Sheria ya Mirathi ya Kiislamu kwa mtoto wa nje ya ndoa ibadilishwe

Sheria ya Mirathi ya Kiislamu kwa mtoto wa nje ya ndoa ibadilishwe

Katika Uislamu kitendo hicho cha zinaa ambacho kimefanywa na mwanaume na mwanamke ndio makosa na waliofanya wanafaa waadhibiwe hapa duniani ili wasafishwe kwa kosa lao hilo hadharani. Na Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala) Ametuagizia Tusikaribie kabisa zinaa (17: 32). Lakini tufahamu ya kwamba yule mtoto anayezaliwa hana hatia yoyote. Allah (Subhaanahu Wa Ta’ala) Anasema:

“Na kila nafsi haichumii ila nafsi yake. Na habebi mwenye kubeba mzigo wa mwenziwe. Kisha marejeo yenu ni kwa Mola wenu Naye Atakuambieni mliyo kuwa mkitofautiana” (6: 164).

Na Mtume (Swalla Allaahu ‘Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam) amesema: ((Kila kinachozaliwa kinazaliwa katika Uislamu .....)) l-Bukhaariy).

Na haifai kwa Muislamu kumuita mtoto aliyezaliwa kwa jina la mwana-haramu kwa sababu mtoto mwenyewe si wa haramu bali kitendo chenyewe ndicho haramu. Na ieleweke kuwa mtoto huyu hataitwa kwa jina la huyu mwanaume aliyezini na mamake kwa sababu kisheria si mtoto wake wala hawa wawili hawarithiani kabisa. Mtoto huyu hatamrithi huyo mwanaume na huyo baba hatamrithi mtoto huyo. Lakini mtoto anaweza kumrithi mama yake na mama kumrithi mtoto wake.

Tanbihi kwa kila mmoja wetu ajichunge sana ili asiingie katika madhambi haya ya zinaa. Na ndio sheria ikafanya ndoa kuwa rahisi na ikaweka adhabu kali kwa wenye kuzini.
Suala hili limeondolewa mushkeri kwa sababu ni moja mtoto wa zinaa kuna kubambikiwa unawez kufikiria ni wao ila kwa kiasi kikubwa sio wako...Leo tunaona hawa wanawake wanaozaa bila ya ndoa wanachanganya watu tena wale ambao mtoto unakuta kafanana na mama.


Mwanamke kama ni mzinifu basi hata mtoto atakudanganya tu , wapo watoto wana kadi za clinic zina majina ya baba tofauti hata watatu. Zinaa ni mbaya sana watoto hawa mara nyingi ni chanzo cha ugomvi ndani ya ndoa ingawa watoto hawana kosa .


Utafiti : Waliozaa nje ya ndoa wengi wanatengenisha watoto wao binafsi na kukosa umoja , juzi tu hapa kifo cha yule mtangaaji clouds yule mwanae mkubwa hana uhusiano mzuri na mdogo wake kisa hawajuani ila wanapendana .
 
Mila nyingi za africa hazitambui mtoto wa zinaa, jamaa kama yupo huru aombe elimu juu ya hilo .
Unaposema mtoto wa zinaa unanikera mzee hakuna Cha mtoto wa zinaa wala nini watoto ni watoto tu
 
MIrathi ya ki-islamu inaongozwa na Quran.
Surat Al Nisa 4: na kuendelea inaongoza na ni muongozo wa "mungu'.
Unataka tu-amend Quran?
Muongo wa Mungu unauhakika kwamba Mungu liwawambia hao wahuni waandike hio qurani au nikikundi kilikaa kikafikilia kuandika sheria zao binafsi tu
 
Wabadishe maandiko alafu wayapeleke wapi kama umeamua kuwa mzinzi we endelea na uzinzi wako waachee na kitabu Chao kisichokuwa na ubabaishaji kitambo kilicho nyooka
 
Unaposema mtoto wa zinaa unanikera mzee hakuna Cha mtoto wa zinaa wala nini watoto ni watoto tu
Mtoto wa zinaa kwa wazazi ila yeye hana kosa wala hafai kuitwa jina baya . Wazazi wameleta mtoto wa zinaa ila mtoto hana kosa
 
