Sheikh wa Mkoa Mwanza (Kuhusu Mjadala wa Bandari): Walaaniwe wote wenye nia ovu na Rais Samia

Sheikh wa Mkoa Mwanza (Kuhusu Mjadala wa Bandari): Walaaniwe wote wenye nia ovu na Rais Samia

TAMKO LA SHEIKH WA MKOA MWANZA KUHUSU MJADALA WA BANDARI

Utangulizi

Kwa kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja kumekuwa na mjadala kuhusu uwekezaji na uendeshaji wa bandari zetu na kampuni kutoka Dubai. Mjadala ulianzishwa na wanasiasa na wanasheria lakini baadae ukachukua sura mpya na ya hatari ambayo nchi yetu haijawahi kushuhudia.

Hoja na mwelekeo wake

Wakati mjadala ulipoanza, hoja kubwa ilikuwa Wazanzibari wawili wanauza bandari za Tanganyika. Baada ya muda si mrefu, mjadala ukachukua sura mpya na kusisitizwa kuwa ni waarabu ndio waliouziwa nchi. Wakati mjadala unaendelea, ulihama kutoka sura ya kisiasa na kuingia udini.

Sote tumeshuhudia viongozi mbalimbali waandamizi wa dini ya kikristo walivyokuwa mstari wa mbele kupinga suala hili na wengine wamediriki kumkejeli Rais Samia Suluhu Hassan. Hii sio mara ya kwanza kwa viongozi wa dini ya kikristo kumkejeli Rais Samia.

Baadhi ya viongozi wa dini ya kikristo wamedai kuwa Rais Samia amevunja Katiba na kwa maana hiyo anastahili kuondolewa madarakani. Mmoja wao ameenda mbali zaidi kwa kutishia kufanyike Mapinduzi ya kumuondoa Rais Samia madarakani. Jambo la ajabu ni kuwa mpaka sasa hakuna hata mtu mmoja ambaye ameupinga mkataba wa bandari kwa hoja za kiuchumi.

Wote waliozungumza na hasa viongozi wa dini ya kikristo wamezungumza kwa jazba na kumshambulia Rais Samia bila sababu za msingi. Kama viongozi hawa wana uchungu na wananchi, tuliwatarajia kupaza sauti zao wakati wa utawala uliopita ambao tumeshuhudia watu wengi kupoteza maisha yao bila maelezo. Pia tumeshuhudia serikali iliyopita imeingia kwenye miradi mikubwa kinyume cha utaratibu. Sote ni mashahidi, hakuna kiongozi hata mmoja wa kiislamu aliyeushambulia uongozi uliopita.

Wito

Mimi ninaamini kuwa mjadala huu umetawaliwa na UDINI na una lengo la kumtoa Rais Samia madarakani kabla ya muda wake. Hivyo basi, kama sheikh wenu wa Mkoa, natoa wito kwa kila mwislam popote alipo katika Mkoa huu, afunge kwa siku 3 na katika kila swala ya Ijumaa kuanzia Ijumaa hii ya tarehe 7 Julai 2023 misikiti YOTE 700 ya Mkoa wa Mwanza isome dua ya kunuti kuwalaani WATU WOTE wenye nia ovu na Rais Samia.

Sheikh Hassan Kabeke ………………………………..

Sheikh wa Mkoa, MWANZA

Tarehe 6 Julai 2023
Mzee Wangu namjua na kumuheshimu sana na najua kuwa amelewa sifa za heshima anayopewa kwenye ngazi tofauti. Ila kwa hili amekurupuka sana au amekosa u shauri ningeomba asikie sana na awe wa mwisho kufungua mdomo wake Ili akidhi Sauti ya waislamu wote anao wasemea
 
Ikiwa ni sheikh wa mkoa ina maanisha ni kutoka BAKWATA na BAKWATA ni tawi la CCM kama ilivyo UWC ama UVCCM, sasa unataraji sheikh aseme nini zaidi ya kusifia na kusupport.

Ukimuuliza huyo sheikh mkataba unahusu nini hana hata moja analolijua. Anachofanya yeye ni kutimiza ada kama mwanchama kufuata maelekezo toka juu.
 
