Sheikh wa Mkoa Mwanza (Kuhusu Mjadala wa Bandari): Walaaniwe wote wenye nia ovu na Rais Samia

Sheikh wa Mkoa Mwanza (Kuhusu Mjadala wa Bandari): Walaaniwe wote wenye nia ovu na Rais Samia

Mohamed Said salam sheikh
Naanza kwa tahadhari kwamba unapoleta jambo ni vema ukajiridhisha na uthabiti wake.

Bandiko kutoka kwa Sheikh Hassan halibebi uzito sana isipokuwa kwa kuletwa nawe kwa umaarufu wako
Chukua tahadhari ili usinasibishwe na 'mzigo' kwavile tu umesimama karibu nayo

Sheikh Said, sidhani kama Sheikh Hassan kafanya 'homework yake' vizuri na ikiwa ni hivyo kuna tatizo .

Kwanza, Hassan anasema hoja ilianza kwamba bandari za Tanganyika zinauzwa.
Ni kweli kwasababu Zanzibar imesema bandari zake hazihusiki hivyo zilizobaki ni za Tanganyika.
Neno bandari zimeuzwa linaweza kuwa na ' semantic '. Hivyo Sheikh Hassan aelewe bandari zilihusu Tanganyika

Pili, kwamba MoU imesainiwa na Wazanzibar wawili, ni Ukweli na sahihi zipo. Kwaninia Wazanzibar wanatajwa? Jibu ni kwamba wizara husika si suala la muungano lakini kubwa zaidi ni kuondolewa kwa bandari za Zanzibar.
Ni Wazanzibar wanaolalamika mambo ya muungano kuongezwa, sasa wanaposaini yasiyowahusu inatia shaka.
Lakini pia wapo wataalamu wanahoji, sahihi ya Mwanasheria mkuu ipo wapi?

Tatu, Mh Mbowe alizungumza kwa kuchagua maneno yake kwa umakini mkubwa sana.
Kwa mtu aliyesikiliza video hakuna mahali alileta taharuki zaidi ya kutahadharisha kile alichokiona na kinachoweza kutafsiriwa kinyume na hali ilivyo. Ile video ukiisikiliza utabaini nia ovu ya wanaojaribu kuipotosha, sina hakika sheikh Said na Sheik Hassan wameiona na kuidurusu kwa kina na utulivu video hiyo!

Tatu, hoja ya bandari haikuanza na bandari za Tanganyika bali MoU iliyovuja kutoka serikalini na ambayo haikuwa katika ratiba za Bunge kwa mujibu wa Wataalam. Kuvuja huko na yale yaliyomo kumeibua hisia na mjadala mkali ukihusisha wanasheria, wanasiasa na hata viongozi wa dini zote akiwemo Sheikh Ponda.

Kwamba walizungumza ni viongozi wa Kikristo, hilo si kweli kwani wapo wa dini zote na wana haki kama Raia wengine. Sheikh Hassan akitazama mijadala kwa jicho la dini hatakosa hoja hata siku moja kwasababu Tanzania ina dini mbali mbali na Rais wake wana haki ya kushiriki mijadala bila kutumia dini zao.

Nne,Kwamba viongozi wa Kikristo walikuwa kimya wakati wa utawala wa JPM, hii ni hoja yenye ukweli nusu.
Ukweli uliokamilika ni kwamba viongozi wa dini zote akiwemo sheikh Hassan walikaa kimya wakati uovu ukitendwa, watu kupigwa risasi au kuokotwa katika viroba.

Hivyo, kukaa kimya halikuwa suala la dini moja, lilikuwa la viongozi wote na hapa umma ulifikia mahali kutilia shaka uadilifu na uongofu wa viongozi wa dini pale wanaposhangilia na kuombea viongozi dua hata za biashara za madini na ujenzi wa madaraja bila kujali utu na uhai wa Raia wao. Sheikh Hassan anakumbuka vizuri hili

Tano, kwamba hoja haijaangaliwa kiuchumi si kweli. Sheikh Hassan anataka kuaminisha umma kwamba tatizo ni mkataba wa uchumi. Ukiwasiliza watu wote wakiwemo Wabunge hakuna anayepinga uwekezaji, watu wanapinga kilichomo ndani ya mkataba ambacho viongozi wa serikali wanapaswa kutetea kwa hoja.

Sheikh Hassan atakumbuka Bunge letu lilijadili kauli ya Mbowe zaidi badala ya Mkataba au basi hoja za kiuchumi.
Tulitarajia Sheikh Hassan aanze kusota vidole kwa Bunge kuliko kushambulia watoa maoni kwa imani zao.

Sita, Bunge la JMT lina watu wa aina na imani zote. Bunge limepitisha Mswada bila kuangalia kingine, na hivyo Sheikh Hassan amekuwa na jicho chongo la kutoona Wabunge walioko ni akina nani.

Saba, kwamba Rais SSH anashambuliwa kwa udini ni hoja dhaifu . Sheikh atueleze ni Rais gani alipata ''immunity' ya kutoshambuliwa ? Urais ni taasisi inayobeba sera na maono ya Taifa.

Ni jambo la ajabu sana kama Rais awaye atapewa ufaulu tu kwa kuangalia jinsia, asili au dini.
Hilo halikuwepo na wenye fikra ongofu hawalifikirii hata kidogo.

