Sheikh wa Mkoa Mwanza (Kuhusu Mjadala wa Bandari): Walaaniwe wote wenye nia ovu na Rais Samia

Sheikh wa Mkoa Mwanza (Kuhusu Mjadala wa Bandari): Walaaniwe wote wenye nia ovu na Rais Samia

sasa kijana elimu ipi duniani hapa Duniani ambayo haijaanzia au kupaishwa na wasomi kutokea madrassa?

Bila neno 'madrassa" hata neno madarasa ungekuwa nalo leo hii.
Hizi dini ni za wapi Faiza? Aliyekwambia dini imetoka mbinguni ni nani? nani alifika huko mbunguni, hawa hawa Waarabu na Wazungu waliowaua babu zetu na kuwauza?

Eti elimu ya dunia. Elimu ya Dunia inakupa uwezo wa kuchambua yaliyopo Duniani na kwingineko. Hizi dini zimebuniwa hapa hapa duniani na wahuni tu. Yaani dini chimbuko ni Waarabu na Wazungu, wote firauni.

Mbinguni ni wapi?
 
Hizi dini ni za wapi Faiza? Aliyekwambia dini imetoka mbinguni ni nani? nani alifika huko mbunguni, hawa hawa Waarabu na Wazungu waliowaua babu zetu na kuwauza?

Eti elimu ya dunia. Elimu ya Dunia inakupa uwezo wa kuchambua yaliyopo Duniani na kwingineko. Hizi dini zimebuniwa hapa hapa duniani na wahuni tu. Yaani dini chimbuko ni Waarabu na Wazungu, wote firauni.

Mbinguni ni wapi?
Nisome ten auone kama kuna "mbinguni" kwenye maandiko yangu. Ushaianza wikiendi mapema/
 
Mbona ametoa fursa ya kujadili na kurekebisha....lakini wanasiasa hawataki
 
TAMKO LA SHEIKH WA MKOA MWANZA KUHUSU MJADALA WA BANDARI

Utangulizi

Kwa kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja kumekuwa na mjadala kuhusu uwekezaji na uendeshaji wa bandari zetu na kampuni kutoka Dubai. Mjadala ulianzishwa na wanasiasa na wanasheria lakini baadae ukachukua sura mpya na ya hatari ambayo nchi yetu haijawahi kushuhudia.

Hoja na mwelekeo wake

Wakati mjadala ulipoanza, hoja kubwa ilikuwa Wazanzibari wawili wanauza bandari za Tanganyika. Baada ya muda si mrefu, mjadala ukachukua sura mpya na kusisitizwa kuwa ni waarabu ndio waliouziwa nchi. Wakati mjadala unaendelea, ulihama kutoka sura ya kisiasa na kuingia udini.

Sote tumeshuhudia viongozi mbalimbali waandamizi wa dini ya kikristo walivyokuwa mstari wa mbele kupinga suala hili na wengine wamediriki kumkejeli Rais Samia Suluhu Hassan. Hii sio mara ya kwanza kwa viongozi wa dini ya kikristo kumkejeli Rais Samia.

Baadhi ya viongozi wa dini ya kikristo wamedai kuwa Rais Samia amevunja Katiba na kwa maana hiyo anastahili kuondolewa madarakani. Mmoja wao ameenda mbali zaidi kwa kutishia kufanyike Mapinduzi ya kumuondoa Rais Samia madarakani. Jambo la ajabu ni kuwa mpaka sasa hakuna hata mtu mmoja ambaye ameupinga mkataba wa bandari kwa hoja za kiuchumi.

Wote waliozungumza na hasa viongozi wa dini ya kikristo wamezungumza kwa jazba na kumshambulia Rais Samia bila sababu za msingi. Kama viongozi hawa wana uchungu na wananchi, tuliwatarajia kupaza sauti zao wakati wa utawala uliopita ambao tumeshuhudia watu wengi kupoteza maisha yao bila maelezo. Pia tumeshuhudia serikali iliyopita imeingia kwenye miradi mikubwa kinyume cha utaratibu. Sote ni mashahidi, hakuna kiongozi hata mmoja wa kiislamu aliyeushambulia uongozi uliopita.