Tamko la mtu asie kuwa na akili hata kidogo ndio tamko gani Hilo lilolenga kuisema dini ya KIKRISTO yani huyu shehe kadhihirisha namba udini ulivyomkaa kwenye mishipa yake ya damu,kaongea pumba tupu sijui hata huwa anaambia nini waumini wake zaidi ya kuwapotosha

THIS IS BULLSHIT
 
Wanalipwa kisirisiri.
Hapo bado hajazungumza mkubwa wao Zuberi, huyo ndio atakuja kumaliza kabisa na lafudhi ya kiarabu feki kama mshihiri aliefilisika kwa kumwaga misifa ya mkataba wa bandari ambao hata haujui unaongelea nini.

Jinsi wanavyomdhihaki Mungu kwa njaa zao usishangae hata wakatoa aya ya uongo kuwa DP World iliandikwa kwenye Quran.
 
Hapo bado hajazungumza mkubwa wao Zuberi, huyo ndio atakuja kumaliza kabisa na lafudhi ya kiarabu feki kama mshihiri aliefilisika kwa kumwaga misifa ya mkataba wa bandari ambao hata haujui unaongelea nini.

Jinsi wanavyomdhihaki Mungu kwa njaa zao usishangae hata wakatoa aya ya uongo kuwa DP World iliandikwa kwenye Quran.
Huyu anatembelea vieite ulinzi na mshahara mrefu vyote vya serikali.
 
Kweli ufinyu we elimu ni mzigo kwa hawa masheikh ubwabwa. Nayeye kaamka kwa kubwatuka na jazba pasina sababu za msingi wala hoja. Ni viongozi gani hao wa kikristo waliomtukana samia suluhu hassan au nae anazusha taharuki.

Sheikh inatakiwa ajue maslahi ya rasilimali za nchi sio swala la waislam au wakristo au wasio na dini bali ni suala la watanzania wote.

Ukosoaji wa uwekezaji huo sio kwa wakristo tu bali hata umma wa waislam nao hawaridhii mkataba huo.

Sheikh inatakiwa afahamu kuwa hata utawala wa bwana magufuli ulikabiliwa na ukosolewaji mkubwa kutoka Kwa viongozi wa kanisa. Pastor mwingira, pastor James makulo, wito wa Tec kwa serikali au sheikh alikuwa asikilizi kipindi hicho! Miradi mingi ilikosolewa ikiwemo ule uwanja wa chato hatukusikia anasema anakosolewa kisa ni mkristo.

Viongozi wa dini na watu baki baada ya mh. Lissu kushambuliwa kwa risasi na nchi kusimama kwa muda huku umma wote wa watanzania ukilaani huku kila mmoja wetu akitoa matamko sheikh huyo akuwepo!. Katika utawala uliokabiriwa na ukosolewaji mkubwa basi ni wabwana magufuli, amini mtu yule alikataliwa na mamilioni ya Watanzania lakini hakuna hata mmoja aliefungua kinywa na kusema anakosolewa kisa ni mkristo au kuna dalili ya udini kwene ukosoaji, huenda sheikh alikuwa kalala.

Umma wa watanganyika hauupingi uwekezaji bali unapinga aina ya mkataba kwa maana watu wanahitaji kujua mashali ya tanganyika katika mkataba. Ni suala dogo tu, Watu wanahitaji mkataba ulio na maslahi kwa taifa. Utampaje mtu uhuru wa bandari zote na hata zitakazo kuwepo si baharini tu hata ziwani au mtoni au iwapo kutatokea fursa za bandari basi DPW wajulishwe.

Suala hili halina chembe ya udini hata kidogo, bali kuna watu wanazusha taharuki za udini ikiwemo sheikh mwenyewe, tawala zote zilizopita zilikumbwa na ukosolewaji lakini watu hawakuona ukosoaji huo kwa minajili ya udini bali kwa maslahi mapana ya taifa.

Ni juzi tu rais Samia alipongezwa na kusifiwa na umma wa watanzania ikiwemo mamilioni ya wakristo nchini, hakuibuka mtu akasema wanamsifia kwasababu ni muislam, Leo kuna ukosolewaji ambao ni jambo la kawaida hata kwa tawala zote zilizopita gafla mtu anasema kuna udini, ohhhh watu wanataka mh raisi eti ajiuzuru, huu ni upuuzi na ujinga unaopaswa kupuuzwa na kila mtanzani mwene akili timamu.