Nane, inaonekana Sheikh Hassan alichukizwa na neno Tanganyika. Neno hilo linasemwa kila siku kule Zanzibar tena kwa indhara, kashfa na matusi, leo likitumiwa na Watanganyika linakuwa tusi! Sheikh Hassan na jicho chongo.

Tisa, kwavile Sheikh Hassan ameeleza kuna faida za kiuchumi, ni yeye mwenye dhima ya kueleza faida hizo ni zipi.
Kutuhumu wanaotoa maoni tofauti na matarajio yake wakati hana alichoweka mezani si jambo sahihi.

Kumi, hoja ya Sheikh Hassan inajengwa katika misingi ya udini badala ya uhalisia. Sheikh arudi na kupita video ya Mbowe, apitie mkataba na malalamiko ya wananchi wakiwemo viongozi wote wa dini, arejee katika mkataba na kufafanua vifungu vinavyolalamikiwa na aeleze faida za uchumi. Bila hayo andiko lake lina sura tofauti

Ni kwa msingi huo tunamshauri tena Mohamed Said kuwa mwangalifu wakati wa 'kubeba mizigo' , mingine inachuruzika shombo na hivyo kuichukiza kanzu yake nadhifu achilia mbali jicho la makumi na mamia ya Wapendwa wanaomtazama kwa mahaba, mfano na wivu mkubwa!

Mag3 Fundi Mchundo JokaKuu Pascal Mayalla
Bahati mbaya Mohamed hatafuata ushauri wako kwa sababu yeye anaangalia kila kitu kwa msingi ya kutetea dini yake na wafuasi wenzake wa dini hiyo dhidi ya udhalimu wa wakristu na dini yao. Wakati wakristu kama Lissu waliwatetea kwa sauti kubwa masheikh waliokuwa mahabusu na walikemea yaliyotokea Kibiti, Mohamed hajawahi kunyanyua sauti yake pale wakristu kama Lissu, Mbowe na wengine walipokuwa wanapitia wakati mgumu. Kwake yeye utu unapimwa kwa misingi ya Umma. Inasikitisha lakini haishangazi kumuona akipigia debe ya hoja kuwa Rais wa sasa anapingwa kwa sababu ya dini yake au/na uzawa ( lakini sio jinsia yake maana hata yeye ana tatizo na hilo) wake.

Profesa Lipumba ni mmoja wa wasomi wa kwanza waliolalamikia huu mkataba. Jopo la TLS lililopitia huu mkataba lilijumuisha waislamu. Profesa Shivji ni msomi mwingine muislamu aliyeukosoa huu mkataba. Hao wote hawaoni anawaona wakina Anna, Tundu, Freeman, John na wamisheni wengine. Hajiulizi kwa nini huu mkataba hautetewi at full throttle na wanasheria wabobezi wa serikali na viongozi wengine?
Humu ndani hakuna Rais aliyepita ambae hajawahi kukosolewa. Wakati wa JPM watu kutoka dini zote walikuwa wakimkosoa. Sikusikia hata siku moja akitetewa kuwa wanaomkosoa wanafanya hivyo kwa sababu wana chuki na wamisheni.

Mohamed anachezea kiberiti petrol station bila kujali kuwa mlipuko wake utatuathiri wote pamoja na yeye. Msingi wa nchi yetu ni secularism na jamii yetu imeishi kwa upendo na ushirikiano bila kujali dini zetu. Mohamed na wenzake wasiruhusiwe kutuharibia nchi yetu.

Amandla....
Nguruvi3 Mag3 JokaKuu
 
Oyaa sheikh ubwabwa huu ndio msimamo wake "Hivyo basi, kama sheikh wenu wa Mkoa, natoa wito kwa kila mwislam popote alipo katika Mkoa huu, afunge kwa siku 3 na katika kila swala ya Ijumaa kuanzia Ijumaa hii ya tarehe 7 Julai 2023 misikiti YOTE 700 ya Mkoa wa Mwanza isome dua ya kunuti kuwalaani WATU WOTE wenye nia ovu na Rais Samia"

Shehe wa hovyo sana,anaonyesha jinsi alivyo mburura.
 
IMG_3873.jpg
 
Muda utaongea...
Wamefungua mlango uliokuwa ukisubiriwa kufunguliwa kwa muda mrefu.

Yatasikika sasa mengi yaliyokuwa yanatafutiwa nafasi yasemwe hadharani kama hivi.

Kuna maswali mengi yanayotakiwa kujibiwa.

Bahati mbaya kwao ni kuwa hawana majibu ya maswali haya.

Ashakum si matusi.
Wamechamba kwa jani la mgomba.

Matokeo yake watabakia na uchafu wao.
 
Ukatili wa magufuli hauhalalishi Bandari yetu kugawiwa kwa Waarabu.
 