Wito

Mimi ninaamini kuwa mjadala huu umetawaliwa na UDINI na una lengo la kumtoa Rais Samia madarakani kabla ya muda wake. Hivyo basi, kama sheikh wenu wa Mkoa, natoa wito kwa kila mwislam popote alipo katika Mkoa huu, afunge kwa siku 3 na katika kila swala ya Ijumaa kuanzia Ijumaa hii ya tarehe 7 Julai 2023 misikiti YOTE 700 ya Mkoa wa Mwanza isome dua ya kunuti kuwalaani WATU WOTE wenye nia ovu na Rais Samia.

Sheikh Hassan Kabeke ………………………………..

Sheikh wa Mkoa, MWANZA

Tarehe 6 Julai 2023
Mkoa w Kigoma unatoa viongozi wenye akili sana. Safi sana sheikh Kabeke. Laana ianzie CHADEMA kisha ifyeke makanisa yote . Aamin.
 
TAMKO LA SHEIKH WA MKOA MWANZA KUHUSU MJADALA WA BANDARI

Utangulizi

Kwa kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja kumekuwa na mjadala kuhusu uwekezaji na uendeshaji wa bandari zetu na kampuni kutoka Dubai. Mjadala ulianzishwa na wanasiasa na wanasheria lakini baadae ukachukua sura mpya na ya hatari ambayo nchi yetu haijawahi kushuhudia.

Hoja na mwelekeo wake

Wakati mjadala ulipoanza, hoja kubwa ilikuwa Wazanzibari wawili wanauza bandari za Tanganyika. Baada ya muda si mrefu, mjadala ukachukua sura mpya na kusisitizwa kuwa ni waarabu ndio waliouziwa nchi. Wakati mjadala unaendelea, ulihama kutoka sura ya kisiasa na kuingia udini.

Sote tumeshuhudia viongozi mbalimbali waandamizi wa dini ya kikristo walivyokuwa mstari wa mbele kupinga suala hili na wengine wamediriki kumkejeli Rais Samia Suluhu Hassan. Hii sio mara ya kwanza kwa viongozi wa dini ya kikristo kumkejeli Rais Samia.

Baadhi ya viongozi wa dini ya kikristo wamedai kuwa Rais Samia amevunja Katiba na kwa maana hiyo anastahili kuondolewa madarakani. Mmoja wao ameenda mbali zaidi kwa kutishia kufanyike Mapinduzi ya kumuondoa Rais Samia madarakani. Jambo la ajabu ni kuwa mpaka sasa hakuna hata mtu mmoja ambaye ameupinga mkataba wa bandari kwa hoja za kiuchumi.

Wote waliozungumza na hasa viongozi wa dini ya kikristo wamezungumza kwa jazba na kumshambulia Rais Samia bila sababu za msingi. Kama viongozi hawa wana uchungu na wananchi, tuliwatarajia kupaza sauti zao wakati wa utawala uliopita ambao tumeshuhudia watu wengi kupoteza maisha yao bila maelezo. Pia tumeshuhudia serikali iliyopita imeingia kwenye miradi mikubwa kinyume cha utaratibu. Sote ni mashahidi, hakuna kiongozi hata mmoja wa kiislamu aliyeushambulia uongozi uliopita.

Wito

Mimi ninaamini kuwa mjadala huu umetawaliwa na UDINI na una lengo la kumtoa Rais Samia madarakani kabla ya muda wake. Hivyo basi, kama sheikh wenu wa Mkoa, natoa wito kwa kila mwislam popote alipo katika Mkoa huu, afunge kwa siku 3 na katika kila swala ya Ijumaa kuanzia Ijumaa hii ya tarehe 7 Julai 2023 misikiti YOTE 700 ya Mkoa wa Mwanza isome dua ya kunuti kuwalaani WATU WOTE wenye nia ovu na Rais Samia.

Sheikh Hassan Kabeke ………………………………..

Sheikh wa Mkoa, MWANZA

Tarehe 6 Julai 2023
Sheikh mamluki, watu wa Mwanza hawana haja na mkalia kiti
 
Muda ni mwalimu mzuri. Hapa sasa nia ya hili bandiko ni geresha tu bali kuna mengi yapo kifuani kwako na hapa ndio unapumulia.