Mtu akisifiwa watu wapo kimya, akikosolewa watu kwa vinywa tena vipana wanasema kisa ni muislam. Pumbafu.
Hawa wanasahau kuwa Hata mangungo Alikua Ana Dini mana ukanda Wa Pwani Ilikua tayari umeshapokea Dini zilizokuja na majahazi Tangu Karne ya 12 . Hata Hivyo mangungo hakuuza Ardhi ya Zanzibar Kwa sababu Ilikua Ina utawala wake. Na mangungo hakuona Mbele kuwa wale Wageni wangekua na athari kiasi Gani Kwa vizazi Mbele yake.

Kwa mkataba Huu Wa DPW Hata usalama Wa nchi Utakua na wakati mgumu sana sana sana. Ni kweli Hawa Jamaa watagawa pesa nyingi sana Kwa watu Kwa sababu Wana agenda ya miaka mingi Mbele .

Ni kweli mashehe na Waislam ni rahisi sana kutumika na kuligawa taifa na Hata kuliingiza kwenye vurugu na ugaidi Mkubwa Zaidi ambao haujawahi kutokea Kwa sababu kubwa kuwa Hawa Waarabu kupitia Dini wanakujaga mara ZOTE na pesa na misaada mikubwa ya kujenga misikiti Kila MAHALI. Kujenga Nyumba za ibada Kwa Waarabu ni thawabu kubwa sana na Serikali zao zinaebdeshwa kidini . Magaidi hua wanaandaliwa na Matajiri Wa Kiarabu kushirikiana na Nchi za Magharibi hasa Marekani.
Hata Hao Dubai wanajua kuwa Mwenyezi MUNGU hakuruhusu Mwanamke kuwa Sultani na kuongoza nchi. Waarabu wanajua wazi kuwa Kipindi hiki Chini ya mwavuli Wa Demokrasia feki ya CCM iliyoruhusu nchi kugawanyika Kwa manufaa ya Wachache ,ndicho kipindi Cha kurejesha Utawala Wa kisultani na koloni lao.

Mfano Ikitokea vita Kati ya Tanzania na Msumbiji au Rwanda nini kitatokea ?
Nadhani wakubwa Wa vyombo Vya Dola hawana habari na hili Kwa sababu vita Kwa nafasi zao haviwagusi wanaweza wakajificha HUKO Dubai na familia zao lakini . Tabú kubwa itabaki Kwa wapiganaji Wa Chini na familia zao.
Ikitokea vitaka Kati ya Tanzania na Msumbiji au Malawi au Rwanda ni wazi kuwa DPW watanunuliwa na upande wenye fedha nyingi ikiwemo upande unaosaidiwa na Marekani na nchi za kibepari.
DPW watazorotesha usalama Wa nchi na kutoa Siri Kwa adui Kwa urahisi sana. Vita za Mataifa na Ukoloni mambo Leo unaongozwa na Nguvu ya kipesa . MWENYE pesa za Kununua mamluki ndiye anayeshinda .
Nchi imeuzwa Kwa mkataba Huu. CCM miaka yote inatumia Dini na ukabila kudhoifisha umoja Wa watanzania dhidi ya udhaifu wao.
Kama hawajui ni Kwamba bandari ni suala la Muungano lakini wameanza na bandari ya DSM Kisha Zanzibar itafuata Kwa mgongo Wa Nyuma. Watapandikiza Kibaraka wao kule na miaka michache ijayo bandari ya Zanzibar itauzwa kutokana na ukweli kuwa mizigo yote itaishia DSM Toka Dubai.
Zanzibar itabidi iuzwe Kwa sababu BIDHAA nyingi watazifuata DSM Badala ya Dubai. Hapo watakwepa vipi kuiuza bandari ya Zanzibar.


Tanzania kiusalama haifungamani na China Wala Marekani lakini Kwa mkataba Huu Tanzania italazimishwa kufungamana na Marekani .
Bandaria kiusalama ni kiungo kikubwa sana wakati Wa uvamizi. Wakoloni walivamia bara la Afrika kupitia majahazi.

Usalama Wa nchi Hii Utakua mdogo sana .

Wazungu wanataka Madini yetu ya kuzalisha Betri Kwa wingi sana .
Wazungu wanataka Urenium, Wazungu wanataka dhahabu ,Wazungu wanataka malaa ya mawe Kwa Sasa , Wazungu wanataka mafuta yatakayopitia Tanga kutoka Uganda.