Bahati mbaya Mohamed hatafuata ushauri wako kwa sababu yeye anaangalia kila kitu kwa msingi ya kutetea dini yake na wafuasi wenzake wa dini hiyo dhidi ya udhalimu wa wakristu na dini yao. Wakati wakristu kama Lissu waliwatetea kwa sauti kubwa masheikh waliokuwa mahabusu na walikemea yaliyotokea Kibiti, Mohamed hajawahi kunyanyua sauti yake pale wakristu kama Lissu, Mbowe na wengine walipokuwa wanapitia wakati mgumu. Kwake yeye utu unapimwa kwa misingi ya Umma. Inasikitisha lakini haishangazi kumuona akipigia debe ya hoja kuwa Rais wa sasa anapingwa kwa sababu ya dini yake au/na uzawa ( lakini sio jinsia yake maana hata yeye ana tatizo na hilo) wake.
Profesa Lipumba ni mmoja wa wasomi wa kwanza waliolalamikia huu mkataba. Jopo la TLS lililopitia huu mkataba lilijumuisha waislamu. Profesa Shivji ni msomi mwingine muislamu aliyeukosoa huu mkataba. Hao wote hawaoni anawaona wakina Anna, Tundu, Freeman, John na wamisheni wengine. Hajiulizi kwa nini huu mkataba hautetewi at full throttle na wanasheria wabobezi wa serikali na viongozi wengine?
Humu ndani hakuna Rais aliyepita ambae hajawahi kukosolewa. Wakati wa JPM watu kutoka dini zote walikuwa wakimkosoa. Sikusikia hata siku moja akitetewa kuwa wanaomkosoa wanafanya hivyo kwa sababu wana chuki na wamisheni.
Mohamed anachezea kiberiti petrol station bila kujali kuwa mlipuko wake utatuathiri wote pamoja na yeye. Msingi wa nchi yetu ni secularism na jamii yetu imeishi kwa upendo na ushirikiano bila kujali dini zetu. Mohamed na wenzake wasiruhusiwe kutuharibia nchi yetu.

Amandla....
Nguruvi3 Mag3 JokaKuu
Fundi...
Upendo gani huu wa kuivunja EAMWS kuzuia Waislam wasijenge Chuo Kikuu 1968?

Upendo gani huu serikali kukataa OIC wasijenge Chuo Kikuu Tanzania miaka ya 1970?

Upendo gani huu Wizara ya Elimu kuhodhiwa na kuwekwa mkakati wa kuzuia Waislam wasipate elimu ya juu?

Upendo gani huu NECTA kuhodhiwa na kuhujumu shule za Waislam?

Au haya huyajui?
Hivi ndiyo kuishi kwa upendo?

Imefikiwa hadi kufuta historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika kuwakwepa Waislam.

Nikairejesha historia hii kupitia kitabu cha Abdul Sykes.

Haya tunayazungumza hapa huu sasa mwaka wa 10.

Yapo mengi ikiwa utapenda nitayaweka hapa kwa ushahidi tujadiliane.

Uko tayari?
 
Fundi...
Upendo gani huu wa kuivunja EAMWS kuzuia Waislam wasijenge Chuo Kikuu 1968?

Upendo gani huu serikali kukataa OIC wasijenge Chuo Kikuu Tanzania miakaya 1970?

Upendo gani huu Wizara ya Elimu kuhodhiwa na kuwekwa mkakati wa kuzuia Waislam wasipate elimu ya juu?

Upendo gani huu NECTA kuhodhiwa na kuhujumu shule za Waislam?

Au haya huyajui?
Hivi ndiyo kuishi kwa upendo?

Imefikiwa hadi kufuta historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika kuwakwepa Waislam.

Nikairejesha historia hii kupitia kitabu cha Abdul Sykes.

Haya tunayazungumza hapa huu sasa mwaka wa 10.

Yapo mengi ikiwa utapenda nitayaweka hapa kwa ushahidi tujadiliane.

Uko tayari?
Mohamed,hayo yote unayosema nayajua.
Kifo cha EAMWS ( taasisi iliyoanzishwa na Aga Khan mShia ambae nyie mnawaona apostate) kilitokana na wao kukataliwa na Karume ambae hakuwa mkristu kwa kuiona kuwa ni taasisi ya waarabu na wahindi. Aga Khan (muasisi wa EAMWS) muislamu hajawahi kuzuiwa kujenga Chuo Kikuu Tanzania.

Upendo ni mmisheni kutaifisha mamia ya shule za wamisheni ili kila raia aweze kupata elimu anayostahili. Upendo ni mmisheni kuchukua chuo kilichojengwa kwa fedha za umma na kuipa bure taasisi ya kiislamu ili wakigeuze kuwa Chuo Kikuu cha Kiislamu. Vyote hivi huvioni kwa sababu chuki za kidini ziko kwenye DNA yako.

Waislamu walipewa eneo la kujenga Chuo Kikuu chao Chang'ombe lakini hamkuweza kukiendeleza mpaka mwishoni mkaamua kukiuza kwa mfanyabiashara mmoja wa kiislamu. OIC haijawahi kuzuiwa kuanzisha Chuo Kikuu Tanzania. Kilichopigiwa kelele na Nyerere ni Zanzibar kujiunga kinyemela na OIC. Sasa kama rushwa ya kujiunga ili kuwa ni kujengewa Chuo Kikuu ndio kwanza nasikia. Na kama walikuwa na nia ya dhati ya kujenga hicho Chuo Kikuu kitu gani kinacho wazuia hadi leo?

