Sheikh Alhad Musa Salum: Rangi ya Kijani inayotumiwa na CCM ndio rangi pekee iliyobarikiwa na Mwenyezi Mungu

Njaa ikiingia kichwani ni hatari
 

Alhad aache kutumia dini kuitetea ccm, Allah ameitaja rangi ya kijani kwa wema na sio rangi aliyowapa CCM , Makosa makubwa sana wanafanya hawa watu kutumia jina Allah kwa maslai ya kidunia

((عَالِيَهُمْ ثِيَابُ سُندُسٍ خُضْرٌ وَإِسْتَبْرَقٌ وَحُلُّوا أَسَاوِرَ مِن فِضَّةٍ وَسَقَاهُمْ رَبُّهُمْ شَرَابًا طَهُورًا))

((Juu yao zipo nguo za hariri laini za kijani kibichi, na hariri nzito ya atilasi. Na watavikwa vikuku vya fedha, na Mola wao Mlezi Atawanywesha kinywaji safi kabisa)) Al-Insaan: 21]

إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ إِنَّا لَا نُضِيعُ أَجْرَ مَنْ أَحْسَنَ عَمَلًا ﴿30﴾ أُوْلَئِكَ لَهُمْ جَنَّاتُ عَدْنٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهِمُ الْأَنْهَارُ يُحَلَّوْنَ فِيهَا مِنْ أَسَاوِرَ مِن ذَهَبٍ وَيَلْبَسُونَ ثِيَابًا خُضْرًا مِّن سُندُسٍ وَإِسْتَبْرَقٍ مُّتَّكِئِينَ فِيهَا عَلَى الْأَرَائِكِ نِعْمَ الثَّوَابُ وَحَسُنَتْ مُرْتَفَقًا ﴿31﴾

30. Hakika wale walioamini na wakatenda mema - hakika Sisi hatupotezi ujira wa anayetenda mema

31. Hao watapata Bustani za milele, zinazo pita mito kati yake. Humo watapambwa kwa mavazi ya mikononi ya dhahabu, na watavaa nguo za kijani za hariri na atilasi, huku wakiegemea humo juu ya makochi. Ni malipo bora hayo! Na matandiko mazuri mno ya kupumzikia! [Al-Kahf:30-31]
 
Shehe alikuwa Msikitini au kwenye Mkutano wa Kisiasa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa muda mrefu nimekuwa najiuliza sana kwanini CCM inabarikiwa sana, sasa ndio nimepata jibu, kumbe ni shauri ya ile rangi ya kijani!. Ndio maana CCM itatawala Tanzania milele kufuatia matumizi ya rangi ya Kijani ambayo ndio rangi iliyobarikiwa na Mungu Allah,

P
 
Huyu sheikh huyu kwakuwa kasifia chama tawala hasemwi kama anachanganya dini na siasa. ila kama angeikosoa serikali angeambiwa avue majoho na kuingia katika siasa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…