Mana Samia ameshindwa kuisimamia uchumi Wa nchi Hii Kwa asilimia mia moja . Haiwezekani uchumi Wa nchi Hii yenye rasilimali nyingi na watu wengi ushindwe kuimarika mpaka aje mgeni Kununua nchi . Hapana.
Mwarabu atakaa pale Bandarini Kwa mwaka mmoja tuu atapata pesa za Kununua vifaa vyote Vya kisasa Kwa pesa atakazovuna pale Bandarini.

Rais Kwa mamlaka aliyopewa ameshindwa kuamuru Bandari ifungwe kamera Kila Kona na Taarifa za mizigo yate na makontena yanayoingia yatumwe ofisini kwake . ?

Mashehe Badala ya kuishauri Serikali irekebishe vifungu vinavyokinzana na Kariba na uhuru Wa nchi yetu wao wanahangaika na wakosoaji na Udini wanaouanzisha wao Kwa manufaa ya MTU mmoja na familia yake?
Hii nchi SIO ya kifalme kuwa Labda Sisi wote ni Kama Watoto Wa Rais . No. Hii ni nchi ya kidemokrasia ,Rais anachaguliwa baada ya Kuomba kura . Anapobainika kuwa aliomba kura Kwa malengo yake basi anatolewa madarakani Kwa kampeni kubwa au Kwa maandamano makubwa . Hafai kama halindi nchi na rasilimali za Nchi na usalama Wa nchi dhidi ya adui Wa NJE?

Hii nchi haikuwa na usalama Mkubwa dhidi ya maadui Wa Nje kimchezo mchezo . Wazee Wetu walijitesa Kwa kukataa kununuliwa na kuiuza nchi Ili kulinda uhuru Wetu na utaifa Wetu , Amani yetu na umoja Wetu. Tungeweza kuwa kama Kongo .
Kongo waliuza nchi Yao Kwa Ufaransa wao wakabaki na magitaa ya kucheza rumba. Sasa Sisi leo tunauza nchi yetu Kwa Waarabu ,tutabaki na Simba na Yanga . Na makanisa feki na manabii feki na misikiti itakayojazana na waumini wasio na Elimu ya kujitawala Wala kuutawala uchumi Wa kimataifa na rasilimali zetu. Taifa la wachuuzi Wa BIDHAA kutoka Nje. Wanyama Sasa watabebwa kwenye Meli na SIO ndege Tena. Miaka mia ijayo hapatakuwa na nchi moja ya Tanzania . Nchi itagawanyika vipande vipande , waafrika weusi watauana Kwa unafiki Wa kuwapigania matajiri Wa Kizungu na Kiarabu kama kule Sudani.
Watakaopata wakati mgumu ni Watoto Wa maskini watakaoajiriwa kwenye Majeshi. Hawatalala usingizi kwenye majumba Yao WAKIWA wameacha Sílaha kwenye maghala . Askari Watakwenda majumbani na Bunduki zao kama kule Kongo.
Hapata kuwa na nchi huru Bali ni pango la wezi.
Tumeuzwa Kwa sababu ya kushindwa kwake.

. Wawaulize WanaCCM Kule Zanzibar na Wazanizibara weusi WALIOKO Zanzibar ni Kwa Nini wapotayari muda wote KUFANYA Mapinduzi alimradi wasitawaliwe Tena na Hao Wageni na masalia yao?
 
Wito

Mimi ninaamini kuwa mjadala huu umetawaliwa na UDINI na una lengo la kumtoa Rais Samia madarakani kabla ya muda wake. Hivyo basi, kama sheikh wenu wa Mkoa, natoa wito kwa kila mwislam popote alipo katika Mkoa huu, afunge kwa siku 3 na katika kila swala ya Ijumaa kuanzia Ijumaa hii ya tarehe 7 Julai 2023 misikiti YOTE 700 ya Mkoa wa Mwanza isome dua ya kunuti kuwalaani WATU WOTE wenye nia ovu na Rais Samia.
images (9) - 2022-04-03T234844.624.jpeg
 
Mohamed Said salam sheikh
Naanza kwa tahadhari kwamba unapoleta jambo ni vema ukajiridhisha na uthabiti wake.