Hawa maprofesa, madaktari na wasomi kibao wa kiislamu walipatikanaje wakati unasema wizara ya elimu haikutaka wapate elimu? Badala ya kujiangalia wenyewe na kujiuliza kwa nini vijana wenu hawafanyi vizuri kama vijana wa dini nyingine, unashinda kutafuta mchawi. Na kwa vile sio waislamu wote ambao hawafanyi vizuri ingekuwa busara zaidi kujifunza kutoka wale wanaofanya vizuri pamoa na wale wa dini nyingine wanaofanya vizuri.

Hizo shule za FEZA, Al-Muntazir ni za wakristu? Shule gani ya kiislamu iliyohujumiwa kwa sababu tu ni ya kiislamu na sio kwa sababu ya matendo ya uongozi wake? Au unazungumzia ile shule iliyomdhulumu maksi binti maskini wa kiislamu na kuwapa wale wenye uwezo wa kifedha? Ulitaka isiadhibiwe kwa sababu ilikuwa inamilikiwa na kuendeshwa na waislamu? Seriously!

Hilo la kufuta historia ya mchango wa waislamu tumeijadili sana humu ndani na imekuwa debunked. Tofauti na unavyotaka mchango wa wazazi wako wa Gerezani wapewe kipaumbele, ukweli ni kuwa watu kutoka dini na makabila yote walipigania uhuru bila kujali dini au kabila zao. Hao wakina Sykes, walipigania kama wazalendo wa kitanganyika na sio waislamu. Hawakupigania uhuru ili kuigeuza Tanganyika iwe Caliphate bali iwe nchi ambayo watoto wao na wa wakina Julius John, Dennis na wengine waweze kuishi pamoja kwa upendo na kuheshimiana katika nchi yao ya Tanganyika. Kitu ambacho kwa kiasi kikubwa walifanikiwa na kitaendelea kufanikiwa pamoja na juhudi zako wewe na wenzako za kupanda mbegu za chuki katika jamii yetu.

Mwenyewe unajua kuwa hamna jipya tunaloweza kujadiliana kuhusu mchango wa waislamu katika jamii yetu. Ushahidi mwingi uliouweka uligundulika kuwa ni fake au ulikuwa wa kupotosha. Mimi sikatai kuwa waislamu kama wakina Sykes, Aziz, Mwapachu walitoa mchango mkubwa katika juhudi za ukombozi wa nchi hii. Ninachokataa ni wewe kutaka mchango wao upewe nafasi kubwa kuliko wa wakina Julius na John kwa sababu tu ni waislamu.

Ninakataa kuwa mchango wao haukupewa uzito uliostahili kwa sababu ya dini yao kwa sababu mchango wa wakristu wengi tu kama wakina Vedastus Kyaruzi, Dennis Phombeah, John mwakangale, John Rupia, Mwanjisi na wengine wengi tu nao haujapewa heshima inayostahili. Nyerere pamoja na kuwa mkatoliki lakini aliwatia kizuizini wakristu wengi na kuwafungulia wengi kesi za uhaini. Kumgeuza mdini ni kutomtendea haki. Nyerere ana mengi ya kukoselewa lakini sio kwenye masuala ya ubaguzi hasa wa dini.

Amandla...

Nguruvi3 JokaKuu Mag3
 
Mohamed,hayo yote unayosema nayajua.
Kifo cha EAMWS ( taasisi iliyoanzishwa na Aga Khan mShia ambae nyie mnawaona apostate) kilitokana na wao kukataliwa na Karume ambae hakuwa mkristu kwa kuiona kuwa ni taasisi ya waarabu na wahindi. Aga Khan (muasisi wa EAMWS) muislamu hajawahi kuzuiwa kujenga Chuo Kikuu Tanzania.

Upendo ni mmisheni kutaifisha mamia ya shule za wamisheni ili kila raia aweze kupata elimu anayostahili. Upendo ni mmisheni kuchukua chuo kilichojengwa kwa fedha za umma na kuipa bure taasisi ya kiislamu ili wakigeuze kuwa Chuo Kikuu cha Kiislamu. Vyote hivi huvioni kwa sababu chuki za kidini ziko kwenye DNA yako.

Waislamu walipewa eneo la kujenga Chuo Kikuu chao Chang'ombe lakini hamkuweza kukiendeleza mpaka mwishoni mkaamua kukiuza kwa mfanyabiashara mmoja wa kiislamu. OIC haijawahi kuzuiwa kuanzisha Chuo Kikuu Tanzania. Kilichopigiwa kelele na Nyerere ni Zanzibar kujiunga kinyemela na OIC. Sasa kama rushwa ya kujiunga ili kuwa ni kujengewa Chuo Kikuu ndio kwanza nasikia. Na kama walikuwa na nia ya dhati ya kujenga hicho Chuo Kikuu kitu gani kinacho wazuia hadi leo?

Hawa maprofesa, madaktari na wasomi kibao wa kiislamu walipataje wizara ya elimu haikutaka wapate elimu? Badala ya kujiangalia wenyewe na kujiuliza kwa nini vijana wenu hawafanyi vizuri kama vijana wa dini nyingine, unashinda kutafuta mchawi. Na kwa vile sio waislamu wote ambao hawafanyi vizuri ingekuwa busara zaidi kujifunza kutoka wale wanaofanya vizuri pamoa na wale wa dini nyingine wanaofanya vizuri.

