Sheikh apinga Urais kwa mwanamke

Sheikh apinga Urais kwa mwanamke

Darsa kwa wote :

Mwenendo wa Mtume Muhammad SAW na nasaha zake katika kuwashirikisha wanawake :

Kinyume na inavyoaminika na wengine, Uislamu haujamzuwia mwanamke kuwa kiongozi kwenye jamii kwa mujibu wa mafundisho na mifano mbalimbali ya kidini kama wanavyosema washiriki hawa wa semina kuhusu Mwanamke wa Kiislamu na Uongozi.


Hao walikubali kuwa chini ya Mtume siyo wao kuwa viongozi. Msipotoshe mafundisho ya Uislamu. Bai'a ni kiapo cha utiifu.
 
Mbona kama unatetea sana mkuu. Kwani hakuna ukweli hapo?! Wewe nyumbani kwako mkeo ndio 100% final decision maker??
Mimi kwanza mke ndiye mwenye kazi, mimi deiwaka. Mke ndiye mwenye nyumba, tuliopanga ubazi mzima wa vyumba viwili na sebule hapa Kwa Mtogole, na yeye ndio hulipa kodi. Hata Ile boda boda yangu, ni yeye aliinunua na ipo Kwa jina lake. Japo mambo hupanga pamoja, Ila wife ndio mwenye sauti zaidi, Mimi kwake nimekufa nimeoza.

P
 
Umemaliza mjadala,huyo Sheikh Ubwabwa.Yupo Mwanamke anaitwa Balkiss,alikuwa mtawala,na Qur'an imetaja kisa chake.Na Qur'an haikupinga utawala wake.
Zipo Chapter,ndani ya Qur'an ,imeitwa kwa jina Maryam,na ni Mwanamke huyu.
Yupo Bi Asia,ametajwa ndani ya Qur'an.
Yupo Bi Aisha,mpaka leo waislamu ,dunia nzima,anawaongoza,kwa kufuata hadithi(miongozo),aliyopokea kutoka kwa Mtume Muhammad(S.A.W.).Mpaka miongozo ya mume na mke,kuanzia chumbani mpaka nje ya chumba.Wapo kina Bi Khadija,na wemgine kina Sumaiya,walipigana vita.Mama wa Nabii Musa,ametajwa,Mtoto wa kike wa huyu Mama wa Nabii Musa,ametajwa Kwenye Qur'an.
Kutajwa tu tayari ni kiongozi?

Unasema Aisha alipewa aya na mtume kweli, kiongozi wake alikywa mtume( mwanaume.

) Qur'an haijazuia mwanamke kuwa kiongozi bali awea chini ya mwanaume.
Hata biblia vilevile hakuna Askofu, Padri au Mchungaji wa kike.

Hawa unaowana wachungaji wa kike kama Zumarid , Lwakatale wanatimiza tu unabii maana ndo wapotoshaji.

Mwanaume ni kichwa cha familia
 
Sheikh akizungumza ukweli ambao jamii na utawala hawautaki kuusikia ni lazima apewe tuhuma za ugaidi ila kina Bagonza na gwajima wakiongea wanaitwa wasema haki.

Double standards
Huyu sheikh akamatwe, nashangaa anatumalizia hewa ya oksijeni mtaani
 
Jiwe ndo aliyeasisi mpaka Sasa tunaongozwa na mwanamke, Kwa kupenda sifa akaamua kumchagua mgombea mwenza mwanamke
 
Wewe ata taifa linaloongoza dunia waliona bora bonzo trump kuliko mwanamke aendeshe nchi.
Vipi kuhusu Angela Merkel? Ameongoza miaka mingapi Germany? Kitu gani kibaya kimetokea huko kwa sababu ya kuongozwa na mwanamke?
 
Kuna vitu vingine vinatia shaka Sana kuhusu afya ya akili ya mzungumzaji na ya washangiliaji wake mapopoma. Wakati anateuliwa mara mbili kuwa makamu WA raisi huyo shekhe 'mufilisi' alikuwa haoni au hasikii au hajui utaratibu WA katiba umekaaje likitokea la kutokea?!!!!!! Alisema nn?!!!!!

Hilo moja, pili kwahiyo mnatakaje sasa maana ni mwaka sasa mama anaongoza na anaendelea kuchanja mbuga tu.....leteni basi jina la mtu anayefaa au pindueni mchukue nyie; acheni kung'orang'ora huko jikoni mnatupigia Keller!
Watasubiri sana!!!! Tunaomba Mungu amuweke mpaka 2030 hiyo!!!!
 
Ipo Aya inasema Wanaume ni viongozi wa wanawake na hadithi sahihi zikisema haitakiwi mwanamke awe mtawala mkuu nikipata nafasi nitakuwekea nambari kwenye vyanzo vyote .
Mnalo hilo!!! Msiotaka kuongozwa na SSH hamieni nchi nyingine mpaka atakapoondoka madarakani
 
Back
Top Bottom