Sheria ya ndoa ifanyiwe marekebisho kuruhusu ndoa za mkataba

Sheria ya ndoa ifanyiwe marekebisho kuruhusu ndoa za mkataba

Ingawa unetumia lugha kali kidogo, ila uko sahihi,
Chanzo cha ndoa nyingi kuingia kwenye mafarakano ni kwasababu ya kumuasi Mungu na kuishi kiholela bila kufuata sheria ya ndoa iliyowekwa na Mungu.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Mkuu mada hizi zimekuwa nyingi na zinachosha kweli kweli.
 
Naingia kwenye mada moja kwa moja na kwa ufupi bila kumchosha mtu yeyote. Kwa utafiti binafsi niliofanya hivi karibuni, ndoa nyingi hapa nchini, na katika nchi nyingine za kiafrika, huingia migogoro au kuvunjika kabisa kwa sababu ya wanawake kuwa na uhakika wa ndoa ya kudumu, hasa hizi ndoa za mke mmoja (one wife, one husband). Mwanamke akishajua kwamba
💯
 
Mikataba kwa ajiri ya nini sasa? Kama haujui unachokwenda kufanya katika ndoa ni vema ujifunze kwanza.

Ndio nyingi zinafeli kutokana na mseto changamoto za kitabia ambazo watu hutoka nazo makwao na kuzipeleka kwa mtu ambaye alimuahidi kuishi nae kwa amani na utulivu wakisaidiana kutafuta maisha.
 
Mkuu nadhani bado hujaelewa hoja yangu na kama umeielwa basi umeilewa nusu.

Kwanza, ndoa ni mkataba lakini sio mkataba wa kudumu na kumbuka kwamba kila aina ya ndoa (ndoa ya kimila, kikristo au kiislamu) ina masharti yake na namna ya kuivunja. Ninachojaribu kusema ni kwamba kuwepo na sheria itakayo harmonize ndoa zote ili kusiwe na mkwamo pindi mwanaume anashindwa kuishi na mke. Kwa kuwa mume ndiye atakuwa anasaini na ku renew mkataba, pindi mke akikengeuka hakuna haja ya kwenda mahakamani. Simply unasubiri mkataba (mfano wa miaka mitatu, mitano, etc) una expire kisha una terminate contract kwa kuto renew mkataba mpya. Huhitaji kupoteza muda na pesa kwenda mahakamani kujieleza au kupeleka mashahidi. Tupo pamoja?

Pili, sitaki ndoa zifike mahakamani.....mashataka yanapoteza muda na pesa.....nataka ndoa iishie mikononi mwa mume (anayesaiani mkataba). Hivi wachezaji wa mpira wasipoongezewa mkataba huwa wanakimbilia mahakamani? La hasha! Timu isipokuongezea mkataba unatafuta timu nyingine au unastaafu (ikiwa umri umeenda).

Tatu, nimetoa pendekezo hili kwa sababu sheria ya ndoa ya Tanzania haisemi ukomo wa ndoa ni kila baada ya miaka mingapi. Haisemi chochote kuhusu ukomo wa ndoa. Serikali itakapoanza kutumia sheria ya ndoa ya mkataba hapa nchini lazima itataja muda wa mkataba (mfano miaka mitatu. mitano, kumi, etc).
Sasa Mkuu kuna mambo unachanganya.

Kwanza inatakiwa ujue kuwa ndoa zote zinasimamiwa na sheria ya ndoa, iwe ya kiislam, iwe ya kikristu au iwe ya kimila zote hizo zinasimamiwa na sheria ya ndoa.

Pili, ndoa ni mkataba ila ni mkataba ambao haujatoa sehemu ya kuuvunja kwenye mazingira hayo ndipo inatumika mahakama. Sasa kwanini mkataba wa ndoa usiseme wazi kuwa wahusika mume na mke wanaweza kuvunja mkataba wao pakitokea kutokuelewana au hata wakiridhiana wenyewe?.

Zipo sababu nyingi miongoni ni matunda ya ndoa ambapo kuna watoto na mali, hivi vitu sidhani kama umeviwaza. Naona sehemu kubwa unamuwaza mwanaume pekee

Endapo ikiwa hivyo unavyopendekeza basi madhara ni mengi zaidi na ugomvi utaongezeka gasa kwenye kulea watoto na kugawanywa kwa mali, ndoa zikiwa rahisi kuvunjwa basi jua ni udhaifu wa kisheria na utapeli wa kimapenzi ndipo utaposhika hatamu.

Kutaibuka watoto waliotelekezwa, kutaibuka nfoa za msimu zenye lengo la kuvuna mali (udangaji rasmi) kutaibuka na vurugu nyingi sana

Wazo lako ni zuri ila wazo lako halitatui changamoto zilizopo zaidi linaongeza changamoto.

Sheria bora inaangalia sio tu haki za walengwa bali haki ya jamii nzima.
 
WATU WANAOISHI BILA KUOANA WANAISHI VIZURI KULIKO HAWA WA KANISANI AU MSIKINI(TENA BORA HAWA)
NYAKATI ZETU HIZI KUOA NI RISK SANA
 
WATU WANAOISHI BILA KUOANA WANAISHI VIZURI KULIKO HAWA WA KANISANI AU MSIKINI(TENA BORA HAWA)
NYAKATI ZETU HIZI KUOA NI RISK SANA
Umeongea ukweli 100% mkuu. Nimeshuhudia ndoa nyingi watu wanaishi bila kuoana zinakuwa na amani sana; hazina hekaheka kama hizi ndoa za kikristo na kiislamu ambazo wanawake hudhani wamepata tiketi kudumu kuendeleza ngebe kwenye ndoa. Wanaudhi sana ujue hawa viumbe kutoka sayari isiyojulikana.
 
Mikataba kwa ajiri ya nini sasa? Kama haujui unachokwenda kufanya katika ndoa ni vema ujifunze kwanza.

Ndio nyingi zinafeli kutokana na mseto changamoto za kitabia ambazo watu hutoka nazo makwao na kuzipeleka kwa mtu ambaye alimuahidi kuishi nae kwa amani na utulivu wakisaidiana kutafuta maisha.
Kumbe hata wewe umeona mkuu? Ndoa nyingi zinavurugwa na wanawake hasa pale wanapokuwa na uhakika wa ndoa ya kudumu. Dawa yao ni ndoa za mikataba tu, hakuna namna nyingine. Hawa viumbe ni wasumbufu sana.
 
Unaokoteza tu mandiko ili kuhalalisha sheria mbovu ya ndoa iliyopo. Ni wapi Mungu aliwaonya au kuwalaani hao waliooa wanawake wengi ktk hayo maandiko ya biblia niliyokuwekea hapo?
Hoja nzuri…
 
Kufuatia kuongezeka matukio ya wanawake kukengeuka kwenye ndoa, nasisitiza serikali ipeleke bungeni muswada wa dharula kuruhusu ndoa za mikataba. Hakuna haja ya kuumizana kichwa na ndoa za kudumu.
 
Back
Top Bottom