Hizo shule za FEZA, Al-Muntazir ni za wakristu? Shule gani ya kiislamu iliyohujumiwa kwa sababu tu ni ya kiislamu na sio kwa sababu ya matendo ya uongozi wake? Au unazungumzia ile shule iliyomdhulumu maksi binti maskini wa kiislamu na kuwapa wale wenye uwezo wa kifedha? Ulitaka isiadhibiwe kwa sababu ilikuwa inamilikiwa na kuendeshwa na waislamu? Seriously!

Hilo la kufuta historia ya mchango wa waislamu tumeijadili sana humu ndani na imekuwa debunked. Tofauti na unavyotaka mchango wa wazazi wako wa Gerezani wapewe kipaumbele, ukweli ni kuwa watu kutoka dini na makabila yote walipigania uhuru bila kujali dini au kabila zao. Hao wakina Sykes, walipigania kama wazalendo wa kitanganyika na sio waislamu. Hawakupigania uhuru ili kuigeuza Tanganyika iwe Caliphate bali iwe nchi ambayo watoto wao na wa wakina Julius John, Dennis na wengine waweze kuishi pamoja kwa upendo na kuheshimiana katika nchi yao ya Tanganyika. Kitu ambacho kwa kiasi kikubwa walifanikiwa na kitaendelea kufanikiwa pamoja na juhudi zako wewe na wenzako za kupanda mbegu za chuki katika jamii yetu.

Mwenyewe unajua kuwa hamna jipya tunaloweza kujadiliana kuhusu mchango wa waislamu katika jamii yetu. Ushahidi mwingi uliouweka uligundulika kuwa ni fake au ulikuwa wa kupotosha. Mimi sikatai kuwa waislamu kama wakina Sykes, Aziz, Mwapachu walitoa mchango mkubwa katika juhudi za ukombozi wa nchi hii. Ninachokataa ni wewe kutaka mchango wao upewe nafasi kubwa kuliko wa wakina Julius na John kwa sababu tu ni waislamu.

Ninakataa kuwa mchango wao haukupewa uzito uliostahili kwa sababu ya dini yao kwa sababu mchango wa wakristu wengi tu kama wakina Vedastus Kyaruzi, Dennis Phombeah, John mwakangale, John Rupia, Mwanjisi na wengine wengi tu nao haujapewa heshima inayostahili. Nyerere pamoja na kuwa mkatoliki lakini aliwatia kizuizini wakristu wengi na kuwafungulia wengi kesi za uhaini. Kumgeuza mdini ni kutomtendea haki. Nyerere ana mengi ya kukoselewa lakini sio kwenye masuala ya ubaguzi hasa wa dini.

Amandla...

Nguruvi3 JokaKuu Mag3
Kiukweli tangu huyu Mzee aliposhindwa kuandika lolote juu ya matukio ya Kibiti na Rufiji nilimpuuza mazima mbaya zaidi kupotosha kwa makusudi juu ya harakati za kudai uhuru kwa kuchochea udini nilimdharau zaidi.

Na hatari yake Wala haioni kabisa na kwakua maisha ni Karma lazma hili litamtafuna na kizazi chake ni miongoni mwa Watu walionyuma ya Ile kampeni ya waliochoma nyaraka na vitabu vya Mwl Nyerere hawampendi Julius lakini hajiulizi kwanini hao anaowapamba ndiyo waliompa Nyerere baraka zote na hii heshima aliyo nayo leo kwa Taifa hili.

Mimi siamini katika dini,kabila Wala itikadi yoyote Mimi ninaamini katika Tanzania yetu.
 
Mohamed,hayo yote unayosema nayajua.
Kifo cha EAMWS ( taasisi iliyoanzishwa na Aga Khan mShia ambae nyie mnawaona apostate) kilitokana na wao kukataliwa na Karume ambae hakuwa mkristu kwa kuiona kuwa ni taasisi ya waarabu na wahindi. Aga Khan (muasisi wa EAMWS) muislamu hajawahi kuzuiwa kujenga Chuo Kikuu Tanzania.

Upendo ni mmisheni kutaifisha mamia ya shule za wamisheni ili kila raia aweze kupata elimu anayostahili. Upendo ni mmisheni kuchukua chuo kilichojengwa kwa fedha za umma na kuipa bure taasisi ya kiislamu ili wakigeuze kuwa Chuo Kikuu cha Kiislamu. Vyote hivi huvioni kwa sababu chuki za kidini ziko kwenye DNA yako.

Waislamu walipewa eneo la kujenga Chuo Kikuu chao Chang'ombe lakini hamkuweza kukiendeleza mpaka mwishoni mkaamua kukiuza kwa mfanyabiashara mmoja wa kiislamu. OIC haijawahi kuzuiwa kuanzisha Chuo Kikuu Tanzania. Kilichopigiwa kelele na Nyerere ni Zanzibar kujiunga kinyemela na OIC. Sasa kama rushwa ya kujiunga ili kuwa ni kujengewa Chuo Kikuu ndio kwanza nasikia. Na kama walikuwa na nia ya dhati ya kujenga hicho Chuo Kikuu kitu gani kinacho wazuia hadi leo?

