Shillingi ya Tanzania yazidi kuporomoka dhidi ya shillingi ya Kenya

Shillingi ya Tanzania yazidi kuporomoka dhidi ya shillingi ya Kenya

Masikini Venus Star...kweli JF imekuwa kokoro. Zamani JF haikuwa hivi...bado nakumbuka siku Makamba alipomwaga viwavi humu baada ya kuyanunulia simu janja makapi yaliyototolewa kwenye mikesha ya mwenge kama wewe!
Niambie haya maelezo yooote uliyoandika yanahusianaje na mada hii? 👇 👇 👇 👇
Shillingi ya Tanzania yazidi kuporomoka dhidi ya shillingi ya Kenya

Unaweza kujikita kwenye context badala ya kwenda nje ya mada?

Tuanzie hapa:
Je, Exchange rate inauhusiano upi na ukuaji wa uchumi?
 
Kati ya Japan na Kenya ni nchi ipi yenye uchumi mkubwa?
Nikiangalia Exchange rate hapo KES ni superior kwa Japanese Yen.

Nipe ufafanuzi hapo mtaalam wa uchumi.
Mi wala sio mtaalam wa uchumi Na sijui chochote cha kiutafiti kuhusu uchumi najiongelea tu hapa kwa mtazamo wangu tu ingawa utalaam wako umeniondolea kaujinga fulani hivi.
 
Mi wala sio mtaalam wa uchumi Na sijui chochote cha kiutafiti kuhusu uchumi najiongelea tu hapa kwa mtazamo wangu tu ingawa utalaam wako umeniondolea kaujinga fulani hivi.
Asante sana. Nilikuwa nadhani wewe ni mtalaam wa uchumi tuende hatua kwa hatua.
 
Tuna devalue our currency kuboresha manunuzi ya bidhaa zetu!! Si tunazalisha sana na tunawauzia sana wakenya....Sasa tykipandisha bei ya shilingi watanunuaje? China waliowahi kufanya mchezo huu dhidi ya dollar ... nadhani walifanikiwa.....!!!

Majibu ya hoja yako yapo mengi sana hili jibu la kwangu usilitilie maanani maana sina utaalamu wa foreign exchange!
Acha uongo mkuu, mme devalue kitu gani wakati ninyi ni wa hivyohivyo tu miaka yote na ndivyo mlivyoumbwa?
Ina maana ninyi ndiyo mmeipandisha shilingi ya Kenya iimarike dhidi ya US$?
Mnaleta siasa za uchawa kwenye mambo serious? Ninyi kweli mnaweza kuja au mpo kwenye position ya ku devalue thamani ya sarafu yenu? Kwa kipi mlicho nacho?
Kitu pekee mnachoweza kufanya na kupelekea devalue ni hizo rushwa na ufisadi wenu, ambazo zinapelekea miradi isiyokamilika au isiyo na tija. Kukosekana kwa utawala bora, lack of commitment n.k
 
Tuna devalue our currency kuboresha manunuzi ya bidhaa zetu!! Si tunazalisha sana na tunawauzia sana wakenya....Sasa tykipandisha bei ya shilingi watanunuaje? China waliowahi kufanya mchezo huu dhidi ya dollar ... nadhani walifanikiwa.....!!!

