatilia kwa undani.. hiyo title ya 'Confessions of an economic hitman' imenishawishi
 
Mambo magumu kama haya huwa hawataki yaongelewe utaanza onekana adui wa serikali badala ya mzalendo.

Kwao mzalendo ni kuwa Chawa na kumsifia sifia Rais Kila ndio mzalendo.

Mambo ya kijinga kabjsa.

"Tatizo hapa hatuna akili kabisa..." -Dr Godwin Mollel.
Ni shida sana mkuu... na hawataki tuhoji pia
 
Nasikitika sana mada kama hizi zina wachangiaji wachache na wafuatiliaji wachache sana, kinyume na mada zisizo na maana zinavyo kimbikiliwa.
Tunaweza tusiwe na mchango wa maana kwenye mada kama hizi kutokana na kiwango cheti cha ufahamu kwenye mambo ya uchumi na fedha lakini hatutakosa mengi ya kujifunza kutokana na maoni ya wataalamu na walio pitia vitu hivyo.
Hongereni sana wadau mlio changia uzi huu pamoja na mleta mada.
 
Back
Top Bottom