Hawa maprofesa, madaktari na wasomi kibao wa kiislamu walipataje wizara ya elimu haikutaka wapate elimu? Badala ya kujiangalia wenyewe na kujiuliza kwa nini vijana wenu hawafanyi vizuri kama vijana wa dini nyingine, unashinda kutafuta mchawi. Na kwa vile sio waislamu wote ambao hawafanyi vizuri ingekuwa busara zaidi kujifunza kutoka wale wanaofanya vizuri pamoa na wale wa dini nyingine wanaofanya vizuri.

Hizo shule za FEZA, Al-Muntazir ni za wakristu? Shule gani ya kiislamu iliyohujumiwa kwa sababu tu ni ya kiislamu na sio kwa sababu ya matendo ya uongozi wake? Au unazungumzia ile shule iliyomdhulumu maksi binti maskini wa kiislamu na kuwapa wale wenye uwezo wa kifedha? Ulitaka isiadhibiwe kwa sababu ilikuwa inamilikiwa na kuendeshwa na waislamu? Seriously!

Hilo la kufuta historia ya mchango wa waislamu tumeijadili sana humu ndani na imekuwa debunked. Tofauti na unavyotaka mchango wa wazazi wako wa Gerezani wapewe kipaumbele, ukweli ni kuwa watu kutoka dini na makabila yote walipigania uhuru bila kujali dini au kabila zao. Hao wakina Sykes, walipigania kama wazalendo wa kitanganyika na sio waislamu. Hawakupigania uhuru ili kuigeuza Tanganyika iwe Caliphate bali iwe nchi ambayo watoto wao na wa wakina Julius John, Dennis na wengine waweze kuishi pamoja kwa upendo na kuheshimiana katika nchi yao ya Tanganyika. Kitu ambacho kwa kiasi kikubwa walifanikiwa na kitaendelea kufanikiwa pamoja na juhudi zako wewe na wenzako za kupanda mbegu za chuki katika jamii yetu.

Mwenyewe unajua kuwa hamna jipya tunaloweza kujadiliana kuhusu mchango wa waislamu katika jamii yetu. Ushahidi mwingi uliouweka uligundulika kuwa ni fake au ulikuwa wa kupotosha. Mimi sikatai kuwa waislamu kama wakina Sykes, Aziz, Mwapachu walitoa mchango mkubwa katika juhudi za ukombozi wa nchi hii. Ninachokataa ni wewe kutaka mchango wao upewe nafasi kubwa kuliko wa wakina Julius na John kwa sababu tu ni waislamu.

Ninakataa kuwa mchango wao haukupewa uzito uliostahili kwa sababu ya dini yao kwa sababu mchango wa wakristu wengi tu kama wakina Vedastus Kyaruzi, Dennis Phombeah, John mwakangale, John Rupia, Mwanjisi na wengine wengi tu nao haujapewa heshima inayostahili. Nyerere pamoja na kuwa mkatoliki lakini aliwatia kizuizini wakristu wengi na kuwafungulia wengi kesi za uhaini. Kumgeuza mdini ni kutomtendea haki. Nyerere ana mengi ya kukoselewa lakini sio kwenye masuala ya ubaguzi hasa wa dini.

Amandla...

Nguruvi3 JokaKuu Mag3
Fundi...
Ahsante sana.
Umeandika mengi.

Mimi sina haja ya kurejea na kusahihisha hayo uliyosema kwani nimeandika kitabu kizima kuhusu historia hii.

Ikiwa kuna atakae kujua ukweli na asome: "The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika," Minerva Press, London 1998.

Hao akina Denis Phombeah wote walifutwa kitabu cha Abdul Sykes ndicho kwa mara ya kwanza kikaeleza mchango wao.

Leo wewe unataka kunisomesha mimi historia ya Dr. Vedasto Kyaruzi olhali mie ndiye niliyemrejesha kundini?
 
Fundi...
Ahsante sana.
Umeandika mengi.

Mimi sina haja ya kurejea na kusahihisha hayo uliyosema kwani nimeandika kitabu kizima kuhusu historia hii.

Ikiwa kuna atakae kujua ukweli na asome: "The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika," Minerva Press, London 1998.

Hao akina Denis Phombeah wote walifutwa kitabu cha Abdul Sykes ndicho kwa mara ya kwanza kikaeleza mchango wao.

Leo wewe unataka kunisomesha mimi historia ya Dr. Vedasto Kyaruzi olhali mie ndiye niliyemrejesha kundini?
Mimi sina haja ya kukusomesha kwa sababu najua kuwa unaamini wewe ndio alpha na omega kwenye suala la uhuru wa Tanganyika.

Nimekutolea mfano wa wakina Vedasto Kyaruzi na Dennis Phombeah kukuonyesha kuwa sio wakina Sykes na ndugu zako peke yao ambao hawakukumbukwa na wale waliokuwa wakiandika historia za ukombozi wa Tanganyika. Kama na wewe ulikuwa unajua kuhusu mchango wao mkubwa basi ni dhahiri unatumia kile unachokiita kuto tendewa haki wakina Sykes kwa kuwa walikuwa waislamu kujenga chuki baina ya dini hizi kwa maksudi tuu kwa sababu wakina Kyaruzi walikuwa wakristu.

Chuki hii ndio inayonifanya niangalie kwa umakini sana kila unachobandika kwa sababu lengo lako nalijua.

Amandla...