Bandiko kutoka kwa Sheikh Hassan halibebi uzito sana isipokuwa kwa kuletwa nawe kwa umaarufu wako
Chukua tahadhari ili usinasibishwe na 'mzigo' kwavile tu umesimama karibu nayo

Sheikh Said, sidhani kama Sheikh Hassan kafanya 'homework yake' vizuri na ikiwa ni hivyo kuna tatizo .

Kwanza, Hassan anasema hoja ilianza kwamba bandari za Tanganyika zinauzwa.
Ni kweli kwasababu Zanzibar imesema bandari zake hazihusiki hivyo zilizobaki ni za Tanganyika.
Neno bandari zimeuzwa linaweza kuwa na ' semantic '. Hivyo Sheikh Hassan aelewe bandari zilihusu Tanganyika

Pili, kwamba MoU imesainiwa na Wazanzibar wawili, ni Ukweli na sahihi zipo. Kwaninia Wazanzibar wanatajwa? Jibu ni kwamba wizara husika si suala la muungano lakini kubwa zaidi ni kuondolewa kwa bandari za Zanzibar.
Ni Wazanzibar wanaolalamika mambo ya muungano kuongezwa, sasa wanaposaini yasiyowahusu inatia shaka.
Lakini pia wapo wataalamu wanahoji, sahihi ya Mwanasheria mkuu ipo wapi?

Tatu, Mh Mbowe alizungumza kwa kuchagua maneno yake kwa umakini mkubwa sana.
Kwa mtu aliyesikiliza video hakuna mahali alileta taharuki zaidi ya kutahadharisha kile alichokiona na kinachoweza kutafsiriwa kinyume na hali ilivyo. Ile video ukiisikiliza utabaini nia ovu ya wanaojaribu kuipotosha, sina hakika sheikh Said na Sheik Hassan wameiona na kuidurusu kwa kina na utulivu video hiyo!

Tatu, hoja ya bandari haikuanza na bandari za Tanganyika bali MoU iliyovuja kutoka serikalini na ambayo haikuwa katika ratiba za Bunge kwa mujibu wa Wataalam. Kuvuja huko na yale yaliyomo kumeibua hisia na mjadala mkali ukihusisha wanasheria, wanasiasa na hata viongozi wa dini zote akiwemo Sheikh Ponda.

Kwamba walizungumza ni viongozi wa Kikristo, hilo si kweli kwani wapo wa dini zote na wana haki kama Raia wengine. Sheikh Hassan akitazama mijadala kwa jicho la dini hatakosa hoja hata siku moja kwasababu Tanzania ina dini mbali mbali na Rais wake wana haki ya kushiriki mijadala bila kutumia dini zao.

Nne,Kwamba viongozi wa Kikristo walikuwa kimya wakati wa utawala wa JPM, hii ni hoja yenye ukweli nusu.
Ukweli uliokamilika ni kwamba viongozi wa dini zote akiwemo sheikh Hassan walikaa kimya wakati uovu ukitendwa, watu kupigwa risasi au kuokotwa katika viroba.

Hivyo, kukaa kimya halikuwa suala la dini moja, lilikuwa la viongozi wote na hapa umma ulifikia mahali kutilia shaka uadilifu na uongofu wa viongozi wa dini pale wanaposhangilia na kuombea viongozi dua hata za biashara za madini na ujenzi wa madaraja bila kujali utu na uhai wa Raia wao. Sheikh Hassan anakumbuka vizuri hili

Tano, kwamba hoja haijaangaliwa kiuchumi si kweli. Sheikh Hassan anataka kuaminisha umma kwamba tatizo ni mkataba wa uchumi. Ukiwasiliza watu wote wakiwemo Wabunge hakuna anayepinga uwekezaji, watu wanapinga kilichomo ndani ya mkataba ambacho viongozi wa serikali wanapaswa kutetea kwa hoja.

Sheikh Hassan atakumbuka Bunge letu lilijadili kauli ya Mbowe zaidi badala ya Mkataba au basi hoja za kiuchumi.
Tulitarajia Sheikh Hassan aanze kusota vidole kwa Bunge kuliko kushambulia watoa maoni kwa imani zao.

Sita, Bunge la JMT lina watu wa aina na imani zote. Bunge limepitisha Mswada bila kuangalia kingine, na hivyo Sheikh Hassan amekuwa na jicho chongo la kutoona Wabunge walioko ni akina nani.