Haya masuala ya EAMWS tulishayajadili miaka na miaka kwa hapa hakuna jipya yote tulishayajadili haya unayaleta kama marudio hapa hakuna jipya.

Swala la OIC na ujenzi wa chuo hii ngonjera iliimbwa hapa miaka na miaka wala hakuna jipya na kiwanja cha chuo mkaamua kwa utashi wenu kumuuzia kanjibah.

Wizara ya elimu ilihodhiwa vipi, tupe huo mkakati na ushahidi wa kuzuia waislam wasipate elimu ya juu ingali wewe umeipata tena UDSM na sio wewe tu bali maelfu ya waislam nchini.

Necta ipi iliyohodhiwa na shule zipi zilizohujumiwa hizo, pamoja na kelele zako hukusoma shule za kiislam bali za kanisa takatifu katoliki la mitume wa kweli. Ningependa kutajiwa shule zilizohujumiwa na zimehujumiwa vipi hizo muslim school?. Hata mtume ashuke leo hii kamwe upande wa shule na ufaulu waislam hamtakaa muwashinde watoto wa missionary na shule zao.

Kwani hapa si suala la sheikh kuhusu bandari au ni suala la historia ya baba yako mzazi abdul Sykes, zaidi kwamba nilitegemea mjadala ujikite kwene suala la bandari, haya masuala ya historia za miaka 60 nyuma hapa hayana nguvu, inshu hapa ni bandari.
Huyu Mzee ni Islamic propagandist na Nia yake ni kutaka kuwachochea waislam watumie njia za kibaguzi kufikia malengo Yao.
 
TAMKO LA SHEIKH WA MKOA MWANZA KUHUSU MJADALA WA BANDARI

Utangulizi

Kwa kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja kumekuwa na mjadala kuhusu uwekezaji na uendeshaji wa bandari zetu na kampuni kutoka Dubai. Mjadala ulianzishwa na wanasiasa na wanasheria lakini baadae ukachukua sura mpya na ya hatari ambayo nchi yetu haijawahi kushuhudia.

Hoja na mwelekeo wake

Wakati mjadala ulipoanza, hoja kubwa ilikuwa Wazanzibari wawili wanauza bandari za Tanganyika. Baada ya muda si mrefu, mjadala ukachukua sura mpya na kusisitizwa kuwa ni waarabu ndio waliouziwa nchi. Wakati mjadala unaendelea, ulihama kutoka sura ya kisiasa na kuingia udini.

Sote tumeshuhudia viongozi mbalimbali waandamizi wa dini ya kikristo walivyokuwa mstari wa mbele kupinga suala hili na wengine wamediriki kumkejeli Rais Samia Suluhu Hassan. Hii sio mara ya kwanza kwa viongozi wa dini ya kikristo kumkejeli Rais Samia.

Baadhi ya viongozi wa dini ya kikristo wamedai kuwa Rais Samia amevunja Katiba na kwa maana hiyo anastahili kuondolewa madarakani. Mmoja wao ameenda mbali zaidi kwa kutishia kufanyike Mapinduzi ya kumuondoa Rais Samia madarakani. Jambo la ajabu ni kuwa mpaka sasa hakuna hata mtu mmoja ambaye ameupinga mkataba wa bandari kwa hoja za kiuchumi.

Wote waliozungumza na hasa viongozi wa dini ya kikristo wamezungumza kwa jazba na kumshambulia Rais Samia bila sababu za msingi. Kama viongozi hawa wana uchungu na wananchi, tuliwatarajia kupaza sauti zao wakati wa utawala uliopita ambao tumeshuhudia watu wengi kupoteza maisha yao bila maelezo. Pia tumeshuhudia serikali iliyopita imeingia kwenye miradi mikubwa kinyume cha utaratibu. Sote ni mashahidi, hakuna kiongozi hata mmoja wa kiislamu aliyeushambulia uongozi uliopita.

Wito

Mimi ninaamini kuwa mjadala huu umetawaliwa na UDINI na una lengo la kumtoa Rais Samia madarakani kabla ya muda wake. Hivyo basi, kama sheikh wenu wa Mkoa, natoa wito kwa kila mwislam popote alipo katika Mkoa huu, afunge kwa siku 3 na katika kila swala ya Ijumaa kuanzia Ijumaa hii ya tarehe 7 Julai 2023 misikiti YOTE 700 ya Mkoa wa Mwanza isome dua ya kunuti kuwalaani WATU WOTE wenye nia ovu na Rais Samia.

