Sheria 13 za mpira wakati tukiwa watoto

Ukisafa mpk mwisho ujue umelala nacho na wimbo unaimbiwa.
 
Hapo kwenye Mdako umenikumbusha mbali.

Mie mwenyewe nilikuwa najichanganya kwenye Mdako.

Tunachora Duara Kibarazani na Chaki ya kokoto.

Kokoto zinakuwa kumi na mbili (12), na Ndimu inakuwa inarushwa juu na kuidaka huku ukizitoa kokoto nje ya Dimba na kuziingiza.

Nakumbuka, unatoa kwa kiganja kimoja zote kumi na mbili (12) kwanza nje ya Dimba, huku Ndimu ikiwa hewani kisha unarudisha ndani kumi na moja (11). Moja unaishika na mkono mwingine ambao haurushi Ndimu.

Kisha na unatoa tena nje ya Dimba kumi na moja (11), unarudisha ndani kumi (10) huku Ndimu ikiwa hewani. Nyingine unaishika na mkono mwingine ambao haurushi Ndimu. Jumla hapo zinakuwa mbili nje.

Unaendelea, unatoa tena nje ya Dimba kumi (10), unarudisha ndani tisa (9) huku Ndimu ikiwa hewani. Jumla hapo zinakuwa tatu nje.

Unaendelea na zoezi hilo mpaka unamaliza zote kumi na mbili (12). Kisha unaziingiza ndani zote kumi na mbili (12) na kuzitoa tena nje zote kumi na mbili (12) kwa mkupuo.

Mimi HARUFU natisha sana kwa Mdako, nna hakika hata sasa hivi ukiomba Mechi na mie lazima nikugalagaze.

Jamani
 
Vingne;
Faulo ya kwanza haikingwi

Faulo ya pili inakingwa na ukingwaji wake sasa mpira unakaa katikati ya miguu ya mkingaji

Kujifunga vitambaa,kamba kichwani ili uonekane noma..

Mkiwa wengi mnagawa timu zinakua tatu atakae fungwa anatoka..

Wengne tulikua na wazazi wakali ukitoka kucheza umepauka miguu unajipaka mate ili uonekane hujachafuka

Mara nyingi mechi ilkua inaanza saa kumi

Mchezaji mkubwa kuliko wote mara nyingi alkua anadaka

Lakini watoto wa siku hizi wamekalia singeli
 
Hyo kwetu inaitwa toka ingia hapo kama marafiki na mnapenda mcheze timu moja mnatafta mtu mnamuweka katikati yenu
 
Reactions: Lee
Mimi hata REDE nilikuwa najichanganya pia.

Wanachukua Soksi wanazifiringisha inakuwa kama Kajimpira, wawili kazi yao kurushiana Kajimpira kumlenga aliekuwa kati.

Aliekuwa kati kazi yake kukwepa.

Mara utasikia "HARUFU nimekubabua" najibu, jamani hamjanibabua. Wanaendelea tena "HARUFU mlalamishi umebabuliwa toka nje" mimi naendelea kukomaa, jamani hamjanibabua, Vilimbwende vinaanza kusema "HARUFU hii mara ya mwisho ukibabuliwa unatoka" nawaambia sawa.

Mchezo unaendelea, mara tena "HARUFU umebabuliwa", nakomaa tena, jamani hamjanibabua , Vilimbwende vinaanza kelele kwa pamoja "hatutaki, HARUFU toka, wewe Mzurumishi" wanapiga kelele mpaka nakuwa matawi ya chini, inabidi nitoke niwapishe wengine.

Utoto raha sana.

Jamani
 
Kuna watu ambao ilikuwa ukipigana nao Bambi lazima mguu uvimbe.
Nakumbuka nilijikata Mguuni (Nyayoni), na kwa jinsi nlivyokuwa naupenda Mpira nilikuwa nakosa raha sana.

Sikudanganyi, mpaka MAZA aligundua kuna kitu nakikosa, sababu anajua fika mimi napenda sana Mpira wa Miguu. Ikafika mpaka kunipeleka sehemu tofauti tofauti zenye starehe za Watoto, mara kwa mara, mtu mbili tu mimi na yeye, lakini mimi amani haikuwemo kabisa. Nawaza kupona ili niendelee na Mpira.

Kisa cha kuumia.

Tulikuwa kwenye Mechi za Kitoto, Mpira ukatoka ukaangukia Jalalani. Mimi si ndio nimeenda kuUkota Mpira ili niurushe, nakwambia balaa,

Pale Jalalani kumbe kulikuwa na kipande cha Chupa iliyovunjika, mimi nilipoenda okota Mpira ili nirushe si ndio kwa bahati mbaya nikakikanyaga kipande cha Chupa, ebwana zilitoka Damu nyingi sana. Na mechi ikaishia hapo hapo ikabidi mimi nipelekwe Hospitali.

Ila huwezi amini Nyayoni hivi sasa sina alama, mkato wa Chupa wote umefutika
 
Wengine wamefurahishwa na huu uzi.Lakn mi nimeumia san.Nimekumbuka maisha ambayo hayatarudi had naingia kaburini
Mkuu usiumie sana,furahia maisha kwa wakati ulio nao coz hata huu wakati ulionao sasa pia utaujutia au utaukumbuka baada ya miaka 10 au 20 ijayo,

Sometimes you will never know the value of a moment until it becomes a memory.
 
Pia nakumbukakulikuwa hakuna idadi maalum ya kubadilisha wachezaji
 
Nakumbuka siku moja nilipewa dakika chache za kucheza halafu nitoke nimpishe mwingine, sasa sinikafunga goli ebwanae nikaambiwa hakuna kutoka mpaka mpira uishe. Hahahaha
 

Vizazi vya science na technologia hawajui haya kabisa, kweli tuliyaenjoy maisha
 
Ambae hajapitia mambo hizi kapitwa sana Sana,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…