Nguruvi3
 
Mimi sina haja ya kukusomesha kwa sababu najua kuwa unaamini wewe ndio alpha na omega kwenye suala la uhuru wa Tanganyika.

Nimekutolea mfano wa wakina Vedasto Kyaruzi na Dennis Phombeah kukuonyesha kuwa sio wakina Sykes na ndugu zako peke yao ambao hawakukumbukwa na wale waliokuwa wakiandika historia za ukombozi wa Tanganyika. Kama na wewe ulikuwa unajua kuhusu mchango wao mkubwa basi ni dhahiri unatumia kile unachokiita kuto tendewa haki wakina Sykes kwa kuwa walikuwa waislamu kujenga chuki baina ya dini hizi kwa maksudi tuu kwa sababu wakina Kyaruzi walikuwa wakristu.

Chuki hii ndio inayonifanya niangalie kwa umakini sana kila unachobandika kwa sababu lengo lako nalijua.

Amandla...

Nguruvi3
Fundi...
Mimi si ninaeamini kuwa ni mjuzi wa historia ya uhuru wa Tanganyika.

Ni kweli kuwa elimu hii nimejaaliwa mimi nchi nzima na kama ikiwa wewe huamini mlete mtu yeyote anaeijua historia hii kunishinda.

Nakusihi usichukue maneno yangu haya kama majigambo chukulia kuwa nimeijua historia hii kwanza kwa kuwa chama cha African Association kiliasisiwa na babu zangu mwaka wa 1929.

Naweza nikakutajia wote majina yao: Cecil Matola (President), Kleist Sykes (Secretary), Mzee bin Sudi, Ali Said Mpima, Zibe Kidasi, Suleiman Majisu, Rawson Watts na Raikes Kusi.

Pili mimi ndiye mtafiti pekee nchi hii niliyefunguliwa nyaraka za Sykes nizikague na kuzisoma kwa minajili ya kuijua historia y AA, TAA na TANU.

Kutokana na nyaraka hizi nikaandika kitabu note naamini mnakijua.
Kuwa nina chuki hili unasema wewe.

Lakini waliosoma kitabu changu hakuna aliyepata kusema kina chuki.

Wanachosema ni kuwa hakika historia iliyokuwa imetamalaki si historia ya kweli ya kupigania uhuru wa Tanganyika.

Sasa yote niliyopata kuandika sijaandika kwa nia ya kujenga chuki katika jamii bali nia ni kueleza ukweli viongozi wetu wajue na warekebishe pale penye dhulma.
 
Fundi...
Upendo gani huu wa kuivunja EAMWS kuzuia Waislam wasijenge Chuo Kikuu 1968?

Upendo gani huu serikali kukataa OIC wasijenge Chuo Kikuu Tanzania miaka ya 1970?

Upendo gani huu Wizara ya Elimu kuhodhiwa na kuwekwa mkakati wa kuzuia Waislam wasipate elimu ya juu?

Upendo gani huu NECTA kuhodhiwa na kuhujumu shule za Waislam?

Au haya huyajui?
Hivi ndiyo kuishi kwa upendo?

Imefikiwa hadi kufuta historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika kuwakwepa Waislam.

Nikairejesha historia hii kupitia kitabu cha Abdul Sykes.

Haya tunayazungumza hapa huu sasa mwaka wa 10.

Yapo mengi ikiwa utapenda nitayaweka hapa kwa ushahidi tujadiliane.

Uko tayari?

Muda ni mwalimu mzuri. Hapa sasa nia ya hili bandiko ni geresha tu bali kuna mengi yapo kifuani kwako na hapa ndio unapumulia.

Haya masuala ya EAMWS tulishayajadili miaka na miaka kwa hapa hakuna jipya yote tulishayajadili haya unayaleta kama marudio hapa hakuna jipya.

Swala la OIC na ujenzi wa chuo hii ngonjera iliimbwa hapa miaka na miaka wala hakuna jipya na kiwanja cha chuo mkaamua kwa utashi wenu kumuuzia kanjibah.

Wizara ya elimu ilihodhiwa vipi, tupe huo mkakati na ushahidi wa kuzuia waislam wasipate elimu ya juu ingali wewe umeipata tena UDSM na sio wewe tu bali maelfu ya waislam nchini.

Necta ipi iliyohodhiwa na shule zipi zilizohujumiwa hizo, pamoja na kelele zako hukusoma shule za kiislam bali za kanisa takatifu katoliki la mitume wa kweli. Ningependa kutajiwa shule zilizohujumiwa na zimehujumiwa vipi hizo muslim school?. Hata mtume ashuke leo hii kamwe upande wa shule na ufaulu waislam hamtakaa muwashinde watoto wa missionary na shule zao.

Kwani hapa si suala la sheikh kuhusu bandari au ni suala la historia ya baba yako mzazi abdul Sykes, zaidi kwamba nilitegemea mjadala ujikite kwene suala la bandari, haya masuala ya historia za miaka 60 nyuma hapa hayana nguvu, inshu hapa ni bandari.
 
TAMKO LA SHEIKH WA MKOA MWANZA KUHUSU MJADALA WA BANDARI

Utangulizi

Kwa kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja kumekuwa na mjadala kuhusu uwekezaji na uendeshaji wa bandari zetu na kampuni kutoka Dubai. Mjadala ulianzishwa na wanasiasa na wanasheria lakini baadae ukachukua sura mpya na ya hatari ambayo nchi yetu haijawahi kushuhudia.