Sheikh Hassan Kabeke ………………………………..

Sheikh wa Mkoa, MWANZA

Tarehe 6 Julai 2023
Ufahamu wa wengi wa ma - shekhe wa kiislamu ambao hushinda kutwa nzima wamevaa majoho na vibaragashia ni mdogo sana...

Mmoja wao ni huyu.

Kwa namna fulani anajaribu kuwa "neutral" Kwa kujitenga na "udini", lakini ameshindwa kufanya hivyo kwani kupitia maandishi yake haya, kajiweka wazi kuwa anatetea dini na anamtetea mwislamu mwenzake..

Shekhe Mohamed Said, fahamu kuwa sisi hatuna shida na dini au uislamu wa huyu mama yenu Rais Samia Suluhu Hassan. Shida ya Watanganyika ni mkataba wa kutoa bure rasrimali bandari zetu Watanganyika za bahari na maziwa Kwa waarabu ambazo urithi wetu na watoto tuliopewa na Mungu baba...

Na shida yetu nyingine Kwa huyu mama ni U - zanzibari wake na Hilo hakuna kumung'unya maneno...!!

Maswali ni haya na kama una akili hebu yajibu bila kujificha kwenye udini. Na ukiitendea haki nafsi yako, na ukajibu Kwa ufasaha, utapanua ufahamu wako sana na utaelewa kuwa mama na mwislamu mwenzenu katukosea sana Watanganyika...

1. Kwamba, iweje Rais wa JMT, ndugu Samia Suluhu Hassan (Mzanzibari) Kwa kushirikiana na waziri wake wa ujenzi na usafirishaji (ambayo si wizara inayohusika na mambo ya muungano) lakini alimteua waziri Mzanzibari Prof. Makame Mnyaa Mbarawa (Mzanzibari) pamoja na Katibu mkuu wa wizara hiyo ambaye naye pia ni (Mzanzibari) wakapanga deal la kuuza bandari za Tanganyika pekee wakiziacha za kwao Zanzibar? Huoni tatizo hapo?

2. Na, Je unajua kwamba mambo ya bandari na bahari ni mambo ya muungano? Iweje Rais wa JMT anafanya jambo kubwa kama hili linalohusu muungano lakini akihusisha upande mmoja tu (Tanganyika) akiacha upande mwingine wa muungano yaani Zanzibar? Je, huku si kuvunja katiba?

3. Na mwisho Unataka Watanganyika wanyamazie jambo Kwa sababu za kijinga za eti kuambiwa wanavunja muungano au kufanya ubaguzi wa kidini?


No way!!, Watanganyika hatunyamaza kwa hili mpaka huyu mama akilli kuwa amekosea na arekebishe kosa lake Hilo mara moja na ikiwezekana aachie U -Rais wetu waingie wenye akili na maarifa ya kutenda...!!
 
Ufahamu wa wengi wa ma - shekhe wa kiislamu ambao hushinda kutwa nzima wamevaa majoho na vibaragashia ni mdogo sana...

Mmoja wao ni huyu.

Kwa namna fulani anajaribu kuwa "neutral" Kwa kujitenga na "udini", lakini ameshindwa kufanya hivyo kwani kupitia maandishi yake haya, kajiweka wazi kuwa anatetea dini na anamtetea mwislamu mwenzake..

Shekhe Mohamed Said, fahamu kuwa sisi hatuna shida na dini au uislamu wa huyu mama yenu Rais Samia Suluhu Hassan. Shida ya Watanganyika ni mkataba wa kutoa bure rasrimali bandari zetu Watanganyika za bahari na maziwa Kwa waarabu ambazo urithi wetu na watoto tuliopewa na Mungu baba...

Na shida yetu nyingine Kwa huyu mama ni U - zanzibari wake na Hilo hakuna kumung'unya maneno...!!