Mtoto wa zinaa kwa wazazi ila yeye hana kosa wala hafai kuitwa jina baya . Wazazi wameleta mtoto wa zinaa ila mtoto hana kosa
Endeleeni kufuata dini za kijinga, mm nishajiengua mapema kbs kama dini hainitambui mm et kisa ni haramu ya kazi gani sasa
 
Niende Moja Kwa Moja kwenye mada, enyi waislamu kwanini hamtambui uwepo wa mtoto wa nje ya ndoa wakati wa mirathi?

Eti mtoto wa nje ya ndoa hana haki ya kirithi mali za baba ake mzazi hivi sheria gani hizi ambazo zinamkandamiza mtoto?

Mtoto ni mtoto tu haijalishi ni kambo au wandoa.

Wanasema kwamba mtoto wa kambo ni mali ya mama hii inakuaje aisee?

Sheria hizi zibadilishwe ili kulinda haki ya mtoto katika taifa hili kwasababu inamharibu mtoto kisaikolojia anajiona kama amelaaniwa kuja duniani .
Inaeonekana kama wewe sio muislamu lakini unakerwa tu na sheria zetu za mirathi za kiislamu, dah hatari!. Haya ngoja tukufahamishe kidogo basi.

Kikawaida sheria yoyote huwa inalenga kuminimize tatizo fulani katika jamii, penalty ya kosa siku zote huwa haivutii na ni yenye kutia simanzi moyoni. Kadri jamii inavyolenga kumimize tatizo fulani ndo kadri adhabu ya kosa husika huwa kubwa kutoka katika sheria husika E.g. China wanaua kwa makosa ya madawa ya kulevya na ufisadi, hii adhabu haivutii hata kidogo kuona mtu anauliwa lakini je wangapi watajaribu kufanya kosa alilolifanya yule jamaa tena? it's obvious the problem will be highly minimized in their society.

Sasa unapswa pia uelewe ya kwamba kutotambua mtoto wa nje ya ndoa katika Uislamu ni katika muendelezo wa kupigana vita na uzinifu katika jamii. Katika uislamu uzinifu unatazamwa kama ni kiini cha matatizo mengi katika jamii kuanzia kwenye miamala ya mtu na mtu mpaka mtu na mola wake. Na ndio maana kosa la zinaa lenyewe limewekewa adhabu kali ili lisipatikane katika jamii.

Ila pia inapaswa kueleweka kwamba sheria ya uislamu imemruhusu mtu kuacha wosia wa up to 33.3% ya mali yake kwa wale wasiomrithi kisheria, sasa kama baba anajua alishakosea kwa kuzini, hapaswi kumuacha yule mtoto aliyepatikana kuishi maisha ya tabu kwakuwa huenda ikampelekea adhabu nyengine kwa mola wake so ni busara kumuhudumia kwa kadri ya uwezo wake kama ambavyo angeweza kumuhudumia muhitaji mwengine asiyekuwa huyo, ila tu hana haki ya ubaba juu yake huyo mtoto. Pia, anaweza kumuwekea wosia wa asilimia kadhaa ya mali yake ilimradi isizidi ile iliyoainishwa kisheria.

Huu ni uelewa wangu lakini naamini mwenye changamoto kama hiyo anaweza kupata ufafanuzi zaidi kwa mashekhe na wajuzi wa dini zaidi.
 
walipoweka hizo sheria walijua kabisa kuna namna itapunguza hayo mambo ya mtoto wa nje..... waislamu mnaruhusiwa kuwa na wake wanne iweje uwe na mtoto nje ya ndoa unaonaje huyo mama ukamfanya mke kabla hujafa ili mwanao ahesabiwe kwenye haki ya ulichotafuta au mleta mda umesahau sheria ni 4mukez

alafu mkuu swala la kubadili hizo sheria inabidi utafute jf ya waarabu watuambie inawezekana kubadili mzigo au iko mambo
 
