Sheria ipi inazuia ukiwa na mkopo wa mshahara NMB (SWL)huwezi kuhamisha mshahara benki nyingine?

Zamani sio siku hizi wanabadili Sheria kila mara leo hivi kesho hivi
Mimi ni mwajiriwa wa umma, masaa machache yaliyopita nilienda kuchukua mzigo bank tofauti na ninayopitishia mshahara na mzigo ukaingia maisha yanaendelea.

Kama hiyo sheria mmeibadili leo sawa sikubishii ila vinginevyo hali iko hivyo.
 
Unahama na mkopo wako.
Huwezi kuwakimbia kuwaachia deni.
Ongea na Bank B hiyo kama wako tayari kulinunua deni lililoko NMB mbona rahisi hiyo
 
Siku acha hata elf 50 humo kwenye akaunti halafu baada ya wiki kaangalie salio
Mkuu kuna hela naacha humo wala sijawahi kuta imepungua,huwa napitisha mishara hata ya miezi mi3 bila kuchukua ,nikiangalia salio liko vile vile tu,kuna shida mahala juu yako
 
We jamaa ni muongo
Kuna makato ya uendeshaji ya mwezi,
Kuna maintenance fee,
Kuna hayo makato ya Mastercard card,
Mi nazungumzia bank ya NMB,
Kama wewe huna hata haya makato basi,
Hutumii nmb,
Au una hela nyingi sana hujui idadi yake
Mkuu kuna hela naacha humo wala sijawahi kuta imepungua,huwa napitisha mishara hata ya miezi mi3 bila kuchukua ,nikiangalia salio liko vile vile tu,kuna shida mahala juu yako
 
Usikope, jitahidi sana usikope, naruria Tena usikope, ukikopa tu, kuwa tayari kutundika nguo ya ndani usiku wakati unalala, Huna Haki yeyote, mkopaji ni mtumwa wa mkopeshaji .
 
Taja kwanza hiyo bank ambayo haina gharama za uendeshaji sijui n.k watu wanaitaka. Ongea na HR inawezekana 100%. Mfano kuna mtu ana mikopo bank 3. Na mambo safi tu.
 
Ni Sheria ya BOT.
Pia ni lazima ukope unapokelea mshahara.
So ukitaka kukopa bank ingine ni lazima uhamishe mshahara kwenye hio bank unayotaka kukopa.
So utafanya kazi ya kuhama bank
Sio kweli mimi nilikuwa na akaunti NMB nikachukua mkopo NMB unapopita mshahara wangu, nikaenda kuchukua kibunda kingine Barclays Bank na Crdb pia.

Kwahiyo hakuna ulazima wa kuhamisha akaunti ya kupokelea mshahara kwenye benki unayokopa kikubwa dhamana yako ni ajira yako/mwajiri wako.
 
Sema kuna aina nyingi za mikataba sasa kwa upande wa mabenki kuna mkataba unaitwa "Standard Form Contract " maana yake ni mkataba ulioandaliwa na upande mmoja ambao ni benki sasa wewe unaenda kusaini tu.

Ulitakiwa uupitie kwa makini mkataba kipengele kwa kipengele ili kama kuna sharti hujakubaliana nalo unamuona meneja mnayajenga.

Inaonekana wewe ulisaini tu bila kupitia vigezo na masharti mkuu.
 
Wanabadilika badilika utaratibu kila mara
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…