Sheria 13 za mpira wakati tukiwa watoto

Sheria 13 za mpira wakati tukiwa watoto

Nilikuwa Mtaalamu sana wa kufuma mipira ya Makaratasi hata uwe na kucha ndefu za Miguu au kupiga 'dochi' huwezi kuufumua. 1965-1975 Mission Quatre Kariakoo mkimaliza mpira mnafata Bagia Mnazi mmona

Shikamoo anko.
 
Tatizo yale maeneo yote ya wazi wameyafisadi na barabarani hawawezi kucheza magari yamekuwa mengi, enzi zile iliogopwa baiskeli. Ila wababe wa mtaa siku hizi siwasikii kabisa.
Hakuna tena wababe sasa
 
sisi kwetu tulikua na deki ya mikanda mikubwa VHS afu mwenye mpira kwao hamna na hua anakuja kumcheki vandame aisee kila jion nkitoka tuition nikifika nkikuta mechi ipo kati inaendelea akiniona tu lazma mmoja atoke niingie
Ha ha ha
 
Kambi itakuwa kwa mwenye mpira tu,timu nzima anavaa jezi peke yake!
 
goli linaweza kuwa ni mawe au ndala/kandambili. Kama tumeshinda au tupo droo na tunaelekea fungwa ilikuwa ni lazima kulitibua goli, kama ni ndala au viatu utapiga teke moja tu, mfungaji atakosa pa kufungia, kama ni jiwe litarushwa mbali na mechi itakuwa imeisha.

Mpira unaoingia golini hautakiwi vuka juu ya magoti, na ukivuka hapo tu basi hakuna goli, itahesabika umepaisha.
Shule Timu yangu tuliiita new balance sababu wengi tulivaa viatu vya mtumba vilivyoandika new balance.

Kwa home mechi iliisha punde tu sauti ya land rover 109 iliposikika, maana ilikuwa inasikika kona 3 kabla ya kufika home, ushahidi wa magoli ulitibuliwa, kama ni ndala kila mtu alivaa zake, kama ni mawe basi tulitupa mbali, watoto wa majilani walikimbilia kwao, huku tukiomngoja baba kwa nje.
 
sheria ilikuwa timu moja lazima ivue shati, timu hiyo itapatikana kwa njia moja tu, nayo ni kuanza kufungwa.
 
hahahahahaha.,.nimekumbuka mambo kibao,kupunguza goli kama mashambuliz yamezidi,ukitukana tu inapgwa faulo,kama kuna refa ukila red unakaa nje dakika 5 na kuingia,filimbi ni mluzi tu.
kuna jamaa alikataa kutoka,tukamtangazia nyama,alipogusa mpira tu,mpinzan alikuja mbio akaingia na miguu minne,jamaa mguu ukateguka na mpira ukaishia hapo,ilikuwa maeneo ya yombo kilakala kwa mzee chakala.kitambo sana.
 
Aisee umenikumbusha mbali sana.

Kuna siku tulicheza mpira kuanzia saa 2 asbuhi mpaka saa 11 jion,mipira ya manaironi ilikuwa inachanika yanachumwa machungwa mabichi gemu linaendelea.

Usiombe kucheza mpira mvua ya rasharasha inapiga.kama mzazi wa mmoja wenu hajaingilia kati ni mpaka giza litawakuta hapo.

Mwenye kiatu shart avue kwanza.
NOTE.idadi ya wachezaji kila timu inategemea na ukubwa wa uwanja mnaweza kuwa hata 25 kila upande.
 
Wachezaji wenye machacha ni ngumu kupata Namba kwa hofu ya kupasua mpira ama kuharibu mpira!
Magwambara au magaga sio mchezo ni bora ukutane na msasa wa chuma kuliko hiyo miguu kuna jamaa alikuwa nayo unaweza kuweka sent ishirini ikazama bila wasiwasi.
 
bahati mbaya sisi tulikua tunacheza barabarani magari na baiskeli ndo vikwazo ole wako upige mpira umgonge mpita njia
mara nyingi tulikua tunacheza doba ngumi yani ukiipigwa doba utapata ngumi za kutosha mpaka ukaushike mti
 
goli linaweza kuwa ni mawe au ndala/kandambili. Kama tumeshinda au tupo droo na tunaelekea fungwa ilikuwa ni lazima kulitibua goli, kama ni ndala au viatu utapiga teke moja tu, mfungaji atakosa pa kufungia, kama ni jiwe litarushwa mbali na mechi itakuwa imeisha.

Mpira unaoingia golini hautakiwi vuka juu ya magoti, na ukivuka hapo tu basi hakuna goli, itahesabika umepaisha.
Shule Timu yangu tuliiita new balance sababu wengi tulivaa viatu vya mtumba vilivyoandika new balance.

Kwa home mechi iliisha punde tu sauti ya land rover 109 iliposikika, maana ilikuwa inasikika kona 3 kabla ya kufika home, ushahidi wa magoli ulitibuliwa, kama ni ndala kila mtu alivaa zake, kama ni mawe basi tulitupa mbali, watoto wa majilani walikimbilia kwao, huku tukiomngoja baba kwa nje.
Haaaahaaaa mlitsha sana aisee kama mtaani kwetu yaan,
 
hahahahahaha.,.nimekumbuka mambo kibao,kupunguza goli kama mashambuliz yamezidi,ukitukana tu inapgwa faulo,kama kuna refa ukila red unakaa nje dakika 5 na kuingia,filimbi ni mluzi tu.
kuna jamaa alikataa kutoka,tukamtangazia nyama,alipogusa mpira tu,mpinzan alikuja mbio akaingia na miguu minne,jamaa mguu ukateguka na mpira ukaishia hapo,ilikuwa maeneo ya yombo kilakala kwa mzee chakala.kitambo sana.
Haaaahaaa umenikumbusha mbali sana na hawa watu waliokuwa wanaitwa nyama kiukweli walikuaga wanapata shida sana uwanjani,
 
Back
Top Bottom