Maswali ni haya na kama una akili hebu yajibu bila kujificha kwenye udini. Na ukiitendea haki nafsi yako, na ukajibu Kwa ufasaha, utapanua ufahamu wako sana na utaelewa kuwa mama na mwislamu mwenzenu katukosea sana Watanganyika...

1. Kwamba, iweje Rais wa JMT, ndugu Samia Suluhu Hassan (Mzanzibari) Kwa kushirikiana na waziri wake wa ujenzi na usafirishaji (ambayo si wizara inayohusika na mambo ya muungano) lakini alimteua waziri Mzanzibari Prof. Makame Mnyaa Mbarawa (Mzanzibari) pamoja na Katibu mkuu wa wizara hiyo ambaye naye pia ni (Mzanzibari) wakapanga deal la kuuza bandari za Tanganyika pekee wakiziacha za kwao Zanzibar? Huoni tatizo hapo?

2. Na, Je unajua kwamba mambo ya bandari na bahari ni mambo ya muungano? Iweje Rais wa JMT anafanya jambo kubwa kama hili linalohusu muungano lakini akihusisha upande mmoja tu (Tanganyika) akiacha upande mwingine wa muungano yaani Zanzibar? Je, huku si kuvunja katiba?

3. Na mwisho Unataka Watanganyika wanyamazie jambo Kwa sababu za kijinga za eti kuambiwa wanavunja muungano au kufanya ubaguzi wa kidini?


No way!!, Watanganyika hatunyamaza kwa hili mpaka huyu mama akilli kuwa amekosea na arekebishe kosa lake Hilo mara moja na ikiwezekana aachie U -Rais wetu waingie wenye akili na maarifa ya kutenda...!!
Uzima....
Mimi sijaandika dini yeyote lakini muhimu ni kuwa Uislam una historia ya pekee sana kuanzia Tanganyika hadi Tanzania.

Mwaka wa 1968 EAMWS ilitaka kujenga Chuo Kikuu serikali ikaivunja ili chuo kisijengwe.

Tatizo Waarabu.

Katika miaka ya 1970 OIC ilitaka kujenga Chuo Kikuu Tanzania serikali ikakataa.

Waarabu.

1993 Zanzibar ilijiunga na OIC ukazuka mgogoro mkubwa.

Waarabu.

1997 Darul Imaan kutoka Saudia walitaka kujenga shule Kibaha ikavumishwa kuwa Waarabu wanapora ardhi Kibaha.

Shule haikujengwa.

Waarabu...
 
TAMKO LA SHEIKH WA MKOA MWANZA KUHUSU MJADALA WA BANDARI

Utangulizi

Kwa kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja kumekuwa na mjadala kuhusu uwekezaji na uendeshaji wa bandari zetu na kampuni kutoka Dubai. Mjadala ulianzishwa na wanasiasa na wanasheria lakini baadae ukachukua sura mpya na ya hatari ambayo nchi yetu haijawahi kushuhudia.

Hoja na mwelekeo wake

Wakati mjadala ulipoanza, hoja kubwa ilikuwa Wazanzibari wawili wanauza bandari za Tanganyika. Baada ya muda si mrefu, mjadala ukachukua sura mpya na kusisitizwa kuwa ni waarabu ndio waliouziwa nchi. Wakati mjadala unaendelea, ulihama kutoka sura ya kisiasa na kuingia udini.

Sote tumeshuhudia viongozi mbalimbali waandamizi wa dini ya kikristo walivyokuwa mstari wa mbele kupinga suala hili na wengine wamediriki kumkejeli Rais Samia Suluhu Hassan. Hii sio mara ya kwanza kwa viongozi wa dini ya kikristo kumkejeli Rais Samia.

Baadhi ya viongozi wa dini ya kikristo wamedai kuwa Rais Samia amevunja Katiba na kwa maana hiyo anastahili kuondolewa madarakani. Mmoja wao ameenda mbali zaidi kwa kutishia kufanyike Mapinduzi ya kumuondoa Rais Samia madarakani. Jambo la ajabu ni kuwa mpaka sasa hakuna hata mtu mmoja ambaye ameupinga mkataba wa bandari kwa hoja za kiuchumi.

