Sheria 13 za mpira wakati tukiwa watoto

Sheria 13 za mpira wakati tukiwa watoto

Mwenye mpira ndo mwenye mamlaka nan acheze nan asicheze, na kama darasan una akili kumzidi mwenye mpira na akikuletea swali umsaidie unakataa, basi wee jua kupata namba ni shughul au haugusi mpira kabisa
 
Daah mmenikumbusha mbali nakumbuka enzi Hizo namaliza mtihani wa mwisho wa la 7 tulichanga mchango kwa ajili ya kununua mpira ambao ulitumika kuchezea siku tumeshafanya mtihani wa mwisho ikiwa ni lengo la kuagana,sa tumecheza ngoma dk 90 watu hawakuridhika zikaongezwa 45 zingine mpaka watu kukimbia ikawa hawawezi ikabidi uishie hapo sa kivumbi nani wa kuchukua mpira aondoke nao mana kila mtu ana haki nayo na kachangia ukatokea mzozo ikabidi tufike muafaka utafutwe wembe mpira uchanwe kila mtu aondoke na kipande ndo jamaa wakaridhika...
Soka la utotoni mwenye mpira anaweza kukunasa vibao kisa huchezi vizuri au umekosea na ukiwa mbishi anaruhusiwa kukutoa
 
umenikumbusha doba ngumii yan ukipigwa doba watu wote wanakupiga ngumi adi ufiikie mti wa kushika umeiva
 
Faulo inakabwa.Ikiwainapigwa faulo mtu mmoja nakaa mbele ya mpira kuzuia faulo hakuna kupiga hatua
 
4. Kama timu yetu hatuna viatu, na ninyi vueni viatu
5. Hakuna refa, uamuzi wa mchezo mf. faulo au kona ni makubaliano
6.Giza likianza kuingia faulo zinaruhusiwa
7.Mtu akiumia akatoka damu na mchezo huishia hapo hapo
 
Ni mara chache sana penati kutolewa labda mchezaji aumie na dam itoke na hapo itapigwa penati bla kujar ilipo tokea hata kama ni Gorin kwa mchezewa mara nyingi hutolewa kama zawadi kwA muathrka na yy ndo huchagua mpigaji wakati yy anaendelea kunyamazishwa
 
1. Mpira unaisha giza likizidi.

2. Wenyeji wanavaa shati wageni vifua wazi.

3. Rafu zikizidi ngumi zinafuatia, mpira unakua umekwisha.
 
Sheria 15 za mpira za kipindi cha utotoni;

1. Mkubwa hachezi na akicheza mnaingia wawili.

2.Mwenye mpira hatolewi hata akicheza vibaya.

3.Inaruhusiwa kubadili kipa kama penati imetokea na baada ya penati. anaruhusiwa kurudi wa mwanzo.

4.Yule mtaalam wa soka hakosi namba hata siku moja.

5. Dogo mnene lazima awe golikipa.

6.Mwenye mpira ataamua nani asicheze.

7.Penati itatokea tu pale mchezaji akiumia sana na kutoka damu.

8.Mechi itaisha kama kila mchezaji atakuwa amechoka.

9. Hakuna free kick, refa wala offside.

10. Ukichaguliwa mwishoni ujue uwezo wako mdogo kuliko wote uwanjani.

11.Mtaalam wa timu akipewa kazi na wazazi wake lazima mumsaidie ndo mwende kucheza.

12.Ukiumia kidonda kinawekwa mchanga.

13.Kipa anaruhusiwa kudaka popote.

14. Wale ambao wamekosa namba kazi yao ni kufata mipira ikitoka.

15. Mwenye mpira akikasirika mechi ndo inakuwa imeisha.
 
Haaaaaaaahaah... [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kuna moja ya Kipa na Ndani,haaahaaaa raha sana.Siku hizi watoto hawachezi kabisa
Sijui watoto wetu wamepumbazwa na ma-TV? Yaani wanacheza kwa kusuasua sana, wakati enzi zile tulikuwa tunatoka mtaa kwenda kushindana na mtaa mwingine au kijiji kimoja na kingine! Mkitoka suluhu zinapigwa ngumi angalau timu moja ionekane bingwa!!
 
SHERIA 15 ZA MPIRA ZA KIPINDI CHA UTOTONI
1. Mkubwa Hachezi Na Akicheza Mnaingia Wawili.
2.Mwenye Mpira Hatolewi Hata Akicheza Vibaya.
3.Inaruhusiwa Kubadili Kipa Kama Penati Imetokea Na Baada Ya Penati Anaruhusiwa Kurudi Wa Mwanzo.
4.Yule Mtaalam Wa Soka Hakosi Namba Hata Siku Moja.
5. Dogo Mnene Lazima Awe Golikipa.
6.Mwenye Mpira Ataamua Nani Asicheze.
7.Penati Itatokea Tu Pale Mchezaji Akiumia Sana Na Kutoka Damu.
8.Mechi Itaisha Kama Kila Mchezaji Atakuwa Amechoka.
9. Hakuna Free Kick,refa Wala Offside.
10. Ukichaguliwa Mwishoni Ujue Uwezo Wako Mdogo Kuliko Wote Uwanjani.
11.Mtaalam Wa Timu Akipewa Kazi Na Wazazi Wake Lazima Mumsaidie Ndo Mwende Kucheza.
12.Ukiumia Kidonda Kinawekwa Mchanga.
13.Kipa Anaruhusiwa Kudaka Popote.
14. Wale Ambao Wamekosa Namba Kazi Yao Ni Kufata Mipira Ikitoka.
15. Mwenye Mpira Akikasirika Mechi Ndo Inakuwa Imeisha
Kwa hiyo mlikuwa na jeuri ya kunyima namba wenye Tv kwao?
 
Back
Top Bottom