Hoja na mwelekeo wake

Wakati mjadala ulipoanza, hoja kubwa ilikuwa Wazanzibari wawili wanauza bandari za Tanganyika. Baada ya muda si mrefu, mjadala ukachukua sura mpya na kusisitizwa kuwa ni waarabu ndio waliouziwa nchi. Wakati mjadala unaendelea, ulihama kutoka sura ya kisiasa na kuingia udini.

Sote tumeshuhudia viongozi mbalimbali waandamizi wa dini ya kikristo walivyokuwa mstari wa mbele kupinga suala hili na wengine wamediriki kumkejeli Rais Samia Suluhu Hassan. Hii sio mara ya kwanza kwa viongozi wa dini ya kikristo kumkejeli Rais Samia.

Baadhi ya viongozi wa dini ya kikristo wamedai kuwa Rais Samia amevunja Katiba na kwa maana hiyo anastahili kuondolewa madarakani. Mmoja wao ameenda mbali zaidi kwa kutishia kufanyike Mapinduzi ya kumuondoa Rais Samia madarakani. Jambo la ajabu ni kuwa mpaka sasa hakuna hata mtu mmoja ambaye ameupinga mkataba wa bandari kwa hoja za kiuchumi.

Wote waliozungumza na hasa viongozi wa dini ya kikristo wamezungumza kwa jazba na kumshambulia Rais Samia bila sababu za msingi. Kama viongozi hawa wana uchungu na wananchi, tuliwatarajia kupaza sauti zao wakati wa utawala uliopita ambao tumeshuhudia watu wengi kupoteza maisha yao bila maelezo. Pia tumeshuhudia serikali iliyopita imeingia kwenye miradi mikubwa kinyume cha utaratibu. Sote ni mashahidi, hakuna kiongozi hata mmoja wa kiislamu aliyeushambulia uongozi uliopita.

Wito

Mimi ninaamini kuwa mjadala huu umetawaliwa na UDINI na una lengo la kumtoa Rais Samia madarakani kabla ya muda wake. Hivyo basi, kama sheikh wenu wa Mkoa, natoa wito kwa kila mwislam popote alipo katika Mkoa huu, afunge kwa siku 3 na katika kila swala ya Ijumaa kuanzia Ijumaa hii ya tarehe 7 Julai 2023 misikiti YOTE 700 ya Mkoa wa Mwanza isome dua ya kunuti kuwalaani WATU WOTE wenye nia ovu na Rais Samia.

Sheikh Hassan Kabeke ………………………………..

Sheikh wa Mkoa, MWANZA

Tarehe 6 Julai 2023
 

Attachments

  • 4EA9E5D4-D0CF-4AE9-B7B2-534E0F8C82CA.jpeg
    4EA9E5D4-D0CF-4AE9-B7B2-534E0F8C82CA.jpeg
    33.9 KB · Views: 3
  • 5960B255-48A6-458B-ACEB-3A6ABC3F2484.jpeg
    5960B255-48A6-458B-ACEB-3A6ABC3F2484.jpeg
    61.2 KB · Views: 5
Kama ni kweli huyo sheikh ameongea hivyo kwa baraka za kuwakilisha waislam wa mkoa wa mwanza, nachelea kusema asilimia kubwa ya waislam ni bogus kabisa. Naomba isiwe kweli bali amelishwa tuu maneno.
 
Muda ni mwalimu mzuri. Hapa sasa nia ya hili bandiko ni geresha tu bali kuna mengi yapo kifuani kwako na hapa ndio unapumulia.

Haya masuala ya EAMWS tulishayajadili miaka na miaka kwa hapa hakuna jipya yote tulishayajadili haya unayaleta kama marudio hapa hakuna jipya.

Swala la OIC na ujenzi wa chuo hii ngonjera iliimbwa hapa miaka na miaka wala hakuna jipya na kiwanja cha chuo mkaamua kwa utashi wenu kumuuzia kanjibah.

Wizara ya elimu ilihodhiwa vipi, tupe huo mkakati na ushahidi wa kuzuia waislam wasipate elimu ya juu ingali wewe umeipata tena UDSM na sio wewe tu bali maelfu ya waislam nchini.

Necta ipi iliyohodhiwa na shule zipi zilizohujumiwa hizo, pamoja na kelele zako hukusoma shule za kiislam bali za kanisa takatifu katoliki la mitume wa kweli. Ningependa kutajiwa shule zilizohujumiwa na zimehujumiwa vipi hizo muslim school?. Hata mtume ashuke leo hii kamwe upande wa shule na ufaulu waislam hamtakaa muwashinde watoto wa missionary na shule zao.

Kwani hapa si suala la sheikh kuhusu bandari au ni suala la historia ya baba yako mzazi abdul Sykes, zaidi kwamba nilitegemea mjadala ujikite kwene suala la bandari, haya masuala ya historia za miaka 60 nyuma hapa hayana nguvu, inshu hapa ni bandari.
Haya maswali magumu sana sidhani kama atakujibu. Sidhani kama bila hicho chama walichoasisi babu zake Tanganyika isingepata uhuru.
 
Back
Top Bottom