Majibu ya hoja yako yapo mengi sana hili jibu la kwangu usilitilie maanani maana sina utaalamu wa foreign exchange!
True kama nchi inazalisha sana na inashindana katika export basi unakuwa na advantage pesa yako ikiwa ina trade chini ila shida kama nyinyi kila kitu import basi tunashida. Ziko nchi pesa zao strong sana against dollar kama Djibout lakini maisha ni expensive sana na pesa yao haina soko. Tusichukuwe kila kitu negative au tusijiaminishe eti kuwa na strong Shilling ndio uchumi bora, hapana uchumi una mambo mengi sana ziko nchi pesa zao zina trade zaidi ya Dollar, mfano Kuwait, Oman hata Bahrain hawa Dinar moja ni kama dollar 3 lakini nchi za KSA na UAE hata Qatar 1 Riyal kama dola 3.6 sasa kwa akili zetu unaweza kusema hawa wanauchumi mkubwa kuliko USA, jibu hapana. Kuwait plus Oman hawafikii uchumi wa Saudia tu. Narudia kama tunashindana na Kenya kwenye export basi pesa yetu kuwa chini ya Kenya ni advantage kwetu kwanini? sababu wakija hapa na dola 100 anapata pesa nzuri Tsh inaweza kununua kwa wingi lakini ikiwa bidhaa yetu ni produce hapa hai link na US. Mfano mazao tutauza sana sababu tunazalisha ndani mkenya ataona 1000 Ksh haileti gunia lakini nikichange Tz napata gunia na nusu. Lakini tukiwa watu wa import tu hapo tutakuwa na shida inflation itakuwa juu kwa bei za bidhaa.
 
Uchumi haupo hivyo kijana wangu. Ukiangalia Exchange rate anagalia pia na Inflation rate.

Uchumi ni kuhusu mtumiaji wa mwisho kijana wangu.

Ukitaka kujua hivyo angalia liter moja ya petrol kenya inauzwa dollar ngapi against bei ta Tanzania.

Kumbuka sote tunanunua mafuta in dollars.
Ok hoja hizo twambie uchumi wetu ukoje? Umepanda? Mfumuko wa bei ukoje? Umeshuka au umepanda? Hebu sema naona unazunguka tuu 😂😂😂😂😂😂😂😂😂
 
Je, Exchange rate inauhusiano upi na ukuaji wa uchumi?
Hebu rudia kusoma michango yangu yote miwili. Ni wapi nimetaja neno UCHUMI? Nimeongelea kuimarika kwa shilingi ya Kenya dhidi ya dola na dhidi ya Tsh. Umeniita dogo, dogo kwa nani?
 
True kama nchi inazalisha sana na inashindana katika export basi unakuwa na advantage pesa yako ikiwa ina trade chini ila shida kama nyinyi kila kitu import basi tunashida. Ziko nchi pesa zao strong sana against dollar kama Djibout lakini maisha ni expensive sana na pesa yao haina soko. Tusichukuwe kila kitu negative au tusijiaminishe eti kuwa na strong Shilling ndio uchumi bora, hapana uchumi una mambo mengi sana ziko nchi pesa zao zina trade zaidi ya Dollar, mfano Kuwait, Oman hata Bahrain hawa Dinar moja ni kama dollar 3 lakini nchi za KSA na UAE hata Qatar 1 Riyal kama dola 3.6 sasa kwa akili zetu unaweza kusema hawa wanauchumi mkubwa kuliko USA, jibu hapana. Kuwait plus Oman hawafikii uchumi wa Saudia tu. Narudia kama tunashindana na Kenya kwenye export basi pesa yetu kuwa chini ya Kenya ni advantage kwetu kwanini? sababu wakija hapa na dola 100 anapata pesa nzuri Tsh inaweza kununua kwa wingi lakini ikiwa bidhaa yetu ni produce hapa hai link na US. Mfano mazao tutauza sana sababu tunazalisha ndani mkenya ataona 1000 Ksh haileti gunia lakini nikichange Tz napata gunia na nusu. Lakini tukiwa watu wa import tu hapo tutakuwa na shida inflation itakuwa juu kwa bei za bidhaa.
Jitahidi kutumia Paragraphs katika uandishi wako.
Hata kama ukiwa na point muhimu uandishi wa namna hii ni wa watu wasio makini.
 
Hebu rudia kusoma michango yangu yote miwili. Ni wapi nimetaja neno UCHUMI? Nimeongelea kuimarika kwa shilingi ya Kenya dhidi ya dola na dhidi ya Tsh. Umeniita dogo, dogo kwa nani?
Kuimarika kwa pesa ya kenya dhidi ya dollar inauhusiano gani na Tsh?
 