Hio sheria ingekuwa inamtambua mtoto wa nje ya ndoa kungekuwa na ugomvi na mtafaruku mkubwa sana kwenye misiba kwasababu anayeweza kuthibitisha ni mtoto wake ameshatangulia mbele ya haki hvyo watu ingekuwa wanafanya usanii sana kuna watu wangekuja na watoto kwenye bajaji ili tu wapate mali hvyo naona ipo sahihi ili kuepusha malumbano.
Kwakuongeze:
Je tunapaswa kusubiri mda gani baada ya kumzika baba ili kuwasubiri watoto wa nje ya ndoa? Maana Yeye ndie anawajua na alipokuwa akiwatengeneza alikuwa peke yake na haijulikani alizaa na wanawake wangapi!
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] labda uwaombe wadogo zako lakn wewe huna Cha kurithi utamrithi mama yako sio baba

Niwaombe nini?? Sema kwa sababu nipo njema kimaisha ila ingekuwa hivyo pangechimbika as long as mali ni za baba,hata kuroga ningeroga
 
Kamlaumu mama'ko aliyekuwa anaigawa kama pipi ya sadaka.

Siyo urithi tu, hata jina la baba hupewi.

Ona unavyojidhihirisha dini jinsi ilivyo na ubaguzi,so wa kulaumiwa ni mama wa mtoto na sio wote?? Baba yeye hapaswi kulaumiwa?
 
Kamlaumu mama'ko aliyekuwa anaigawa kama pipi ya sadaka.

Siyo urithi tu, hata jina la baba hupewi.

Ona unavyojidhihirisha dini jinsi ilivyo na ubaguzi,so wa kulaumiwa ni mama wa mtoto na sio wote?? Baba yeye hapaswi kulaumiwa?
 
Endeleeni kufuata dini za kijinga, mm nishajiengua mapema kbs kama dini hainitambui mm et kisa ni haramu ya kazi gani sasa
Mtoto umempata kwa zinaa kawaulize wenzio wanavyopata tabu hata huko serikalini.. Siwezi kufuata uzinzi kama ujinga wako .

Ww umempata kwa zinaa ila sio mtoto haramu , unatakiwa kuwa na elimu sio ubishi wapi nimesema mtoto haramu.. Sio ruhusu kumuita mtoto haramu wala hausiki na makosa ya wazazi .

Ishu ni uhalali wengi wenu watoto wa nje mnapigwa sio wenu , wanaojua watoto wao wanawaandika kweny urithi na wanapewa urithi sehemu ili kutoingilia watoto wa ndoa .. Kama mzinifu usioe zaa wote nje ili wawe na haki sawa
 
Kama wewe muislam unatakiwa uwende sehemu ya mirathi wakupe elimu ya mirathi.

Kila sehemu ina sheria zake mfano Tanzania ina sheria ya raia pacha kwa mtoto mpaka afike 18y anatakiwa achague uraia. Sasa huyu mtoto nae atasema hana haja ya kuifata sheria ya Tanzania ?.

Concern yangu ni kwamba kama dini inaonyesha kumbagua kiumbe ambae hakuamua pa kuzaliwa.Kama sheria ingekuwa inawaadhibu hao waliomleta sawa ila kama ni mtoto ndo anakomolewa then hakuna cha kunifanya niende kujifunza kwenye mirathi
 
Niwaombe nini?? Sema kwa sababu nipo njema kimaisha ila ingekuwa hivyo pangechimbika as long as mali ni za baba,hata kuroga ningeroga
Duuuuh hii hatari kweli
 
Concern yangu ni kwamba kama dini inaonyesha kumbagua kiumbe ambae hakuamua pa kuzaliwa.Kama sheria ingekuwa inawaadhibu hao waliomleta sawa ila kama ni mtoto ndo anakomolewa then hakuna cha kunifanya niende kujifunza kwenye mirathi
Haki swa huoni hata mzazi ndio chanzo kwa nn asimzae kweny ndoa? 😀 😀
 
Back
Top Bottom