Sheikh Mkuu wa Tanzania: Muislam hajiendei endei tu,bila amani na utulivu hatuwezi kufanya Ibada zetu na kuishi vyema

Sheikh Mkuu wa Tanzania: Muislam hajiendei endei tu,bila amani na utulivu hatuwezi kufanya Ibada zetu na kuishi vyema

Amani na utulivu..

Ametuasa TUSIJIENDEE ENDEE tu....tusifuate mambo bila kujua undani wake.....

Tusipelekwe pelekwe tu kwani Uislam unataka tutumie vyema matumizi ya akili.....

Amesema ,tufahamu UMUHIMU WA AMANI na UTULIVU katika nchi.

#Nchi Kwanza😍
#Uwe na uchungu na nchi yako 😍
Naunga mkono hoja, kwa lugha nyingine ni Mufti wa Tanzania, Sheikh Mkuu amepiga marufuku Waislamu kushiriki maandamano ya Chadema!.

Hii maana yake ni the "the status quo" imetishika na maandamano haya sasa inawatumia viongozi dini kuwatisha waumini wao. Mtashuhudia viongozi mamluki wa dini, wakiingiza siasa mimbarini na madhabahuni!.

Jana nimemsikia Mufti akizunguka zunguka na kujiuma uma kulitangaza hili ikiwa ni kiashiria amechomekewa!.
Nakumbuka enzi zangu niko newsroom, ile uchaguzi wa 2010 awamu ya pili ya JK, Mzee wa Msoga alikuwa na hali mbaya, ikabidi kutumika rescue strategies kuwatumia viongozi wa dini kusaidia kuokoa jahazi, na kiukweli walisaidia sana , vinginevyo jahazi lingezama! Elections 2010 - Ni nani aliyeingiza udini kwenye kampeni hizi?

P
 
Naunga mkono hoja, kwa lugha nyingine ni Mufti wa Tanzania, Sheikh Mkuu amepiga marufuku Waislamu kushiriki maandamano ya Chadema!.

Hii maana yake ni the "the status quo" imetishika na maandamano haya sasa inawatumia viongozi dini kuwatisha waumini wao. Mtashuhudia viongozi mamluki wa dini, wakiingiza siasa mimbarini na madhabahuni!.

Jana nimemsikia Mufti akizunguka zunguka na kujiuma uma kulitangaza hili ikiwa ni kiashiria amechomekewa!.
Nakumbuka enzi zangu niko newsroom, ile uchaguzi wa 2010 awamu ya pili ya JK, Mzee wa Msoga alikuwa na hali mbaya, ikabidi kutumika rescue strategies kuwatumia viongozi wa dini kusaidia kuokoa jahazi, na kiukweli walisaidia sana , vinginevyo jahazi lingezama! Elections 2010 - Ni nani aliyeingiza udini kwenye kampeni hizi?

P
Mkuu P mbona umekwenda mbali sana ?!!

Umemsikiliza vyema na kwa utuo sheikh mkuu ili uje na hizo tuhuma ?!!!
 
Wenzetu wakishiba tu Ubwabwa inatosha
Wewe ubwabwa huutaki?!!

Kuna binadamu anayeweza kupata nguvu ya kununua mchele pale ambako kuna machafuko na kukosekana amani na utulivu ?!!

Acha kufikiri kitoto....
 
Nafuatilia sherehe za mazazi ya Bwana Mtume Muhammad (SAW) zinazofanyika mkoani Geita.

Nimemsikiliza Mufti wa BAKWATA Sheikh Zuberi, ambaye ameongea mengi na zaidi kaongelea suala la amani.

Ingawa sio moja kwa moja, ila amewasihi waislamu wasijihusishe na kurukia mambo (kwa uelewa wangu alikuwa analenga maandamano yaliyotangazwa na Chadema).

Nchi yetu ipo katika mtanzuko wa utekaji na mauaji. Nilitegemea leo aweze kukemea tabia hii, lakini amepiga kimya kama hakuna kinachoendelea.
Mchawi wa hızı dini ni ela. Siku hizi wanaita asali.
 
MEANWHILE,

Baraza la Maaskofu wa Katoliki limetoa tamko kulaani utekaji, utesaji na mauaji, na kuvitaka vyombo vya usalama kutimiza majukumu yao ya kulinda nchi na raia.
Jana katika "ekaristi takatifu" kumeongelewa sana kuhusu kuitunza AMANI na UTULIVU.....uwe makini kusikiliza....
 
Nafuatilia sherehe za mazazi ya Bwana Mtume Muhammad (SAW) zinazofanyika mkoani Geita.

Nimemsikiliza Mufti wa BAKWATA Sheikh Zuberi, ambaye ameongea mengi na zaidi kaongelea suala la amani.

Ingawa sio moja kwa moja, ila amewasihi waislamu wasijihusishe na kurukia mambo (kwa uelewa wangu alikuwa analenga maandamano yaliyotangazwa na Chadema).

Nchi yetu ipo katika mtanzuko wa utekaji na mauaji. Nilitegemea leo aweze kukemea tabia hii, lakini amepiga kimya kama hakuna kinachoendelea.
Amani ni zao la nini
 
BAKWATA ni tawi la CCM kama ilivyo UWT.

Al Duktur Zuberi anateta ubwabwa wake na kutumikia chama chake.
Matusi kwetu wafuasi wa BAKWATA tumeyazoea....

Tunatukanwa sana na wenye fikra za vurugu ,machafuko ,kukosa nidhamu kwa wengine na hata magaidi .....

Kwetu amani na utulivu ndio uislamu wenyewe....nje ya hapo si yetu. ...
 
Kupelekwa pelekwa na Nani?🐼
Una usingizi joo....

Ukiamka msikilize vyema....

Yaani muislam hatakiwi kuwa "kasuku"....anatakiwa atumie akili vyema kupitia aya tukufu "pindipo inapowajia hoja ichunguzeni kwanza ili msije mkadhuru wasio na hatia....".

Alamsiki Joo
 
MCHAWI Kalaba anayemtumia Mafwele kunyonya damu za wasio na hatia
Tumeaswa waislamu tuwe na tabia ya "pindipo inapotufikia hoja basi tuichunguze vyema mawanda yake".

Mtume SAW ndivyo alivyotufundisha tusiwe BENDERA FUATA UPEPO....na leo tunamuadhimisha mazazi yake....

Allahumma Swalli alaa habibina Muhammad SAW😍
 
Inawezekana huko kuteka na kuua baadhi ya waTanzania ambao hawapo upande anao ukubali yeye ndiyo amani yenyewe na kupendana!

Mambo ya aina hii wala hayahitaji kisomo kukubwa mtu awe nacho kuyatambua. Akili ya utu tu, ubinaadam inatosha kumfahamisha mhusika yeyote mazuri na mabaya
Fikra dhaifu kabisa....

Ally Mohamed Kibao alikuwa ni mwanaBAKWATA mwenzetu....sufi na Qadiriyya....unaongea kutokea sayari ya jupiter ?!!
 
Sio zao la Haki
Assalaam alaykum "amani ijuu yako".

Salaam ni amani ...

Dar es salaam (mji wa amani).

Mawanda ya amani ni mapana sana...huanzia na utulivu (haki) na mwendelezo wake.....

Haki yoyote inapokesekana hutafutiwa tiba na si JAZBA ZA KUJILIPUA.......
 
Back
Top Bottom