Sheria 13 za mpira wakati tukiwa watoto

Sheria 13 za mpira wakati tukiwa watoto

Nimekumbuka mbali sana kipindi hicho tupo kota...kuna jamaa ailikua ana mashuti na vyenga vingi, kuna siku ukatengenezwa mpira wa makaratasi ukawekwa jiwe ndani, sasa ile giza linaingia anatakiwa apige penati tukambadilishia mpira ...duh siji kusahau jamaa alikua na kigugumizi ila siku hiyo ailiongea vizuri kabisa kwa maumivu na vichapo vilianza.
Mimi sikua mchezaji mzuri lakini ilikua lazima nicheze, wasiponipanga mpira ukitoka nje nikiuokota speed yake watanikuta nyumbani na ndio mwisho wa mpira...Tv hamna kipindi hicho
Daaah mkuu umenikumbusha mbali sana, me mwenyewe nimeshawahi wekewa jiwe daah acha tu maumivu yake usiombe
 
SHERIA 15 ZA MPIRA ZA KIPINDI CHA UTOTONI
1. Mkubwa Hachezi Na Akicheza Mnaingia Wawili.
2.Mwenye Mpira Hatolewi Hata Akicheza Vibaya.
3.Inaruhusiwa Kubadili Kipa Kama Penati Imetokea Na Baada Ya Penati Anaruhusiwa Kurudi Wa Mwanzo.
4.Yule Mtaalam Wa Soka Hakosi Namba Hata Siku Moja.
5. Dogo Mnene Lazima Awe Golikipa.
6.Mwenye Mpira Ataamua Nani Asicheze.
7.Penati Itatokea Tu Pale Mchezaji Akiumia Sana Na Kutoka Damu.
8.Mechi Itaisha Kama Kila Mchezaji Atakuwa Amechoka.
9. Hakuna Free Kick,refa Wala Offside.
10. Ukichaguliwa Mwishoni Ujue Uwezo Wako Mdogo Kuliko Wote Uwanjani.
11.Mtaalam Wa Timu Akipewa Kazi Na Wazazi Wake Lazima Mumsaidie Ndo Mwende Kucheza.
12.Ukiumia Kidonda Kinawekwa Mchanga.
13.Kipa Anaruhusiwa Kudaka Popote.
14. Wale Ambao Wamekosa Namba Kazi Yao Ni Kufata Mipira Ikitoka.
15. Mwenye Mpira Akikasirika Mechi Ndo Inakuwa Imeisha
Kanzu na tobo vina hadhi sawa tu na goli
 
Sijui watoto wetu wamepumbazwa na ma-TV? Yaani wanacheza kwa kusuasua sana, wakati enzi zile tulikuwa tunatoka mtaa kwenda kushindana na mtaa mwingine au kijiji kimoja na kingine! Mkitoka suluhu zinapigwa ngumi angalau timu moja ionekane bingwa!!
Kulikuwa hamna bodaboda mkuu
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]no. 13
nilikua nikiona mpira unakuja naingia mpaka kati kati nadaka narudi nao golini[emoji23][emoji23]

team moja lazima mvue mashati ingine wavae ili mjuaje

gombania goli lazima ukifunga unamtoa usiempenda....
halafu kuna goli la upande mmoja mnaliopenda sanaa
mtu akija akiomba namba anacheza haijalishi team ina watu 20 au zaidi
mnajazana tu ilimradi.. [emoji23][emoji23]

mpira mnacheza mchana pekupeku...
uwanja ni popote
mnacheza wasichana , wavulana humo humo

akifika mchezaji bora mjinga mjinga unatolewa... au unakua kipa
ukikataa kutoka wanakwita nyama. hapo mtu yeyote anaruhusiwa kukuchezea rafu.
 
Kipindi hicho Jezi mnatajiwa rangi tu na kila mtu anaenda mtumbani kivyake kununua jezi yake.

Kupaka mafuta ya nguruwe mwilini hili timu pinzani wakiroga uchawi usitupate.

Kwenda kwenye mechi na upupu hili kumuekea mchezaji mkali wa timu pinzani.
 
Mpira wa utotoni raha sana.

Yaani mtu huchoki, hiyo hata kula huoni umuhimu wake.

Hasa siku ya Jumamosi, nakumbuka Muda wa kula ukifika nikisikia naitwa "HARUFU, we HARUFU Chakula tayari" hiyo lazima niende sehemu nikajifiche, Maana tulikuwa na Dada wa Kazi mmoja, Muda wa Chakula ukifika lazima aite kwa makelele kabla ya kufika eneo husika.

Nakumbuka mambo ya kubambikiana, kupiga madochi ukipiga kijiwe, au lami ujue mpaka vidole vinatoka vidonda.

Mara ngumi zinaanza mpirani, ukinitukana ujue lazima tuzichape. Kupigana mpirani ni jambo la kawaida sana.

Magoli madogo, Gombania Goli, Kuchonga Kona, N.K.