Saba, kwamba Rais SSH anashambuliwa kwa udini ni hoja dhaifu . Sheikh atueleze ni Rais gani alipata ''immunity' ya kutoshambuliwa ? Urais ni taasisi inayobeba sera na maono ya Taifa.

Ni jambo la ajabu sana kama Rais awaye atapewa ufaulu tu kwa kuangalia jinsia, asili au dini.
Hilo halikuwepo na wenye fikra ongofu hawalifikirii hata kidogo.

Nane, inaonekana Sheikh Hassan alichukizwa na neno Tanganyika. Neno hilo linasemwa kila siku kule Zanzibar tena kwa indhara, kashfa na matusi, leo likitumiwa na Watanganyika linakuwa tusi! Sheikh Hassan na jicho chongo.

Tisa, kwavile Sheikh Hassan ameeleza kuna faida za kiuchumi, ni yeye mwenye dhima ya kueleza faida hizo ni zipi.
Kutuhumu wanaotoa maoni tofauti na matarajio yake wakati hana alichoweka mezani si jambo sahihi.

Kumi, hoja ya Sheikh Hassan inajengwa katika misingi ya udini badala ya uhalisia. Sheikh arudi na kupita video ya Mbowe, apitie mkataba na malalamiko ya wananchi wakiwemo viongozi wote wa dini, arejee katika mkataba na kufafanua vifungu vinavyolalamikiwa na aeleze faida za uchumi. Bila hayo andiko lake lina sura tofauti

Ni kwa msingi huo tunamshauri tena Mohamed Said kuwa mwangalifu wakati wa 'kubeba mizigo' , mingine inachuruzika shombo na hivyo kuichukiza kanzu yake nadhifu achilia mbali jicho la makumi na mamia ya Wapendwa wanaomtazama kwa mahaba, mfano na wivu mkubwa!

Mag3 Fundi Mchundo JokaKuu Pascal Mayalla
Hii ungemperekea Sheikh inbox kabisa ili ajielimishe.
Nakuunga mkono
 
..SHURA YA MAIMAMU walitoa waraka mzuri kushinda huu wa Shekhe wa Mkoa wa Mwanza.

..Namuomba Shekhe wetu awasihi upande wa serikali warekebishe mkataba kwani umepingwa na kukosolewa vikali na wanazuoni wakubwa wa masuala ya sheria na mikataba.

cc Nguruvi3
Kuna mambo 'interesting' na sijui kama watu wanayaona

Waraka wa Shura sikumbuki kama Mo aliuleta hapa kwasababu ulikuwa na ''Facts'
Huu wa Sheikh wa Bakwata ambayo Mo anaipinga kwa maneno na maandiko kauleta - ' Fanatic'

Sheikh Mohamed Said atachukua upande kama hoja ina 'fit narrative' yake.

Wabunge walimshambulia Mbowe kwasababu hawakuwa na hoja za kutetea mswada.
Mjadala wa Bunge ukazama kwa Mbowe na si Mkataba (Tulia A) uliopelekwa Bungeni.
Mbowe akaziba Ombwe la hoja kwasababu Wabunge wengine hata kuelewa kimendikwa nini sina hakika

Hoja yao dhidi ya Mbowe ni kutahadharisha, wakachukua maneno ya Utanganyika na Uzanzibar wakayafanya agenda. Wabunge hawasemi kuhusu Utanganyika na Uzanzibar unaonezwa kwa chuki na ACT Wazalendo ya akina Jussa, Duni na Othman Masoud

Wanamtuhumu Mbowe eti kwa kugusa muungano, lakini Wabunge hao hao hawasemi lolote wakati Jussa, Duni Haji na Masoud Othman wakitaka mamlaka kamili kwa maana moja, kuvunja muungano.

Upotoshaji umetumika kusema Wananchi hawataki uwekezaji. Hakuna anayekataa uwekezaji, Wananchi wanahoji maudhui (contents) za mkataba ambazo hatma yake itakuwa kama ile ya umeme wa Dowans.
Ndege za ATC haziruki kwasababu ya mikataba mibovu ya huko nyuma. Ubaya wa kuhoji upo wapi!

Na Ombwe la kujibu hoja limepelekea kuchomeka hoja ya udini. Watu wanaoshadidia hoja hii hawajibu hoja za maudhui ya mkataba, wamekomalia fulani ni mwislam na wawekezaji ni Waarabu.

