Sheria 13 za mpira wakati tukiwa watoto

Sheria 13 za mpira wakati tukiwa watoto

Mwenye mpira ana mamlaka kumtoa anaepiga sana mashuti
Kuna wale walikuwa na mtindo wa kukanyaga mpira mpaka duara linapotea, dah nilikuaga nabeba mpira wangu kwa leo au kama bado mapema basi jamaa anaambiwa atoke
 
SHERIA 15 ZA MPIRA ZA KIPINDI CHA UTOTONI
1. Mkubwa Hachezi Na Akicheza Mnaingia Wawili.
2.Mwenye Mpira Hatolewi Hata Akicheza Vibaya.
3.Inaruhusiwa Kubadili Kipa Kama Penati Imetokea Na Baada Ya Penati Anaruhusiwa Kurudi Wa Mwanzo.
4.Yule Mtaalam Wa Soka Hakosi Namba Hata Siku Moja.
5. Dogo Mnene Lazima Awe Golikipa.
6.Mwenye Mpira Ataamua Nani Asicheze.
7.Penati Itatokea Tu Pale Mchezaji Akiumia Sana Na Kutoka Damu.
8.Mechi Itaisha Kama Kila Mchezaji Atakuwa Amechoka.
9. Hakuna Free Kick,refa Wala Offside.
10. Ukichaguliwa Mwishoni Ujue Uwezo Wako Mdogo Kuliko Wote Uwanjani.
11.Mtaalam Wa Timu Akipewa Kazi Na Wazazi Wake Lazima Mumsaidie Ndo Mwende Kucheza.
12.Ukiumia Kidonda Kinawekwa Mchanga.
13.Kipa Anaruhusiwa Kudaka Popote.
14. Wale Ambao Wamekosa Namba Kazi Yao Ni Kufata Mipira Ikitoka.
15. Mwenye Mpira Akikasirika Mechi Ndo Inakuwa Imeisha
Kichwa cha mwendawazimu kilianzia hapo.
 
Mmenikumbusha ule mpira unaoitwa nyuzi mbanano ulikuwa unauzwa pale kinondoni mosko tsh 500 tu!
nyuzi mbanano.jpeg
 
Hapo umenena kweli mkuu,, kwa iyo suluhisho watoto wameona wajikalie nyumbani tu kuangalia TV. Hii ni changamoto kwa serikali yetu, inatakiwa hili ilifanyie kazi ili watoto wapate muda wa kucheza.
Tulicheza hata barabarani
 
Hapo umenena kweli mkuu,, kwa iyo suluhisho watoto wameona wajikalie nyumbani tu kuangalia TV. Hii ni changamoto kwa serikali yetu, inatakiwa hili ilifanyie kazi ili watoto wapate muda wa kucheza.
Kabisaaa lkn sio rahisi kutatua hili
 
Sisi tulikuwa na sheria chache.
1.faulo pekee hata penati ni kushika
2.mpira ukitoka anaewahi ndio anarusha
3.hamna kona
4.hamna half time
5.giza ndio linaamua mpira uishe
6.mwenye mpira lazima acheze
7.mnyonge ndio kipa
8.hamna jezi,mwendo ni kuvaa au kuvua shati
9.hamna kucheza na viatu
10.anaejua yaani fundi lazima acheze mara nyingi huwa wanaringa sana
Kuna wakati sisi kukiwa na mbalamwezi tulikuwa tuna cheza usiku, hapo sio kung'oana kucha sasa!!!! Kurubasi zilikuwa zinaruhusiwa kuvaliwa
 
Mwenye mpira ana haki ya kucheza na viatu wengine wote peku peku labda rafiki zake wa karibu ambao wako upande wake. Anayefunga magoli dhidi ya timu ya mwenye mpira mwenye mpira anaweza kuamua kumtoa nje ili kuipa nafasi timu yake ishinde.

SHERIA 15 ZA MPIRA ZA KIPINDI CHA UTOTONI
1. Mkubwa Hachezi Na Akicheza Mnaingia Wawili.
2.Mwenye Mpira Hatolewi Hata Akicheza Vibaya.
3.Inaruhusiwa Kubadili Kipa Kama Penati Imetokea Na Baada Ya Penati Anaruhusiwa Kurudi Wa Mwanzo.
4.Yule Mtaalam Wa Soka Hakosi Namba Hata Siku Moja.
5. Dogo Mnene Lazima Awe Golikipa.
6.Mwenye Mpira Ataamua Nani Asicheze.
7.Penati Itatokea Tu Pale Mchezaji Akiumia Sana Na Kutoka Damu.
8.Mechi Itaisha Kama Kila Mchezaji Atakuwa Amechoka.
9. Hakuna Free Kick,refa Wala Offside.
10. Ukichaguliwa Mwishoni Ujue Uwezo Wako Mdogo Kuliko Wote Uwanjani.
11.Mtaalam Wa Timu Akipewa Kazi Na Wazazi Wake Lazima Mumsaidie Ndo Mwende Kucheza.
12.Ukiumia Kidonda Kinawekwa Mchanga.
13.Kipa Anaruhusiwa Kudaka Popote.
14. Wale Ambao Wamekosa Namba Kazi Yao Ni Kufata Mipira Ikitoka.
15. Mwenye Mpira Akikasirika Mechi Ndo Inakuwa Imeisha
 
Sijui watoto wetu wamepumbazwa na ma-TV? Yaani wanacheza kwa kusuasua sana, wakati enzi zile tulikuwa tunatoka mtaa kwenda kushindana na mtaa mwingine au kijiji kimoja na kingine! Mkitoka suluhu zinapigwa ngumi angalau timu moja ionekane bingwa!!
Ukweli ni kwamba watoto wa kizazi hiki... hawafahidi kitu kabisa... utoto wetu ulikuwa raha sana... mitoto ya sasa hiv..bkutwa tv.. simu
 
Ha ha ha haaaaaaa, mkuu kweli we kijana wa zamani
 
HAUKUNA KUCHEZA NA VIATU MANA UTAUMIZA WENGINE.....
KILA MCHEZAJI NI KOCHA.....
HAKUNA IDADI YA WACHEZAJI HATA WATATU MNAUNDA TIMU...
HAKUNA MAPUMZIKO...
TIMU A WATAVUA MASHAT TIM B WATABAK NA MASHAT..
Mbambe hanyimwi no.
Hakuna no maalum beki a naweza kuwa mshambuliaji
 
Back
Top Bottom