Jamani
 
Daaah hii imenikumbusha mbali, enzi hizo kipindi cha dochi
 
mgeni,ambaye kwao kuna tv kisogo,monita/kiranja wa shule,wote hao lazima wapate namba.
mi nilikua nakapenda sana ka mchezo ka "tobo ngumi" namvizia nisiyempenda apigwe tobo hapo ndio atajua makonzi ni nini nilikua naenda kukaba mti ili asiushike aendelee kudundwa tu,
 
Viwanja viko wapi mkuu? Labda kwa vijijini tu lakni mjini watu wamejenga kila sehemu
Viwanja sio issue tulikuwa tunacheza barabaran wakubwa wakipita tunashika mpira kwa kusema "heshima" wakishapita Ngoma inaendelea Na magari yakipita mwendo n huohuo
 
SHERIA 15 ZA MPIRA ZA KIPINDI CHA UTOTONI
1. Mkubwa Hachezi Na Akicheza Mnaingia Wawili.
2.Mwenye Mpira Hatolewi Hata Akicheza Vibaya.
3.Inaruhusiwa Kubadili Kipa Kama Penati Imetokea Na Baada Ya Penati Anaruhusiwa Kurudi Wa Mwanzo.
4.Yule Mtaalam Wa Soka Hakosi Namba Hata Siku Moja.
5. Dogo Mnene Lazima Awe Golikipa.
6.Mwenye Mpira Ataamua Nani Asicheze.
7.Penati Itatokea Tu Pale Mchezaji Akiumia Sana Na Kutoka Damu.
8.Mechi Itaisha Kama Kila Mchezaji Atakuwa Amechoka.
9. Hakuna Free Kick,,refa Wala Offside.
10. Ukichaguliwa Mwishoni Ujue Uwezo Wako Mdogo Kuliko Wote Uwanjani.
11.Mtaalam Wa Timu Akipewa Kazi Na Wazazi Wake Lazima Mumsaidie Ndo Mwende Kucheza.
12.Ukiumia Kidonda Kinawekwa Mchanga.
13.Kipa Anaruhusiwa Kudaka Popote.
14. Wale Ambao Wamekosa Namba Kazi Yao Ni Kufata Mipira Ikitoka.
15. Mwenye Mpira Akikasirika Mechi Ndo Inakuwa Imeisha
Liseman anatumia shati la mmoja wenu kama kibendera!!!
 
Viwanja sio issue tulikuwa tunacheza barabaran wakubwa wakipita tunashika mpira kwa kusema "heshima" wakishapita Ngoma inaendelea Na magari yakipita mwendo n huohuo
Wamachinga wameziacha hizo bara bara pia population imekuwa kubwa mno
 
Hahahah! ! Si ruhusa kucheza na viatu kama wenzako wako peku
 
Nyie watu munenichekesha sana . Yaani nimecheka hadi mbavu zng zinauma!!!
 
Ubabe ulikuwa unakuja kama goli halina kamba kwa juu halafu mpira upite sehemu yenye utata kama ni goli au mpira umepita juu!
Hapo timu yenye wababe na waongeaji sana ndo wanaamua!
 
Ubabe ulikuwa unakuja kama goli halina kamba kwa juu halafu mpira upite sehemu yenye utata kama ni goli au mpira umepita juu!
Hapo timu yenye wababe na waongeaji sana ndo wanaamua!
Au magoli ya kuweka Mawe.

Jiwe moja kulia, jiwe moja kushoto.

Yale ndio hayafahai kabisa.

Ulalamishi unakuwa mwingi sana pale Mpira upite juu kidogo ya jiwe.

Hapo ndio mtaanza, wengine wanasema "Goli", wengine wanasema "sio Goli".

Ukifanya mchezo, kama ni Mechi inaweza kuishia hapo.

Nakumbuka haya Magoli ya Mawe, anaepima anaweka jiwe moja kwanza, kisha anaanza kupiga hatua zake mpaka atakapotaka yeye kuwekwa jiwe la pili. Na hapa napo kunakuwaga na Ulalamishi wake, ambao:-

Wengine watasema Goli kubwa lipunguzwe, wengine watasema liachwe hivyohivyo.

Maisha haya, tunatoka mbali sana
 
Dana dana kuhesabihana, iwe ya mguu mmoja au iwe ya miguu miwili.

Kontroo, Vichwa, Tobo bao.

Mtu kati (unasafa), hapa zipo za aina mbili. Kuna ile moja ukigusa tu Mpira kwa yule aliekuwa nao, ujue hapo umejikomboa na yeye inakuwa zamu yake kusafa.

Na kuna ile nyingine lazima unyang'anye Mpira ndio ujikomboe na yule uliemnyang'anya inakuwa zamu yake kusafa.

Hapa kwenye kusafa panakuwaga patamu, pale inapotokea mmoja wenu kusafa kwa muda mrefu, mpaka anaesafa anakasirika.

Kabla ya kuanza napenda zaidi pale mnapoanza kuweka uamuzi kusafa kwa aina gani, Kugusa au kunyang'anya.

Maisha haya.

Eti sasa hivi na mie HARUFU naitwa Baba.

Jamani
 
Back
Top Bottom