Hivi Netgroup ya Mkapa, Dowans na Richmond za Kikwete zilikuwa za Waarabu!
JNHPP ya JPM si ya Waarabu, SGR si inajengwa na Edogan wa Turkiye anayelinda maslahi ya Waislam duniani kuliko Waarabu. Je, lini tuliacha kusema ya Mkapa, JK na JPM?

Suala zima ni upungufu wa hoja za kujibu na wanaposhindwa kujibu wanakimbilia Vihoja vya Mbowe na Udini.
 
Shehe ubwabwa,amejaa naye kaingia kwa vile hata uelewa tu wa mambo hajui zaidi ya mihemuko,angejenga hoja juu ya mkataba angeonekana wa maana,hakuna mtu asiyetaka mwekezaji inshu ni mkataba,mkataba mbovu haufai kila mwenye akili na mwenye kuipanda hii nchi hawezi akakubali aina hii ya mkataba.
Oyaa sheikh ubwabwa huu ndio msimamo wake "Hivyo basi, kama sheikh wenu wa Mkoa, natoa wito kwa kila mwislam popote alipo katika Mkoa huu, afunge kwa siku 3 na katika kila swala ya Ijumaa kuanzia Ijumaa hii ya tarehe 7 Julai 2023 misikiti YOTE 700 ya Mkoa wa Mwanza isome dua ya kunuti kuwalaani WATU WOTE wenye nia ovu na Rais Samia"
 
Kuna mambo 'interesting' na sijui kama watu wanayaona

Waraka wa Shura sikumbuki kama Mo aliuleta hapa kwasababu ulikuwa na ''Facts'
Huu wa Sheikh wa Bakwata ambayo Mo anaipinga kwa maneno na maandiko kauleta - ' Fanatic'

Sheikh Mohamed Said atachukua upande kama hoja ina 'fit narrative' yake.

Wabunge walimshambulia Mbowe kwasababu hawakuwa na hoja za kutetea mswada.
Mjadala wa Bunge ukazama kwa Mbowe na si Mkataba (Tulia A) uliopelekwa Bungeni.
Mbowe akaziba Ombwe la hoja kwasababu Wabunge wengine hata kuelewa kimendikwa nini sina hakika

Hoja yao dhidi ya Mbowe ni kutahadharisha, wakachukua maneno ya Utanganyika na Uzanzibar wakayafanya agenda. Wabunge hawasemi kuhusu Utanganyika na Uzanzibar unaonezwa kwa chuki na ACT Wazalendo ya akina Jussa, Duni na Othman Masoud

Wanamtuhumu Mbowe eti kwa kugusa muungano, lakini Wabunge hao hao hawasemi lolote wakati Jussa, Duni Haji na Masoud Othman wakitaka mamlaka kamili kwa maana moja, kuvunja muungano.

Upotoshaji umetumika kusema Wananchi hawataki uwekezaji. Hakuna anayekataa uwekezaji, Wananchi wanahoji maudhui (contents) za mkataba ambazo hatma yake itakuwa kama ile ya umeme wa Dowans.
Ndege za ATC haziruki kwasababu ya mikataba mibovu ya huko nyuma. Ubaya wa kuhoji upo wapi!

Na Ombwe la kujibu hoja limepelekea kuchomeka hoja ya udini. Watu wanaoshadidia hoja hii hawajibu hoja za maudhui ya mkataba, wamekomalia fulani ni mwislam na wawekezaji ni Waarabu.

Hivi Netgroup ya Mkapa, Dowans na Richmond za Kikwete zilikuwa za Waarabu!
JNHPP ya JPM si ya Waarabu, SGR si inajengwa na Edogan wa Turkiye anayelinda maslahi ya Waislam duniani kuliko Waarabu. Je, lini tuliacha kusema ya Mkapa, JK na JPM?

Suala zima ni upungufu wa hoja za kujibu na wanaposhindwa kujibu wanakimbilia Vihoja vya Mbowe na Udini.
Ndugu hawa jamaa ikija hoja ya udini yuko tayari atunge uongo ili aonekane ana haki.
Mfuatilie huyu mzee uongo anaomwaga daliy humu.
Kutwa kucha kuongelea wapigania uhuru. Muulize kuhusu John Okelo atakuambia hamjui
 
Back
Top Bottom