Wote waliozungumza na hasa viongozi wa dini ya kikristo wamezungumza kwa jazba na kumshambulia Rais Samia bila sababu za msingi. Kama viongozi hawa wana uchungu na wananchi, tuliwatarajia kupaza sauti zao wakati wa utawala uliopita ambao tumeshuhudia watu wengi kupoteza maisha yao bila maelezo. Pia tumeshuhudia serikali iliyopita imeingia kwenye miradi mikubwa kinyume cha utaratibu. Sote ni mashahidi, hakuna kiongozi hata mmoja wa kiislamu aliyeushambulia uongozi uliopita.

Wito

Mimi ninaamini kuwa mjadala huu umetawaliwa na UDINI na una lengo la kumtoa Rais Samia madarakani kabla ya muda wake. Hivyo basi, kama sheikh wenu wa Mkoa, natoa wito kwa kila mwislam popote alipo katika Mkoa huu, afunge kwa siku 3 na katika kila swala ya Ijumaa kuanzia Ijumaa hii ya tarehe 7 Julai 2023 misikiti YOTE 700 ya Mkoa wa Mwanza isome dua ya kunuti kuwalaani WATU WOTE wenye nia ovu na Rais Samia.

Sheikh Hassan Kabeke ………………………………..

Sheikh wa Mkoa, MWANZA

Tarehe 6 Julai 2023
Huyu si Shehe wa Mkoa wa Mwanza , huyu ni Shehe wa BAKWATA Mkoa wa Mwanza
 
Uzima....
Mimi sijaandika dini yeyote lakini muhimu ni kuwa Uislam una historia ya pekee sana kuanzia Tanganyika hadi Tanzania.

Mwaka wa 1968 EAMWS ilitaka kujenga Chuo Kikuu serikali ikaivunja ili chuo kisijengwe.

Tatizo Waarabu.

Katika miaka ya 1970 OIC ilitaka kujenga Chuo Kikuu Tanzania serikali ikakataa.

Waarabu.

1993 Zanzibar ilijiunga na OIC ukazuka mgogoro mkubwa.

Waarabu.

1997 Darul Imaan kutoka Saudia walitaka kujenga shule Kibaha ikavumishwa kuwa Waarabu wanapora ardhi Kibaha.

Shule haikujengwa.

Waarabu...
Vipi kuhusu content za huu mkataba Maalim,umeridhika nazo?
 
Mwenyekiti wa CUF Prof Lipumba naye amepinga mkataba huu mapema tu. mnasemaje? ni udini au la tuwe makini sana na ndimi zetu,tunachafua taasisi ya Rais.
 
Sheikh Qaasimu Ibn Mafuta Ibn Qaasimu Ibn Othmaan Kutokea Markaz Ibn Taymiyyah Pongwe Tanga Tanzania, Katika Khutba Yake Ya Ijumaa, Ametoa Ujumbe Kwa Viongozi Kuwachukulia Hatua Kali Wale Wanaohamasisha Uvunjifu Wa Amani Kwasababu Ya Mkataba Wa Bandari, Pia Viongozi Wa Dini Kukemea Ubaguzi Wa Kidini Kikanda Unaletwa Na Wanasiasa Kwa Maslahi Yao, Pia Kaeleza Kwa Ufupo Histori Ya Uislamu Pwani Ya Afrika Mashariki (Sofala)
"Khutba Ipo Youtube Kasikilize Kwa Faida Na Wasambazie Wengine"
Kwa Pamoja Tukemee Uvunjifu Wa Amani Na Ubaguzi.
 

Attachments

  • VID-20230822-WA0000.mp4
    2.6 MB
Hivi ni wapi kwenye waraka wa TEC umeongelea kuhusu dini? Na pia kwenye vipengele vya mkataba wa Tanzania na Dubai ni wapi pameandikwa Uislamu? Maana kinapingwa ni vipengele vya kumkabidhi mwarabu sehemu nyeti za nchi. Uwekezaji maalum ndo umeifanya China kufika ilipo leo. Inakuaje tunampa mtu vyote kwa consideration ha Tsh sifuri? Vipi na njia yetu ya kuingia nchini? Bandari ni lango. Langoni hakai adui yako. Kila Taif lingine ambalo sio Tanzania ni adui yetu. Humkabidhi adui lango akulindie
 
Back
Top Bottom