Kuimarika kwa pesa ya kenya dhidi ya dollar inauhusiano gani na Tsh?
1. Thamani ya shilingi ya Tanzania dhidi ya shilingi ya Kenya...shilingi ya Tanzania imepororomoka
2, Thamani ya shilingi ya Tanzania dhidi ya dola...shilingi ya Tanzania imeporomoka.

Ni kitu gani usichoelewa? Incidence, coincidence or enemy action!
 
1. Thamani ya shilingi ya Tanzania dhidi ya shilingi ya Kenya...shilingi ya Tanzania imepororomoka
2, Thamani ya shilingi ya Tanzania dhidi ya dola...shilingi ya Tanzania imeporomoka.

Ni kitu gani usichoelewa?
Tueleze sasa baada ya kuporomoka TSh kuna impacts gani zinazoweza kumuathili mtanzania?
 
Tueleze sasa baada ya kuporomoka TSh kuna impacts gani zinazoweza kumuathili mtanzania?
Soma mada (thread) kama ilivyoletwa. Kama unataka anzisha mada yako ya uchumi, tutachangia!
 
Soma mada (thread) kama ilivyoletwa. Kama unataka anzisha mada yako ya uchumi, tutachangia!
Hoja yoyote ikiletwa lazima tujikite kwenye context kwa kutumia methodology ya
4WH (What, Who, When, Why, and How) Sasa kijana wangu tukikuuliza maswali ya How na Why usikimbie mada.

Kama umeshindwa kujibu waache wataalam wajibu. 🤣 🤣 🤣 🤣
Wewe unalazimisha tuendelee kuongelea WHAT tu.
 
Jitahidi kutumia Paragraphs katika uandishi wako.
Hata kama ukiwa na point muhimu uandishi wa namna hii ni wa watu wasio makini.
Sasa ndugu yangu mimi napeleka ujumbe tu nianze tena kuandika kama niko kwenye chumba za mitihani? Muda huo wa kupanga paragraph nitautoa wapi? Ndio maana kuna barua rasmi na zisizo kuwa rasmi. Hapa JF ujumbe tu muhimu ila kama naandika barua rasmi kiserikali au taasisi hapo natumia elimu ya darasani.
 
Shilingi ya Kenya kuna kipindi iligonga mpaka 23, ni kwamba hio 16 ilishuka of recent..., Sasa hivi imeanza kurudi ilipotoka....

Cha maana zaidi tusiangalie upandaji au ushukaji wa Tshs na pesa nyingine cha maana tuweze kujitegemea kwa bidhaa nyingi kuliko kwenda kuagiza / kununua huku na kule na mwisho wa siku tukiwa na bidhaa tutashangilia hapa pesa yetu ikiwa cheaper sababu bidhaa zetu zitakuwa bei rahisi ukilinganisha na wenzetu wenye pesa yenye gharama...
 
Jitahidi kutumia Paragraphs katika uandishi wako.
Hata kama ukiwa na point muhimu uandishi wa namna hii ni wa watu wasio makini.
Ila nashukuru nitazingatia maoni yako nitalifanyia kazi.
 
Sasa ndugu yangu mimi napeleka ujumbe tu nianze tena kuandika kama niko kwenye chumba za mitihani? Muda huo wa kupanga paragraph nitautoa wapi? Ndio maana kuna barua rasmi na zisizo kuwa rasmi. Hapa JF ujumbe tu muhimu ila kama naandika barua rasmi kiserikali au taasisi hapo natumia elimu ya darasani.
Huo ni ushauri tu. Unaweza kuuchukua au kuacha. Maamuzi ni yako.
Kwenye uandishi wako jitahidi kutumia paragraphs
 
Back
Top Bottom