Sheikh Alhad Musa Salum: Rangi ya Kijani inayotumiwa na CCM ndio rangi pekee iliyobarikiwa na Mwenyezi Mungu

Sheikh Alhad Musa Salum: Rangi ya Kijani inayotumiwa na CCM ndio rangi pekee iliyobarikiwa na Mwenyezi Mungu

Sheikh wa mkoa wa Dsm Alhad Musa Salum amesema CCM imepewa upendeleo na mwenyezi Mungu kwa sababu wanatumia rangi ya kijani ambayo ndio rangi pekee iliyobarikiwa na Mungu.

Alhad Musa amesema hayo wakati akiiombea dua CCM katika katika sherehe za miaka 43 ya chama hicho inayofanyika kitaifa jijini Dsm leo.

Mgeni wa heshima ni mama Samia Suluhu, makamu wa Rais wa JMT

Source: Channel ten

Maendeleo hayana vyama!
Mbona nasikia huyu mboga yake kubwa ni Kitimoto? Kwani siku hizi hiyo mboga inaruhusiwa? Mnawapa watu majina wasiyostahili kabisa.
 
CCM izo rangi hawakuzichagua kwa bahati mbaya, Wazee walizitafuta hizo rangi wakatafuta maanayake ndio zikatumika katika bendera ya chamacha mapinduzi na taifa kwa ujumla. Zamani mambo yalifanywa kwa weredi mkubwa sio sasa watu wanakurupuka tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sheikh wa mkoa wa Dsm Alhad Musa Salum amesema CCM imepewa upendeleo na mwenyezi Mungu kwa sababu wanatumia rangi ya kijani ambayo ndio rangi pekee iliyobarikiwa na Mungu.

Alhad Musa amesema hayo wakati akiiombea dua CCM katika katika sherehe za miaka 43 ya chama hicho inayofanyika kitaifa jijini Dsm leo.

Mgeni wa heshima ni mama Samia Suluhu, makamu wa Rais wa JMT

Source: Channel ten

Maendeleo hayana vyama!
Mungu yupi?? Maana wako wengi sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah inasikitisha sana siku hizi kuona "VIONGOZI WA DINI (Masheikh na Mapadri) wakijisahau kumtumikia mungu na kujiingiza kwenye siasa. Viongozi wa dini wanajivalisha ngozi ya unafiki.

Wanajifanya kujinyamazisha na kujisahaulisha ukweli kuwa mungu amekataza na hapendi kwa kutilia mkazo "MAUWAJI/UTEKWAJI/UKANDAMIZWAJI/UONEVU" wa raia.

Vyeo vyote ni dhamana mbele ya mungu, na kila mwenye cheo atahojiwa siku ya kiama kuhusu utawala aliokua nao na aliowatawala (Wataulizwa kama walitenda "UADILIFU" mpaka kwa wanyama kama mbwa waliokua chini ya utawala wao).

DUNIA ni "PEPO" kwa wasiomuogopa mungu, na ni "GEREZA" kwa wanaomuogopa mungu.
Viongozi wa dini na wana siasa wanategemeana. Wote mtajinwao ni watu. Kiongozi wa kidini akitumia watu dhidi ya kiongozi wa kisiasa hawezi kuwa salama, hali kadhalika kiongozi wa kidini akiwapiga vita 'waumini' na viongozi wao hatakuwa salama. Nikune nikukune.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sheikh wa mkoa wa Dsm Alhad Musa Salum amesema CCM imepewa upendeleo na mwenyezi Mungu kwa sababu wanatumia rangi ya kijani ambayo ndio rangi pekee iliyobarikiwa na Mungu.

Alhad Musa amesema hayo wakati akiiombea dua CCM katika katika sherehe za miaka 43 ya chama hicho inayofanyika kitaifa jijini Dsm leo.

Mgeni wa heshima ni mama Samia Suluhu, makamu wa Rais wa JMT

Source: Channel ten

Maendeleo hayana vyama!
But we dont have green saints

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom